Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 48

Uendelee “Kuangalia Mbele”

Uendelee “Kuangalia Mbele”

“Macho yako yanapaswa kuangalia mbele moja kwa moja, ndiyo, kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.”​—MEZ. 4:25.

WIMBO 77 Nuru Katika Ulimwengu Wenye Giza

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Namna gani tunaweza kufuata shauri lenye kuwa mu Mezali 4:25? Leta mufano.

FIKIRIA mifano yenye kufuata. Dada Mukristo mwenye kuzeeka anafikiri juu ya wakati muzuri wenye alipitisha zamani. Hata kama iko na magumu mingi leo mu maisha yake, anaendelea kufanya yake yote ili kumutumikia Yehova. (1 Ko. 15:58) Kila siku anawazia namna maisha itakuwa wakati ataishi pamoja na wapendwa wake mu dunia mupya. Dada mwingine anakumbuka jambo lenye Mukristo mwenzake alifanya lenye lilimukwaza. Lakini anaamua kuacha kufikiria ile jambo. (Kol. 3:13) Na ndugu mwingine anakumbuka makosa yenye alifanyaka zamani, lakini anakaza akili juu ya mambo yenye anaweza kufanya leo ili kuendelea kuwa muaminifu kwa Yehova.​—Zb. 51:10.

2 Wale Wakristo wote watatu wanakumbuka mambo yenye ilitokea zamani mu maisha yao. Lakini kuliko kukaza akili juu ya ile mambo, wanaendelea “kuangalia mbele.”​—Soma Mezali 4:25.

3. Juu ya nini ni jambo la maana tuendelee “kuangalia mbele”?

3 Juu ya nini ni jambo la maana tuendelee “kuangalia mbele,” ni kusema, tuendelee kukaza akili juu ya wakati wenye kuja? Mutu mwenye iko anatembea lakini iko anaangalia-angalia nyuma hawezi kuona muzuri mambo yenye kuwa mbele yake. Vilevile hatuwezi kuendelea kumutumikia Yehova kwa uwezo wetu wote kama tunazoea kufikiria mambo ya zamani.​—Lu. 9:62.

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Mu hii habari tutazungumuzia mitego tatu yenye inaweza kutufanya tuendelee kufikiria mambo ya zamani: (1) Kutamani maisha yetu ya zamani, (2) kuendelea kukasirika, na (3) kuendelea kujihukumu. Wakati tutakuwa tunazungumuzia ile mambo tatu, tutaona kanuni za Biblia zenye zinaweza kutusaidia tusikaze akili juu ya “mambo ya nyuma,” lakini tuendelee kukaza akili juu ya “mambo yenye kuwa mbele.”​—Flp. 3:13.

KUTAMANI MAISHA YETU YA ZAMANI

Nini njo inaweza kutuzuia tusiendelee kuangalia mbele? (Ona fungu la 5, 9, 13) *

5. Kulingana na Muhubiri 7:10, hatupaswe kufanya nini?

5 Soma Muhubiri 7:10. Ile andiko haiseme kama ni mubaya kujiuliza hivi: “Sababu gani siku za zamani zilikuwa muzuri?” Haiko mubaya kujiuliza vile, juu Yehova anapenda tukumbuke mambo ya muzuri. Lakini hivi njo ile andiko inasema: “Usiseme: ‘Sababu gani siku za zamani zilikuwa muzuri zaidi kuliko siku hizi?’” Ni kusema, haiko muzuri kulinganisha hali yetu ya zamani na hali yetu ya leo, na kisha kusema kama hali yetu ya leo njo ya mubaya zaidi. Mu tafsiri ingine ya Biblia, ile andiko inasema hivi: “Usijiulize hata kidogo, ‘Oh, juu ya nini mambo ilikuwa muzuri zaidi zamani?’ Haiko muzuri kujiuliza vile.”

