Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 45

Muendelee Kuonyeshana Upendo Mushikamanifu

Muendelee Kuonyeshana Upendo Mushikamanifu

“Mutendeane kwa upendo mushikamanifu na rehema.”​—ZEK. 7:9.

WIMBO 107 Tuonyeshe Upendo Kama Mungu

KIFUPI YA HABARI *

1-2. Ni sababu gani tatu za muzuri zenye zinatusukuma tuonyeshane upendo mushikamanifu?

 TUKO na sababu mingi za muzuri za kuonyeshana upendo mushikamanifu. Sababu gani kwa mufano? Mezali za Biblia zenye kufuata, zinatusaidia kupata jibu. Zinasema hivi: “Usiruhusu upendo mushikamanifu na uaminifu vikuache. . . . Halafu utakubaliwa na kupata ufahamu muzuri mbele ya macho ya Mungu na ya mwanadamu.” “Mutu mwenye upendo mushikamanifu anajiletea faida.” “Kila mutu mwenye anafuatilia haki na upendo mushikamanifu atapata uzima.”​—Mez. 3:3, 4; 11:17, maelezo ya chini; 21:21.

2 Hizi mezali, zinataja sababu tatu za kutusukuma tuonyeshe upendo mushikamanifu. Kwanza, wakati tunaonyesha upendo mushikamanifu, ile inafanya Mungu atuone kuwa watu wa maana sana. Pili, wakati tunaonyesha upendo mushikamanifu, tunajiletea faida. Kwa mufano, kunatusaidia kufanya urafiki wa bila mwisho pamoja na wengine. Tatu, kama tunaonyesha upendo mushikamanifu, tutapata baraka za wakati wenye kuja, kutia ndani uzima wa milele. Kusema kweli, tuko na sababu za muzuri za kufuata hii maneno ya Yehova: “Mutendeane kwa upendo mushikamanifu na rehema.”​—Zek. 7:9.

3. Tutazungumuzia maulizo gani mu hii habari?

3 Mu hii habari, tutapata majibu ya maulizo ine. Ni nani njo tunapaswa kuonyesha upendo mushikamanifu? Kitabu ya Rutu inatufundisha nini kuhusu kuonyesha upendo mushikamanifu? Tunaweza kufanya nini leo ili kuonyesha upendo mushikamanifu? Wale wenye wanaonyesha upendo mushikamanifu wanapata baraka gani?

NI NANI NJO TUNAPASWA KUONYESHA UPENDO MUSHIKAMANIFU?

4. Namna gani tunaweza kumuiga Yehova kwa kuonyesha upendo mushikamanifu? (Marko 10:29, 30)

4 Mu habari yenye inatangulia, tulijifunza kama Yehova anaonyeshaka upendo mushikamanifu kwa wale tu wenye wanamupenda na kumutumikia. (Da. 9:4) Tunapenda kuwa “waigaji wa Mungu, kama watoto wapendwa.” (Efe. 5:1) Kwa hiyo, tunapaswa kuonyesha ndugu na dada zetu upendo mushikamanifu, ni kusema, kuambatana nao kabisa.​—Soma Marko 10:29, 30.

5-6. Neno “ushikamanifu” inaweza kutumiwa juu ya kuzungumuzia nini? Toa mufano

5 Kusema kweli, kadiri tunaelewa muzuri zaidi maana ya upendo mushikamanifu, ni vile itakuwa mwepesi kwetu kuionyesha kwa ndugu na dada zetu. Ili tuelewe muzuri kabisa maana ya upendo mushikamanifu, tuzungumuzie tofauti kati ya upendo mushikamanifu na ushikamanifu, kwa kufikiria namna neno ushikamanifu inaweza kutumiwa.

6 Kama mufanyakazi fulani ametumika miaka mingi mu kompanyi fulani, tunaweza kusema kama iko mushikamanifu ku ile kompanyi. Lakini, pengine mu ile miaka yote, hayaonanaka na musimamizi wa ile kompanyi. Na pengine hakubalianake kila mara na maamuzi ya ile kompanyi. Hatuwezi kusema kama anapenda kompanyi yake. Anafurahia tu kutumika pale juu ile kazi njo inamusaidiaka apate makuta. Ataendelea kutumika mule mupaka afikie miaka ya kuacha kazi. Lakini akipata kazi ya muzuri fasi ingine, anaweza kuacha ile kazi.

