Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Waliitwa Kutoka Katika Giza

Waliitwa Kutoka Katika Giza

‘[Yehova] aliwaita ninyi kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.’ —1 PETRO 2:9.

NYIMBO: 116, 102

1. Ni nini ilitokea wakati Yerusalemu iliharibiwa?

KATIKA mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Mufalme Nebukadneza wa Pili na jeshi lake kubwa walishambulia Yerusalemu. Biblia inasema kama mufalme aliua vijana wanaume kwa upanga. ‘Hakumuhurumia kijana wala bikira, muzee wala mukongwe [muzee sana].’ Kisha, “akaiteketeza [akaiunguza] nyumba ya Mungu wa kweli na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu; na minara yake yote ya makao wakaiteketeza kwa moto na pia vyombo vyake vyote vyenye kutamanika.”—2 Mambo ya Nyakati 36:17, 19.

2. Yehova alitoa onyo gani, na Wayahudi wangepatwa na nini?

2 Wayahudi hawangepaswa kushangazwa na uharibifu wa Yerusalemu. Kwa miaka mingi, Mungu alikuwa ametuma manabii ili kuonya watu kama ikiwa wangeendelea kukosa kumutii, Wababiloni wangewashambulia. Wababiloni wangeua Wayahudi wengi kwa upanga, na wale wenye wangeokoka wangepelekwa katika uhamisho katika Babiloni. (Yeremia 15:2) Maisha yao yalikuwa namna gani katika uhamisho? Wakristo nao wamekwisha kupatwa na hali fulani yenye kufanana na utumwa wa Babiloni? Kama ni ndiyo, wakati gani?

MAISHA KATIKA UHAMISHO

3. Namna gani maisha katika uhamisho wa Babiloni yalikuwa tofauti na maisha ya utumwa katika Misri?

3 Yehova alikuwa amewaambia Wayahudi kama walipaswa kukubali hali yao mupya na kuishi maisha ya muzuri kulingana na uwezo wao. Kupitia nabii Yeremia, aliwaambia hivi: ‘Mujenge nyumba na kukaa ndani yake, mupande bustani [mashamba] na kula matunda yake. Pia, mutafute amani kwa ajili ya jiji ambamo nimewapeleka ninyi uhamishoni, nanyi musali kwa ajili yake kwa Yehova, kwa maana katika amani ya jiji hilo kutakuwa na amani kwa ajili yenu wenyewe.’ (Yeremia 29:5, 7) Wayahudi wenye walifuata maagizo ya Yehova waliishi kwa kiasi fulani maisha ya kawaida. Wababiloni waliruhusu Wayahudi washugulikie mambo yao mengi na wasafiri katika inchi yote kwa uhuru. Wakati huo watu wengi walikuwa wanakuja kufanyia biashara katika Babiloni. Maandishi ya zamani yanaonyesha kama Wayahudi wengi wenye walikuwa katika uhamisho, walijifunza kuuza na kuuzisha na walikuwa mafundi wazuri wa kutengeneza vitu. Wayahudi fulani walifikia hata kuwa matajiri. Maisha katika uhamisho wa Babiloni hayakukuwa magumu kama maisha ya utumwa yenye Waisraeli walikuwa nayo katika Misri mamia ya miaka hapo mbele.—Soma Kutoka 2:23-25.

4. Ni watu gani wengine walipaswa kuteseka pamoja na Wayahudi wenye walikosa uaminifu, na sababu gani ilikuwa vigumu kwao kufanya mambo yote yenye Sheria iliwaomba?

4 Wayahudi fulani wenye walipelekwa katika uhamisho walikuwa waaminifu kwa Mungu. Hata kama hawakufanya jambo lolote la mubaya, walipaswa kuteseka pamoja na Wayahudi wengine. Wayahudi walikuwa na mambo ya kimwili yenye walikuwa nayo lazima, lakini wangemuabudu Yehova namna gani? Hekalu na mazabahu yake vilikuwa vimeharibiwa, na makuhani hawangefanya kazi kwa njia yenye kupangwa muzuri. Lakini Wayahudi waaminifu walijikaza kufuata Sheria ya Mungu. Kwa mufano, Danieli, Shadraki, Meshaki, na Abednego walikataa kula chakula chenye Wayahudi walikatazwa. Na Biblia inasema kama Danieli alisali kwa Mungu kwa ukawaida. (Danieli 1:8; 6:10) Lakini, kwa sababu walikuwa wanatawaliwa na taifa la wapagani, Wayahudi waaminifu hawangeweza kufanya mambo yote yenye Sheria iliwaomba.

