Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 44

Watoto Wako Watamutumikia Yehova Wakati Watakomaa?

Watoto Wako Watamutumikia Yehova Wakati Watakomaa?

“Yesu akaendelea kuwa na hekima zaidi na kukomaa kimwili na akaendelea kukubaliwa na Mungu na wanadamu.”​—LU. 2:52.

WIMBO 134 Watoto Amana Kutoka kwa Mungu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni uamuzi gani njo wa muzuri zaidi?

MARA mingi maamuzi yenye wazazi wanakamata inaweza kuwa na matokeo ya muda murefu mu maisha ya watoto wao. Kama wazazi wanakamata maamuzi ya mubaya, wanaweza kuletea watoto wao matatizo. Lakini kama wanakamata maamuzi ya muzuri, wanaweza kusaidia watoto wao wakuwe na maisha yenye furaha. Hata vile, watoto pia wanapaswa kukamata maamuzi ya muzuri. Kumutumikia Yehova, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, njo uamuzi wa muzuri zaidi wenye kila mutu anaweza kukamata.​—Zb. 73:28.

2. Yesu na wazazi wake walikamata maamuzi gani ya muzuri?

2 Yosefu na Maria walipenda sana kusaidia watoto wao wamutumikie Yehova. Na maamuzi yenye walikamata ilionyesha kama ile njo ilikuwa jambo la maana mu maisha yao. (Lu. 2:40, 41, 52) Yesu pia alikamata maamuzi ya muzuri yenye ilimusaidia afanye mapenzi ya Yehova. (Mt. 4:1-10) Yesu alifikia kuwa mwanaume muaminifu, hodari, na mwenye kuhangaikia wengine. Kwa kweli, kila muzazi mwenye kumupenda Yehova, anaweza kufurahia kuwa na mutoto mwenye iko na sifa kama za Yesu.

3. Tutajibia maulizo gani mu hii habari?

3 Mu hii habari, tutajibia maulizo yenye kufuata: Yehova alikamata maamuzi gani ya muzuri kumuhusu Yesu? Wazazi Wakristo wanaweza kujifunza nini wakati wanafikiria maamuzi yenye Yosefu na Maria walikamata? Na vijana Wakristo wanaweza kujifunza nini wakati wanafikiria maamuzi yenye Yesu alikamata?

WAZAZI, MUJIFUNZE KUPITIA MUFANO WA YEHOVA

4. Yehova alikamata uamuzi gani wa maana kuhusu Mwana wake?

4 Yehova alichagua wazazi wazuri sana kwa ajili ya Yesu. (Mt. 1:18-23; Lu. 1:26-38) Maneno ya Maria yenye kutoka ku moyo yenye kupatikana mu Biblia inaonyesha kama alimupenda sana Yehova na alipenda sana Neno lake. (Lu. 1:46-55) Na namna Yosefu alitii mambo yenye Yehova alimuomba afanye inaonyesha kama alikuwa anamuogopa Yehova, na alipenda kumufurahisha.​—Mt. 1:24.

5-6. Yehova aliruhusu Mwana wake apatwe na magumu gani?

5 Yehova hakuchagua watu wenye kuwa matajiri ili wakuwe wazazi wa Yesu. Zabihu yenye Yosefu na Maria walitoa kisha Yesu kuzaliwa inaonyesha kama walikuwa maskini. (Lu. 2:24) Inawezekana Yosefu alikuwa na kanyumba pembeni ya kwake, mwenye alikuwa anafanyia kazi ya useremala. Yosefu na Maria hawakukuwa na feza mingi ao vitu mingi vya kimwili, zaidi sana wakati familia yao ilifikia kuongezeka na kuwa na watoto karibu saba.​—Mt. 13:55, 56.

6 Wakati fulani Yehova alimulinda Yesu ili mambo fulani ya mubaya isimupate. Lakini wakati mwingine aliruhusu Yesu apatwe na magumu. (Mt. 2:13-15) Kwa mufano, ku mwanzo watu fulani wa familia ya Yesu hawakuamini kama alikuwa Masiya, na bila shaka ile ilimuhuzunisha sana. (Mk. 3:21; Yoh. 7:5) Inawezekana Yosefu alikufa wakati Yesu alikuwa angali kijana na ile ilimuhuzunisha sana Yesu. Kwa sababu Yesu njo alikuwa mutoto wa kwanza, ni yeye njo alipaswa kuendelesha kazi yenye baba yake alikuwa anafanya. (Mk. 6:3) Wakati alikuwa anakomaa, Yesu alijifunza kuhangaikia familia yake. Inawezekana alikuwa anatumika sana ili kuwategemeza. Kwa hiyo, alielewa namna mutu anajisikiaka wakati anachoka kisha kutumika muchana muzima.

