Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unajikaza Kuwa na Mawazo Kama ya Yehova?

Unajikaza Kuwa na Mawazo Kama ya Yehova?

“Mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu.”​—RO. 12:2.

NYIMBO: 56, 123

1, 2. Wakati tunaendelea kufanya maendeleo, tunajifunza nini? Leta mufano.

WAZIA mutu fulani anapatia mutoto mudogo zawadi. Wazazi wa mutoto huyo wanamuambia, “Sema aksanti.” Anasema aksanti kwa sababu wanamuambia afanye vile. Lakini wakati mutoto anaendelea kukomaa, anaanza kuelewa juu ya nini wazazi wake wanawaza kama ni jambo la maana akuwe mwenye shukrani wakati wengine wanamufanyia mambo ya muzuri. Mwishowe, anachochewa kushukuru wengine bila mutu kumuambia afanye vile, kwa sababu amejifunza kuwa mwenye shukrani.

2 Sisi pia tulikuwa katika hali kama hiyo. Wakati tulianza kujifunza kweli, tulijifunza kama ni jambo la maana sana kutii amri za musingi za Yehova. Lakini wakati tunaendelea kufanya maendeleo, tunajifunza mambo mengi juu ya mawazo yake, ni kusema, mambo yenye anapenda, mambo yenye anachukia, na namna anaona mambo mbalimbali. Wakati tunaacha mawazo ya Yehova yachochee maamuzi na matendo yetu, tunajikaza kuwa na mawazo kama yake.

3. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kuwa na mawazo kama ya Yehova?

3 Hata kama tunafurahia kujifunza kuwaza kama Yehova, wakati fulani ni vigumu kuwa na mawazo kama yake kwa sababu hatukamilike. Kwa mufano, tunajua mawazo ya Yehova juu ya mwenendo muzuri, kupenda sana vitu vya kimwili, kazi ya kuhubiri, kutumia damu mubaya, na mambo mengine. Lakini inaweza kuwa vigumu kwetu kuelewa juu ya nini anaona mambo hayo kwa njia hiyo. Kwa hiyo, namna gani tunaweza kujifunza kuwaza zaidi kama Yehova? Na namna gani hilo litatusaidia kufanya mambo yenye kuwa sawa sasa na wakati wenye kuja?

NAMNA YA KUWA NA MAWAZO KAMA YA MUNGU

4. Kufanya upya akili yetu, maana yake nini?

4 Soma Waroma 12:2. Katika andiko hili, mutume Paulo alieleza mambo yenye tunapaswa kufanya ili tukuwe na mawazo kama Yehova. Alisema kama tunapaswa ‘kuacha kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo.’ Kama vile tulijifunza mu habari yenye ilitangulia, hilo linamaanisha kama tunapaswa kuepuka mawazo na tabia za ulimwengu. Lakini Paulo alisema pia kama tunapaswa kufanya upya akili yetu. Maana yake, tunapaswa kujifunza Neno la Mungu, kuelewa mawazo yake, kufikiri sana juu ya mawazo hayo, na kujikaza sana ili tukuwe na mawazo kama ya Mungu.

5. Kuko tofauti gani kati ya kusoma na kujifunza? Fasiria.

5 Kujifunza haiko kusoma mbiombio habari na kutia mistari kwenye majibu ya maulizo ya funzo. Wakati tunajifunza habari fulani, tunafikiria ikiwa habari hiyo inatufundisha nini juu ya Yehova, njia zake, na mawazo yake. Tunajikaza kuelewa juu ya nini Yehova anatuambia tufanye jambo fulani na tuepuke jambo lingine. Tunafikiria pia mabadiliko yenye tunapaswa kufanya katika maisha yetu na katika mawazo yetu. Kwa kweli, pengine haitawezekana kufikiri sana juu ya mambo hayo yote kila wakati tunajifunza. Lakini, ni muzuri kutumia wakati, pengine nusu ya wakati wa funzo, ili kufikiri sana juu ya mambo yenye tumesoma.​—Zb. 119:97; 1 Ti. 4:15.

