Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 44

Upendo Mushikamanifu wa Yehova Uko na Faida Gani Kwako?

Upendo Mushikamanifu wa Yehova Uko na Faida Gani Kwako?

‘Upendo mushikamanifu wa [Yehova] unadumu milele.’​—ZB. 136:1.

WIMBO 108 Mungu Iko na Upendo Mushikamanifu

KIFUPI YA HABARI *

1. Yehova anatutia moyo tufanye nini?

 YEHOVA anapendezwa na upendo mushikamanifu. (Ho. 6:6) Njo maana anatia moyo watumishi wake wafanye pia vile. Kupitia nabii Mika, Mungu wetu anatuomba “tupende upendo mushikamanifu.” (Mik. 6:8, maelezo ya chini) Lakini, juu tuweze kufanya vile, inaomba tuelewe kwanza maana ya upendo mushikamanifu.

2. Upendo mushikamanifu njo nini?

2 Upendo mushikamanifu njo nini? Maneno “upendo mushikamanifu” inapatikana mara 230 hivi mu Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Upendo mushikamanifu njo nini? Kulingana na “Maana ya Maneno ya Biblia” yenye kuwa mu hii tafsiri, upendo mushikamanifu ni “upendo wenye kuchochewa na kujitoa, uaminifu-mushikamanifu, ushikamanifu, na kuambatana sana. Mara nyingi usemi huu unatumiwa ili kuzungumuzia upendo wa Mungu kwa wanadamu, lakini pia upendo wenye wanadamu wanaweza kuonyeshana.” Mu mambo ya kuonyesha upendo mushikamanifu, Yehova njo wa kwanza. Mu hii habari, tutazungumuzia namna Yehova anaonyesha upendo mushikamanifu kwa wanadamu. Mu habari yenye kufuata, tutazungumuzia namna siye watumishi wa Yehova Mungu, tunaweza kumuiga kwa kuonyeshana upendo mushikamanifu.

YEHOVA NI MWENYE “UPENDO MWINGI MUSHIKAMANIFU”

3. Namna gani Yehova alijifunua mbele ya Musa?

3 Wakati mufupi kisha Waisraeli kutoka Misri, Yehova alijifunua mbele ya Musa kwa kumuambia jina yake na sifa zake. Alimuambia hivi: “Yehova, Yehova, Mungu mwenye rehema na huruma, hakasirike haraka na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu na kweli, mwenye kuonyesha upendo mushimamanifu kwa maelfu, mwenye kusamehe kosa na uovu na zambi.” (Kut. 34:6, 7) Mu hii maneno, Yehova alimuambia Musa jambo fulani ya pekee kuhusu upendo wake mushikamanifu. Ni jambo gani?

4-5. (a) Yehova alisema nini kuhusu upendo wake mushikamanifu? (b) Tutazungumuzia maulizo gani?

4 Yehova haseme tu kama ni mwenye upendo mushikamanifu, lakini anasema kama ni “mwenye upendo mwingi mushikamanifu.” Maneno “upendo mwingi mushikamanifu” inapatikana mara mingi mu Biblia. (Hes. 14:18; Ne. 9:17; Zb. 86:15; 103:8; Yoe. 2:13; Yon. 4:2) Kila fasi kwenye inatumiwa, inamuhusu Yehova hapana wanadamu. Hauone kama ni jambo ya kufurahisha sana kuona vile Yehova yeye mwenyewe anakazia sifa yake ya upendo mushikamanifu? Kwa kweli, anapendezwa na upendo mushikamanifu. * Njo maana Mufalme Daudi alisema hivi: “Ee Yehova, upendo wako mushikamanifu unafika mupaka mbinguni . . . Upendo wako mushikamanifu ni wenye samani sana, Ee Mungu! Katika kivuli cha mabawa yako, wana wa binadamu wanakimbilia.” (Zb. 36:5, 7) Sawa vile Daudi, na siye tunapendezwa na upendo mushikamanifu wa Mungu?

5 Ili tuelewe kabisa maana ya upendo mushikamanifu, tuzungumuzie maulizo mbili: Yehova anaonyesha nani upendo mushikamanifu? Matendo ya Yehova ya upendo mushikamanifu inatuletea faida gani?

YEHOVA ANAONYESHA NANI UPENDO MUSHIKAMANIFU?

6. Yehova anaonyesha nani upendo mushikamanifu?

6 Yehova anaonyesha nani upendo mushikamanifu? Biblia inataja mambo mingi yenye tunaweza kupenda, sawa vile “kilimo,” “divai na mafuta,” “nizamu,” “ujuzi,” “hekima,” na mambo ingine. (2 Ny. 26:10; Mez. 12:1; 21:17; 29:3) Upendo mushikamanifu haionyeshwake vitu; ni watu tu njo wanaweza kuonyeshwa ile upendo. Lakini, haiko kila mutu njo Yehova anaonyeshaka upendo mushikamanifu. Anaonyeshaka tu ile upendo kwa wale wenye kuwa na urafiki wa pekee pamoja naye. Mungu wetu ni muaminifu kwa marafiki wake. Atawafanyia mambo ya muzuri sana, na ataendelea kuwapenda.