Kisha Waisraeli kutoka mu inchi ya Misri, walifanya kosa gani? (Ona fungu la 6)

6. Juu ya nini haiko muzuri kuendelea kufikiri kama maisha yetu ilikuwa muzuri zaidi zamani? Leta mufano.

6 Juu ya nini haiko muzuri kuendelea kufikiri kama maisha yetu ilikuwa muzuri zaidi zamani? Juu ile inaweza kutufanya tukumbuke tu mambo ya muzuri ya zamani, lakini tusahau magumu yenye tulikuwa nayo. Fikiria mufano wa Waisraeli. Kisha kutoka Misri, bila kukawia walisahau namna walikuwa wanateseka wakati walikuwa kule. Walianza tu kukumbuka chakula ya muzuri yenye walikuwa wanakula wakati walikuwa Misri. Walisema hivi: “Tunakumbuka sana samaki wenye tulikuwa tunakula bila kulipa katika inchi ya Misri, na matango, matikiti-maji, vitunguu vya majani, vitunguu, na vitunguu saumu!” (Hes. 11:5) Ni kweli kwamba walikuwa wanakula ile chakula “bila kulipa”? Hapana! Walikuwa wanateseka sana kwa sababu ile wakati walikuwa watumwa na Wamisri walikuwa wanawatendea mubaya. (Kut. 1:13, 14; 3:6-9) Hata vile, Waisraeli walisahau ile magumu yote, na wakaanza kukumbuka sana mambo ya zamani. Waliamua kukaza akili juu ya mambo yenye waliwaza kama ilikuwa ya muzuri, kuliko kukaza akili juu ya mambo ya muzuri yenye Yehova alikuwa amewafanyia. Na Yehova hakufurahia jambo hilo.​—Hes. 11:10.

7. Nini njo ilisaidia dada mumoja asiendelee kufikiri kama maisha yake ilikuwa muzuri zaidi zamani?

7 Tunaweza kufanya nini ili tusiendelee kufikiri kama maisha yetu ilikuwa muzuri zaidi zamani? Fikiria mufano wa dada mumoja mwenye alianza kutumikia ku Beteli ya Brooklyn mu mwaka wa 1945. Kisha miaka fulani, aliolewa na ndugu mwenye naye alikuwa Mwanabeteli. Na waliendelea kutumika ku Beteli pamoja kwa miaka mingi. Lakini mu mwaka wa 1976, bwana yake aligonjwa. Ule dada anasema kama wakati bwana yake aliona kuwa anakaribia kufa, alimupatia mashauri. Ile mashauri ingemusaidia ule dada wakati bwana yake angekufa. Bwana yake alimuambia hivi: “Watu wengi hawakuwake na furaha mu ndoa. Lakini sisi tumekuwa na furaha kabisa.” Hata vile, bwana yake alimuambia tena hivi: “Utaendelea kukumbuka mambo ya muzuri yenye tumefanya pamoja, lakini usikaze akili juu ya ile mambo. Kadiri wakati itaendelea kupita, ni vile huzuni yako itaendelea kupunguka. Usivunjike moyo na kuhuzunika juu ya mambo yenye ilikufikia. Ufurahie wakati muzuri wenye tumefanya pamoja mu kazi ya Yehova. . . . Yehova anapenda tukumbuke mambo ya muzuri.” Hauone kama ile ilikuwa mashauri ya muzuri?

8. Dada yetu alipataka faida gani juu alifuataka mashauri ya bwana yake?

8 Ule dada alifuata mashauri ya bwana yake. Alimutumikia Yehova kwa uaminifu mupaka wakati alikufa akiwa na miaka 92. Miaka fulani mbele akufe alisema hivi: “Wakati ninafikiria miaka 63 yenye nimemutumikia Yehova mu utumishi wa wakati wote, ninaweza kusema kama nimekuwa na maisha yenye furaha kabisa.” Juu ya nini? Alisema hivi: “Mambo yenye inafanyaka mutu akuwe na furaha, ni kuwa mu familia ya muzuri ya ndugu na dada, kuwa na tumaini la kuishi pamoja nao mu dunia paradiso, na kumutumikia Yehova, Muumbaji wetu Mukubwa na Mungu wa kweli, kwa umilele.” * Ule dada alikaza akili juu ya wakati wenye kuja, na mufano wake unaweza kutufundisha mambo mingi!