6. Ni nini inatokea wakati tunafikiri sana juu ya Neno la Mungu?

6 Jambo fulani la ajabu linatokea wakati tunafikiri sana kwa ukawaida juu ya Neno la Mungu. ‘Tunajihakikishia sisi wenyewe,’ ao tunajisadikisha kama mawazo ya Yehova ni makamilifu. Tunaanza kuelewa namna anaona mambo, na mwishowe tunakubaliana na mawazo yake. Kwa hiyo, tunafanya upya akili yetu na kuanza kuwaza katika njia ya mupya. Pole kwa pole, tunakuwa na mawazo kama ya Yehova.

MAWAZO YETU YAKO NA MATOKEO JUU YA MATENDO YETU

7, 8. (a) Namna gani Yehova anaona vitu vya kimwili? (Ona picha ku mwanzo wa habari hii.) (b) Kama tunaona vitu vya kimwili namna Yehova anaviona, ni jambo gani lenye tutaona kuwa la maana zaidi sikuzote?

7 Mawazo yetu yako na matokeo juu ya matendo yetu. (Mk. 7:21-23; Yak. 2:17) Tuone basi mifano fulani ya kutusaidia kuelewa jambo hilo. Mufano moja wenye kupatikana katika habari yenye kuzungumuzia kuzaliwa kwa Yesu, unaonyesha waziwazi mawazo ya Yehova juu ya vitu vya kimwili. Mungu mwenyewe alichagua Yosefu na Maria ili wakomalishe Mwana wake hata kama hawakukuwa na feza za mingi. (Law. 12:8; Lu. 2:24) Wakati Yesu alizaliwa, Maria ‘alimulalisha katika chombo cha kulishia wanyama, kwa sababu hawakupata nafasi katika vyumba vya wageni.’ (Lu. 2:7) Ikiwa Yehova angependa, angehakikisha kama Yesu anazaliwa nafasi ya muzuri zaidi. Lakini alipenda Yesu akomalie mu familia yenye kutia ibada ya Mungu pa nafasi ya kwanza. Hilo ndilo jambo lenye Yehova aliona kuwa la maana zaidi.

8 Habari hiyo juu ya kuzaliwa kwa Yesu inatufundisha namna Yehova anaona vitu vya kimwili. Wazazi fulani wanapenda watoto wao wakuwe na vitu vya muzuri sana vya kimwili, hata kama hilo linaharibu urafiki wa watoto wao pamoja na Yehova. Lakini kwa kweli, Yehova anaona kuwa urafiki wetu pamoja naye ndilo jambo la maana zaidi. Uko na mawazo kama ya Yehova juu ya jambo hilo? Matendo yako yanaonyesha nini?​—Soma Waebrania 13:5.

9, 10. Namna gani tunaonyesha kama tunaona kukwaza wengine namna Yehova anaona jambo hilo?

9 Mufano mwingine unaonyesha namna Yehova anaona mutu mwenye kukwaza wengine, ni kusema, kufanya wengine watende zambi ao waache kumutumikia Yehova. Yesu alisema hivi: “Kila mutu mwenye anamukwaza mumoja wa hawa wadogo wenye kuwa na imani, ingekuwa muzuri zaidi kwake ikiwa jiwe la kusagia lenye linazungushwa na punda lingewekwa kwenye shingo yake na atupwe katika bahari.” (Mk. 9:42) Hayo ni maneno mazito sana! Na tunajua kama Yesu anaiga sifa za Baba yake. Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama Yehova anachukia sana wakati mutu fulani anakwaza mumoja kati ya wanafunzi wa Yesu.​—Yoh. 14:9.

10 Tunaona kukwaza wengine kama vile Yehova na Yesu wanaona jambo hilo? Matendo yetu yanaonyesha nini? Kwa mufano, pengine tunapenda aina fulani ya kuvaa na kujipamba. Lakini tutafanya nini ikiwa tunajua kama aina hiyo inakwaza watu fulani katika kutaniko ao kufanya wengine wakuwe na mawazo machafu? Upendo wetu kwa ndugu na dada zetu utatuchochea tuachane na mambo yenye tunapenda?​—1 Ti. 2:9, 10.

