Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 48

‘Umalizie Kile Chenye Ulianza’

‘Umalizie Kile Chenye Ulianza’

‘Mumalizie kile chenye mulianza.’​—2 KO. 8:11.

WIMBO 35 “Mhakikishe Mambo Muhimu Zaidi”

KIFUPI CHA HABARI *

1. Yehova anatupatia uhuru wa kufanya nini?

YEHOVA anatupatia uhuru wa kuamua namna tutatumia maisha yetu. Anatufundisha namna ya kukamata maamuzi ya muzuri, na anatusaidia tupate matokeo ya muzuri wakati tunakamata maamuzi yenye kumufurahisha. (Zb. 119:173) Kama tunatumia sana hekima yenye kuwa mu Neno la Mungu, tutakamata maamuzi ya muzuri.​—Ebr. 5:14.

2. Tunaweza kuwa na tatizo gani kisha kukamata maamuzi fulani?

2 Lakini, hata kama tunakamata maamuzi ya muzuri, inaweza kuwa nguvu tumalizie kile chenye tulianza. Fikiria mifano fulani: Kijana mwanaume anaamua kusoma Biblia yote. Anafanya vile kwa majuma fulani, lakini kisha anaacha kusoma juu ya sababu fulani. Dada anaamua kuwa painia wa kawaida, lakini anaendelea kuchelewesha tarehe ya kuanza. Baraza la wazee linaamua kwa umoja kufanya zaidi kazi za uchungaji, lakini kisha miezi fulani wanashindwa kutimiza maamuzi yao. Hali hizi zote ziko tofauti, lakini zinafanana katika jambo fulani. Wote walikamata maamuzi lakini hawakuitimiza. Wakristo wa kutaniko la Korinto la wakati wa mitume walipambana na tatizo hilo. Tuone mufano wao unaweza kutufundisha nini.

3. Wakristo wa Korinto walikamata uamuzi gani, lakini ni nini ilitokea?

3 Katika mwaka wa 55 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, Wakristo wa Korinto walikamata uamuzi fulani wa maana. Walisikia kama ndugu na dada zao wa Yerusalemu na Yudea walikuwa wanateseka kwa sababu ya magumu fulani na umaskini na kama Wakristo wa makutaniko ingine walikuwa wanakusanya michango ya feza ili kuwasaidia. Kwa sababu Wakristo wa Korinto walikuwa na sifa ya wema na ukarimu, waliamua kutoa michango ili kusaidia ndugu na dada wenye walikuwa na lazima ya musaada, na waliuliza mutume Paulo namna wangeweza kutoa musaada wao. Alitumia kutaniko hilo maagizo na akamuweka Tito awasaidie kukusanya ile michango. (1 Ko. 16:1; 2 Ko. 8:6) Lakini kisha miezi fulani, Paulo alipata habari kama Wakristo wa Korinto walikuwa hawajatoa michango yenye walisema kama watatoa. Kwa hiyo, inawezekana zawadi yao haingekuwa tayari kwa wakati wenye uliwekwa ili kuipeleka Yerusalemu pamoja na michango ya makutaniko ingine.​—2 Ko. 9:4, 5.

4. Kulingana na 2 Wakorinto 8:7, 10, 11, Paulo alitia moyo Wakristo wa Korinto wafanye nini?

4 Wakristo wa Korinto walikuwa wamekamata uamuzi wa muzuri, na Paulo aliwapongeza kwa sababu ya imani yao yenye nguvu na kwa sababu walipenda kuonyesha ukarimu. Lakini alipaswa kuwatia moyo wamalizie kile chenye walianza. (Soma 2 Wakorinto 8:7, 10, 11.) Mufano wao unatufundisha kama inaweza kuwa nguvu hata kwa Wakristo waaminifu kutimiza maamuzi yao.