5. Yehova alipatia watu wake tumaini gani, na sababu gani ahadi hiyo ilikuwa yenye kushangaza?

5 Waisraeli wangeweza tena kuabudu Yehova kwa njia yenye anakubali kabisa? Wakati huo, ingeonekana kama haiwezekane kabisa kwa sababu Babiloni haikukuwa hata kidogo inaachilia watumwa wake. Lakini Yehova Mungu alikuwa ameahidi kama watu wake wangeachiliwa huru, na walifikia kuachiliwa. Ahadi za Mungu zinatimia sikuzote!—Isaya 55:11.

WAKRISTO WAMEKWISHA KUWA WATUMWA WA BABILONI?

6, 7. Sababu gani ni jambo la lazima tubadilishe namna yetu ya kuelewa?

6 Wakristo wamekwisha kupatwa na hali yenye kuwa kama utumwa wa Babiloni? Kwa miaka mingi, Gazeti Munara wa Mulinzi lilisema kama Wakristo waliingia katika utumwa wa Babiloni katika mwaka wa 1918 na wakaachiliwa katika mwaka wa 1919. Lakini, katika habari hii na yenye kufuata tutajifunza sababu gani ni jambo la lazima kubadilisha namna yetu ya kuelewa.

7 Fikiria jambo hili: Babiloni Mukubwa ni dini zote za uongo. Na watu wa Mungu hawakuingia katika utumwa wa dini ya uongo katika mwaka wa 1918. Ni kweli kwamba wakati huo Wakristo watiwa-mafuta waliteswa. Hata hivyo, mateso yao hayakutokana na dini ya uongo, lakini waliteswa zaidi sana na serikali mbalimbali. Muda murefu mbele ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, watiwa-mafuta wa Mungu walikuwa wameanza kujitenga kabisa na dini ya uongo. Kwa hiyo, inaonekana kama watu wa Yehova hawakuingia katika utumwa wa Babiloni katika mwaka wa 1918.

NI WAKATI GANI WATU WA MUNGU WALIKUWA KATIKA UTUMWA WA BABILONI?

8. Ni nini ilitokea kisha kifo cha mitume? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

8 Kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33, maelfu ya Wakristo wapya walitiwa mafuta kwa roho takatifu. Wakristo hao walifikia kuwa “jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa kuwa mali ya pekee.” (Soma 1 Petro 2:9, 10.) Wakati mitume walikuwa wangali wazima walichunga kutaniko kwa uangalifu. Lakini, zaidi sana kisha kifo cha mitume, wanaume fulani katika makutaniko walianza kufundisha mambo ya uwongo, na walipenda kutosha wanafunzi katika njia ya kweli. Wanaume hao walipenda filozofia za Aristote na Plato na wakaanza kufundisha mawazo yao kuliko kufundisha kweli ya Neno la Mungu. (Matendo 20:30; 2 Wathesalonike 2:6-8) Wengi walikuwa wanaume wenye kujulikana na waangalizi katika makutaniko. Kwa hiyo, hata kama Yesu alikuwa ameambia wafuasi wake hivi: “Ninyi nyote ni ndugu,” kikundi chenye watu wenye kujiita viongozi wa dini kilianzishwa.​—Mathayo 23:8.

