Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Waliachiliwa Huru Kutoka Katika Dini ya Uongo

Waliachiliwa Huru Kutoka Katika Dini ya Uongo

‘Mutoke kwake, watu wangu.’—UFUNUO 18:4.

NYIMBO: 101, 93

1. Namna gani tunajua kama watu wa Mungu wangeachiliwa huru kutoka katika Babiloni Mukubwa, na tutajibia maulizo gani?

KATIKA habari yenye ilitangulia, tulijifunza kama Wakristo waaminifu walikuwa katika utumwa wa Babiloni Mukubwa. Habari njema ni kwamba hawangebakia katika utumwa huo milele. Tunajua jambo hilo kwa sababu katika Biblia, Mungu anaamuru watu wake ‘watoke’ katika dini ya uongo. (Soma Ufunuo 18:4.) Hilo linahakikisha kama Wakristo wangeachiliwa huru kutoka katika Babiloni Mukubwa. Tuko na hamu ya kujua wangeachilia wakati gani! Lakini, tunapaswa kwanza kujibia maulizo haya: Wanafunzi wa Biblia waliazimia kufanya nini juu ya Babiloni Mukubwa hata mbele ya mwaka wa 1914? Ndugu zetu walikuwa wenye bidii kwa kadiri gani katika kazi ya kuhubiri wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu? Watu wa Mungu walikuwa katika utumwa wa Babiloni wakati huo kwa sababu walikuwa na lazima ya kusaidiwa kufanya mabadiliko?

“KUANGUKA KWA BABILONI”

2. Wanafunzi wa Biblia wa kwanza-kwanza waliamua kufanya nini hata mbele ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu?

2 Miaka mingi mbele ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu (1914-1918), Charles Taze Russell na Wanafunzi wengine wa Biblia walitambua kama dini zenye kujiita kuwa za Kikristo hazikukuwa zinafundisha kweli ya Biblia. Kwa hiyo, walipenda kujitenga kabisa na dini ya uongo. Hata katika mwaka wa 1879, gazeti Le Phare de la Tour de Sion lilisema kama kila kanisa lenye kujiita bibi-arusi mushikamanifu wa Kristo lakini linaunga mukono serikali, liko kabisa sehemu ya Babiloni Mukubwa, yenye Biblia inaita Kahaba.​—Soma Ufunuo 17:1, 2.

3. Wanafunzi wa Biblia walifanya nini ili kuonyesha kama hawakukuwa tena sehemu ya dini ya uongo? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

3 Wanaume na wanawake waaminifu walijua kama ikiwa wangeendelea kuunga mukono dini ya uongo, Mungu hangewabariki. Wengi kati yao walituma barua kwenye makanisa yao zenye kuonyesha kama wametoka kabisa katika makanisa hayo. Wamoja wao walisoma hata barua zao kwa sauti mbele ya kanisa lote. Katika makanisa kwenye jambo hilo halikuruhusiwa, walituma barua zao kwa kila mutu wa kanisa. Wanafunzi wa Biblia walionyesha waziwazi kama walipenda kujitenga kabisa na dini ya uongo! Miaka fulani mbele ya hapo, wangeuawa kwa sababu ya kufanya hivyo. Lakini kufikia mwaka wa 1870, serikali nyingi hazikukuwa tena zinaunga sana mukono makanisa kama zamani. Sasa, watu walikuwa huru kuzungumuza juu ya Biblia na hata kupinga mafundisho ya makanisa.

4. Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, Wanafunzi wa Biblia walikuwa na mawazo gani juu ya Babiloni Mukubwa? Eleza.

4 Wanafunzi wa Biblia walielewa kwamba walipaswa kufanya jambo lingine zaidi ya kuwaambia watu wa familia, marafiki, na watu wa makanisa yao kama hawaunge tena mukono dini ya uongo. Walipenda watu katika dunia yote wajue kama Babiloni Mukubwa ni kahaba! Kwa hiyo, kati ya Mwezi wa 12, mwaka wa 1917 na mwanzo wa mwaka wa 1918, maelfu kidogo ya Wanafunzi wa Biblia walitolea watu kwa bidii trakte 10000000 yenye ilikuwa na habari yenye kichwa “Kuanguka kwa Babiloni Mukubwa.” Trakte hiyo ilifunua wazi kweli juu ya dini zenye kujiita kuwa za Kikristo. Kwa kweli, viongozi wa dini walikasirika sana! Lakini Wanafunzi wa Biblia hawakuacha. Waliazimia kuendelea kuhubiri na kutii ‘Mungu kuwa mutawala kuliko wanadamu.’ (Matendo 5:29) Hilo linatuonyesha nini? Linaonyesha kama wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu wanaume na wanawake hao Wakristo hawakukuwa wanaingia katika utumwa; lakini, walikuwa wanatoka kabisa katika dini ya uongo na walikuwa wanasaidia wengine kufanya hivyo.