KUENDELEA KUKASIRIKA

9. Kama vile Walawi 19:18 inaonyesha, ni wakati gani inaweza kuwa nguvu sana kusamehe?

9 Soma Walawi 19:18. Wakati fulani inakuwaka nguvu kusamehe kama mutu mwenye alitukosea ni Mukristo mwenzetu, ni rafiki wa karibu, ao mutu wa familia yetu. Kwa mufano, dada mumoja alisema kama dada mwingine alimuiba feza. Lakini wakati alifikia kuona kama haiko ule dada njo alimuiba feza, alimuomba musamaha. Dada mwenye alisingiziwa alikasirika sana, na aliendelea kufikiria ile mambo. Na wewe ulishakajisikia vile? Hata kama pengine hali kama ile haijatufikiaka, wengi kati yetu tulishaka kasirika na kuona kama hatutaweza kusamehe mutu fulani mwenye alitukosea.

10. Nini njo inaweza kutusaidia tusiendelee kukasirikia mutu mwenye alitukosea?

10 Nini njo inaweza kutusaidia tusiendelee kukasirikia mutu mwenye alitukosea. Kwanza, tukumbuke kama Yehova anaonaka mambo yote. Anajua mambo yote yenye inatufikia, na hata anajua wakati wengine wanatutendea bila haki. (Ebr. 4:13) Anasikiaka mubaya wakati anaona tuko tunateseka. (Isa. 63:9) Na anatuahidi kama atamaliza mambo yote ya mubaya yenye imetufikia kwa sababu ya kutendewa bila haki.​—Ufu. 21:3, 4.

11. Tunapata faida gani wakati tunasamehe wengine?

11 Tunapaswa pia kukumbuka kama tutapata faida wakati tunasamehe wengine. Ni vile ule dada mwenye alisingiziwa alifikia kuelewa. Kisha wakati fulani, alifikia kusamehe na hakuendelea tena kuwa na kasirani. Alitambua kama wakati tunasamehe wengine, Yehova pia anatusamehe. (Mt. 6:14) Alijua kama mambo yenye walimufanyia ilikuwa mubaya, lakini aliamua kusamehe. Ile ilimusaidia akuwe na furaha na aendelee kukaza akili juu ya utumishi wake kwa Yehova.

KUENDELEA KUJIHUKUMU

12. Andiko la 1 Yohana 3:19, 20 linatufundisha nini?

12 Soma 1 Yohana 3:19, 20. Sisi wote tunakuwaka tunajihukumu wakati fulani. Kwa mufano, watu fulani wanakuwaka wanajihukumu kwa sababu ya makosa yenye walifanya mbele wajifunze kweli. Wengine wanakuwaka wanajihukumu kwa sababu ya makosa yenye walifanya kisha kubatizwa. Ni kawaida kujihukumu. (Ro. 3:23) Kusema kweli tunapenda kufanya mambo yenye kuwa sawa. Lakini “sisi wote tunajikwaa mara nyingi.” (Yak. 3:2; Ro. 7:21-23) Hata kama hatufurahiake wakati moyo wetu unatuhukumu, kujihukumu kunaweza kuwa na matokeo fulani ya muzuri. Juu ya nini? Juu kujihukumu kunaweza kutusaidia tufanye mabadiliko na tujikaze ili tusirudilie makosa yetu.​—Ebr. 12:12, 13.

