Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

“Yehova Hakunisahau”

“Yehova Hakunisahau”

NINAISHI mu kijiji cha Orealla, chenye kuwa na watu karibu 2 000, kinapatikana mu inchi ya Guyana, katika Amerika ya Kusini. Inaomba kutumia ndege ya kidogo ao mashua ili kufika mu kijiji chetu kwa sababu kiko mbali sana.

Nilizaliwa mu mwaka wa 1983. Mu miaka ya kwanza ya maisha yangu, nilikuwa mutoto mwenye afya ya muzuri. Lakini wakati nilikuwa na miaka kumi, nilianza kusikia maumivu makali mu mwili wote. Kisha miaka mbili hivi, asubui moja niliamuka lakini sikuweza kutikisika. Hata kama nilijikaza sana kutikisa miguu yangu, sikuweza kufanya vile. Kuanzia ile siku, sijaweza kutembea. Pia ugonjwa wangu ulifanya niache kukomaa. Leo ningali na mwili sawa ya mutoto mudogo.

Tangu wakati niligonjwa, sikukuwa ninatoka ku nyumba. Kisha miezi fulani, wanamuke wawili Mashahidi wa Yehova walikuja kunitembelea. Mara mingi wakati wageni walikuwa wanakuja kwetu nilikuwa najificha, lakini ile siku nilikubali kuzungumuza na wale wanamuke. Wakati walikuwa wanazungumuza juu ya Paradiso, nilikumbuka mambo yenye nilisikiaka wakati nilikuwa na miaka tano. Ile wakati Jethro, misionere mumoja mwenye alikuwa anaishi Suriname, alikuwa anatembelea kijiji chetu mara moja kila mwezi, na alikuwa anajifunza Biblia na baba yangu. Jethro alikuwa ananitendea muzuri, na nilimupenda sana. Pia, wakati fulani wazazi wa baba yangu walikuwa wananipeleka ku mikutano fulani ya Mashahidi wa Yehova yenye ilikuwa inafanywa mu kijiji chetu. Kwa hiyo, wakati Florence, mumoja kati ya wale wanamuke wenye walinitembelea ile siku, aliniuliza kama ninapenda kujua mengi zaidi, nilisema ndiyo.

Wakati Florence alirudia tena alikuja na bwana yake na walianza kujifunza Biblia pamoja na mimi. Wakati waliona kama sijue kusoma, walinisaidia nijue kusoma. Kisha wakati fulani nilianza kusoma mimi mwenyewe. Siku moja, waliniambia kama wamepewa mugao wa kuenda kutumikia Suriname. Ilihuzunisha kwa sababu katika Orealla, hakuna mutu mwenye angeendelea kujifunza Biblia pamoja na mimi. Lakini jambo la kufurahisha ni kwamba, Yehova hakunisahau.

Kisha wakati mufupi, painia mwenye kuitwa Floyd alifika Orealla, na wakati alikuwa anahubiri nyumba kwa nyumba alikutana na mimi. Wakati alizungumuza na mimi juu ya kujifunza Biblia, nilicheka. Akaniuliza hivi: “Juu ya nini uko unacheka?” Nilimuambia kama nilikuwa nimejifunza broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Na nilikuwa nimeanza kujifunza kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. * Nilimufasiria juu ya nini sikuendelea tena kujifunza. Floyd alijifunza na mimi sehemu yenye ilikuwa imebakia ya kitabu Ujuzi, lakini yeye pia alipewa mugao wa kuenda kutumikia fasi ingine. Na mara ingine nikabakia bila mwalimu.

Lakini mu mwaka wa 2004, mapainia wa pekee wawili, Granville na Joshua, walipewa mugao wa kutumikia Orealla. Wakati walikuwa wanahubiri nyumba kwa nyumba walinipata. Wakati waliniuliza kama nilipenda kujifunza Biblia, nilicheka. Niliwaomba wajifunze na mimi kitabu Ujuzi kuanzia mwanzo. Nilipenda kuona kama mambo yenye wangenifundisha itafanana na mambo yenye walimu wangu wa zamani walinifundisha. Granville aliniambia kama mikutano ilikuwa inafanywa mu kijiji chetu. Hata kama nilikuwa sijatoka kwetu kwa karibu miaka kumi, nilipenda kuhuzuria mikutano. Kwa hiyo, Granville alikuja kunichukua akanitia mu kinga ya vilema na akanisukuma mupaka ku Jumba la Ufalme.