11, 12. Kama tunajifunza kuchukia mambo yenye Yehova anachukia na kuonyesha sifa ya kujizuia, hilo linatulinda namna gani?

11 Mufano wa tatu ni huu: Yehova anachukia ukosefu wa haki. (Isa. 61:8) Kwa kweli, anajua kama wakati fulani ni vigumu kwetu kufanya mambo yenye kuwa sawa, kwa sababu hatukamilike. Lakini, anapenda tuchukie mambo ya mubaya kama vile anayachukia. (Soma Zaburi 97:10.) Kama tunafikiri sana juu ya sababu zenye kufanya Yehova achukie mambo ya mubaya, hilo litatusaidia kuwa na mawazo kama yake na litatupatia nguvu ya kuepuka kufanya mambo ya mubaya.

12 Kama tunajifunza kuchukia mambo ya mubaya, hilo litatusaidia pia kutambua kama mambo fulani ni ya mubaya, hata kama Biblia haizungumuzie waziwazi mambo hayo. Kwa mufano, aina moja ya mwenendo muchafu wenye unaendelea kuenea sana leo ni dansi kwenye mapaja. Watu fulani wanawaza kama dansi hiyo haiko sawa na kufanya uasherati na mutu fulani, kwa hiyo wanawaza kama dansi hiyo haiko mubaya. * (Ona maelezo ya chini.) Lakini ni vile kabisa Yehova anaona dansi hiyo? Kumbuka kama Yehova anachukia aina yote ya ubaya. Kwa hiyo, tuepuke kabisa jambo lolote lenye kuwa la mubaya kwa kujikaza kuonyesha sifa ya kujizuia na kwa kuchukia mambo yenye Yehova anachukia.​—Ro. 12:9.

WAZA SASA JUU YA MAMBO YENYE UTAFANYA WAKATI WENYE KUJA

13. Juu ya nini tunapaswa kufikiri sasa juu ya namna Yehova anaona mambo ili tukamate maamuzi yenye hekima wakati wenye kuja?

13 Wakati tunajifunza, tunapaswa kuwaza juu ya namna Yehova anaona mambo mbalimbali kwa sababu hilo linaweza kutusaidia kukamata maamuzi yenye hekima. Kisha, kama siku moja tunajikuta mu hali yenye kuomba tukamate maamuzi ya haraka, hatutashangaa kabisa. (Mez. 22:3) Tuzungumuzie basi mifano fulani yenye kuwa mu Biblia.

14. Jibu lenye Yosefu alimupatia bibi ya Potifa linatufundisha nini?

14 Wakati bibi ya Potifa alijaribu kumutongoza Yosefu, Yosefu alikataa mara moja. Ni wazi kama Yosefu alikuwa amefikiri sana juu ya namna Yehova anaona ndoa. (Soma Mwanzo 39:8, 9.) Yosefu alimuambia bibi ya Potifa hivi: “Ninaweza namna gani kufanya ubaya huu mukubwa na kwa kweli nimutendee Mungu zambi?” Hilo linaonyesha kama alikuwa amejikaza kuwa na mawazo kama ya Yehova. Halafu sisi? Utafanya nini kama mufanyakazi mwenzako anaanza kukuchezea kimapenzi? Utafanya nini kama mutu fulani anakutumia kwenye telefone ujumbe ao picha yenye kuonyesha mambo ya ngono? * (Ona maelezo ya chini.) Ni mwepesi zaidi kubakia washikamanifu kwa Yehova kama tayari tumejifunza na kukubali mawazo yake juu ya mambo hayo na tumeamua tayari jambo lenye tutafanya.