WALIKUWA NA BIDII WAKATI WA VITA YA KWANZA YA ULIMWENGU

5. Sababu gani tunasema kama ndugu na dada walikuwa na bidii sana wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu?

5 Zamani, tulikuwa tunasema kama Mungu hakukubali watu wake wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu kwa sababu hawakuhubiri kwa bidii. Ndiyo sababu tulifikiri kama Yehova aliacha Babiloni Mukubwa awakamate katika utumwa kwa muda mufupi. Lakini, ndugu na dada waaminifu wenye walitumikia Mungu kati ya mwaka wa 1914 na 1918 walifikia kufasiria kama wote walifanya yao yote ili kuendelea kuhubiri. Kuelewa muzuri zaidi mambo yenye yalipata Wanafunzi wa Biblia wakati huo kunatusaidia kuelewa matukio fulani yenye kuzungumuziwa katika Biblia.

6, 7. (a) Wanafunzi wa Biblia walikuwa na magumu gani wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu? (b) Ni nini inaonyesha kama Wanafunzi wa Biblia walikuwa na bidii?

6 Kwa kweli, wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, Wanafunzi wa Biblia walikuwa na bidii sana katika kazi ya kuhubiri. Lakini walikuwa pia na magumu mbalimbali. Tuone magumu mawili kati ya hayo. Kwanza, Wanafunzi wa Biblia hawakukuwa wamejifunza namna ya kuhubiri kwa kutumia tu Biblia. Walikuwa wamezoea kutolea watu vitabu na kuacha vichapo vifasirie kweli. Kwa hiyo, wakati kitabu Le mystère de Dieu accompli kilikatazwa na serikali katika mwanzo wa mwaka wa 1918, ndugu na dada wengi walikuwa na magumu ya kuhubiri. Magumu ya pili ilikuwa homa ya Kihispania yenye ilianza mwaka huo. Ugonjwa huo mubaya ulikuwa wenye kuambukiza sana na ukafanya ikuwe vigumu kwa ndugu na dada kusafiri na kuhubiri. Hata kama walikuwa na magumu hayo, Wanafunzi wa Biblia walifanya yao yote ili kuendelea kuhubiri.

Wanafunzi hao wa Biblia walikuwa wenye bidii!(Picha hizi zinapatana na fungu la 6, 7)

7 Katika mwaka wa 1914, kikundi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia, walionyesha filme “Foto-Drama ya Uumbaji.” Filme hiyo yenye ilikuwa na sauti zenye kurekodiwa na picha zenye kucheza-cheza, ilikuwa jambo la mupya wakati huo. Drama hiyo, ilikuwa historia ya wanadamu kuanzia wakati Adamu aliumbwa mupaka mwisho wa Utawala wa Kristo. Ilionyeshwa kwa mara ya kwanza katika mwaka wa 1914, na watu zaidi ya 9000000 waliiona. Fikiria jambo hili: Hesabu hiyo inapita hesabu ya Mashahidi ya Yehova katika dunia yote leo! Ripoti zingine zinaonyesha kama katika mwaka wa 1916, watu zaidi ya 809000 walihuzuria mikutano ya watu wote katika Amerika, na katika mwaka wa 1918, hesabu ya watu hao iliongezeka na kuwa 950000. Wanafunzi hao wa Biblia walikuwa na bidii!

8. Namna gani ndugu wenye kuongoza walitia nguvu Wanafunzi wa Biblia wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu?

