Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Nani Anafinyanga Mawazo Yako?

Ni Nani Anafinyanga Mawazo Yako?

“Muache kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo.”​—RO. 12:2.

NYIMBO: 88, 45

1, 2. (a) Namna gani Yesu alijibu wakati Petro alimuambia ajitendee kwa fazili? (Ona picha ku mwanzo wa habari hii.) (b) Juu ya nini Yesu alijibu vile?

WANAFUNZI wa Yesu walivunjika moyo kwa sababu walikuwa wanawaza kama Yesu angerudishia Israeli ufalme, lakini Yesu alisema kama alikuwa karibu kuteseka na kufa. Kwa hiyo, mutume Petro alimuambia hivi: “Jitendee kwa fazili, Bwana; mambo hayo hayatakupata hata kidogo.” Yesu alimujibu hivi: “Pita nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa sababu unawaza mawazo ya wanadamu, lakini haiko mawazo ya Mungu.”​—Mt. 16:21-23; Mdo. 1:6.

2 Wakati alisema vile, Yesu alionyesha wazi kama mawazo ya Yehova iko tofauti na mawazo ya ulimwengu huu wenye kutawaliwa na Shetani. (1 Yo. 5:19) Petro alimuchochea Yesu akuwe na roho ya kujipenda mwenyewe yenye watu wengi wako nayo mu ulimwengu. Lakini Yesu alijua kama Yehova alipenda ajitayarishe kwa ajili ya mateso na kifo chenye kilikaribia kumupata. Jibu la Yesu lilionyesha wazi kama alikubali kabisa mawazo ya Yehova na alikataa kabisa mawazo ya ulimwengu.

3. Juu ya nini ni vigumu kukubali mawazo ya Yehova na kukataa mawazo ya ulimwengu?

3 Halafu sisi? Tunawaza kama Yehova ao tunawaza kama watu wa ulimwengu? Kwa sababu sisi ni Wakristo, tunajikaza sana ili kuhakikisha kama tunamupendeza Mungu. Lakini tuseme nini juu ya namna yetu ya kuwaza? Tunajikaza sana ili kuwa na mawazo kama ya Yehova, ni kusema, kuona mambo namna Yehova anayaona? Inaomba kujikaza sana ili kufanya vile. Lakini, ni mwepesi sana kuwa na mawazo kama ya watu wa ulimwengu. Hiyo ni kwa sababu roho ya ulimwengu inaenea kila mahali. (Efe. 2:2) Pia, mara nyingi watu wa ulimwengu wanajifikiria wenyewe, na tunaweza kushawishiwa kuwaza kama wao. Kwa kweli, ni vigumu kuwa na mawazo kama ya Yehova lakini ni mwepesi sana kuwa na mawazo kama ya watu wa ulimwengu.

4. (a) Ni nini itatufikia kama tunaacha ulimwengu uchochee mawazo yetu? (b) Tutajifunza nini mu habari hii?

4 Kama tunaacha ulimwengu uchochee mawazo yetu, tutakuwa na muelekeo wa kujipenda wenyewe na tutapenda kujiamulia mambo yenye kuwa ya muzuri na yenye kuwa ya mubaya. (Mk. 7:21, 22) Kwa hiyo, ni jambo la maana sana tujifunze kuwa na “mawazo ya Mungu,” hapana “mawazo ya wanadamu.” Habari hii itatusaidia kufanya vile. Tutazungumuzia juu ya nini kuona mambo namna Yehova anayaona hakutuime kabisa uhuru, lakini kunatuletea faida. Tutazungumuzia pia namna tunaweza kuepuka kufinyangwa, ao kuchochewa na mawazo ya ulimwengu huu. Mu habari yenye kufuata, tutajifunza namna tunaweza kujua mawazo ya Yehova juu ya mambo mbalimbali na kujikaza kuwa na mawazo kama yake.