9. Fasiria namna Wakristo waasi-imani walianza kutumika na serikali ya Roma. Matokeo yalikuwa gani?

9 Katika mwaka wa 313 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Constantin alitawala Roma ya wapagani na akafanya aina hiyo ya dini ya Wakristo waasi-imani kuwa dini yenye kukubaliwa na sheria. Kisha, Kanisa lilianza kutumika sana na serikali ya Roma. Kwa mufano, Constantin alifanya mukutano pamoja na viongozi wa dini, na mukutano huo ulijulikana kwa jina la Baraza la Nicée. Kisha mukutano huo, mutawala huyo alituma katika uhamisho padri mwenye kuitwa Arius kwa sababu alikataa kuamini kama Yesu ni Mungu. Kisha, Théodose akakuwa mutawala wa Roma, na Kanisa Katoliki likakuwa dini ya Utawala wa Roma yenye kukubaliwa na sheria. Wanahistoria wanasema kama Roma ya wapagani iligeuka na kuwa ya “Kikristo” wakati wa Mutawala Théodose. Lakini ukweli ni kwamba hata mbele ya hapo, Wakristo waasi-imani walikuwa wamekubali mafundisho ya wapagani; kwa hiyo, walikuwa tayari sehemu ya Babiloni Mukubwa. Lakini, kulikuwa kungali Wakristo fulani watiwa-mafuta waaminifu. Walikuwa kama ngano yenye Yesu alizungumuzia. Wakristo hao waaminifu walikuwa wanafanya yao yote ili kumuabudu Mungu, lakini ni hesabu kidogo ya watu ndiyo walikuwa wanasikiliza mambo yenye walikuwa wanasema. (Soma Mathayo 13:24, 25, 37-39.) Kwa kweli, walikuwa katika utumwa wa Babiloni!

10. Sababu gani watu walianza kuwa na mashaka juu ya mafundisho ya kanisa?

10 Kwa mamia fulani ya miaka kisha kuzaliwa kwa Yesu, watu wengi wangeweza kusoma Biblia katika Kigiriki ao Kilatini. Wangeweza kulinganisha mafundisho ya Neno la Mungu na mafundisho ya kanisa. Wakati watu fulani waliona kama mafundisho ya kanisa yalikuwa ya uongo, walipinga mafundisho hayo. Lakini ilikuwa hatari kuambia wengine mawazo yao, na wangeweza hata kuuawa kwa sababu ya kufanya hivyo.

11. Namna gani kanisa lilizuia watu wasikuwe na Biblia?

11 Kadiri wakati ulipita, ni hesabu kidogo ya watu ndio walizungumuza Kigiriki ao Kilatini. Na viongozi wa kanisa hawakuruhusu Neno la Mungu litafsiriwe katika luga za watu wa kawaida. Kwa hiyo, ni viongozi wa dini na watu fulani wenye elimu tu ndio wangeweza kujisomea Biblia, na hata wamoja kati ya viongozi hao hawakujua kusoma ao kuandika muzuri. Kila mutu mwenye alipinga mafundisho ya kanisa alipewa malipizi makali. Wakristo watiwa-mafuta waaminifu walipaswa kukutana kwa uficho katika vikundi vidogo-vidogo, na wengine kati yao hawakuweza hata kufanya hivyo. Kama vile Wayahudi wenye walikuwa katika uhamisho Babiloni, watiwa-mafuta wa “ukuhani wa kifalme” hawangeweza kuabudu Yehova kwa njia yenye kupangwa muzuri. Babiloni Mukubwa alikuwa na mamlaka yenye nguvu juu ya watu!

KULIKUWA SABABU ZA KUWA NA TUMAINI

12, 13. Ni sababu gani mbili zenye zilipatia Wakristo tumaini la kutoka katika utumwa? Eleza.

12 Wakristo wa kweli wangefikia kuwa na uhuru wa kumuabudu Mungu waziwazi na kwa njia yenye anakubali? Ndiyo! Kulikuwa sababu mbili za maana za kuwa na tumaini. Sababu ya kwanza ilikuwa kutengenezwa kwa mashini ya kuchapa yenye herufi zenye kupangwa. Mbele mashine hiyo itengenezwe katika mwaka wa 1450 hivi, watu walipaswa kufanya kopi za Biblia kwa kutumia mikono, na kazi hiyo haikukuwa mwepesi. Ili kufanya kopi moja tu ya Biblia, muandikaji mwenye uzoefu angefanya miezi kumi! Pia, waandikaji hao walikuwa wanaandika kwenye vitu vyenye kutengenezwa kwa ngozi ya wanyama. Kwa hiyo, kulikuwa hesabu kidogo ya kopi za Biblia, na zilikuwa bei sana. Lakini, kwa kutumia mashini ya kuchapa na karatasi, mutu mwenye kuwa na uzoefu angechapa zaidi ya kurasa 1300 kila siku!