Wazazi mufundishe watoto wenu ili wajue kama wakati wanapata magumu wanapaswa kutafuta mashauri mu Biblia (Ona fungu la 7) *

7. (a) Bibi na bwana wanapaswa kujiuliza nini kuhusu kukomalisha watoto? (b) Namna gani Mezali 2:1-6 inaweza kusaidia wazazi wazoeze watoto wao?

7 Bibi na bwana wenye wanapenda kuwa na watoto, wanapaswa kujiuliza hivi: ‘Kama Yosefu na Maria, tuko watu wenye kumupenda Yehova na Neno lake, wenye Yehova anaweza kuchagua ili kukomalisha mutoto?’ (Zb. 127:3, 4) Wazazi wanapaswa kujiuliza hivi: ‘Tuko tunafundisha watoto wetu kama kutumika sana ni jambo la maana?’ (Muh. 3:12, 13) ‘Tuko tunalinda watoto wetu wasipatwe na mambo ya mubaya mu ulimwengu wa Shetani?’ (Mez. 22:3) Kwa kweli, hata kama munajikaza sana ili kulinda watoto wenu, wakati fulani wanaweza kupata magumu. Lakini kama munaendelea kuwatayarisha kwa kuwafundisha kwa upendo, watajua kama wakati wanapata magumu wanapaswa kutafuta mashauri mu Biblia. (Soma Mezali 2:1-6.) Kwa mufano, kama mutu fulani wa familia anaacha kumutumikia Yehova, utumie Biblia ili kusaidia watoto wako wajue juu ya nini ni jambo la maana waendelee kubakia washikamanifu kwa Yehova. (Zb. 31:23) Ao kama mutu fulani mwenye wanapenda anakufa, uwaonyeshe maandiko fulani ya Biblia yenye inaweza kuwasaidia wapiganishe huzuni yao na wakuwe na amani.​—2 Ko. 1:3, 4; 2 Ti. 3:16.

WAZAZI, MUJIFUNZE KUPITIA MUFANO WA YOSEFU NA MARIA

8. Kulingana na Kumbukumbu la Torati 6:6, 7, Yosefu na Maria walikuwa na daraka gani?

8 Yosefu na Maria walifuata muongozo wa Yehova wakati walikuwa wanamuzoeza Yesu. Ile ilifanya Yesu akubaliwe na Yehova wakati alifikia kukomaa. (Soma Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.) Yosefu na Maria walimupenda sana Yehova, na walijikaza sana ili kusaidia watoto wao pia wamupende sana Yehova.

9. Yosefu na Maria walikamata uamuzi gani wa maana?

9 Yosefu na Maria waliamua kuendelea kumutumikia Yehova kwa ukawaida pamoja na familia yao. Bila shaka, walikuwa wanahuzuria mikutano kwa ukawaida kwenye sinagogi katika Nazareti. Na kila mwaka walikuwa wanaenda Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka. (Lu. 2:41; 4:16) Inawezekana wakati walikuwa wanasafiri ili kuenda Yerusalemu, walikuwa wanafundisha Yesu na ndugu zake kuhusu historia ya watu wa Yehova. Na pengine walikuwa wanawaonyesha nafasi mbalimbali zenye kutajwa mu Maandiko. Wakati familia yao iliongezeka, inawezekana haikukuwa mwepesi kwa Yosefu na Maria kuendelea kumuabudu Yehova kwa ukawaida. Lakini kwa sababu waliendelea kutia ibada ya Yehova pa nafasi ya kwanza, Yehova aliwabariki. Waliendelea kuwa na uhusiano muzuri pamoja naye.

10. Wazazi Wakristo wanaweza kujifunza mambo gani kupitia mufano wa Yosefu na Maria?

10 Wazazi, munaweza kujifunza nini kupitia mufano wa Yosefu na Maria? Jambo la maana lenye munaweza kujifunza ni hili: kupitia maneno na matendo yenu musaidie watoto wenu waone kama munamupenda sana Yehova. Munapaswa kujua kama zawadi ya muzuri zaidi yenye munaweza kupatia watoto wenu ni kuwasaidia wamupende Yehova. Na jambo la maana zaidi lenye munaweza kuwafundisha ni kuendelea kujifunza, kusali, kukusanyika, na kuhubiri kwa ukawaida. (1 Ti. 6:6) Ni kweli kama munapaswa kupatia watoto wenu vitu vya kimwili vyenye wako navyo lazima. (1 Ti. 5:8) Lakini munapaswa kukumbuka kama haiko vitu vya kimwili njo vitasaidia watoto wenu waokolewe na kuingia katika ulimwengu mupya. Ili wapate zile baraka wanapaswa kuwa na urafiki wa karibu pamoja na Yehova. *​—Eze. 7:19; 1 Ti. 4:8.