8 Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ndugu walifanya yao yote ili kuchapisha vichapo vyenye kutegemea Biblia na kutia moyo Wanafunzi wote wa Biblia. Musaada huo wenye kutolewa kwa upendo uliwatia nguvu waendelee kuhubiri. Richard Barber, mwenye alikuwa muhubiri mwenye bidii wakati huo, alisema hivi: “Tuliweza kuendelea kutumia hesabu kidogo ya waangalizi wenye kusafiri na kuendelea kutolea watu gazeti Munara wa Mulinzi na kulituma katika inchi ya Kanada kwenye lilikuwa limekatazwa.” Aliendelea kusema hivi: “Nilikuwa na pendeleo la kutuma chapa ndogo ya kitabu Le mystère accompli kwa marafiki wenye walikuwa wamenyanganywa vitabu vyao. Ndugu Rutherford aliomba tufanye mikusanyiko katika miji mbalimbali ya mangaribi mwa Amerika na kutuma wasemaji ili wajikaze sana kutia moyo marafiki.”

WALIPASWA KUFANYA MABADILIKO

9. (a) Sababu gani watu wa Mungu walikuwa na lazima ya kufanya mabadiliko fulani kati ya mwaka wa 1914 na 1919? (b) Hata kama walikuwa na lazima yakufanya mabadiliko fulani, itakuwa makosa kuwa na mawazo gani?

9 Kulikuwa jambo fulani lenye Wanafunzi wa Biblia walipaswa kubadilisha. Hawakuelewa muzuri kile Yehova alimaanisha wakati alisema tutii serikali. (Waroma 13:1) Ndiyo sababu wakati fulani walijiingiza katika mambo ya vita. Kwa mufano, wakati raisi wa Amerika aliomba watu wasali kwa ajili ya amani, gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 30 Mwezi wa 5, 1918, lilitia moyo Wanafunzi wa Biblia wasali pia. Wanafunzi fulani wa Biblia walitoa feza ili kutegemeza vita, na wamoja kati yao wakakuwa hata maaskari na kuenda kwenye vita. Lakini, hata kama walikuwa na lazima ya kufanya mabadiliko fulani, ni makosa kuwaza kama ndiyo sababu walifanywa kuwa watumwa wa Babiloni Mukubwa. Ukweli ni kwamba kufikia wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, walikuwa wamejitenga kwa kiasi kikubwa na dini zote za uongo.​—Soma Luka 12:47, 48.

10. Namna gani Wanafunzi wa Biblia walionyesha kama wanaheshimia uzima?

10 Ni kweli kwamba wanafunzi wa Biblia hawakuelewa muzuri inamaanisha nini kwa Wakristo kukataa kujiingiza katika mambo ya vita. Lakini walijua kama ilikuwa mubaya kuua mutu yeyote. Kwa hiyo hata kama ndugu fulani walifikia kuwa maaskari na kubeba silaha wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, walikataa kutumia silaha hizo ili kuua mutu mwengine. Ndugu fulani wenye walikataa kuua, waliwekwa nafasi ya mbele katika vita ili wauawe.

11. Serikali ilitenda namna gani wakati Wanafunzi wa Biblia walikataa kupigana katika vita?

11 Shetani alikuwa na hasira kwa sababu ndugu hao waliendelea kuwa washikamanifu kwa Mungu. Kwa hiyo, aliamusha ‘matatizo kwa njia ya amri [sheria].’ (Zaburi 94:20) Jenerali mumoja wa jeshi la Amerika, James Franklin Bell, aliambia Ndugu Rutherford na Van Amburgh kama serikali ilikuwa imejaribu kufanya sheria mupya. Sheria hiyo ingepatia serikali ruhusa ya kuhukumu kifo mutu yeyote mwenye alikataa kupigana katika vita. Alikuwa anazungumuzia Wanafunzi wa Biblia. Jenerali huyo alikasirika sana na kumuambia ndugu Rutherford kama sheria hiyo haikufanywa kwa sababu raisi wa Amerika aliikataa. Kisha Jenerali huyo alisema hivi: “Lakini tunajua namna ya kuwapata, na tutawapata tu!”

12, 13. (a) Sababu gani ndugu munane walihukumiwa kufungwa kwa muda murefu katika gereza? (b) Ndugu waliachilia uamuzi wao wa kumutii Yehova kwa sababu walifungwa katika gereza? Eleza.