7-8. (a) Ni nini njo inapaswa kutusukuma kuonyesha upendo mushikamanifu? (b) Juu ya nini tutachunguza maandiko fulani yenye kuwa mu kitabu ya Rutu?

7 Kuko tofauti gani kati ya mufanyakazi mwenye iko mushikamanifu ku komapanyi yake na mutu mwenye kuonyesha upendo mushikamani? Tofauti ni nia ya kila mumoja, ao jambo yenye inamusukuma kutenda. Nini njo ilisukuma watumishi wa Yehova wa zamani waonyeshe upendo mushikamanifu? Walionyesha upendo mushikamanifu, hapana juu ya kutafuta faida fulani, lakini juu moyo wao uliwasukuma kufanya vile. Tufikirie mufano wa Daudi. Moyo wake njo ulimusukuma aonyeshe Yonatani rafiki yake upendo mushikamanifu, hata kama baba yake alikuwa natafuta kumuua Daudi. Na miaka mingi kisha Yonatani kufa, Daudi aliendelea pia kuonyesha Mefibosheti, mutoto wa Yonatani, upendo mushikamanifu.​—1 Sa. 20:9, 14, 15; 2 Sa. 4:4; 8:15; 9:1, 6, 7.

8 Tunaweza kujifunza mambo mingi kuhusu upendo mushikamanifu kwa kuchunguza maandiko fulani yenye kuwa mu kitabu ya Rutu. Watu wenye kuzungumuziwa mu kitabu ya Rutu wanaweza kutufundisha nini kuhusu upendo mushikamanifu? Namna gani tunaweza kutumikisha ile mambo mu kutaniko? *

KITABU YA RUTU INAWEZA KUTUFUNDISHA NINI KUHUSU KUONYESHA UPENDO MUSHIKAMANIFU?

9. Juu ya nini Naomi aliwaza kama ni Yehova njo alikuwa namupinga?

9 Mu kitabu ya Rutu, tunapata historia ya Naomi, Rutu binti-mukwe wake, na Boazi, mwanaume mwenye alikuwa anamuogopa Mungu na mwenye alikuwa mutu wa familia ya bwana yake na Naomi. Juu njala iliingia mu Israeli, Naomi na bwana yake, na watoto wao wawili wanaume walihamia Moabu. Wakati walikuwa kule, bwana ya Naomi alikufa. Watoto wao wawili walioa, lakini jambo ya kuhuzunisha, nao pia walikufa. (Rut. 1:3-5; 2:1) Ile magumu yote, ilifanya Naomi aone sawa vile dunia imemugeukia. Alivunjika moyo sana, mupaka akawaza kama ni Yehova njo iko namupinga. Ona maneno yenye alisema kuhusu vile alikuwa anajisikia juu ya Mungu: “Mukono wa Yehova umenigeukia.” “Mweza-Yote amefanya maisha yangu yakuwe machungu sana.” Alisema pia hivi: “Ni Yehova ndiye alinipinga na Mweza-Yote ndiye aliniletea musiba.”​—Rut. 1:13, 20, 21.

10. Maneno ya buchungu ya Naomi, ilifanya Yehova atende namna gani?

10 Maneno ya buchungu ya Naomi, ilifanya Yehova atende namna gani? Ile haikufanya ageuzie Naomi mugongo. Lakini alijitia pa nafasi yake na kumuelewa. Yehova anajua kama “kukandamizwa kunaweza kumufanya mutu mwenye hekima akuwe wazimu.” (Muh. 7:7) Lakini, juu Naomi aelewe kama Yehova alikuwa angali naye, alipaswa kusaidiwa. Mungu alimusaidia namna gani? (1 Sa. 2:8) Alichochea Rutu amuonyeshe upendo mushikamanifu. Rutu alisaidia mama-mukwe wake kwa upendo na mu njia ya muzuri ili asimame tena na aelewe kama Yehova alikuwa angali anamupenda. Mufano wa Rutu unatufundisha nini?

11. Juu ya nini ndugu na dada wanafanyaka yao yote ili kusaidia wenye kuwa na huzuni ao wenye kuvunjika moyo?

11 Upendo mushikamanifu unatusukuma kusaidia wenye kuvunjika moyo. Rutu alishikamana na Naomi. Leo pia, kuko ndugu na dada wenye wanafanyaka yao yote ili kusaidia wengine mu kutaniko wenye kuwa na huzuni ao wenye kuvunjika moyo. Wanapenda ndugu na dada zao, na njo maana wanafanyaka yote yenye wanaweza ili kuwasaidia. (Mez. 12:25, malezo ya chini; 24:10) Ile inapatana na hii maneno ya mutume Paulo: “Museme kwa namna yenye kufariji wale wenye wameshuka moyo, musaidie wazaifu, mukuwe wavumilivu kwa watu wote.”​—1 Te. 5:14.