Kisha wakati fulani, Granville alinitia moyo nijiandikishe ku Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi. Alisema hivi: “Uko mulemavu, lakini unaweza kuongea. Siku moja, utatoaka hotuba ya watu wote. Bila shaka utafanyaka vile.” Maneno yake yenye kutia moyo ilinisaidia nisiogope.

Nilianza kuhubiri pamoja na Granville. Lakini, juu mu kijiji chetu barabara zilikuwa za mubaya, ilikuwa nguvu kutumia kinga ya vilema. Kwa hiyo, nilimuomba Granville akuwe ananisukuma mu brouette. Ile ilinisaidia sana. Mu Mwezi wa 4, 2005, nilibatizwa. Muda mufupi kisha pale, ndugu walinizoeza kushugulikia vichapo na vikuza-sauti mu Jumba la Ufalme.

Lakini, jambo la kuhuzunisha ni kwamba, mu mwaka wa 2007, baba yangu alikufa kisha kupatwa na aksida mu mashua. Familia yetu ilihuzunika sana. Granville alisali pamoja na sisi na alitusomea maandiko yenye kutia moyo. Miaka mbili kisha pale, tulihuzunika tena sana wakati tulipata ingine musiba, Granville alikufa mu aksida ya mashua.

Kutaniko letu la kidogo lilibakia na huzuni. Tulikuwa tu na mutumishi mumoja wa huduma, na hatukukuwa tena na muzee. Kifo cha Granville kilinihuzunisha sana; alikuwa rafiki yangu mupendwa. Alikuwa ananihangaikia kiroho na kimwili. Kwenye mukutano wenye ulifuata, nilikuwa na mugao wa kusoma mafungu kwenye Funzo la Munara wa Mulinzi. Nilisoma mafungu mbili tu, kisha nikaanza kulia na machozi ikaendelea kunitoka. Nililazimika tu kutoka kwenye jukwaa.

Nilianza kujisikia muzuri wakati ndugu wa mu kutaniko lingine walikuwa wanakuja kutusaidia katika Orealla. Pia biro ya tawi ilitutumia painia wa pekee mwenye kuitwa Kojo. Nilifurahi sana wakati mama yangu na mudogo yangu mwanaume walianza kujifunza Biblia na wakafikia kubatizwa. Kisha, mu Mwezi wa 3, 2015, niliwekwa kuwa mutumishi wa huduma. Kisha wakati fulani, nilitoa hotuba ya watu wote. Ile siku, nilifurahi sana na kutokwa na machozi wakati nilikumbuka maneno yenye Granville aliniambiaka miaka mingi mbele ya pale: “Siku moja utatoaka hotuba ya watu wote. Bila shaka, utafanyaka vile.”

Kupitia programu zenye kuwa ku JW Télédiffusion, nimejifunza kuhusu Wakristo wenzangu wenye kuwa mu hali kama yangu. Hata kama wako na ulemavu mbalimbali, wako wanafanya mambo mingi mu kazi ya Yehova na wako na furaha. Mimi pia ningali na nguvu ya kufanya mambo fulani. Kwa sababu nilipenda kumutumikia Yehova kwa nguvu yangu yote, niliamua kuwa painia. Na mu Mwezi wa 9, 2019, nilipata habari ya muzuri sana! Nilijulishwa kama nimewekwa kuwa muzee mu kutaniko letu lenye kuwa na wahubiri 40.

Ninashukuru ndugu na dada wenye walijifunza na mimi na wenye walinisaidia niweze kumutumikia Yehova. Zaidi ya yote, ninamushukuru sana Yehova, kwa sababu hakunisahau.

^ fu. 8 Kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova lakini sasa hakichapishwe tena.