Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Ununue Kweli na Usiiuzishe Hata Kidogo”

“Ununue Kweli na Usiiuzishe Hata Kidogo”

“Ununue kweli na usiiuzishe hata kidogo, pia hekima na nizamu na uelewaji.”​—MEZ. 23:23.

NYIMBO: 94, 96

1, 2. (a) Ni jambo gani lenye kuwa la maana zaidi mu maisha yako? (b) Ni kweli gani zenye tunaona kuwa za maana sana, na juu ya nini? (Ona picha ku mwanzo wa habari hii.)

NI JAMBO gani lenye kuwa la maana zaidi mu maisha yako? Sisi watu wa Yehova, jambo la maana zaidi lenye tuko nalo ni urafiki wetu pamoja naye. Hatuwezi kubadilisha hata kidogo urafiki huo na kitu kingine chochote. Tunaona pia kweli yenye kutoka mu Biblia kuwa ya maana, kwa sababu inatusaidia kuwa marafiki wa Yehova.​—Kol. 1:9, 10.

2 Yehova ni Mufundishaji wetu Mukubwa, mwenye kutufundisha kweli nyingi za maana sana zenye kuwa katika Neno lake, Biblia. Anatufundisha kama jina lake ni la maana sana na anatuambia juu ya sifa zake za muzuri sana. Anatuambia kama anatupenda sana na ndiyo sababu alitoa uzima wa Mwana wake mupendwa kwa ajili yetu. Yehova anatufundisha juu ya Ufalme wa Kimasiya. Anatupatia tumaini la wakati wenye kuja: watiwa-mafuta wataishi mbinguni na “kondoo wengine” wataishi mu dunia Paradiso. (Yoh. 10:16) Yehova anatufundisha namna tunapaswa kuishi. Tunaona kweli hizo kuwa za maana sana kwa sababu zinatusaidia kumukaribia Muumbaji wetu na zinatupatia kusudi mu maisha.

3. Yehova anatuomba tulipe feza ili kujifunza kweli?

3 Yehova ni Mungu mukarimu. Kwa sababu ni mukarimu sana, alimutoa Mwana wake kwa ajili yetu. Wakati Yehova anaona kuwa mutu fulani anatafuta kweli, anasaidia mutu huyo kuipata. Hawezi hata kidogo kutuomba tulipe feza ili kujifunza kweli. Wakati fulani, mwanaume mumoja mwenye kuitwa Simoni alimutolea mutume Petro feza ili apate mamlaka ya kupatia wengine roho takatifu. Petro alionyesha kama mawazo yake yalikuwa ya mubaya. Alisema hivi: “Feza zako ziangamie pamoja na wewe, kwa sababu uliwaza kama unaweza kupata zawadi ya bure ya Mungu kupitia feza.” (Mdo. 8:18-20) Kwa hiyo, ‘kununua [ao, kuuza] kweli,’ maana yake nini?

‘KUNUNUA KWELI,’ MAANA YAKE NINI?

4. Mu habari hii, tutajifunza nini juu ya kweli?

4 Soma Mezali 23:23. Inaomba kujikaza sana ili kujifunza kweli kutoka katika Biblia. Tunapaswa kuachana na mambo mengine kwa ajili ya kweli. Na kisha ‘kununua kweli,’ maana yake kujifunza kweli, tunapaswa kuwa waangalifu ili ‘tusiiuzishe’ hata kidogo, ni kusema, kuiacha. Namna gani ‘tunanunua’ kweli ya Biblia? Iko na bei gani? Majibu ya maulizo hayo yatatusaidia kuona kweli kuwa ya maana zaidi na yatatufanya tuazimie zaidi kuepuka kuacha kweli hiyo. Tutaelewa juu ya nini kweli kutoka kwa Yehova ni ya maana sana kuliko jambo lingine lolote.

5, 6. (a) Namna gani tunaweza kununua kweli bila kulipa feza? Fasiria. (b) Namna gani kweli inatuletea faida?

