Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tumepangwa Kupatana na Neno la Mungu

Tumepangwa Kupatana na Neno la Mungu

‘Kwa hekima Yehova mwenyewe aliuweka musingi wa dunia. Aliziweka mbingu imara kwa utambuzi.’—METHALI 3:19.

NYIMBO: 105, 107

1, 2. (a) Watu fulani wanasema nini juu ya wazo lenye kuonyesha kama Mungu ana tengenezo? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

KUHUSU mambo ya ibada, watu fulani wanasema hivi: “Hatuna lazima ya kuongozwa na tengenezo fulani. Tuko tu na lazima ya kuwa na urafiki pamoja na Mungu.” Hilo ni kweli? Ukweli wa mambo unaonyesha nini?

2 Katika habari hii tutaona kama Yehova anafanya mambo kwa utaratibu na anapanga watu wake. Tutazungumuzia pia mambo yenye tunapaswa kufanya wakati tengenezo la Yehova linatutolea muongozo. (1 Wakorintho 14:33, 40) Wakati wa mitume, watu wa Yehova walifuata muongozo wenye kuwa katika Maandiko na waliweza kuhubiri habari njema katika maeneo mengi. Kama Wakristo hao, sisi pia tunaacha Biblia ituongoze leo. Na tunatii maagizo yenye tengenezo la Mungu linatutolea. Kufanya hivyo kunatuwezesha kuhubiri habari njema katika dunia yote. Pia, tunalinda usafi, amani, na umoja wa kutaniko.

YEHOVA NI MUNGU MWENYE KUPANGA MAMBO MUZURI

3. Ni nini inatuhakikishia kama Yehova ni Mungu mwenye kupanga mambo muzuri?

3 Wakati tunaangalia vitu vyenye Yehova aliumba, tunaona wazi kuwa yeye ni Mungu mwenye kupanga mambo muzuri. ‘Aliuweka musingi wa dunia. Aliziweka mbingu imara kwa utambuzi.’ (Methali 3:19) Kuko mambo mengi yenye hatujue juu ya vitu vyenye Yehova aliumba. Kwa kweli, ni ‘munongono [mambo madogo sana] ulioje wa jambo lililosikiwa juu yake.’ (Ayubu 26:14) Lakini mambo madogo yenye tunajua juu ya ulimwengu yanaonyesha wazi kama ni wenye kupangwa muzuri sana. (Zaburi 8:3, 4) Mamilioni ya nyota zinatembea katika anga kwa njia yenye kupangwa muzuri. Pia, fikiria namna sayari (planètes) zenye kuwa katika mufumo wa jua zinazunguka-zunguka jua. Utaratibu huo unawezekana tu kwa sababu Yehova amepanga namna sayari na nyota zinazunguka. Wakati tunafikiria namna ‘amezifanya mbingu kwa uelewaji’ na dunia pia, tunapenda kumusifu, kumuabudu, na kuwa washikamanifu kwake.—Zaburi 136:1, 5-9.

4. Ni nini inafanya wanasayansi washindwe kupata majibu ya maulizo mengi ya maana?

4 Wanasayansi wametumia mambo yenye wamejifunza juu ya ulimwengu na dunia yetu ili kufanya maisha yetu yakuwe ya muzuri zaidi. Lakini, wameshindwa kupata majibu ya maulizo mengi ya maana. Kwa mufano, watu wenye kujifunza nyota, sayari, na vitu vingine katika anga, hawawezi kutufasiria kabisa namna ulimwengu ulianza ao sababu gani mimea, wanyama, na wanadamu wako katika dunia. Na watu wengi hawawezi kufasiria sababu gani wanadamu wanatamani sana kuishi milele. (Mhubiri 3:11) Sababu moja yenye kufanya watu wasipate majibu ya maulizo hayo ni kwamba wanasayansi na watu wengine wanasema kama hakuna Mungu na wanafundisha mageuzi.