MAWAZO YA YEHOVA YANATULETEA FAIDA

5. Juu ya nini watu fulani hawapendi mutu yeyote achochee mawazo yao?

5 Watu fulani hawapendi mutu yeyote achochee namna yao ya kuwaza. Wanasema hivi: “Hakuna mutu mwenye anapaswa kuwaza pa nafasi yangu.” Inawezekana wanamaanisha kama wanapenda kukamata maamuzi yao wao wenyewe na kama wako na haki ya kufanya vile. Hawapendi wengine wawachochee ao kuwakaza wakuwe tu kama watu wengine. * (Ona maelezo ya chini.)

6. (a) Yehova anatupatia uhuru gani? (b) Je, uhuru huo uko na mipaka?

6 Ni muzuri kujua kama, ikiwa tunakubali mawazo ya Yehova, tunaweza kuendelea kuwa na mawazo yetu juu ya mambo fulani. Andiko la 2 Wakorinto 3:17 linasema hivi: “Mahali kwenye kuko roho ya Yehova, kuko uhuru.” Yehova anatupatia uhuru wa kuchagua ikiwa tunapenda kuwa watu wa namna gani. Tunaweza kuwa na mambo yenye tunapendelea na kuchagua mambo yenye tunafurahia. Ni vile Yehova alituumba. Lakini hilo halimaanishe kama tuko na uhuru wenye hauna mipaka. (Soma 1 Petro 2:16.) Wakati tunapenda kujua ikiwa jambo fulani ni la muzuri ao la mubaya, Yehova anapenda tutumie Neno lake ili lituongoze. Kufanya vile kunatuima kabisa uhuru, ao kunatuletea faida?

7, 8. Kuona mambo namna Yehova anapenda tuyaone kunatuima kabisa uhuru? Leta mufano.

7 Ili kuelewa jambo hilo, tufikirie mufano huu. Wazazi wanajikaza kufundisha watoto wao kanuni za muzuri. Wanaweza kuwafundisha wakuwe wenye kuaminika, wafanye kazi kwa bidii, na wahangaikie watu wengine. Kanuni hizo haziwaime kabisa uhuru. Lakini wazazi wanatayarisha watoto wao ili wakuwe na maisha ya muzuri. Wakati watoto watakomaa na kuondoka nyumbani, watakuwa na uhuru wa kukamata maamuzi yao wenyewe. Kama wanachagua kuishi kulingana na kanuni za muzuri zenye wazazi wao waliwafundisha, inawezekana kabisa kuwa watakamata maamuzi ya muzuri na wataepuka magumu na mahangaiko mengi, na hawatahuzunika juu ya maamuzi yenye walikamata.

8 Kama vile muzazi muzuri, Yehova anataka watoto wake wakuwe na maisha ya muzuri zaidi. (Isa. 48:17, 18) Kwa hiyo, anatufundisha kanuni za musingi juu ya mwenendo muzuri na juu ya namna tunapaswa kutendea wengine. Anatuomba tujifunze kuona mambo namna anayaona na kuishi kulingana na kanuni zake. Kufanya vile haiko kutuima kabisa uhuru. Lakini, kunatufanya tukuwe wenye hekima zaidi na kunatusaidia kukamata maamuzi ya muzuri. (Zb. 92:5; Mez. 2:1-5; Isa. 55:9) Tunaweza kuendelea kuwa na mambo yenye tunapendelea, lakini tutakamata maamuzi yenye yatatufanya tukuwe na furaha. (Zb. 1:2, 3) Wakati tuko na mawazo ya Yehova, tunapata faida katika njia za mingi!

MAWAZO YA YEHOVA NI YA JUU SANA

9, 10. Ni nini inaonyesha kama mawazo ya Yehova ni ya juu sana kupita mawazo ya ulimwengu?