5 Hata kama kitu fulani ni cha bure, hilo halimaanishe kama haiombe kufanya jambo fulani ili kukipata. Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa ‘kununua’ mu andiko la Mezali 23:23 linaweza pia kumaanisha ‘kujipatia.’ Maneno hayo mbili yanaonyesha kama mutu anajikaza sana ao anaachana na jambo fulani ili kupata kitu fulani chenye anaona kuwa cha maana. Ili kutusaidia kuelewa namna tunaweza kununua kweli, wazia kuwa mu soko fulani wanatolea watu ndizi kwa bure. Tunaweza kungojea ndizi zijifikishe mu nyumba yetu? Hapana, tunapaswa kuenda kwenye soko ili kuzikamata na kuzileta mu nyumba. Kwa hiyo, hata kama haiombe kulipa feza ili kupata ndizi hizo, tunapaswa kufanya jambo fulani ili kuzipata. Vilevile, hatuna lazima ya kulipa feza ili kujifunza kweli, lakini inaomba kujikaza na kujinyima mambo fulani ili kujifunza kweli.

6 Soma Isaya 55:1-3. Maneno yenye Yehova alisema yanatusaidia kuelewa maana ya kununua kweli. Katika andiko hili, Yehova analinganisha maneno yake ya kweli na maji, maziwa, na divai. Kama vile tu maji ya baridi inafanya mutu mwenye kuwa na kiu ajisikie muzuri, kweli inatufanya tujisikie muzuri. Na kama vile tu maziwa inafanya mutoto akuwe na nguvu, kweli ya Biblia inafanya urafiki wetu pamoja na Yehova ukuwe wenye nguvu. Yehova analinganisha pia maneno yake na divai. Juu ya nini? Biblia inasema kama divai inafanya watu wafurahi. (Zb. 104:15) Kwa hiyo, wakati Yehova anatuambia ‘tununue divai,’ anapenda tujue kama wakati tunafuata muongozo wake mu maisha yetu, tutakuwa na furaha. (Zb. 19:8) Yehova anatumia ulinganifu huo ili kutusaidia kuelewa kama tunaweza kupata faida wakati tunajifunza kweli na kuitumia mu maisha yetu. Sasa, tuzungumuzie mambo tano yenye pengine tunapaswa kuachana nayo ili kununua kweli.

UMEACHANA NA MAMBO GANI ILI KUNUNUA KWELI?

7, 8. (a) Juu ya nini inaomba wakati ili kujifunza kweli? (b) Namna gani mwanafunzi mumoja alijitoa sana, na hilo lilileta matokeo gani?

7 Wakati. Inaomba wakati ili mutu asikilize ujumbe wa Ufalme, asome Biblia na vichapo vyenye kutegemea Biblia, ajifunze Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, atayarishe mikutano yetu, na kuenda kwenye mikutano hiyo. Ili kufanya mambo hayo yote, tunapaswa kutumia wakati wenye tulikuwa tunapitisha katika mambo mengine yenye haiko ya maana sana. (Soma Waefeso 5:15, 16 na maelezo ya chini.) Inaomba wakati gani ili kujifunza kweli za musingi za Biblia? Inategemea kila mutu. Hakuna mipaka juu ya mambo yenye tunaweza kujifunza juu ya hekima ya Yehova, njia zake, na mambo yenye amefanya. (Ro. 11:33) Gazeti la kwanza la Munara wa Mulinzi lililinganisha kweli na “ua ndogo” na lilisema hivi: “Usitosheke na ua moja la kweli. Kama ua moja la kweli lingetosha, Mungu hangetoa maua mingi sana ya kweli. Endelea kukusanya, tafuta mengine zaidi.” Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Nimejifunza mambo mengi kabisa juu ya Yehova?’ Hata kama tunaishi milele, sikuzote kutakuwa mambo mengi ya kujifunza juu ya Yehova. Hata hivyo, leo ni jambo la maana tutumie wakati wetu muzuri ili kujifunza mambo mengi zaidi kulingana na hali yetu. Ona mufano wa mutu fulani mwenye alifanya vile.