Inafurahisha sana kuona kama wazazi wengi Wakristo wako wanasaidia watoto wao wamukaribie Yehova! (Ona fungu la 11) *

11. (a) Namna gani shauri lenye kuwa mu 1 Timoteo 6:17-19 linaweza kusaidia wazazi wakamate maamuzi ya muzuri wakati wako wanakomalisha watoto wao? (b) Ni miradi gani yenye familia inaweza kujiwekea, na wanaweza kupata baraka gani kama wanafanya vile? (Ona kisanduku “ Mutajiwekea Miradi Gani?”)

11 Inafurahisha sana kuona kama wazazi wengi Wakristo wako wanasaidia watoto wao wamukaribie Yehova. Wanaendelea kumuabudu Yehova. Wanahuzuria mikutano na mikusanyiko, na wanajikaza kuhubiri habari njema. Familia fulani zinaenda kutumikia mahali kwenye kuwa lazima ya wahubiri. Wengine wanaenda kutembelea Beteli, ao wanasaidia kazi ya ujenzi. Familia zenye kujikaza kufanya ile mambo zinapaswa kutumia feza, na haiko mwepesi kwa familia fulani kupata feza. Lakini baraka zenye wanapata zinawafanya wakuwe matajiri kiroho. (Soma 1 Timoteo 6:17-19.) Watoto wenye wamekomalia mu familia za vile wanaendelea kufanya ile mambo wakati wanakomaa. Na wako wenye furaha kwa sababu wazazi wao waliwakomalisha mu ile njia! *​—Mez. 10:22.

VIJANA, MUJIFUNZE KUPITIA MUFANO WA YESU

12. Yesu alipaswa kufanya nini wakati alikomaa?

12 Sikuzote Yehova, Baba wa mbinguni wa Yesu, anakamata maamuzi ya muzuri. Wazazi wake wa ku dunia pia walikamata maamuzi ya muzuri. Lakini wakati Yesu alikomaa alipaswa pia kujikamatia maamuzi ya muzuri. (Gal. 6:5) Juu ya nini? Juu kama sisi, yeye pia alikuwa na uhuru wa kuchagua. Angependa angeamua kama hatamutumikia Yehova. Lakini hakufanya vile. Alichagua kuendelea kuwa na uhusiano muzuri pamoja na Yehova. (Yoh. 8:29) Namna gani mufano wake unaweza kusaidia vijana leo?

Vijana musizarau mashauri ya wazazi wenu hata siku moja (Ona fungu la 13) *

13. Ni uamuzi gani wenye Yesu alikamata wakati alikuwa angali kijana?

13 Wakati Yesu alikuwa kijana mudogo, alichagua kuendelea kutii wazazi wake. Hata siku moja hakuzarau mashauri yao kwa kuwaza kama alikuwa anajua mambo mingi kuliko wao. Lakini, ‘aliendelea kujitiisha kwao.’ (Lu. 2:51) Kwa sababu Yesu alikuwa mutoto wa kwanza, alipaswa kufanya mambo fulani ili kusaidia familia yake. Bila shaka, alijikaza sana ili kujua kazi ya useremala yenye Yosefu alikuwa anafanya, juu ile ingemusaidia aweze kutegemeza familia yao.

14. Ni nini inatusaidia kujua kama Yesu alizoea kujifunza Neno la Mungu?

14 Inawezekana wazazi wa Yesu walimuambia kama alizaliwa kwa njia ya muujiza. Na inawezekana walimuambia mambo yenye wajumbe wa Mungu walisema juu yake. (Lu. 2:8-19, 25-38) Lakini Yesu hakutosheka tu na mambo yenye wazazi wake walimuambia. Alikuwa anajifunza Maandiko yeye mwenyewe. Ni nini inatusaidia kujua kama Yesu alizoea kujifunza Neno la Mungu? Wakati alikuwa angali kijana, walimu katika Yerusalemu “waliendelea kushangazwa na uwezo wake wa kuelewa na majibu yake.” (Lu. 2:46, 47) Na wakati alikuwa na miaka 12 tu, tayari alikuwa hakika kama Yehova ni Baba yake.​—Lu. 2:42, 43, 49.

15. Namna gani Yesu alionyesha kama alipenda kufanya mapenzi ya Baba yake?

15 Wakati Yesu alielewa mambo yenye Yehova alipenda afanye, alichagua kufanya mapenzi ya Yehova. (Yoh. 6:38) Alijua kama watu wengi watamuchukia. Na hata kama ile ilimuhuzunisha, alichagua tu kumutii Yehova. Wakati Yesu alibatizwa mu mwaka wa 29, jambo lenye alihangaikia sana lilikuwa kufanya mapenzi ya Yehova. (Ebr. 10:5-7) Hata wakati Yesu alikaribia kufa kwenye muti wa mateso, aliendelea kuazimia kufanya mapenzi ya Baba yake.​—Yoh. 19:30.