5. Ni katika njia gani mbalimbali watu wanategemea sheria za asili?

5 Yehova aliumba sheria nyingi za asili. Sheria hizo hazibadilike. Mafundi wa umeme, wa mabomba ya maji, watu wenye kuendesha ndege, wanganga wenye kufanya upasuaji, na mafundi wengine, wanategemea sheria hizo ili kufanya kazi yao. Kwa mufano, moyo wa kila mwanadamu unapatikana nafasi ileile katika mwili. Kwa hiyo, munganga mwenye kufanya upasuaji anajua mahali pa kuupata katika mwili wa kila mugonjwa. Na kila mutu anajua kama ikiwa mutu anaruka kutoka mahali pa juu sana, ataanguka na anaweza kufa. Tunatii sheria za asili, kama vile nguvu za uvutano, kwa sababu hatupendi kufa.

MAMBO YENYE MUNGU AMEPANGA

6. Ni nini inaonyesha kama Yehova anapenda watu wamuabudu katika njia yenye kupangwa muzuri?

6 Kwa kweli, Yehova amepanga ulimwengu katika njia yenye kupendeza sana. Kwa hiyo, anapenda kabisa watu wake wamuabudu katika njia yenye kupangwa muzuri. Kwa kweli, Yehova ametutolea Biblia ili kutufundisha namna ya kumuabudu. Tutakuwa na maisha ya muzuri na yenye furaha ikiwa tu tunafuata muongozo wenye anatutolea kupitia Biblia na tengenezo lake.

7. Namna Biblia iliandikwa inaweza kutufundisha nini?

7 Biblia ni zawadi ya pekee kabisa yenye kutoka kwa Mungu. Watu fulani wenye elimu wanasema kama Biblia ni vitabu tu vya Wayahudi na vya Wakristo vyenye watu wamekusanya pamoja. Lakini, Mungu aliamua ni nani wangeandika vitabu hivyo, wangeandika wakati gani, na wangeandika mambo gani. Ndiyo sababu vitabu vyote vya Biblia vinatusaidia kuelewa ujumbe wa Mungu. Kuanzia kitabu cha Mwanzo mupaka Ufunuo, Biblia inaonyesha kama kungekuwa “uzao” wenye utafanya dunia ikuwe paradiso tena. Na tumejifunza kama “uzao” huo ni Yesu Kristo na kama Ufalme wake utaonyesha wazi kwamba Yehova ana haki ya kutawala watu wote.​—Soma Mwanzo 3:15; Mathayo 6:10; Ufunuo 11:15.

8. Ni katika njia gani Waisraeli walikuwa wenye kupangwa muzuri?

8 Waisraeli walifuata Sheria yenye Mungu aliwapatia na walikuwa wenye kupangwa muzuri. Kwa mufano, kulikuwa ‘wanawake ambao walifanya utumishi uliopangwa kwenye mwingilio wa hema la mukutano.’ (Kutoka 38:8) Waisraeli walikuwa pia na maagizo juu ya namna ya kuhama na kuhamisha hema la ibada kwa utaratibu. Kisha, Mufalme Daudi alipanga makuhani na Walawi ili wafanye kazi mbalimbali kwenye hekalu. (1 Mambo ya Nyakati 23:1-6; 24:1-3) Wakati Waisraeli walimutii Yehova, aliwabariki. Walikuwa wenye kupangwa muzuri na waliishi katika amani na umoja.—Kumbukumbu la Torati 11:26, 27; 28:1-14.

9. Namna gani makutaniko yalikuwa yenye kupangwa wakati wa mitume?

9 Wakati wa mitume, makutaniko yalikuwa pia yenye kupangwa muzuri. Kulikuwa baraza lenye kuongoza, ni kusema, kikundi fulani cha wanaume wenye walitolea makutaniko muongozo. Mwanzoni, kikundi hicho kilifanyizwa na mitume. Kisha, wazee wengine waliongezwa. (Matendo 6:1-6; 15:6) Yehova aliongoza wanaume fulani wa baraza lenye kuongoza na wengine wenye walitumika nao ili waandike barua zenye kutolea makutaniko mashauri na maagizo. (1 Timotheo 3:1-13; Tito 1:5-9) Makutaniko yalipata faida gani wakati yalifuata muongozo wa baraza lenye kuongoza?