8 Mariko, * (ona maelezo ya chini) kijana mwanamuke kutoka Japani, alihamia mu inchi ya Amerika ili kusomea mu Muji wa New York. Siku moja, painia mumoja alizungumuza naye juu ya habari njema ya Ufalme kwenye nyumba yake. Mariko alikuwa tayari katika dini fulani, lakini alianza kujifunza Biblia na dada huyo. Kwa sababu alipenda sana mambo yenye alikuwa anajifunza, aliomba akuwe anajifunza mara mbili katika juma. Hata kama Mariko alikuwa na mambo mengi sana ya kufanya kwa sababu ya masomo na kazi, alianza kuenda kwenye mikutano bila kukawia. Alipitisha wakati kidogo katika mambo ya kujifurahisha ili akuwe na wakati mwingi zaidi wa kujifunza kweli. Kwa sababu alijitoa sana vile, Mariko alimukaribia Yehova zaidi na kisha miezi fulani alibatizwa. Na kisha miezi sita, mu mwaka wa 2006, akakuwa painia, na anaendelea kufanya kazi hiyo.

9, 10. (a) Namna gani kujifunza kweli kunabadilisha mawazo yetu juu ya vitu vya kimwili? (b) Kijana mumoja mwanamuke aliachana na jambo gani, na anajisikia namna gani juu ya uamuzi wake?

9 Vitu vya kimwili. Ili tujifunze kweli, tunaweza kulazimika kuacha kazi ya mushahara muzuri katika ulimwengu huu. Kwa mufano, Petro na Andrea walikuwa wanafanya kazi ya kuvua samaki, lakini wakati Yesu aliwaomba wakuwe wanafunzi wake, waliacha kazi yao ya kuvua samaki. (Mt. 4:18-20) Haiko kusema kama wakati unajifunza kweli, unapaswa kuacha kazi yako. Mutu anapaswa kutumika ili aweze kutimizia familia yake mambo ya lazima. (1 Ti. 5:8) Lakini wakati unajifunza kweli, mawazo yako juu ya vitu vya kimwili yanabadilika. Unatambua jambo lenye kuwa la maana kabisa katika maisha. Yesu alisema hivi: “Muache kujiwekea hazina katika dunia.” Lakini, alitutia moyo hivi: “Mujiwekee hazina mbinguni.” (Mt. 6:19, 20) Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Maria alifanya vile.

10 Maria alipenda kucheza golf tangu wakati alikuwa mudogo. Wakati alikuwa kwenye masomo ya segondere aliendelea kuwa muchezaji muzuri zaidi. Alifikia kuwa muchezaji muzuri sana wa golf mupaka akapewa nafasi ya kusoma masomo ya juu kwa bure. Mu maisha yake, Maria alikuwa na muradi wa kuwa muchezaji muzuri sana wa golf na kupata feza nyingi. Kisha akaanza kujifunza Biblia. Maria alipenda mambo yenye alijifunza na akaanza kuyatumia mu maisha yake. Anasema hivi: “Niliendelea kuwa mwenye furaha zaidi wakati niliendelea kufanya mawazo na maisha yangu yapatane na kanuni za Biblia.” Maria alitambua kama ingekuwa vigumu kukaza akili yake juu ya urafiki wake pamoja na Yehova na juu ya muradi wake wa kuwa muchezaji muzuri sana. (Mt. 6:24) Kwa hiyo, aliamua kuachana na muradi wake wa kuwa muchezaji muzuri sana wa golf ili kufanya jambo la maana zaidi. Leo, Maria ni painia na anasema kama iko na “maisha yenye furaha sana na yenye kusudi kabisa.”

11. Wakati tunajifunza kweli, marafiki wetu fulani na watu fulani wa familia wanaweza kutenda namna gani?

11 Uhusiano pamoja na wengine. Wakati tunaanza kutumia mambo yenye tunajifunza kutoka katika Biblia, uhusiano wetu pamoja na marafiki wetu na watu wa jamaa unaweza kubadilika. Yesu alitusaidia kuelewa sababu gani jambo hilo linatokea wakati alisali hivi juu ya wanafunzi wake: “Uwatakase kwa njia ya ile kweli; neno lako ni kweli.” (Yoh. 17:17; maelezo ya chini) ‘Kutakasa’ kunaweza kumaanisha ‘kuweka pembeni.’ Wakati tunaanza kutumia kweli mu maisha yetu, tunawekwa pembeni kutoka katika ulimwengu kwa sababu tunafuata kanuni za Biblia. Hata kama tunajikaza kuendelea kuwa na uhusiano muzuri pamoja na marafiki wetu na watu wa familia, pengine wamoja kati yao hawatatupenda tena namna walikuwa wanatupenda zamani na wanaweza hata kupinga mambo mapya yenye tunaamini. Jambo hilo halitushangaze. Yesu alisema hivi: “Kwa kweli, maadui wa mutu watakuwa watu wa nyumba yake mwenyewe.” (Mt. 10:36) Lakini Yesu aliahidi pia kuwa, hata kama tunaacha mambo gani kwa ajili ya kweli, tutapata mambo mengi zaidi kuliko mambo yenye tumeacha!​—Soma Marko 10:28-30.