12 Mwishowe, serikali ilipata njia ya kupatia Wanafunzi wa Biblia malipizi. Ndugu Rutherford na Van Amburgh, pamoja na ndugu wengine sita wenye walikuwa pia wanawakilisha Shirika la Watch Tower, walifungwa. Muamuzi mwenye aliwahukumu alisema kama ndugu hao walikuwa hatari sana kuliko kikundi cha maaskari wa Ujerumani. Alisema kama walikuwa wamekosea serikali, jeshi, na makanisa yote na kwamba wanapaswa kupewa malipizi makali. Kwa hiyo, Wanafunzi hao wa Biblia munane walihukumiwa kufungwa katika gereza kwa muda murefu katika Atlanta, Georgia. Lakini, wakati vita iliisha, waliachiliwa huru na mambo yenye walikuwa wameshitakiwa yaliondolewa.

13 Hata wakati walikuwa katika gereza, wanaume hao munane waliazimia kutii sheria ya Mungu. Tunajua hilo namna gani? Waliandikia raisi wa Amerika barua na kumuomba waachiliwe kutoka katika gereza. Katika barua hiyo, walisema kwamba Biblia inatuambia kama hatupaswe kuua, kwa hiyo, kila mutu mwenye kujitoa kwa Mungu na mwenye anakosa kumutii kwa kupenda hatakubaliwa naye na ataharibiwa. Walifasiria kama hiyo ndiyo sababu hawawezi na hawangeua hata kidogo mutu mwengine. Iliomba ujasiri kabisa ili kuandikia raisi maneno hayo! Kwa kweli, ndugu hao hawangeachilia hata kidogo uamuzi wao wa kumutii Yehova.

MWISHOWE WATU WA MUNGU WALIACHILIWA HURU!

14. Kwa kutumia Maandiko, fasiria mambo yenye yalitokea kuanzia mwaka wa 1914 mupaka 1919.

14 Andiko la Malaki 3:1-3 linafasiria mambo yenye yalipata Wanafunzi wa Biblia kati ya mwaka wa 1914 na mwanzoni mwa mwaka wa 1919. (Soma.) Yehova Mungu, “Bwana wa kweli,” na Yesu Kristo, ‘mujumbe wa agano,’ walikuja kuchunguza “wana wa Lawi,” wenye waliwakilisha watiwa-mafuta. Kisha Yehova kuwasaidia wafanye mabadiliko na kuwasafisha, walikuwa tayari kupokea mugawo mupya. Katika mwaka wa 1919, Yesu aliweka ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara,’ mwenye alipewa mugawo wa kuongoza na kufundisha watumishi wote wa Mungu. (Mathayo 24:45) Mwishowe, watu wa Mungu waliachiliwa huru kutoka katika Babiloni Mukubwa. Tangu hapo, wanaendelea kujifunza mengi juu ya mapenzi ya Mungu, na upendo wao kwake umekuwa wenye nguvu hata zaidi. Ni wenye shukrani sana kwa sababu amewabariki! [1] —Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.

15. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa sababu tumeachiliwa huru kutoka katika Babiloni Mukubwa?

15 Tuko wenye shukrani sana kwa sababu tumeachiliwa huru kutoka katika Babiloni Mukubwa. Shetani hajaweza kuharibu ibada ya kweli. Ameshindwa! Lakini, tunapaswa kukumbuka sababu gani Yehova ametuachilia huru. Kusudi lake ni kwamba watu wote waokolewe. (2 Wakorintho 6:1) Lakini dini ya uongo inaendelea kuongoza mamilioni ya watu wenye moyo muzuri, na wako na lazima ya musaada wetu! Tufanye basi yetu yote ili kuiga ndugu zetu waaminifu, kwa kusaidia watu wakuwe huru.

^ [1] (fungu la 14) Kuko mambo mengi yenye kufanana kati ya utumwa wa Wayahudi katika Babiloni na mambo yenye yalifikia Wakristo kisha uasi-imani kuanza. Lakini, hatuwezi kusema kama utumwa wa Wayahudi ulifananisha mambo yenye yalipata Wakristo watiwa-mafuta; kwa hiyo, hatupaswe kutafuta maana ya kiunabii katika kila jambo lenye lilitokea. Kuko mambo fulani yenye kuwa tofauti. Mufano moja ni kwamba Wayahudi walikuwa katika utumwa kwa miaka 70, lakini Wakristo walikuwa katika utumwa miaka mingi zaidi.