10. Matokeo yalikuwa namna gani wakati makutaniko ya wakati wa mitume yalifuata maagizo ya baraza lenye kuongoza? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

10 Soma Matendo 16:4, 5. Wakati wa mitume, ndugu fulani walikuwa wanatembelea ndugu na dada katika makutaniko ili kuwaambia “maagizo yaliyokuwa yameamuliwa na mitume na wanaume wazee waliokuwa katika Yerusalemu,” ni kusema, baraza lenye kuongoza. Makutaniko yalifuata maagizo hayo na “yakaendelea kufanywa imara katika imani na kuongezeka hesabu siku baada ya siku.” Mufano wao unaweza kutufundisha mambo gani yenye yanaweza kutusaidia katika kutaniko letu leo?

UNAFUATA MUONGOZO?

11. Wazee na watumishi wa huduma wanapaswa kufanya nini wakati wanapata muongozo wenye tengenezo la Mungu linawatolea?

11 Ndugu wa Halmashauri ya Tawi ao Halmashauri ya Inchi, waangalizi wa muzunguko, na wazee wanapaswa kutii muongozo wenye tengenezo la Mungu linawatolea. Ni wazi kama Neno la Yehova linatuambia sisi wote tutii wale wenye kutuongoza. (Kumbukumbu la Torati 30:16; Waebrania 13:7, 17) Wale wenye kuwa washikamanifu kwa Yehova hawako waasi, na hawanungunike juu ya muongozo wenye wanapewa. Hatupendi kuwa kama Diotrefe, mwenye hakuheshimia ndugu wenye walikuwa wanaongoza. (Soma 3 Yohana 9, 10.) Wakati tunafuata muongozo wenye tunapewa, tunasaidia kulinda amani na umoja katika kutaniko. Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ninatia moyo ndugu na dada zangu wakuwe washikamanifu kwa Yehova? Niko tayari kufuata muongozo wenye tengenezo la Mungu linanitolea?’

12. Wazee na watumishi wa huduma wanawekwa namna gani?

12 Hivi karibuni, Baraza Lenye Kuongoza lilitoa maagizo mapya juu ya namna ya kuweka wazee na watumishi wa huduma katika kutaniko. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 11, 2014, kwenye habari yenye kichwa “Maulizo ya wasomaji wetu,” lilifasiria kama wakati wa mitume, baraza lenye kuongoza lilipatia waangalizi wenye kusafiri daraka la kuweka wazee na watumishi wa huduma katika kutaniko. Kwa hiyo, kuanzia Mwezi wa 9 mwaka wa 2014, waangalizi wa muzunguko wamekuwa wakiweka ndugu hao katika makutaniko. Wakati wazee wa kutaniko wanapendekeza ndugu fulani ili akuwe muzee ao mutumishi wa huduma, mwangalizi wa muzunguko anajikaza kujua ndugu huyo na familia yake. Kwa mufano, anaweza kuhubiri naye. (1 Timotheo 3:4, 5) Kisha mwangalizi wa muzunguko na wazee wanafanya mukutano. Wanachunguza kwa uangalifu Maandiko yenye kuzungumuzia sifa zenye muzee ao mutumishi wa huduma anapaswa kuwa nazo.—1 Timotheo 3:1-10, 12, 13; 1 Petro 5:1-3.

13. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaunga mukono muongozo wenye wazee wanatutolea?