13. Juu ya nini tunapaswa kuepuka kuendelea kujihukumu?

13 Ni kweli kama haiko mubaya kujihukumu kwa kiasi fulani, lakini tunaweza kuangukia katika mutego wa kuendelea kujihukumu hata kama tulishatubu, na Yehova ameonyesha kama ametusamehe. Kujihukumu vile kunaweza kuwa na matokeo ya mubaya. (Zb. 31:10; 38:3, 4) Juu ya nini? Fikiria mufano wa dada mumoja mwenye aliendelea kujihukumu juu ya zambi zenye alifanya zamani. Anasema hivi: “Niliwaza kama haiko lazima nikuwe na bidii mu kazi ya Yehova, juu pengine sitaokolewa.” Wengi kati yetu wanaweza kujisikia vile. Ni jambo la maana tuepuke kuendelea kujihukumu, juu ile inaweza kufanya tuache kumutumikia Yehova hata kama Yehova alishatusamehe. Na Shetani atafurahi sana kama tunafanya vile!​—Linganisha na 2 Wakorinto 2:5-7, 11.

14. Ni nini inaweza kutusaidia tujue kama Yehova anaweza kutusamehe?

14 Hata vile, tunaweza kujiuliza: ‘Nitajua namna gani kama Yehova anaweza kunisamehe?’ Kusema kweli, wakati tunajiuliza vile, ile inaonyesha kama Yehova anaweza kutusamehe. Kumepita miaka mingi gazeti Munara wa Mulinzi lilisema hivi: “[Tunaweza] kurudilia kosa ileile tena na tena. Pengine hatujaweza kushinda uzaifu fulani wenye tulikuwa nao mbele tuanze kumutumikia Yehova. . . . Usipoteze tumaini. Usiwaze kama ulifanya zambi yenye haiwezi kusamehewa. Vile njo Shetani anapenda ufikiri. Lakini ikiwa unajisikia mubaya juu ya makosa yenye ulifanya, ile inaonyesha kama hauko mutu mubaya na kama Yehova anaweza kukusamehe. Ukuwe munyenyekevu na uendelee kumuomba Yehova akusamehe na akusaidie ukuwe tena na zamiri safi. Sawa vile mutoto anamuombaka baba yake musaada juu ya tatizo fulani tena na tena, uendelee kumuomba Yehova akusaidie. Kama unafanya vile atakusaidia kwa sababu ya fazili zake zenye hazistahiliwe.”

15-16. Watu fulani wamejisikia namna gani kwa kujua kama Yehova anaweza kuwasamehe?

15 Watumishi wengi wa Yehova wametiwa moyo kwa kujua kama Yehova anaweza kuwasamehe. Kwa mufano, miaka fulani yenye imepita ndugu mumoja alitiwa moyo wakati alisoma habari moja kati ya habari zenye kichwa “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu.” Dada mwenye kuzungumuziwa mu ile habari, alisema kama mambo yenye ilimufikiaka zamani ilifanya awaze kama Yehova hawezi kumupenda. Aliendelea kuwaza vile kwa miaka mingi hata kisha kubatizwa. Lakini kufikiri sana juu ya bei ya ukombozi kulimusaidia aamini kama Yehova anamupenda. *

16 Mambo yenye ule ndugu alisoma juu ya ule dada ilimusaidia namna gani? Aliandika hivi: “Wakati nilikuwa kijana nilizoea kuangalia pornografia, na haikuwa mwepesi kwangu kuachana na ile tabia. Hivi majuzi nilianza tena kufanya vile. Nilitafuta musaada wa wazee na niko najikaza ili kuachana na ile tabia. Wazee walinihakikishia kama Yehova ananipenda na kama anaweza kunisamehe. Lakini wakati fulani ninawazaka kama niko mutu wa bure na kama Yehova hawezi kunipenda. Kusoma habari [ya ule dada], kulinisaidia sana. Sasa ninaelewa kama wakati ninasema kama Mungu hawezi kunisamehe, ni sawa vile ninasema kama zabihu ya Mwana wake haiwezi kufunika zambi zangu. Niliweka ile habari ya ule dada ili nikuwe naisoma na kuifikiria kila mara wakati ninawaza kama Yehova hanipendi.”

