Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Watenda-mema wenye Yesu alizungumuzia mangaribi mbele ya kifo chake ni nani, na juu ya nini walipewa jina hilo la cheo?

Mangaribi mbele ya kifo chake, Yesu alishauria mitume wake wasitafute kuwa na cheo kati ya waamini wenzao. Aliwaambia hivi: “Wafalme wa mataifa wanapiga ubwana juu yao, na wale wenye kuwa na mamlaka juu yao wanaitwa Watenda-mema. Hata hivyo, ninyi hamupaswe kuwa vile.”​—Lu. 22:25, 26.

Watenda-mema wenye Yesu alizungumuzia ni nani? Vichele, maandishi yenye kuwa kwenye vitu kama vile majiwe, vyuma, na maandishi mengine vinaonyesha kama lilikuwa jambo la kawaida kwa Wagiriki na Waroma kuonyesha heshima watu wenye cheo na watawala kwa kuwaita kwa jina la cheo Évergète, ao Mutenda-mema. Watu hao walipewa jina hilo la cheo kwa sababu walikuwa wamefanyia watu jambo fulani la muzuri.

Wafalme fulani waliitwa kwa jina la cheo Mutenda-mema. Kati ya wafalme hao kulikuwa mutawala Mumisri mwenye aliitwa Ptolémée wa Tatu Évergète (247 hivi-222 M.K.Y.) na Ptolémée wa Munane Évergète wa Pili (147 hivi-117 M.K.Y.). Mutawala Muroma Yulio Kaisari (48-44 M.K.Y.) na Augusto (31 M.K.Y.–14 K.K.Y.) nao pia walikuwa na jina hilo la cheo, na pia Herode Mukubwa, mufalme wa Yudea. Kuhusu Herode, pengine alipewa jina hilo la cheo wakati alileta ngano kutoka mu inchi zingine ili kumaliza njaa yenye ilitesa watu wake na akatolea manguo watu wenye walikuwa maskini.

Kulingana na Adolf Deissmann, mutu mumoja mwenye elimu ya Biblia wa inchi ya Ujerumani, watu walizoea sana kutumia jina la cheo Mutenda-mema. Alisema hivi: “Kama mutu angejaribu kutafuta maandishi [ya jina hilo la cheo] kwenye vitu vya zamani, angeweza kupata maandishi mia moja kwa vyepesi.

Kwa hiyo, Yesu alipenda kusema nini wakati aliambia mitume wake hivi: “Hata hivyo, ninyi hamupaswe kuwa vile”? Je, Yesu alipenda kuwaambia kama hawapaswe kuhangaikia hali ya muzuri ya watu wengine? Hapana kabisa. Inaonekana kuwa jambo lenye Yesu alipenda kukazia ni nia yenye ilichochea watu wafanyie wengine matendo ya ukarimu.

Katika siku za Yesu, matajiri walipenda kujifanyia jina la muzuri kwa kutoa feza ili kutegemeza maonyesho na michezo mu viwanja vya michezo, kwa kujenga mabustani na mahekalu, na kwa kutegemeza mambo mengine kama hayo. Lakini walifanya vile ili watu wawasifu, ili wajulikane na watu, ao ili wachochee watu wawachague. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Hata kama kuko matendo fulani ya ukarimu wa kweli yenye watenda-mema hao walifanya, mara nyingi walifanya vile ili kutafuta faida zao wenyewe mu mambo ya politike.” Yesu alishauria wanafunzi wake waepuke roho kama hiyo ya kutafuta mambo makubwa na kutafuta faida zao wenyewe.

Miaka fulani kisha pale, mutume Paulo alikazia kweli hiyohiyo ya maana juu ya kuwa na nia ya muzuri wakati mutu anaonyesha ukarimu. Aliandikia Wakristo wenzake katika Korinto hivi: “Kila mumoja afanye kama vile alikusudia katika moyo wake, haiko kwa kutokupenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha.”​—2 Ko. 9:7.