13 Wazee wanatutolea muongozo wenye kutoka katika Biblia kwa sababu wanapenda kulinda na kuhangaikia kutaniko. Tunapaswa kuwaunga mukono kwa sababu wanatutolea maagizo hayo kwa faida yetu. (1 Timotheo 6:3) Wakati wa mitume, Wakristo fulani walijiendesha “bila utaratibu.” Hawakukuwa wanatumika hata kidogo lakini walikuwa wanajiingiza katika mambo yenye hayakuwahusu. Wazee walijikaza kuwasaidia, lakini walikataa kubadilika. Mutume Paulo aliambia ndugu na dada katika kutaniko namna wanapaswa kutendea mutu kama huyo. Alisema hivi: ‘Mumutie alama mutu huyo, muache kushirikiana naye.’ Walipaswa kuacha kufanya urafiki pamoja na mutu huyo, lakini wasimuone kama adui. (2 Wathesalonike 3:11-15) Leo, wazee wanajikaza kusaidia mutu mwenye hatii kanuni za Mungu, kwa mufano, ndugu ao dada mwenye anachumbiana na mutu mwenye haiko Shahidi. (1 Wakorintho 7:39) Ikiwa ndugu ao dada huyo anakataa kubadilisha tabia yake, wazee wanaweza kuamua kutoa hotuba yenye kufasiria namna tabia hiyo inaweza kufanya watu waseme mubaya juu ya kutaniko. Ikiwa wazee wanatoa hotuba kama hiyo katika kutaniko lenu, utatenda namna gani? Ikiwa unajua ndugu ao dada mwenye kuwa na tabia hiyo, utaepuka kufanya urafiki pamoja naye? Ukifanya hivyo, unaweza kumusaidia aone kama tabia yake itamuletea matokeo ya mubaya na kama haimupendeze Yehova, na anaweza kubadilisha tabia yake. [1]—Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.

TUENDELEE KULINDA USAFI, AMANI, NA UMOJA WA KUTANIKO

14. Namna gani tunaweza kusaidia kulinda usafi wa kutaniko?

14 Neno la Mungu linatuambia jambo lenye sisi wote tunapaswa kufanya ili tusiruhusu mambo ya mubaya katika makutaniko. Fikiria jambo lenye lilitokea katika Korintho. Mutume Paulo alipenda ndugu na dada wa muji huo. Alisaidia wengi wao wajifunze kweli. (1 Wakorintho 1:1, 2) Kwa hiyo, fikiria namna alijisikia wakati alijua kama mumoja wao alikuwa anafanya mambo ya uasherati na kama ndugu waliacha mutu huyo aendelee kuwa katika kutaniko! Mutume Paulo aliambia wazee ‘wamukabizi [wamutoe] mutu wa namna hiyo kwa Shetani.’ Walipaswa kuondoa mutu huyo katika kutaniko, ni kusema, walipaswa kumutenga. (1 Wakorintho 5:1, 5-7, 12) Leo, wazee wanaweza kuamua kama Mukristo fulani mwenye amefanya zambi nzito na anakosa kutubu atengwe na kutaniko. Ikiwa jambo hilo linatokea, tutatendea mutu huyo mwenye kutengwa kama vile Maandiko yanatuomba? Ikiwa tunafanya hivyo, tunasaidia kulinda usafi wa kutaniko. Na tunaweza kusaidia mutu huyo atambue kama anapaswa kutubu na kuomba Yehova amusamehe.

15. Namna gani tunaweza kulinda amani katika kutaniko?

15 Kulikuwa tatizo lingine katika Korintho. Wakristo fulani walikuwa wanashitaki Wakristo wenzao kwenye tribinali. Paulo aliwauliza hivi: ‘Kwa nini musiache mukosewe badala ya hivyo?’ (1 Wakorintho 6:1-8) Leo, Wakristo fulani katika kutaniko wamefanya makubaliano ya biashara pamoja na ndugu na dada zao, lakini walipoteza feza ao waliona kuwa ndugu na dada zao wamewaiba kwa kutumia udanganyifu. Kwa hiyo, wameshitaki Wakristo wenzao kwenye tribinali. Lakini wakati jambo hilo linatokea, linaweza kufanya watu waseme mambo ya mubaya juu ya Yehova na watu wake. Na linaweza kuleta muvurugo katika kutaniko. Neno la Mungu linatusaidia kuona kama tunapaswa kuendelea kufanya amani na ndugu zetu, hata kama tutapoteza feza kwa sababu ya kufanya hivyo. [2] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) Kwa kweli, Yesu alitufundisha namna ya kumaliza matatizo makubwa na kutoelewana. (Soma Mathayo 5:23, 24; 18:15-17.) Wakati tunatii muongozo wake, tunalinda amani na umoja wa kutaniko.