Tunaweza kusaidia ndugu ao dada mwenye kuvunjika moyo kwa kumusikiliza (Ona fungu ya 12)

12. Mara mingi, ni njia gani njo ya muzuri zaidi ya kusaidia ndugu ao dada mwenye kuvunjika moyo?

12 Mara mingi, njia ya muzuri zaidi yenye unaweza kutumia ili kusaidia ndugu ao dada mwenye kuvunjika moyo, ni kumusikiliza kabisa na kumuhakikishia kama unamupenda. Yehova anafurahiaka wakati anaona vile unasikiliza kwa uangalifu kondoo wake wenye anaona kuwa wa maana. (Zb. 41:1) Mezali 19:17 inasema hivi: “Mwenye anaonyesha mutu wa hali ya chini wema anamukopesha Yehova, na Yeye atamulipa kwa sababu ya mambo yenye anatenda.”

Rutu anaamua kushikamana na Naomi mama yake mukwe, Orpa anaamua kurudia Moabu. Rutu anamuambia Naomi hivi: “Kwenye utaenda nitaenda.” (Ona fungu ya 13)

13. Ni maamuzi gani tofauti yenye Rutu na Orpa walikamata, na juu ya nini tunaweza kusema kama uamuzi wa Rutu ulikuwa tendo ya upendo mushikamanifu? (Ona picha kwenye jalada.)

13 Jambo yenye inatusaidia kuelewa tena muzuri zaidi maana ya upendo mushikamanifu, ni kuchunguza mambo yenye ilimufikia Naomi kisha kifo ya bwana yake na ya watoto wake wawili. Wakati Naomi alijua kama “Yehova alikuwa amegeuzia watu wake uangalifu kwa kuwapatia chakula,” aliamua kurudia kwenye alitokaka. (Rut. 1:6) Alianza safari yake ya kurudia pamoja na mabinti-wakwe wake. Lakini wakati walikuwa mu njia, aliwaomba mara tatu warudie Moabu. Ni mambo gani ilitokea? Tunasoma hivi: “Orpa akamubusu mama-mukwe wake na kuondoka. Lakini Rutu akashikamana naye.” (Rut. 1:7-14) Orpa alichagua kufuata mambo yenye Naomi aliwaambia, na akarudia Moabu. Lakini Rutu yeye, hakufuata maneno ya mama-mukwe wake, alifanya zaidi ya ile. Naye pia alikuwa huru kurudia, lakini juu alipenda kushikamana sana na Naomi hakupenda kumuacha. (Rut. 1:16, 17) Rutu aliamua kushikamana na Naomi, hapana juu alilazimika kufanya vile, lakini ni juu alipenda. Ile tendo Rutu alifanya njo upendo mushikamanifu. Hii habari inatufundisha nini?

14. (a) Leo, ndugu na dada wengi wameamua kufanya nini? (b) Kulingana na Waebrania 13:16, Mungu anapendezwaka na zabihu za namna gani?

14 Upendo mushikamanifu unaenda zaidi ya ile yenye inatazamiwa. Sawa tu vile zamani, leo pia kuko ndugu na dada wengi, wenye wako naonyesha upendo mushikamanifu kwa waamini wenzao, hata kwa wale wenye hawayaonanaka nao. Kwa mufano, wakati tu wanapata habari kama mu eneo fulani mulitokea musiba wa asili, wanapendaka palepale kujua namna wanaweza kusaidia. Wakati mutu fulani mu kutaniko anakuwa na magumu ya kupata makuta, wanajikazaka kujua mambo yenye iko nayo lazima, na kumusaidia. Sawa vile Wamakedonia wa wakati wa mitume, wanafanya zaidi ya ile yenye inatazamiwa. Wanajitolea kabisa, wanatoa wakati na mali yao ‘hata kupita uwezo wao’ ili kusaidia ndugu wenye wako mu magumu. (2 Ko. 8:3) Yehova anafurahiaka sana wakati anaona namna wako naonyesha upendo mushikamanifu!​—Soma Waebrania 13:16.

TUNAWEZA KUFANYA NINI LEO ILI KUONYESHA UPENDO MUSHIKAMANIFU?