9 Sababu ingine yenye kutuchochea tukuwe na mawazo ya Yehova ni hii: mawazo yake ni ya juu zaidi kupita mawazo ya ulimwengu. Ulimwengu unatoa mashauri juu ya mwenendo muzuri, namna ya kuwa na familia yenye furaha, na namna ya kupata matokeo ya muzuri mu kazi yetu na mu mambo mengine ya maisha. Lakini, mashauri mengi kati ya mashauri hayo, yanapingana na mawazo ya Yehova. Kwa mufano, mara nyingi ulimwengu unachochea watu watafute tu faida zao wenyewe na waone mambo ya uasherati kuwa yenye kukubalika. Na wakati fulani ulimwengu unaonyesha kama, bibi na bwana watakuwa na furaha ikiwa wanatengana ao kuvunja ndoa kwa sababu ya mambo madogo-madogo. Mashauri hayo hayapatane na mambo yenye Biblia inafundisha. Lakini, je, mashauri ya ulimwengu yanafaa zaidi wakati wetu kuliko mashauri ya Biblia?

10 Yesu alisema hivi: “Hekima inaonekana kuwa yenye haki kupitia kazi zake.” (Mt. 11:19) Hata kama ulimwengu umefanya maendeleo mengi katika mambo ya teknolojia, haujaweza kumaliza matatizo makubwa yenye yanafanya watu wasikuwe na furaha; matatizo kama vile vita, ubaguzi wa rangi ya ngozi, na matendo ya kuvunja sheria. Zaidi ya hilo, ulimwengu unaona mambo ya uasherati kuwa yenye kukubalika. Lakini watu wengi wanakubali kama hilo linavunja familia nyingi, linaleta matatizo ya afya, na liko na matokeo mengine ya mubaya. Lakini, mashauri ya Yehova yanaleta matokeo gani? Wakristo wenye wamekubali mawazo ya Yehova wako na familia zenye furaha, wako na afya ya muzuri, na wako na amani pamoja na ndugu na dada zao mu dunia yote. (Isa. 2:4; Mdo. 10:34, 35; 1 Ko. 6:9-11) Hilo linaonyesha waziwazi kama mawazo ya Yehova ni ya juu sana kuliko mawazo ya ulimwengu.

11. Ni nani alifinyanga mawazo ya Musa, na hilo lilileta matokeo gani?

11 Watumishi waaminifu wa zamani wa Yehova walijua kama mawazo ya Yehova ni ya juu sana. Kwa mufano, hata kama Musa alifundishwa “hekima yote ya Wamisri,” alijua kama hekima ya kweli inatoka kwa Yehova. (Mdo. 7:22; Zb. 90:12) Kwa hiyo, alimuomba Yehova hivi: “Nijulishe njia zako.” (Kut. 33:13) Kwa sababu Musa alimuacha Yehova afinyange mawazo yake, Yehova alimutumia kwa njia ya ajabu ili kutimiza kusudi lake na alimupatia Musa heshima kwa kumuita mwanaume mwenye imani kubwa.​—Ebr. 11:24-27.

12. Maamuzi ya Paulo yalitegemea nini?

12 Mutume Paulo alikuwa mwanaume mwenye akili, mwenye kusoma sana, na alijua kuzungumuza Kigiriki na Kiebrania. (Mdo. 5:34; 21:37, 39; 22:2, 3) Lakini, aliepuka hekima ya ulimwengu na alikamata maamuzi yenye yalitegemea Neno la Mungu. (Soma Matendo 17:2; 1 Wakorinto 2:6, 7, 13.) Kwa hiyo, utumishi wake ulikuwa na matokeo ya muzuri sana, na alingojea kwa hamu kupata zawabu ao baraka ya milele.​—2 Ti. 4:8.

13. Ni nani iko na daraka la kubadilisha mawazo yetu ili tuone mambo namna Yehova anayaona?

13 Kwa kweli, mawazo ya Mungu ni ya juu zaidi kupita mawazo ya ulimwengu. Kama tunafuata kanuni za Mungu, tutakuwa wenye furaha kabisa na tutapata matokeo ya muzuri. Lakini Yehova hatatukaza tukuwe na mawazo kama yake. “Mutumwa muaminifu na mwenye busara,” wala wazee hawawezi kufanya vile pia. (Mt. 24:45; 2 Ko. 1:24) Kila mumoja wetu iko na daraka la kubadilisha mawazo yake mwenyewe ili aone mambo namna Yehova anayaona. Namna gani tunaweza kufanya vile?