16. Sababu gani watu wa Mungu wako na umoja?

16 Neno la Yehova linatuambia hivi: “Tazama! Jinsi ilivyo vyema na jinsi inavyopendeza ndugu kukaa pamoja kwa umoja!” (Zaburi 133:1) Wakati Waisraeli walitii Yehova, walikuwa wenye kupangwa muzuri na wenye umoja. Mungu alitabiri hivi juu ya watu wake: “Nitawaunganisha, kama kundi zizini, kama kundi la wanyama katikati ya malisho yake.” (Mika 2:12) Yehova alitabiri pia kama watu wake watajifunza kweli katika Maandiko na watamutumikia kwa umoja. Alisema hivi: ‘Nitabadilisha luga ya vikundi vya watu na kuwapa luga safi, ili wote waliitie jina la Yehova, wamutumikie bega kwa bega.’ (Sefania 3:9) Tuko wenye shukrani sana kwa sababu tunamuabudu Yehova katika umoja!

Wazee wanasaidia mutu fulani mwenye ‘amejikwaa katika kosa fulani.’ (Picha hii inapatana na fungu la 17)

17. Wazee wanapaswa kufanya nini wakati Mukristo fulani katika kutaniko anafanya zambi nzito?

17 Ikiwa Mukristo fulani anafanya zambi nzito, wazee wanapaswa kutenda haraka ili kumusaidia kwa upendo. Wanajua kama Yehova anapenda walinde kutaniko ili lisichafuliwe na matendo ya mubaya ya watenda-zambi na walinde umoja na usafi wa kutaniko. (Methali 15:3) Mutume Paulo alipenda sana ndugu na dada zake wa Korintho na aliwasaidia wakati walikuwa na lazima ya musaada, kama vile tunasoma katika barua yake ya kwanza yenye aliwaandikia. Tunajua kama wazee wenye walikuwa huko walifuata bila kukawia muongozo wa Paulo kwa sababu kisha miezi fulani, aliwapongeza katika barua ya pili yenye aliwaandikia. Mukristo fulani “akijikwaa katika kosa fulani kabla [mbele] ya yeye kulijua,” wazee wanapaswa kumusaidia kwa upole.—Wagalatia 6:1.

18. (a) Namna gani muongozo wenye kuwa katika Neno la Mungu ulisaidia makutaniko ya wakati wa mitume? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

18 Ni wazi kwamba wakati Wakristo wa wakati wa mitume walifuata muongozo wenye kuwa katika Neno la Mungu, makutaniko yao yalikuwa safi, yenye amani, na yenye umoja. (1 Wakorintho 1:10; Waefeso 4:11-13; 1 Petro 3:8) Kwa hiyo, ndugu na dada hao waliweza kuhubiri habari njema “katika uumbaji wote ulio chini ya mbingu.” (Wakolosai 1:23) Leo pia, watu wa Yehova ni wenye umoja na wenye kupangwa muzuri, na wanahubiri habari njema katika dunia yote. Habari yenye kufuata itazungumuzia mambo mengine yenye kuhakikisha kama wanatamani sana kuheshimia Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova, na kutii muongozo wenye kuwa katika Neno lake, Biblia.—Zaburi 71:15, 16.

^ [1] (fungu la 13) Soma kitabu Tengenezo Lenye Kufanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 134-136.

^ [2] (fungu la 15) Ili kupata habari zaidi juu ya hali zenye zinaweza kumufanya Mukristo ashitaki Mukristo mwenzake kwenye tribinali, Soma kitabu Mubaki “Katika Upendo wa Mungu,” ukurasa wa 223, maelezo ya chini.

[Caption on page 13]