Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 42

Ukuwe Hakika Kabisa Kama Uko na Kweli

Ukuwe Hakika Kabisa Kama Uko na Kweli

“Muchunguze mambo yote; mushikamane na mambo ya muzuri.” ​—1 TE. 5:21.

WIMBO 142 Tusiache Tumaini Yetu

KIFUPI YA HABARI *

1. Juu ya nini watu wengi wanachanganikiwa?

 LEO, dini za mingi zinajiita kuwa za Kikristo na zinasema kama zinamuabudu Mungu mu njia yenye inamupendeza. Njo maana watu wengi wanachanganikiwa! Wanajiuliza hivi, “kuko dini moja ya kweli, ao dini zote zinamupendeza Mungu?” Tuko hakika kabisa kama mambo yenye tunafundisha ni ya kweli, na kama namna ya kuabudu yenye Mashahidi wa Yehova wanafuata leo njo njia moja yenye inamupendeza Yehova? Inawezekana kabisa kuwa hakika juu ya ile mambo? Tuone basi ushuhuda fulani.

2. Kulingana na 1 Watesalonike 1:5, juu ya nini mutume Paulo alikuwa hakika kabisa kama mambo yenye aliamini ilikuwa kweli?

2 Mutume Paulo aliamini kama alipata kweli. (Soma 1 Watesalonike 1:5.) Na hakuamini tu juu ile ingefanya ajisikie muzuri. Paulo alikuwa anajifunza kwa uangalifu Neno ya Mungu. Aliamini kama “kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Ti. 3:16) Mambo yenye alikuwa anajifunza ilionyesha nini? Mu Maandiko, Paulo alipata ushuhuda wenye kuonyesha kama Yesu njo Masiya mwenye aliahidiwa, ushuhuda wenye viongozi wa dini Wayahudi walikatala kukubali. Wale viongozi wanafiki, walisema kama walikuwa wanafundisha watu kweli kuhusu Mungu, lakini walifanya mambo yenye Mungu anachukia. (Tit. 1:16) Tofauti nao, Paulo hakuchagua mambo fulani katika Neno ya Mungu yenye angeamini na yenye hangeamini. Alikuwa tayari kufundisha na kutumikisha “shauri lote la Mungu.”​—Mdo 20:27.

3. Tunapaswa kupata majibu ya maulizo yetu yote ili kujihakikishia kama tuko na kweli? (Ona kisanduku, “ Kazi na Mawazo ya Yehova​—‘Ni Nyingi Sana Kusimulia.’”)

3 Watu fulani wanawaza kama dini ya kweli inapaswa kujibia ku kila ulizo, hata maulizo yenye Biblia haijibie moja kwa moja. Ile inawezekana kabisa? Ona mufano wa Paulo. Alitia moyo waamini wenzake “wachunguze mambo yote,” lakini alisema pia kama, kulikuwa mambo ya mingi yenye hakuelewa. (1 Te. 5:21) Aliandika hivi: “Tunajua kwa sehemu tu,” na aliongezea hivi, “tunaona kwa njia yenye haiko ya waziwazi kupitia kioo cha metali.” (1 Ko. 13:9, 12) Paulo hakuelewa mambo yote; na siye pia. Lakini Paulo alijua kwa ujumla kusudi ya Yehova. Alijua mambo mingi yenye ilimufanya kuwa hakika kama mambo yenye aliamini ni ya kweli!

4. Namna gani tunaweza kujihakikishia kama tumepata kweli, na ni mambo gani tutachunguza kuhusu Wakristo wa kweli?

4 Njia moja ya kujihakikishia kama tumepata kweli ni kwa kulinganisha namna ya kuabudu yenye Yesu alituachia na namna yenye Mashahidi wa Yehova wanaabudu leo. Mu hii habari, tutaona kama Wakristo wa kweli (1) wanakatala ibada ya sanamu, (2) wanaheshimia jina Yehova, (3) wanapenda kweli, na (4) wanapendana kabisa.

TUNAKATALA IBADA YA SANAMU

5. Yesu anatufundisha nini kuhusu namna ya muzuri ya kuabudu Mungu, na namna gani tunaweza kutumikisha mambo yenye alifundisha?