16. Watoto wanaweza kujifunza nini kupitia mufano wa Yesu?

16 Utii wazazi wako. Kama Yosefu na Maria, wazazi wako hawako wakamilifu. Lakini Yehova aliwapatia daraka la kukuzoeza, kukulinda, na kukuongoza. Kama unasikiliza mashauri yao na kuheshimia mamlaka yao, mambo ‘yatakuendea muzuri.’​—Efe. 6:1-4.

17. Kulingana na Yoshua 24:15, vijana wanapaswa kujikamatia uamuzi gani?

17 Uamue ni nani utatumikia. Unapaswa kumujua Yehova muzuri, kujua mapenzi yake, na kujua namna unaweza kufanya mapenzi yake mu maisha yako. (Ro. 12:2) Ile itakusaidia ukamate uamuzi wa maana sana mu maisha yako, ni kusema, uamuzi wa kumutumikia Yehova. (Soma Yoshua 24:15; Muh. 12:1) Kama unajifanyia programu ya kuendelea kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida, upendo wako kwa Yehova utaendelea kuongezeka, na imani yako itakuwa nguvu zaidi.

18. Vijana wanapaswa kuchagua kufanya nini, na ile itawaletea faida gani?

18 Uchague kutia mapenzi ya Yehova pa nafasi ya kwanza mu maisha yako. Ulimwengu wa Shetani unaweza kukufanya ufikiri kama ikiwa unatumia uwezo wenye uko nao ili kujitafutia faida, utakuwa na furaha. Kusema kweli, watu wenye wanapenda sana kuwa matajiri wanajitoboa wenyewe “kila mahali kwa maumivu mengi.” (1 Ti. 6:9, 10) Lakini kama unamusikiliza Yehova na unachagua kutia mapenzi yake pa nafasi ya kwanza, utakuwa na maisha ya muzuri, na “utatenda kwa hekima.”​—Yos. 1:8.

UTAFANYA NINI?

19. Wazazi wanapaswa kukumbuka nini?

19 Wazazi, mufanye yote yenye munaweza ili kusaidia watoto wenu wamutumikie Yehova. Mumutegemee na atawasaidia mukamate maamuzi ya muzuri. (Mez. 3:5, 6) Mukumbuke kama mambo yenye munafanya njo inaweza kusaidia watoto wenu sana kuliko mambo yenye munasema. Kwa hiyo, mukamate maamuzi yenye inaweza kuwasaidia wafikie kukubaliwa na Yehova.

20. Vijana watapata baraka gani kama wanachagua kumutumikia Yehova?

20 Vijana, wazazi wenu wanaweza kuwasaidia mukamate maamuzi ya muzuri mu maisha. Lakini ninyi wenyewe njo muko na daraka la kukamata ile maamuzi juu mukubaliwe na Mungu. Kwa hiyo, umuige Yesu na uchague kumutumikia Baba yako wa mbinguni mwenye upendo. Kama unafanya vile, utakuwa na maisha ya muzuri na yenye furaha leo. (1 Ti. 4:16) Na wakati wenye kuja utakuwa na maisha yenye furaha zaidi!

WIMBO 133 Mwabudu Yehova Ujanani

^ fu. 5 Wazazi Wakristo wanapenda watoto wao wakuwe na furaha na wamutumikie Yehova wakati watakomaa. Ni maamuzi gani yenye wanaweza kukamata ili kusaidia watoto wao wamutumikie Yehova? Vijana Wakristo wanapaswa kukamata maamuzi gani ili kuwa na maisha ya muzuri? Tutajibia ile maulizo mu hii habari.

^ fu. 11 Ona kisanduku chenye kichwa “Siwezi Kuwazia Kuwa na Wazazi Bora Kuliko Hawa” mu Amuka! ya Mwezi wa 10, 2011, uku. 20, na habari yenye kichwa “Barua ya Pekee kwa Wazazi Wao” mu Amuka! ya tarehe 8 Mwezi wa 3, 1999, uku. 25.

^ fu. 66 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati Yesu alikuwa mutoto, bila shaka Maria alimusaidia amupende Yehova. Leo pia, mama Wakristo wanajikaza kusaidia watoto wao wamupende Yehova.

^ fu. 68 MAFASIRIO YA PICHA: Yosefu alipenda sana kuenda kumuabudu Yehova kwenye sinagogi pamoja na familia yake. Leo pia, baba Wakristo wanajikaza sana kuendelea kuhuzuria mikutano kwa ukawaida pamoja na familia zao.

^ fu. 70 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu alijifunza kufanya kazi yenye Baba ake alikuwa anafanya. Leo pia, vijana wanaweza kujifunza kufanya kazi yenye baba zao wanafanya.