15-16. Rutu alifanya nini hata kama Naomi alikuwa alishakatala kuenda naye?

15 Kuko mambo mingi ya muzuri yenye tunaweza kujifunza, wakati tunachunguza namna Rutu alimusaidia Naomi. Tuzungumuzie mambo fulani.

16 Usiache. Wakati Rutu aliamua kuenda Yuda pamoja na mama-mukwe wake Naomi, ku mwanzo Naomi alikatala. Lakini Rutu hakuachia pale. Mambo ilikuwa namna gani? “Wakati Naomi aliona kwamba Rutu anakazana kumufuata, akaacha kumusadikisha arudie.”​—Rut. 1:15-18.

17. Nini njo itatusaidia tusiache haraka-haraka kusaidia ndugu zetu?

17 Mambo yenye tunajifunza: Inaomba uvumilivu ili kusaidia watu wenye kuwa na huzuni na wenye kuvunjika moyo. Njo maana hatupaswe kuacha haraka-haraka kuwasaidia. Ku mwanzo, dada mwenye kuwa mu uhitaji anaweza kukatala tumusaidie. * Lakini, upendo mushikamanifu utatusukuma kufanya yote yenye tunaweza juu ya kushikamana naye. (Gal. 6:2) Tunatumaini kama siku moja atafikia kukubali tumusaidie na kumufariji.

18. Ni nini ingefanya Rutu aumie sana?

18 Usikasirike. Wakati Naomi na Rutu walifika Betlehemu, Naomi alionana tena na majirani wake wa zamani. Aliwaambia hivi: “Nilikuwa nimejaa wakati nilienda, lakini Yehova amenifanya nirudie nikiwa mikono wazi.” (Rut. 1:21) Unawaza Rutu alijisikia namna gani kisha kusikia ile maneno ya Naomi? Kumbuka, Rutu alikubali kuacha mambo yote nyuma juu ya kumusaidia Naomi. Rutu alilia pamoja naye, alimufariji, na alitembea naye masiku mingi. Hata kama alifanya ile yote, Naomi alisema hivi: “Yehova amenifanya nirudie nikiwa mikono wazi.” Hata kama Rutu alishikamana na Naomi, maneno ya Naomi inaonyesha kama, hakuona musaada wenye Rutu alimutolea kuwa wa maana. Pengine ile maneno ingefanya Rutu aumie sana! Hata vile, aliendelea tu kushikamana na Naomi.

19. Ni nini itatusaidia tushikamane na mutu mwenye kuvunjika moyo?

19 Mambo yenye tunajifunza: Leo, tunaweza kufanya yetu yote ili kusaidia dada mwenye kuvunjika moyo. Hata vile, inawezekana ku mwanzo aseme maneno yenye inaweza kutuumiza. Kama ile inatokea, tusikasirike. Tuendelee tu kushikamana na dada yetu mwenye iko na lazima ya musaada, na tumuombe Yehova atusaidie ili tujue namna ya kumufariji.​—Mez. 17:17.

Wazee Wakristo leo, wanaweza kufanya nini ili kumuiga Boazi? (Ona fungu ya 20-21)

20. Ni nini ilifanya Rutu aendelee kusaidia Naomi?

20 Utie wengine moyo kwa wakati wenye kufaa. Hata kama Rutu alionyesha Naomi upendo mushikamanifu, naye pia alikuwa na lazima ya kutiwa moyo. Yehova alitumia Boazi ili kumutia moyo. Boazi alimuambia Rutu hivi: “Yehova akupatie zawabu kwa sababu ya mambo yenye ulifanya, na upate malipo kamili kutoka kwa Yehova Mungu wa Israeli, mwenye umekuja kutafuta ulinzi chini ya mabawa yake.” Ile maneno ilimugusa sana Rutu. Rutu alimuambia hivi Boazi: “Umenifariji na kusema na mutumishi wako kwa njia yenye kutuliza.” (Rut. 2:12, 13) Boazi aliambia Rutu ile maneno kwa wakati wenye kufaa, na ile ilifanya Rutu aendelee kumusaidia Naomi.

21. Andiko ya Isaya 32:1, 2, inasema nini juu ya wazee wenye upendo?

21 Mambo yenye tunajifunza: Wenye wanaonyesha wengine upendo mushikamanifu, nao wanakuwaka na lazima ya kutiwa moyo wakati fulani. Boazi alimupongeza sana Rutu juu ya mambo ya muzuri yenye alitendea Naomi. Leo pia, wazee wanapongeza ndugu na dada, wakati wanaona mambo ya muzuri yenye wanatendea wengine mu kutaniko. Wakati wanawapongeza kwa moyo wao wote na kwa wakati wenye kufaa, ile inapatia ndugu na dada nguvu ya kuendelea kufanya vile.​—Soma Isaya 32:1, 2.