5 Juu Yesu alimupenda sana Yehova Mungu, ile ilimuchochea amuabudu yeye tu. Alifanya vile wakati alikuwa mbinguni na hata wakati alikuwa ku dunia. (Lu. 4:8) Alifundisha pia wanafunzi wake wafanye vile. Hakuna siku yenye Yesu, wala wanafunzi wake waaminifu, walitumiaka sanamu mu ibada. Juu Mungu ni roho, hakuna mutu mwenye anaweza kutengeneza kitu yenye inaweza kumufanana! (Isa. 46:5) Tutasema nini kuhusu kufanya sanamu ya wale wenye kuitwa watakatifu na kuiabudu? Yehova anasema hivi katika amri ya pili ya zile amri kumi: “Haupaswe kujifanyia sanamu ya kuchongwa wala umbo ya kitu fulani chenye kuwa juu mbinguni wala chenye kuwa chini juu ya dunia . . . Haupaswe kuviinamia.” (Kut. 20:4, 5) Hii maneno iko wazi kwa wale wenye wanapenda kufurahisha Yehova.

6. Ni namna gani ya kuabudu yenye Mashahidi wa Yehova wako wanafuata leo?

6 Wanahistoria fulani walikubali kama Wakristo wa kwanza, walishikamana tu na Mungu. Kwa mufano, kitabu moja inasema kama Wakristo wa kwanza “wangechukia kabisa” wazo ya kutumia sanamu mu ibada. (History of the Christian Church) Leo, Mashahidi wa Yehova wanafuata namna ya kuabudu yenye Wakristo wa karne ya kwanza waliacha. Hatutoe sala kwa sanamu za “watakatifu” ao kwa malaika, na hata hatusali kwa Yesu. Na hatufanyie sanamu za serikali tendo ya ibada. Hata kutokee nini, tumeamua kabisa kutii hii maneno ya Yesu: “Yehova Mungu wako ndiye unapaswa kuabudu.”​—Mt. 4:10.

7. Kuko tofauti gani kati ya Mashahidi wa Yehova na dini zingine?

7 Leo, watu wanapendaka sana kusikiliza viongozi wa dini wenye kujulikana sana. Wanawapendaka sana na karibu tu waanze kuwaabudu. Watu wengi wanaenda mu makanisa yao, wanauza vitabu vyao, na wanatoa sana makuta juu ya kuwategemeza. Watu fulani wanaamini kila kitu wale viongozi wanasema. Ni nguvu sana kuwaza kama wale watu wenye wanaendaka ku makanisa mbalimbali, wanaweza kushituka kama Yesu anaonekana mu hii wakati! Tofauti ni kwamba, waabudu wa kweli wa Yehova hawafuatake wanadamu. Hata kama tunaheshimia wale wenye kuongoza, tunakubali fundisho ya Yesu yenye kuwa wazi, yenye inasema: “Ninyi wote, ni ndugu.” (Mt. 23:8-10) Hatukuwake tunaabudu wanadamu, hata kama ni viongozi wa dini ao wakubwa wa serikali. Na hatuungake mukono mambo yao ya dini ao ya politike. Lakini, tunajikaza kila mara kutokuwa sehemu ya ulimwengu. Kusema kweli, mu hii mambo yote, siye tuko tofauti kabisa na dini zenye zinajiita kuwa za Kikristo.​—Yoh. 18:36.

TUNAHESHIMIA JINA YEHOVA

Wakristo wa kweli wanaona kama ni pendeleo kubwa sana kuambia wengine juu ya Yehova (Ona fungu ya 8-10) *

8. Tunajua namna gani kama Yehova anapenda jina yake itukuzwe na ijulikane kwa watu wote?

8 Siku moja, Yesu alisali hivi: “Baba, tukuza jina lako.” Yehova alijibia ile sala na sauti kubwa kutoka mbinguni, yenye kusema kama atatukuza jina yake. (Yoh. 12:28) Katika utumishi wake wote, Yesu alitukuza jina ya baba yake. (Yoh. 17:26) Kwa hiyo Wakristo wa kweli leo, wanaona kuwa pendeleo kubwa sana kutumia jina ya Mungu na kuiambia wengine.

9. Namna gani Wakristo wa karne ya kwanza walionyesha kama waliheshimia jina ya Mungu?

9 Mu karne ya kwanza kisha kuzaliwa kwa Yesu, muda kidogo kisha kuzaliwa kwa kutaniko ya Kikristo, Yehova “alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kati yao watu kwa ajili ya jina lake.” (Mdo. 15:14) Wale Wakristo wa karne ya kwanza, walifurahia sana kutumia jina ya Mungu na kuiambia pia wengine. Walitumia jina ya Mungu mu utumishi wao, na mu maandishi yao. * Walionyesha kabisa kama walikuwa watu kwa ajili ya jina ya Mungu.​—Mdo. 2:14, 21.