17. Ni nini ilimusaidia mutume Paulo aepuke kuendelea kujihukumu?

17 Habari za vile zinatukumbusha mambo yenye ilimufikia mutume Paulo. Mbele akuwe Mukristo alifanya mambo mingi ya mubaya. Alikuwa anakumbuka mambo yenye alifanyaka, lakini hakuendelea kuifikiria. (1 Ti. 1:12-15) Aliamini kama anaweza kusamehewa kwa sababu ya zabihu ya bei ya ukombozi, na kama bei ya ukombozi ni zawadi yenye Mungu alimutolea. (Gal. 2:20) Ile ilimusaidia aepuke kuendelea kujihukumu na akaze akili juu ya utumishi wake kwa Yehova. Na aliendelea kumutumikia Yehova kwa bidii.

UKAZE AKILI JUU YA WAKATI WENYE KUJA!

Tujikaze basi kukaza akili juu ya wakati wenye kuja (Ona fungu la 18-19) *

18. Tumejifunza nini mu hii habari?

18 Tumejifunza nini mu hii habari? (1) Yehova anapenda tukumbuke mambo ya muzuri yenye imetufikia, lakini hata kama tulikuwa na maisha ya muzuri zamani, ni mu dunia mupya tu njo tutakuwa na maisha ya muzuri zaidi. (2) Watu wengine wanaweza kutukosea, lakini kama tunaamua kuwasamehe tunaweza kukaza akili juu ya utumishi wetu kwa Yehova. (3) Kuendelea kujihukumu kunaweza kutuzuia kumutumikia Yehova kwa furaha. Kwa hiyo, kama mutume Paulo tunapaswa kuamini kama Yehova ametusamehe.

19. Tunajua namna gani kama mu dunia mupya hatutaendelea kuwaza juu ya mambo yenye inaweza kutufanya tujisikie mubaya?

19 Tuko na tumaini la uzima wa milele. Na mu dunia mupya, hatutakumbuka jambo lolote lenye linaweza kutufanya tujisikie mubaya. Kuhusu ile wakati Biblia inasema hivi: “Mambo ya zamani hayatakumbukwa.” (Isa. 65:17) Waza kidogo: Wamoja kati yetu wamezeeka mu utumishi wa Yehova, lakini mu dunia mupya, sisi wote tutakuwa vijana. (Yob. 33:25) Kwa hiyo, tuepuke kukaza akili juu ya mambo ya zamani. Lakini tukaze akili juu ya wakati wenye kuja na tufanye yote yenye tunaweza ili tuingie mu dunia mupya!

WIMBO 142 Kushikilia Tumaini Letu

^ fu. 5 Inaweza kuwa muzuri kufikiri juu ya mambo ya zamani. Lakini kama tunafikiri sana juu ya ile mambo tunaweza kuacha kumutumikia Yehova kwa nguvu yetu yote leo ao tunaweza kuacha kufikiria ahadi zake za wakati wenye kuja. Hii habari itazungumuzia mitego tatu yenye inaweza kutufanya tuendelee kufikiria mambo ya zamani. Tutazungumuzia pia kanuni za Biblia na mifano ya ndugu na dada yenye inaweza kutusaidia tuepuke ile mitego.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Kama tunaendelea kutamani maisha yetu ya zamani, kama tunaendelea kukasirika, na kama tunaendelea kujihukumu, ni sawa vile tuko tunakokota mizigo mizito yenye inaweza kutuzuia kuendelea kutembea mu barabara yenye kuongoza kwenye uzima wa milele.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Kama tunaachana na ile mambo tatu yenye kuwa sawa vile mizigo, tutajisikia muzuri, tutakuwa na furaha, na tutakuwa tena na nguvu. Kisha tutaweza kuangalia mbele.