15. Tunaweza kufanya nini ili tubakie waaminifu kwa Yehova, kama vile wale Waebrania tatu walifanya?

15 Fikiria pia mufano wa Waebrania tatu, ni kusema, Shadraki, Meshaki, na Abednego. Wakati Mufalme Nebukadneza aliwaamuru waabudu sanamu ya zahabu yenye alikuwa ametengeneza, walikataa kabisa. Jibu la wazi lenye walijibu mufalme lilionyesha kama walikuwa wamefikiria tayari jambo lenye lingetokea ikiwa wangebakia washikamanifu kwa Yehova. (Kut. 20:4, 5; Da. 3:4-6, 12, 16-18) Halafu leo? Utafanya nini kama mukubwa wako wa kazi anakuomba ufanye muchango wa feza kwa ajili ya sikukuu fulani yenye kuwa na upatano na dini za uongo? Kuliko kungojea jambo kama hilo litokee, itakuwa muzuri kufikiri sasa juu ya namna Yehova anaona mambo hayo. Kisha, kama siku moja tunajikuta mu hali kama hiyo, itakuwa mwepesi kwetu kufanya na kusema jambo lenye kufaa, kama vile wale Waebrania tatu walifanya.

Umetafuta habari, umejaza kikaratasi cha matunzo chenye kukubaliwa na sheria, na umezungumuza na munganga wako? (Picha hizi zinapatana na fungu la 16)

16. Namna gani kuelewa muzuri mawazo ya Yehova kunatusaidia kujitayarisha kwa ajili ya matunzo ya haraka?

16 Kufikiri sana juu ya mawazo ya Yehova kunaweza pia kutusaidia tubakie washikamanifu kwake ikiwa tuko mu hali yenye kuomba matunzo ya haraka. Kwa kweli, tunaazimia kukataa kutiwa damu mu mishipa ao kutumia moja kati ya sehemu zake ine kubwa. (Mdo. 15:28, 29) Lakini kuko aina fulani za matunzo zenye kuhusisha damu zenye kuomba kila Mukristo afanye uamuzi wa kipekee wenye kutegemea kanuni za Biblia. Ni wakati gani wenye kufaa wa kuamua jambo la kufanya? Ni wakati tuko mu hospitali, na pengine tuko na maumivu na tunakazwa kukamata uamuzi wa haraka? Hapana kabisa. Sasa njo wakati wa kutafuta habari, na kujaza kikaratasi cha matunzo chenye kukubaliwa na sheria kama vile karte DPA ili kufasiria matunzo yenye tunapenda, na kuzungumuza na munganga wetu. * (Ona maelezo ya chini.)

17-19. Juu ya nini ni jambo la maana kujua sasa mawazo ya Yehova juu ya mambo mbalimbali? Leta mufano.

17 Mwishowe, fikiria jibu lenye Yesu alimupatia Petro palepale wakati alimutolea shauri hili lenye haliko la hekima: “Jitendee kwa fazili, Bwana.” Yesu alikuwa amefikiri sana juu ya mambo yenye Mungu alipenda afanye na juu ya unabii wenye kuhusu maisha yake na kifo chake mu dunia. Ujuzi huo ulimupatia nguvu ya kubakia muaminifu kwa Yehova na kutoa uzima wake kuwa zabihu kwa ajili yetu sisi wote.​—Soma Matayo 16:21-23.

18 Leo, Mungu anapenda tukuwe marafiki wake na kufanya nguvu yetu yote ili kuhubiri habari njema. (Mt. 6:33; 28:19, 20; Yak. 4:8) Lakini watu fulani wenye hawana nia ya mubaya wanaweza kujaribu kutuvunja moyo, kama vile Petro alijaribu kumuvunja Yesu moyo. Kwa mufano, mukubwa wako wa kazi anaweza kukuambia kama atakupatia feza nyingi zaidi lakini unajua kama utalazimika kutumika saa nyingi zaidi na hautakuwa na wakati wa kutosha wa kuenda kwenye mikutano na kuhubiri pamoja na kutaniko. Ao kama uko mwanafunzi, wazia walimu wako wanakupatia nafasi ya kuhama kutoka kwenu ili uendeleshe masomo nafasi ingine. Kama jambo hilo linatokea, je, utasali, utatafuta habari, na kuzungumuza na watu wa familia yako ao wazee wa kutaniko mbele ya kukamata uamuzi fulani? Itakuwa muzuri zaidi kama unajifunza sasa namna Yehova anaona mambo hayo na kuwa na mawazo kama yake. Kisha, ikiwa siku fulani unapewa mambo hayo, unaweza kuona kama haiko kishawishi kabisa. Unajua kabisa mambo ya kufanya kwa sababu tayari umeamua kukaza akili yako juu ya kumutumikia Yehova.