5. Tutajibu maulizo gani katika habari hii?

5 Kama Wakristo wa Korinto, tunaweza kuona kama ni nguvu kutimiza maamuzi yetu. Juu ya nini? Juu hatukamilike, tunaweza tu kuchelewesha mambo. Ao mambo fulani yenye hatukutazamia inaweza kutokea na kufanya ikuwe nguvu kutimiza maamuzi yetu. (Muh. 9:11; Ro. 7:18) Tunapaswa kufanya nini kama tuko na lazima ya kuchunguza tena uamuzi fulani na kuamua kama tunaweza kubadilisha uamuzi wetu? Na tunaweza kufanya nini ili tukuwe tunamalizia kile chenye tunaanza?

MBELE YA KUKAMATA UAMUZI

6. Juu ya nini tunaweza kuwa na lazima ya kubadilisha uamuzi fulani?

6 Kuko maamuzi fulani ya maana yenye hatuwezi kubadilisha hata kidogo. Kwa mufano, tunashikamana na uamuzi wetu wa kumutumikia Yehova, na tunaazimia kuwa waaminifu kwa bibi ao bwana yetu. (Mt. 16:24; 19:6) Lakini, kuko maamuzi ingine yenye tunaweza kubadilisha. Juu ya nini? Juu hali zinabadilikaka. Ni nini inaweza kutusaidia tukamate maamuzi ya muzuri?

7. Tunapaswa kumuomba Yehova nini, na juu ya nini?

7 Usali ili upate hekima. Yehova alimuongoza mwanafunzi Yakobo kupitia roho yake ili kuandika hivi: “Kama mutu yeyote kati yenu anakosa hekima, aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anapatia wote kwa ukarimu.” (Yak. 1:5) Katika njia fulani, sisi wote ‘tunakosa hekima.’ Kwa hiyo, umuombe Yehova akusaidie wakati unakamata uamuzi fulani na wakati unapaswa kubadilisha uamuzi huo. Kama unafanya vile, Yehova atakusaidia ukamate maamuzi ya muzuri.

8. Namna gani tunaweza kutafuta habari mbele ya kukamata uamuzi fulani?

8 Utafute habari kwa uangalifu. Uchunguze Neno la Mungu, usome vichapo vya tengenezo la Yehova, na uzungumuze na watu wenye wanaweza kukupatia mashauri ya muzuri. (Mez. 20:18) Kutafuta habari vile ni jambo la maana sana mbele ya kukamata uamuzi wa kubadilisha kazi yako, kuhama, ao kuchagua masomo yenye itakusaidia upate feza za kukusaidia upate mambo ya lazima ili uendelee kumutumikia Yehova.

9. Juu ya nini ni muzuri tuchunguze nia yetu wakati tunakamata maamuzi?

9 Uchunguze nia yako. Yehova anaonaka nia yenye inatuchochea kufanya mambo fulani. (Mez. 16:2) Wakati tunajichunguza, tutaona ikiwa nia yetu ni gani kabisa. Lakini, tunapaswa kufikiria kwa uangalifu ikiwa nia yenye inatuchochea kabisa kukamata uamuzi fulani ni ile yenye tuko nayo kabisa mu moyo, ao ikiwa kuko sababu zingine. Kwa kweli, tunafanya mambo yenye kuwa sawa, kama tunachunguza kabisa nia yenye kuwa mu moyo wetu. Kama nia yenye inatuchochea kukamata uamuzi fulani ni ya mubaya, hilo litafanya ikuwe nguvu kutimiza uamuzi wetu wakati tunapata magumu. Kwa mufano, ndugu kijana anaweza kuamua kuwa painia wa kawaida. Lakini, kisha wakati fulani, inaweza kuwa nguvu kwake kutimiza saa zenye zinaombwa na kwa hiyo, anakosa furaha katika utumishi wake. Juu ya nini? Pengine aliwaza kama nia yenye ilimuchochea kabisa akuwe painia ni kupenda kumufurahisha Yehova. Lakini, pengine nia yenye ilimuchochea kabisa ni kupenda kufurahisha wazazi wake ao mutu mwingine.

10. Ni nini inatusaidia kufanya mabadiliko?

10 Fikiria mufano wa mwanafunzi wa Biblia mwenye anaamua kuacha kuvuta tumbako. Kwanza, anajikaza sana, na anaacha kuvuta tumbako kwa juma moja ao majuma mbili, lakini anaanza tena kuvuta tumbako. Hata hivyo, anafikia kuacha kabisa kuvuta tumbako! Kumupenda Yehova na kupenda kumufurahisha kumemusaidia ashinde tabia hiyo.​—Kol. 1:10; 3:23.