12. Mwanaume mumoja Muyahudi aliachana na nini kwa ajili ya kweli?

12 Katika maisha yake yote, mwanaume mumoja Muyahudi mwenye kuitwa Aaron aliamini kama ilikuwa mubaya kutamka jina la Mungu. Lakini alipenda kabisa kujua kweli juu ya Mungu. Siku moja, Shahidi fulani wa Yehova alimuambia kama ikiwa anaongeza herufi za sauti kwenye herufi ine za Kiebrania za jina la Mungu, jina hilo lingeweza kutamkwa “Yehova.” Aaron alifurahi sana kujifunza jambo hilo, kwa hiyo, akaenda kwenye sinagogi ili kuelezea marabi! Aliwaza kama watafurahi kujifunza kweli juu ya jina la Mungu, lakini hawakufurahi. Walimutemea mate na kumufukuza. Watu wa familia ya Aaron nao walimupinga. Lakini hakuruhusu jambo hilo limufanye aache kujifunza mengi zaidi juu ya Yehova. Aaron alifikia kuwa Shahidi wa Yehova na alimutumikia Yehova kwa uaminifu maisha yake yote. Tunaweza pia kutazamia kama uhusiano wetu pamoja na wengine unaweza kubadilika wakati tunajifunza kweli.

13, 14. Wakati tunajifunza kweli, ni mabadiliko gani yenye tunapaswa kufanya katika namna yetu ya kuwaza na kutenda? Leta mufano.

13 Mawazo na matendo machafu. Wakati tunajifunza kweli na kuanza kutumia kanuni za Biblia katika maisha yetu, tunapaswa kuwa tayari kubadilisha namna yetu ya kuwaza na kutenda. Mutume Petro aliandika hivi: “Kama watoto watiifu, muache kufinyangwa na tamaa zenye mulikuwa nazo zamani katika hali yenu ya kukosa kujua.” Kisha aliongeza hivi: “Mukuwe watakatifu katika mwenendo wenu wote.” (1 Pe. 1:14, 15) Katika muji wa zamani wa Korinto, watu wengi walikuwa na mwenendo mubaya. Wale wenye walikubali kweli katika muji huo, walipaswa kufanya mabadiliko makubwa ili Yehova awaone kuwa safi. (1 Ko. 6:9-11) Leo, watu wengi wanafanya mabadiliko kama hayo wakati wanajifunza kweli. Petro alionyesha jambo hilo wakati aliandika hivi: “Wakati wenye ulipita uliwatosha ninyi kufanya mapenzi ya mataifa wakati mulifanya matendo ya mwenendo mupotovu wa bila haya, tamaa kali yenye haiwezi kuzuiwa, kunywa kupita kiasi, karamu za kupitisha mipaka, mashindano ya kunywa, na ibada za sanamu zenye kuchukiza.”​—1 Pe. 4:3.