EPUKA KUFINYANGWA NA ULIMWENGU HUU

14, 15. (a) Ili tukuwe na mawazo kama ya Yehova, tunapaswa kufikiri sana juu ya jambo gani? (b) Juu ya nini hatupaswe kuacha mawazo ya ulimwengu yaingie katika akili yetu? Leta mufano.

14 Andiko la Waroma 12:2 linasema hivi: “Muache kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo, lakini mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mujihakikishie ninyi wenyewe mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.” Andiko hilo linatufundisha kuwa hata kama mawazo yetu yalifinyangwa ao kuchochewa na jambo gani mbele tujifunze kweli, tunaweza kubadilisha mawazo yetu ili yafanane zaidi na mawazo ya Mungu. Hata kama mambo yenye tuliriti wakati tulizaliwa na mambo yenye tulikutana nayo mu maisha yanaweza kuchochea mawazo yetu kwa kadiri fulani, akili yetu inaweza kuendelea kubadilika. Na ili akili yetu ibadilike, hilo linategemea sana mambo yenye tunachagua kufikiria. Kama tunafikiri sana juu ya mawazo ya Yehova, tutajihakikishia wenyewe kama mawazo yake ni sawa sikuzote. Kisha, tutakuwa tayari kuona mambo namna anayaona.

15 Lakini, ili kufanya upya akili yetu kusudi tukuwe na mawazo kama ya Yehova, tunapaswa ‘kuacha kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo.’ Maana yake, tunapaswa kuacha kusoma, kuangalia na kusikiliza jambo lolote lenye kupingana na mawazo ya Mungu. Ili kuelewa kama ni jambo la maana sana kufanya vile, wazia mufano wa chakula. Mutu mwenye anapenda akuwe na afya ya muzuri anaweza kuamua kula chakula cha muzuri. Lakini bidii yake itakuwa ya bure kama anazoea kula pia chakula chenye kuoza! Vilevile, bidii yetu ya kujifunza juu ya mawazo ya Yehova itakuwa ya bure kama tunaacha mawazo ya ulimwengu yaingie katika akili yetu.

16. Tunaweza kujilinda juu ya mambo gani?

16 Tunaweza kuepuka kabisa mawazo ya ulimwengu? Hapana, hatuwezi kuepuka mawazo fulani ya ulimwengu kwa sababu hatuwezi kutoka mu ulimwengu moja kwa moja. (1 Ko. 5:9, 10) Hata wakati tuko tunahubiri, tutasikia watu wanasema mawazo ya mubaya na mafundisho ya uongo. Lakini hata kama hatuwezi kuepuka kabisa mawazo ya mubaya, hatupaswe kuendelea kuwaza juu ya mawazo hayo ao kuyakubali. Kama Yesu, tunapaswa kutenda haraka ili kuepuka mawazo yenye Shetani anaweza kupenda tukuwe nayo. Na tunaweza kujilinda kwa kuepuka kujitia katika hatari ya kuambukizwa na mawazo ya ulimwengu.​—Soma Mezali 4:23.

17. Tunaweza kufanya nini ili tuepuke kujitia katika hatari ya kuambukizwa na mawazo ya ulimwengu?

17 Kwa mufano, tunapaswa kuchagua marafiki wetu kwa hekima. Biblia inatuonya kama ikiwa tunakuwa marafiki wa sana wa watu wenye hawamuabudu Yehova, tutaanza kuwaza kama watu hao. (Mez. 13:20; 1 Ko. 15:12, 32, 33) Tunapaswa pia kuchagua kwa hekima mambo ya kujifurahisha. Wakati tunaepuka mambo ya kujifurahisha yenye kuchochea fundisho la mageuzi, jeuri, na mwenendo mubaya, tunaepuka kuchafua akili yetu kupitia mawazo yenye “kupinga ujuzi wa Mungu.”​—2 Ko. 10:5.

