Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Kazi Ni Kubwa”

“Kazi Ni Kubwa”

NI WAKATI wa mukutano wa maana sana katika Yerusalemu. Mufalme Daudi ameita wakubwa, maofisa, na wanaume wenye nguvu. Wanafurahi kusikia tangazo la pekee. Yehova amechagua Sulemani, mutoto wa Daudi, ili ajenge jengo la pekee kwa ajili ya ibada ya Mungu wa kweli. Mufalme Daudi mwenye kuzeeka, amepewa plan ya jengo hilo kupitia roho ya Mungu na ameipatia Sulemani. Daudi anasema hivi: “Kazi ni kubwa; kwa kuwa jumba hilo la kifalme si la mwanadamu, bali ni la Yehova Mungu.”—1 Nya. 28:1, 2, 6, 11, 12; 29:1.

Kisha Daudi anauliza hivi: ‘Na ni nani anayejitolea kuujaza mukono wake leo kwa zawadi kwa ajili ya Yehova?’ (1 Nya. 29:5) Ikiwa ulikuwa hapo, ungetenda namna gani? Moyo wako ungekuchochea kutegemeza kazi hiyo kubwa? Waisraeli walitenda bila kukawia. Kwa kweli, ‘walishangilia kutokana na matoleo yao ya hiari [ya kujipendea] waliyotoa, kwa maana walimutolea Yehova matoleo ya hiari kwa moyo kamili.’—1 Nya. 29:9.

Mamia ya miaka kisha hapo, Yehova alianzisha jambo kubwa zaidi kuliko hekalu hilo. Alianzisha hekalu kubwa la kiroho, ni kusema, mupango ili wanadamu wamukaribie katika ibada kwa musingi wa zabihu ya Yesu. (Ebr. 9:11, 12) Namna gani Yehova anasaidia watu wamukaribie leo? Ni kupitia kazi yetu ya kufanya wanafunzi. (Mt. 28: 19, 20) Kupitia kazi hiyo, kila mwaka tunaongoza mamilioni ya mafunzo ya Biblia, maelfu ya wanafunzi wanabatizwa, na mamia ya makutaniko yanaanzishwa.

Kwa sababu ya ongezeko hilo, inaomba kuchapisha vichapo vingi zaidi vyenye kutegemea Biblia, kujenga na kutunza Majumba ya Ufalme, na kupata Majumba kwa ajili mikusanyiko. Kwa kweli, kazi yetu ya kutangaza habari njema ni kazi kubwa na yenye kuleta baraka!—Mt. 24:14.

Upendo kwa Mungu na jirani, na kujua kama kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme ni ya haraka, vinachochea watu wa Mungu ‘kuujaza mukono wao . . . kwa zawadi kwa ajili ya Yehova’ kwa kutoa michango ya kujipendea. Ni jambo lenye kufurahisha sana ‘kumuheshimu Yehova kwa vitu [vyetu] vyenye samani’ na kuona namna michango hiyo inatumiwa kwa uaminifu na kwa busara ili kufanya kazi kubwa zaidi katika historia ya wanadamu!—Met. 3:9.