Kutengenezwa kwa mashini ya kuchapa na bidii ya watafsiri wa Biblia vilitoa tumaini la kutoka katika utumwa wa Babiloni (Picha hii inapatana na fungu la 12, 13)

13 Sababu ya pili ilikuwa kutafsiriwa kwa Biblia. Katika mwaka wa 1500 hivi, hesabu kidogo ya wanaume wenye bidii walitafsiri Neno la Mungu katika luga za watu wa kawaida. Walifanya kazi hiyo hata kama walijua kuwa wangeuawa kwa sababu ya kazi hiyo. Viongozi wa kanisa waliogopa sana. Sababu gani? Kwa sababu waliogopa kwamba ikiwa wanaume na wanawake wenye kuwa na mioyo mizuri wanasoma Biblia katika luga zao, wangeanza kuwauliza maulizo kama vile: ‘Fundisho la pirgatori linapatikana wapi katika Biblia? Ni wapi Biblia inasema kama mutu anapaswa kulipa padri ili afanye misa kwa ajili ya mutu mwenye amekufa? Ni wapi Biblia inazungumuzia juu ya papa na makardinali?’ Mafundisho mengi ya uongo ya kanisa yalitegemea filozofia ya Aristote na Plato; wanaume hao waliishi mamia ya miaka mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Viongozi wa kanisa walikasirika wakati watu waliwauliza maulizo. Wanaume na wanawake wenye walipinga mafundisho yao walihukumiwa kifo. Viongozi wa kanisa walipenda kukataza watu kusoma Biblia na kuuliza maulizo, na mara nyingi waliweza kufanya hivyo. Lakini watu fulani wenye ujasiri walikataa kuongozwa na Babiloni Mukubwa. Walikuwa wamepata kweli kutoka katika Neno la Mungu, na walipenda kujua mengi zaidi! Walikuwa karibu kutoka katika utumwa wa dini ya uongo.

14. (a) Watu wenye walipenda kujifunza Biblia walifanya nini? (b) Eleza namna Ndugu Russell alitafuta kweli.

14 Watu wengi walipenda kusoma na kujifunza Biblia na kuambia wengine mambo yenye walikuwa wamejifunza. Hawakupenda viongozi wa kanisa wawaambie mambo yenye walipaswa kuamini. Kwa hiyo, walikimbilia katika inchi ambamo walikuwa huru kujifunza Biblia. Moja kati ya inchi hizo ilikuwa Amerika. Katika mwaka wa 1870, Charles Taze Russell na hesabu kidogo ya watu wengine walianza kujifunza sana Biblia katika inchi hiyo. Mwanzoni, Ndugu Russell alipenda kujua dini yenye ilikuwa inafundisha kweli. Alilinganisha kwa uangalifu mafundisho ya Biblia na mafundisho ya dini zenye kujiita kuwa za Kikristo, na hata mafundisho ya dini zenye haziko na Kikristo. Bila kukawia, alitambua kama hakuna hata dini moja yenye ilikuwa inafuata kabisa Neno la Mungu. Wakati fulani, alizungumuza na viongozi wa dini nyingi wa eneo lake. Ndugu Russell alitumaini kama wangekubali kweli yenye yeye na kikundi chake walikuwa wamepata katika Biblia na kufundisha kweli hiyo katika makanisa yao. Lakini viongozi hao wa dini hawakupendezwa. Bila kukawia, Wanafunzi wa Biblia walitambua kama hawangemuabudu Mungu pamoja na watu wenye walikuwa katika dini ya uongo.—Soma 2 Wakorintho 6:14.

15. (a) Ni wakati gani Wakristo wa kweli waliingia katika utumwa wa Babiloni? (b) Habari yenye kufuata itajibia maulizo gani?

15 Katika habari hii, tumejifunza kama Wakristo wa kweli waliingia katika utumwa wa Babiloni muda fulani kisha kifo cha mutume wa mwisho. Hata hivyo, tungali na lazima ya kujua majibu ya maulizo haya: Namna gani tunajua kama Wakristo watiwa-mafuta walikuwa wanatoka kabisa katika utumwa wa Babiloni Mukubwa miaka fulani mbele ya mwaka wa 1914? Ni kweli kwamba Yehova hakupendezwa na watumishi wake kwa sababu walipunguza bidii katika kazi ya kuhubiri wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu? Ndugu na dada zetu fulani wakati huo walivunja uaminifu wao kwa kujiingiza katika mambo ya vita, na hilo likafanya Yehova awakatae? Na, ikiwa Wakristo waliingia katika utumwa wa dini ya uongo kisha kifo cha mitume, ni wakati gani walitoka katika utumwa huo? Hayo ni maulizo ya maana sana, na habari yenye kufuata itajibia maulizo hayo.