Tunasaidia watoto wetu ili waepuke mambo ya mubaya ya kujifurahisha? (Picha hii inapatana na fungu la 18, 19)

18, 19. (a) Juu ya nini tunapaswa kuwa waangalifu ili kuepuka mawazo ya ulimwengu yenye kuchochewa katika njia zenye hazionekane waziwazi? (b) Tunapaswa kujiuliza maulizo gani, na juu ya nini?

18 Tunapaswa pia kutambua na kuepuka mawazo ya ulimwengu yenye kuchochewa katika njia zenye hazionekane waziwazi. Kwa mufano, vyombo fulani vya kutangaza habari vinatoa habari kwa njia yenye kuunga mukono mawazo fulani ya politike. Na habari fulani zenye kutolewa kwenye vyombo hivyo zinachochea miradi na mambo yenye kutimizwa na watu yenye ulimwengu unafurahia. Filme na vitabu fulani vinachochea mawazo ya “mimi kwanza” na “familia yangu kwanza” na vinafanya mawazo hayo yaonekane kuwa yenye kufaa, yenye kuvutia, na hata ya muzuri. Lakini, mawazo hayo yanapingana na Biblia. Biblia inasema kama sisi na familia yetu tutakuwa na furaha kabisa ikiwa tunamupenda Yehova kupita mambo yote. (Mt. 22:36-39) Pia, habari fulani za watoto, hata kama zinaweza kukubaliwa na watu wengi, zinaweza kufanya watoto wakubali mwenendo mubaya bila wao kujua.

19 Lakini, haiko kusema kama ni mubaya kujifurahisha kwa njia yenye kufaa. Lakini tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Ninatambua mawazo ya ulimwengu hata wakati yanaonyeshwa katika njia yenye haionekane waziwazi? Ninajilinda mimi mwenyewe na watoto wangu kwa kuepuka programu fulani za televizyo ao kusoma vitabu fulani? Ninasaidia watoto wangu wakuwe na mawazo ya Yehova juu ya mambo mbalimbali ili wasichochewe na mawazo ya ulimwengu yenye wanasikia na kuona?’ Ikiwa tunatambua tofauti kati ya mawazo ya Mungu na mawazo ya ulimwengu, tunaweza kuepuka “kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo.”

NI NANI ANAKUFINYANGA SASA?

20. Ni nini itaonyesha kama tunachochewa na mawazo ya Mungu ao mawazo ya ulimwengu?

20 Tunapaswa kukumbuka kama kuko nafasi mbili tu za kupata habari. Tunapata habari kutoka kwa Yehova ao kutoka kwa Shetani na ulimwengu wake. Ni nani mwenye anakufinyanga? Ni ule mwenye anakutolea habari. Kama tunakubali mawazo ya ulimwengu, ulimwengu utafinyanga mawazo yetu na tutawaza na kutenda kwa kujifikiria wenyewe. Kwa hiyo, ni jambo la maana tuchague kwa uangalifu mambo yenye tunaangalia, tunasoma, tunasikiliza na mambo yenye tunafikiria.

21. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

21 Mu habari hii tumejifunza kama ili tukuwe na mawazo kama ya Yehova, tunapaswa kuepuka mawazo ya ulimwengu. Tunapaswa pia kufikiri sana juu ya mawazo ya Mungu ili tukuwe zaidi na mawazo kama yake. Mu habari yenye kufuata, tutajifunza namna tunaweza kufanya vile.

^ fu. 5 Ukweli ni kwamba, hata watu wenye kujitegemea sana wanachochewa na wengine. Kwa mufano, ikuwe tunawaza juu ya namna maisha yalianza, ao tunachagua tu manguo yenye tutavaa, watu wengine wanatuchochea kwa kadiri fulani. Lakini tunaweza kuchagua ni nani tunapenda achochee mawazo yetu.