14 Devynn na Jasmine walikuwa walevi kwa miaka mingi. Hata kama Devynn alijua muzuri kuangalia mambo ya feza, alifukuzwa ku kazi mara kwa mara kwa sababu ya kunywa pombe sana. Jasmine alijulikana kuwa mutu mwenye kasirani na mwenye jeuri. Siku moja wakati alikuwa amelewa, alikutana na wamisionere wawili Mashahidi mu barabara. Walimuomba ajifunze Biblia. Lakini wakati walienda kuwatembelea kwenye nyumba yao juma lenye lilifuata, Jasmine na Devynn walikuwa wamelewa. Hawakuamini kama wamisionere hao wangewahangaikia kabisa na kuja kuwatembelea kwenye nyumba yao. Wakati wamisionere hao walikuja tena, hali ilikuwa tofauti. Jasmine na Devynn walikuwa wanangojea kwa hamu kujifunza kweli ya Biblia, na bila kukawia walianza kutumia mambo yenye walijifunza. Katika kipindi cha karibu miezi tatu, waliacha kunywa pombe, na kisha wakati fulani, wakaandikisha ndoa yao kwenye serikali. Watu wengi katika kijiji chao waliona namna Jasmine na Devynn walikuwa wamebadilika, na wao pia wakaanza kujifunza Biblia.

15. Ni badiliko gani moja lenye kuwa kati ya mabadiliko ya nguvu sana yenye tunapaswa kufanya kwa ajili ya kweli, na juu ya nini?

15 Desturi na mazoea yenye hayamupendeze Yehova. Badiliko moja kati ya mabadiliko yenye kuwa nguvu sana kufanya ni kuachana na mazoea na desturi zenye hazimupendeze Yehova. Hata kisha watu fulani kujifunza mawazo ya Yehova juu ya mambo hayo wanaendelea kuona kuwa ni vigumu kuachana nayo. Wanakuwa na wasiwasi juu ya namna watu wa familia yao, wafanyakazi wenzao, ao marafiki wao watatenda. Wanajua kama mara nyingi watu wanashikilia sana desturi fulani, kama vile desturi za kuheshimia watu wa jamaa wenye wamekufa. (Kum. 14:1) Kwa hiyo, ni nini inaweza kutusaidia kufanya mabadiliko yenye kuombwa? Tunaweza kujifunza mambo fulani kwa kufikiria mifano ya muzuri ya watu wa zamani wenye walifanya mabadiliko wakati walijifunza kweli, kama vile Wakristo wa kwanza-kwanza katika Efeso.

16. Watu fulani mu muji wa Efeso waliachana na nini?

16 Mu muji wa zamani wa Efeso, watu walizoea kufanya mambo ya uchawi. Watu wenye walikuwa wanafanya mambo ya uchawi walifanya nini wakati walikubali kuwa Wakristo? Biblia inasema hivi: “Hesabu kubwa ya wale wenye walizoea kufanya uchawi wakakusanya vitabu vyao pamoja na wakaviteketeza kwa moto mbele ya watu wote. Na wakafanya hesabu na kuona kwamba vitabu hivyo vilikuwa na samani ya vipande elfu makumi tano (50 000) vya feza. Hivyo kwa njia yenye nguvu, neno la Yehova likaendelea kuongezeka na kuwa lenye nguvu zaidi.” (Mdo. 19:19, 20) Wakristo hao waaminifu walikuwa tayari kuachana na vitabu vyao vya bei sana, na Yehova aliwabariki kwa sababu ya jambo hilo.

17. (a) Pengine tumeachana na mambo gani kwa ajili ya kweli? (b) Tutajibu maulizo gani mu habari yenye kufuata?

17 Umeachana na mambo gani ili kujifunza kweli? Sisi wote tumetoa wakati wetu. Wamoja kati yetu wameacha nafasi za kuwa matajiri. Na pengine uhusiano wetu pamoja na watu wengine umebadilika. Wengi kati yetu wamebadilisha namna yao ya kuwaza na kutenda na wameachana na desturi na mazoea yenye hayamupendeze Yehova. Lakini tuko hakika kama kweli ya Biblia ni ya maana sana kuliko jambo lolote lenye tumeachana nalo. Kweli ya Biblia inatusaidia kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova; urafiki huo ndilo jambo la maana zaidi katika maisha yetu. Wakati tunafikiria baraka zote zenye tuko nazo kwa sababu ya kweli, ni vigumu kuelewa juu ya nini mutu anaweza ‘kuiuzisha.’ Jambo hilo linaweza kutokea namna gani? Na tunaweza kufanya nini ili tuepuke kufanya kosa hilo kubwa? Tutajibu maulizo hayo mu habari yenye kufuata.

^ fu. 8 Katika habari hii, majina fulani yamebadilishwa.