19 Pengine unaweza kufikiria hali zingine zenye zinaweza kujaribu ushikamanifu wako kwa Yehova mu njia zenye hazitazamiwe. Kwa kweli, hatuwezi kujitayarisha kwa ajili ya kila hali yenye inaweza kutokea. Lakini, kama tunafikiri sana juu ya mawazo ya Yehova wakati wa funzo letu la pekee, tutaweza kabisa kukumbuka mambo yenye tumejifunza na kujua namna ya kuyatumia katika hali yoyote. Kwa hiyo, wakati tunajifunza, tujikaze basi kuelewa mawazo ya Yehova juu ya mambo mbalimbali, tukuwe na mawazo kama yake, na tufikirie namna kuwa na mawazo kama ya Mungu kutatusaidia kukamata maamuzi yenye hekima sasa na wakati wenye kuja.

MAWAZO YA YEHOVA NA WAKATI WAKO WENYE KUJA

20, 21. (a) Juu ya nini tutafurahia uhuru wetu mu ulimwengu mupya? (b) Tunaweza kufanya nini ili tukuwe na furaha mu maisha sasa?

20 Sisi wote tunangojea kwa hamu ulimwengu mupya. Wengi kati yetu wako na tumaini la kuishi milele mu dunia Paradiso. Wakati Ufalme wa Mungu utatutawala, tutakuwa huru kutokana na maumivu na mateso yote yenye tunapambana nayo katika ulimwengu huu. Na kwa kweli, tutaendelea kuwa na uhuru wa kukamata maamuzi kulingana na mambo yenye tunapenda na kulingana na tamaa zetu.

21 Lakini haiko kusema kama uhuru wetu hautakuwa na mipaka. Wapole wataendelea kukamata maamuzi kwa kutegemea sheria za Yehova na mawazo yake. Na hilo litaleta furaha nyingi na amani kabisa. (Zb. 37:11) Mbele wakati huo ufike, tunaweza kuwa na furaha mu maisha sasa wakati tunajikaza kuwa na mawazo kama ya Yehova.

^ fu. 12 Dansi kwenye mapaja, ao sehemu za miguu zenye kuwa juu ya magoti, ni dansi yenye muchezaji mwenye anaweza kuwa nusu uchi anajitikisa-tikisa kwa njia chafu akiwa mwenye kukaa juu ya mapaja ya mutu mwenye atamulipa feza. Kulingana na hali, jambo hilo linaweza kuonwa kuwa uasherati na kuomba wazee waunde halmashauri ya hukumu. Mukristo mwenye amekwisha kushiriki katika jambo hilo anapaswa kuomba musaada kwa wazee wa kutaniko.​—Yak. 5:14, 15.

^ fu. 14 Watu fulani wanatumia wengine kwenye telefone ujumbe, picha, ao video zenye kuonyesha mambo ya ngono. Kulingana na hali, inaweza kuomba wazee waunde halmashauri ya hukumu. Katika hali fulani, wakubwa wa serikali wamewahukumu vijana kuwa wenye makosa ya kingono, kwa sababu ya kutumia wengine mambo ya ngono. Ili kupata habari zaidi, fungua site yetu ya Enternete jw.org na usome habari yenye kichwa “Vijana Wanauliza​—Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Kutuma Ujumbe Mchafu?” (Fungua habari yenye kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > MATINEJA.) Ao usome habari yenye kichwa “Namna ya Kuzungumuza na Kijana Wako Kuhusu Tabia ya Kutuma Mambo ya Ngono Kupitia Telefone” mu Amuka! ya Mwezi wa 11, 2013, ukurasa wa 4-5.

^ fu. 16 Ili kupata habari zaidi juu ya kanuni za Biblia zenye zinaweza kukusaidia, ona kwa mufano, kitabu Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu, ukurasa 246-249.