11. Juu ya nini unapaswa kuwa na miradi yenye kuwa wazi?

11 Ukuwe na miradi yenye kuwa wazi. Kama uko na miradi yenye kuwa wazi, inawezekana kabisa utamalizia kile chenye ulianza. Kwa mufano, pengine umeamua kusoma Biblia mara mingi. Lakini, kama hauna programu yenye kuwa wazi, itakuwa nguvu kutimiza mambo yenye umepanga. * Ao wazee wa kutaniko fulani wanaweza kuamua kufanya zaidi kazi za uchungaji, lakini kisha wakati fulani, wanaona kama hawajatimiza uamuzi wao. Ili waweze kutimiza uamuzi wao, wangepaswa kujiuliza maulizo kama hii: “Tumeona ni ndugu na dada gani wenye wanaweza kufaidika kabisa na kazi zetu za uchungaji? Tumepanga siku na saa ya kuwatembelea?”

12. Inaweza kuwa lazima kufanya nini, na juu ya nini?

12 Ukuwe na usawaziko. Hakuna mutu kati yetu mwenye kuwa na wakati, uwezo, na nguvu za kufanya kila kitu chenye anapenda kufanya. Kwa hiyo, ukuwe na usawaziko. Wakati fulani, inaweza kuwa lazima kubadilisha uamuzi fulani wenye unakushinda kutimiza. (Muh. 3:6) Lakini, tuseme umechunguza uamuzi wako, umebadilisha uamuzi huo kama vile inaombwa, na unaona kama unaweza kuutimiza. Ona mambo tano yenye inaweza kukusaidia umalizie kile chenye unaanza.

MAMBO YA KUKUSAIDIA UTIMIZE MAAMUZI YAKO

13. Namna gani unaweza kupata nguvu zenye uko nazo lazima ili kutimiza uamuzi fulani?

13 Usali kwa Yehova akupatie nguvu za kutenda. Mungu anaweza kukupatia “nguvu za kutenda” na kutimiza uamuzi wako. (Flp. 2:13) Kwa hiyo, umuombe Yehova roho yake takatifu ili ikupatie nguvu zenye uko nazo lazima. Endelea kusali hata wakati unaona kama sala yako inakawia kujibiwa. Kama vile Yesu alisema: ‘Endelea kuomba, na utapewa [roho takatifu].’​—Lu. 11:9, 13.

14. Namna gani kanuni yenye iko mu Mezali 21:5 inaweza kukusaidia kutimiza uamuzi wako?

14 Upange namna utatimiza maamuzi yako. (Soma Mezali 21:5.) Ili kumalizia jambo fulani lenye umeanza, unapaswa kupanga namna utalitimiza. Kisha, unapaswa kutenda kulingana na mambo yenye umepanga. Vilevile, wakati unakamata uamuzi fulani, fanya liste ya mambo yenye utafanya ili kutimiza uamuzi wako. Kama uko na kazi kubwa, uigawanye katika sehemu za kidogo-kidogo; kama unafanya vile itakuwa mwepesi kuona mahali kwenye unafikia. Paulo alitia moyo Wakristo Wakorinto waweke kitu fulani pembeni kwa ajili ya muchango “siku ya kwanza ya kila juma.” Hawakupaswa kungojea na kujaribu kukusanya michango wakati angefika. (1 Ko. 16:2) Kugawanya kazi kubwa katika sehemu za kidogo-kidogo kunaweza kukusaidia pia usichoke sana.