10. Ni ushuhuda gani unaonyesha kama Mashahidi wa Yehova njo watu kwa ajili ya jina ya Yehova?

10 Je, Mashahidi wa Yehova, ni watu kwa ajili ya jina ya Yehova? Fikiria ushuhuda wenye kufuata. Leo, viongozi wengi wa dini wamefanya yao yote ili kuonyesha kama Mungu hana jina. Wametosha jina ya Mungu mu tafsiri zao za Biblia, na mu hali fulani, wamekataza watu kutumia jina ya Mungu mu makanisa yao. * Ni wazi kama, ni Mashahidi wa Yehova tu njo wenye wanapatia jina ya Mungu heshima. Nani atabisha ile? Hakuna dini ingine yenye inajulisha jina ya pekee ya Mungu, sawa vile Mashahidi wa Yehova. Kusema kweli, tuko tunafanya yetu yote ili kuishi kulingana na jina yetu Mashahidi wa Yehova. (Isa. 43:10-12) Tumechapisha zaidi ya kopi millioni 240 za Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, yenye iko na jina Yehova fasi kwenye iliondolewa na watafsiri wa Biblia. Tena, tumechapisha vichapo vyenye kutegemea Biblia, vyenye vinatumia sana jina Yehova katika luga zaidi ya 1 000!

TUNAPENDA KWELI

11. Namna gani Wakristo wa kwanza walionyesha kama walipenda kweli?

11 Yesu alipenda kweli, ni kusema, kweli kuhusu Mungu na makusudi yake. Yesu aliishi kulingana na ile kweli, na alijulisha watu wengine ile kweli. (Yoh. 18:37) Wafuasi wa kweli wa Yesu nao pia walipenda sana kweli. (Yoh. 4:23, 24) Kwa kweli, mutume Petro aliita dini ya Kikristo “njia ya kweli.” (2 Pe. 2:2) Juu walipenda kweli sana, Wakristo wa kwanza walikatala mafundisho ya dini, desturi na hata mawazo ya kipekee yenye ilipingana na kweli. (Kol. 2:8) Vilevile leo, Wakristo wa kweli wanafanya yao yote ili “kutembea katika kweli” kwa kufanya mambo yenye wanaamini na namna yao ya kuishi ipatane na Neno ya Yehova.​—3 Yo. 3, 4.

12. Baraza Yenye Kuongoza, inafanyaka nini wakati inatambua kama namna yetu ya kuelewa mambo inapaswa kubadilishwa, na juu ya nini inafanyaka vile?

12 Mashahidi wa Yehova hawaseme kama kila mara wao njo wanaelewa muzuri kila kitu yenye iko mu Biblia. Wakati fulani, walifanya makosa mu namna yao ya kufasiria mafundisho fulani ya Biblia na mu namna yao ya kupanga kutaniko. Ile haipaswe kutushangaza, juu Maandiko inasema kama ujuzi wenye hauna makosa utakuwa unaongezeka hatua kwa hatua. (Kol. 1:9, 10) Yehova anafunuaka kweli hatua kwa hatua, na tunapaswa kuwa tayari kumungojea ili afunue ile kweli hatua kwa hatua. (Mez. 4:18) Wakati Baraza Yenye Kuongoza inaona kama ni lazima kubadilisha namna tulikuwa tunaelewa ao kufanya jambo fulani, inakuwaka tayari kufanya vile bila kukawia. Dini za mingi leo, zinakuwaka zinabadilisha mafundisho yao juu zinapenda kupendeza washiriki wao ao juu tu zinapenda kujulikana. Lakini Mashahidi wa Yehova, wanafanyaka mabadiliko juu wanapenda kumukaribia zaidi Yehova na kumuabudu mu njia yenye Yesu alifanya. (Yak. 4:4) Wakati tunafanya mabadiliko fulani, haiko juu mawazo ya watu wa hii dunia imebadilika, lakini ni juu tunaelewa muzuri zaidi Biblia. Tunapenda kweli!​—1 Te. 2:3, 4.

TUNAPENDANA SANA

13. Ni sifa gani ya maana zaidi yenye Wakristo wa kweli walionyesha, na ile inaonekana namna gani leo kati ya Mashahidi wa Yehova?