WALE WENYE WANAONYESHA UPENDO MUSHIKAMANIFU WANAPATA BARAKA GANI?

22-23. Ni nini inaonyesha kama Naomi alibadilika, na ni nini ilifanya abadilike? (Zaburi 136:23, 26)

22 Kisha masiku fulani kupita, Boazi alionyeshaka ukarimu Rutu na Naomi kwa kuwapatia chakula. (Rut. 2:14-18) Naomi alifanya nini kisha kuona matendo ya ukarimu ya Boazi? Alisema hivi: “Mutu huyo abarikiwe na Yehova, mwenye hajakosa kuonyesha upendo mushikamanifu kwa wazima na wafu.” (Rut. 2:20a) Naomi alikuwa amebadilika kabisa! Ku mwanzo, alisemaka hivi na iko nalia: “Yehova . . . alinipinga,” lakini sasa iko na furaha na anasema hivi: “Yehova . . . hajakosa kuonyesha upendo mushikamanifu.” Ni nini ilifanya Naomi abadilike?

23 Naomi alifikia kuelewa kama Yehova alikuwa angali naye. Yehova alitumia Rutu ategemeze Naomi mu safari ya kurudia Yuda. (Rut. 1:16) Naomi pia aliona mukono wa Yehova wakati Boazi, mumoja wa “wakombozi” wao, aliwaonyesha wote wawili ukarimu. * (Rut. 2:19, 20b) Pengine Naomi aliwaza hivi: ‘Sasa naelewa, kumbe Yehova hayaniachaka hata siku moja. Amekuwa na miye mu hii wakati yote!’ (Soma Zaburi 136:23, 26.) Kusema kweli, inaonekana Naomi alikuwa mwenye shukurani sana kuona vile Rutu na Boazi hawakumuacha hata kidogo. Tunaweza kusema kama wote watatu walifurahi kuona vile naomi alikuwa na furaha tena, na nguvu ya kumutumikia Yehova.

24. Juu ya nini tunapaswa kuonyesha waamini wenzetu upendo mushikamanifu?

24 Habari yenye kuwa mu kitabu ya Rutu, imetufundisha nini kuhusu upendo mushikamanifu? Upendo mushikamanifu unatusukuma tusiache haraka-haraka ndugu na dada zetu wenye kuvunjika moyo. Unatusukuma pia kufanya zaidi ya ile yenye inatazamiwa juu ya kuwasaidia. Wazee wanapaswa kutia moyo wale wote wenye wako wanajikaza kuonyesha wengine mu kutaniko upendo mushikamanifu, na wanapaswa kufanya vile kwa moyo wote na kwa wakati wenye kufaa. Tunakuwa wenye furaha sana, wakati tunaona wale wenye walikuwa na lazima ya musaada, wanakuwa na furaha na nguvu tena ya kumutumikia Yehova. (Mdo. 20:35) Lakini, sababu kubwa yenye inafanya tuendelee kuonyesha upendo mushikamanifu ni nini? Ni juu tunapenda kuiga na kufurahisha Yehova, “mwenye upendo mwingi mushikamanifu.”​—Kut. 34:6; Zb. 33:22.

WIMBO 130 Tusameheane

^ Yehova anapenda tuonyeshe ndugu na dada zetu mu kutaniko upendo mushikamanifu. Jambo yenye inaweza kutusaidia tuelewe muzuri kabisa maana ya upendo mushikamanifu, ni kuchunguza namna watumishi wa Mungu wa zamani walionyesha ile sifa. Mu hii habari, tutajifunza mambo fulani juu ya mufano wa Rutu, Naomi, na Boazi.

^ Juu ufaidike kabisa na hii habari, tunakutia moyo kujisomea Rutu sura ya 1 na ya 2.

^ Juu tuko nazungumuzia habari ya Naomi, njo maana tunasema dada wenye kuwa mu uhitaji. Lakini hii habari inahusu pia ndugu.

^ Ili kupata habari zaidi juu ya daraka ya Boazi ya kuwa mukombozi, ona habari “Uige Imani Yao​—‘Mwanamuke Bora Sana,’” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Tarehe 1 Mwezi wa 10, 2012, uku. 20.