15. Kisha kupanga namna utatimiza maamuzi yako, unaweza kufanya nini sasa?

15 Kama unaandika waziwazi mambo yenye unapanga kufanya, hilo linaweza kukusaidia utimize maamuzi yako. (1 Ko. 14:40) Kwa mufano, baraza la wazee linapewa muongozo wa kuomba muzee mumoja aandike maamuzi yote yenye baraza la wazee linakamata, wale wenye watashugulikia ile maamuzi na wakati wenye wanapaswa kumaliza kuishugulikia. Kama wazee wanafuata muongozo huo, itakuwa mwepesi kwao kutimiza mambo yenye walipanga kufanya. (1 Ko. 9:26) Unaweza kujaribu kufanya vile katika mambo yako yenye unafanya kila siku. Kwa mufano, unaweza kuandika liste ya mambo ya kufanya kila siku na ku liste yako uanze na mambo yenye utapenda kufanya kwanza. Kufanya vile kutakusaidia umalizie kile chenye ulianza na utimize mambo mingi zaidi mu wakati kidogo.

16. Unapaswa kufanya jambo gani lingine ili utimize maamuzi yako, na namna gani Waroma 12:11 inaunga mukono jambo hilo?

16 Ujikaze sana. Inaomba kujikaza sana ili kutimiza mambo yenye umepanga na kumalizia kile chenye unaanza. (Soma Waroma 12:11.) Paulo alimuambia Timoteo ‘aendelee kufanya bidii’ na ‘aendelee’ kujikaza ili akuwe mwalimu muzuri zaidi. Tunaweza kutumia shauri hilo la mutume Paulo katika miradi ingine ya kiroho.​—1 Ti. 4:13, 16.

17. Namna gani Waefeso 5:15, 16 inaweza kutusaidia kutimiza mambo yenye tulipanga kufanya?

17 Utumie wakati wako kwa hekima. (Soma Waefeso 5:15, 16.) Upange wakati wa kufanya mambo yenye umeamua kufanya na usibadilishe wakati huo. Usingoje mupaka hali zikuwe muzuri kabisa ili uanze kazi yako; pengine hali hazitakuwa muzuri kabisa. (Muh. 11:4) Ukuwe muangalifu ili usiache mambo yenye haiko ya lazima ikamate wakati wako na ukose nguvu ya kufanya mambo ya maana zaidi. (Flp. 1:10) Kama inawezekana, upange wakati wa kufanya ile mambo wakati watu wengine hawatakufanya usimamishe mambo yenye uko unafanya. Uambie wengine kama uko na lazima ya kupata wakati wa kukaza akili yako juu ya mambo yenye uko unafanya. Unaweza kufunga telefone yako na kusoma ujumbe wako ku Enternete ao ku site za Enternete za kupashana habari na watu wengi kisha kumaliza kazi yako. *

18-19. Ni nini inaweza kukusaidia uendelee kujikaza ili kutimiza uamuzi wako hata kama unapata vizuizi?

18 Ufikirie matokeo ya muzuri ya uamuzi wako. Matokeo ya uamuzi wako iko kama vile kufika mahali kwenye ulikuwa unaenda. Kama unapenda kabisa kufika mahali kwenye uko unaenda, utaendelea na safari yako hata kama barabara inafungwa na unapaswa kupita katika barabara ingine. Vilevile, kama tunafikiria matokeo ya maamuzi yetu, hatutaacha palepale wakati tunakutana na vizuizi ao wakati tunapaswa kutumia njia ingine ili kutimiza maamuzi yetu.​—Gal. 6:9.

19 Haiko mwepesi kukamata maamuzi ya muzuri, na inaweza kuwa nguvu kutimiza ile maamuzi. Lakini Yehova anaweza kukusaidia kupata hekima na nguvu zenye uko nazo lazima ili kumalizia kile chenye unaanza.

WIMBO 65 Songa Mbele!

^ fu. 5 Unahuzunika juu ya maamuzi fulani yenye umekamata? Ao unashindwa kukamata maamuzi ya muzuri na kuitimiza? Habari hii itakusaidia kushinda ile matatizo na kumalizia kile chenye unaanza.

^ fu. 11 Ili kukusaidia ufanye programu yako ya usomaji wa Biblia, unaweza kutumia “Ratiba ya Usomaji wa Biblia” yenye kupatikana ku jw.org®.

^ fu. 17 Ili kupata mashauri ingine juu ya namna ya kutumia wakati wako, ona habari yenye kichwa “Mbinu 20 za Kutafuta Wakati Zaidi” katika Amuka! ya Mwezi wa 4, 2010.