13 Wakristo wa karne ya kwanza walikuwa na sifa mingi za muzuri, lakini sifa ya maana sana yenye iliwatambulisha, ilikuwa upendo. Yesu alisema hivi: “Kwa jambo hili, watu watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu​—kama muko na upendo kati yenu.” (Yoh. 13:34, 35) Leo, Mashahidi wa Yehova wako na upendo na umoja wa kweli mu dunia yote. Wako tofauti sana na dini zote, juu wako kama familia hata kama wanatoka mu inchi mbalimbali na wako na desturi mbalimbali. Siye Mashahidi wa Yehova, tunajionea upendo wa kweli ku mikutano yetu, ku mikusanyiko ya muzunguko na ya eneo. Ile inatusaidia kuwa hakika kama, namna yetu ya kumuabudu Yehova, inamupendeza.

14. Kulingana na Wakolosai 3:12-14, ni mu njia gani ya muzuri tunaweza kuonyeshana upendo mwingi kati yetu?

14 Biblia inasema “tukuwe na upendo mwingi kati yetu.” (1 Pe. 4:8) Njia ya muzuri ya kuonyesha kama tuko na ile upendo, ni kwa kusameheana na kuvumiliana sababu siye wote hatukamilike. Tena tunatumia nafasi mbalimbali ili kuonyesha ukarimu kwa watu wote mu kutaniko, hata kwa wale wenye pengine walitukosea. (Soma Wakolosai 3:12-14.) Kusema kweli, ile kifungo ya upendo njo alama kubwa yenye kututambulisha kuwa Wakristo wa kweli.

“IMANI MOJA”

15. Ni mu njia gani zingine, tunafuata namna ya kuabudu yenye Wakristo wa karne ya kwanza walituachia?

15 Tunafuata namna ya kuabudu yenye inafanana kabisa na ile ya Wakristo wa karne ya kwanza. Kwa mufano, tengenezo yetu imepangwa mu njia yenye kufanana kabisa na vile ilikuwa zamani kwa Wakristo wa karne ya kwanza. Tuko na waangalizi, wazee, na watumishi wa huduma sawa vile wao. (Flp. 1:1; Tit. 1:5) Na sawa vile wale Wakristo, tunaheshimia sheria ya Yehova kuhusu ngono na ndoa, na mambo yenye Mungu anasema kuhusu kutumia damu, na pia tunalinda kutaniko kwa kuondoa ule mwenye anakatala kufuata sheria ya Mungu​—Mdo. 15:28, 29; 1 Ko. 5:11-13; 6:9, 10; Ebr. 13:4.

16. Maneno yenye kuwa mu Waefeso 4:4-6, inatufundisha nini?

16 Yesu alisema kama watu wengi wangesema kuwa wangekuwa wanafunzi wake, lakini haiko wote njo wangekuwa wafuasi wake wa kweli. (Mt. 7:21-23) Tena Biblia imetuonya kama katika siku za mwisho, wengi, kwa inje “wangeonekana kuwa na ushikamanifu kwa Mungu.” (2 Ti. 3:1, 5) Lakini, Biblia inasema waziwazi kama kuko tu “imani moja” yenye Mungu anakubali.​—Soma Waefeso 4:4-6.

17. Leo, nani njo wako wanafuata Yesu na wako na imani ya kweli?

17 Leo, nani njo wako na imani ya kweli? Tumechunguza ushuhuda. Tumeona pia namna ya kuabudu ya muzuri yenye Yesu alifundisha, na yenye Wakristo wa karne ya kwanza walifanya. Jibu iko wazi, na hakuna ingine: Ni Mashahidi wa Yehova tu. Tuko na pendeleo kubwa sana ya kuwa watu wa Yehova na kujua kweli kumuhusu Yehova na makusudi yake! Kwa hiyo basi, tuendelee kuwa hakika kabisa kama tuko na kweli.

WIMBO 3 Nguvu Yangu, Tumaini Yangu, Ninakutegemea

^ Mu hii habari, tutaona namna ya kuabudu ya kweli yenye Yesu alituachia na namna wafuasi wake wa kwanza waliifuata. Tutaona pia ushuhuda wenye kuonyesha kama leo Mashahidi wa Yehova wako wanafuata ile namna ya kuabudu.

^ Ona kisanduku, “Je, Wakristo wa Karne ya Kwanza Walitumia Jina la Mungu?” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Tarehe 1 Mwezi wa 7, 2010, uku. 6.

^ Kwa mufano, mu 2008, Papa Benoît 16 alikataza Wakatoliki “kutumia jina ya Mungu ao kuitamuka” mu kanisa, mu nyimbo ao mu sala.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Tengenezo ya Yehova imetoa Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya mu luga zaidi ya 200 ili kusaidia watu wasome Biblia yenye inatumia jina ya Mungu mu luga yao ya kizalikio.