Yehova anapatia watu wote mambo ya muzuri, hata wale wenye hawamuabudu (Ona fungu ya 7) *

7. Yehova alifanya nini ili kuonyesha kama anapenda watu wote?

7 Yehova alionyesha kama anapenda watu wote. Yesu aliambia hivi, mwanaume mwenye kuitwa Nikodemu: “Mungu alipenda ulimwengu [wa watu] sana, na hivi akamutoa mwana wake muzaliwa wa pekee, ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.”​—Yoh. 3:1, 16; Mt. 5:44, 45.

Kulingana na maneno yenye Mufalme Daudi na nabii Danieli walisema, Yehova anaonyeshaka watumishi wake upendo mushikamanifu juu wanamujua, wanamuogopa, wanamupenda, na wanashika amri zake (Ona fungu ya 8-9)

8-9. (a) Juu ya nini Yehova anaonyeshaka watumishi wake upendo mushikamanifu? (b) Tutazungumuzia nini?

8 Lakini sawa vile tuliona, Yehova anaonyeshaka upendo wake mushikamanifu kwa wale tu wenye kuwa na urafiki wa karibu pamoja naye, ni kusema, watumishi wake. Maneno yenye Mufalme Daudi na nabii Danieli walisema, inahakikisha ile. Kwa mufano, Daudi alisema: “Endelea kuonyesha upendo wako mushikamanifu kwa wale wenye kukujua.” “Upendo mushikamanifu wa Yehova ni wa umilele wote kuelekea wale wenye kumuogopa.” Na Danieli alisema hivi: “Ee Yehova Mungu wa kweli, [mwenye] kuonyesha upendo mushikamanifu kwa wale wenye wanamupenda na kushika amri zake.” (Zb. 36:10; 103:17; Da. 9:4) Hii maneno yenye iliongozwa na roho, inatusaidia kuelewa kama Yehova anaonyeshaka watumishi wake upendo mushikamanifu juu wanamujua, wanamuogopa, wanamupenda, na wanashika amri zake. Yehova anaonyeshaka watu wake upendo wake mushikamanifu, ni kusema, waabudu wake wa kweli.

9 Mbele tuanze kumutumikia Yehova Mungu, alikuwa anatupenda sawa vile tu anapendaka watu wote. (Zb. 104:14) Lakini sasa, juu tuko waabudu wake, tuko nafaidika pia na upendo wake mushikamanifu. Yehova anahakikishia hivi kila mutumishi wake: “Upendo wangu mushikamanifu hautaondolewa kwako.” (Isa. 54:10) Kwa kweli, sawa vile Daudi alijionea, “Yehova atamutendea mushikamanifu wake kwa njia ya pekee.” (Zb. 4:3) Vile tunajua kama Yehova anatuhangaikia, tunapaswa kufanya nini? Muandikaji wa zaburi alisema hivi: “Mutu yeyote mwenye kuwa na hekima atachunguza mambo hayo na atafikiria kwa uangalifu matendo ya Yehova ya upendo mushikamanifu.” (Zb. 107:43) Tuchunge ile mawazo mu akili, wakati tuko nazungumuzia namna Yehova anaonyeshaka watumishi wake upendo mushikamanifu mu njia tatu, na namna ile inawaletea faida.

MATENDO YA YEHOVA YA UPENDO MUSHIKAMANIFU INATULETEA FAIDA GANI?

Yehova anaongezea waabudu wake mambo ingine ya muzuri (Ona fungu ya 10-16) *

10. Kujua kama upendo mushikamanifu wa Mungu unadumu milele, kunatuletea faida gani? (Zaburi 31:7)

10 Upendo mushikamanifu wa Mungu unadumu milele. Maneno “unadumu milele” inatajwa mara 26 mu Zaburi ya 136. Tunasoma hivi mu mustari wa kwanza: “Mumushukuru Yehova, kwa maana ni mwema; upendo wake mushikamanifu unadumu milele.” (Zb. 136:1) Mu mustari wa 2 mupaka 26, muko hii refree “kwa maana, upendo wake mushikamanifu unadumu milele.” Wakati tunasoma mistari yenye kubakia ya hii zaburi, tunashangaa kuona namna Yehova anaendelea kuonyesha upendo wake mushikamanifu mu njia mingi. Refree yenye inasema “kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele” inatuhakikishia kama, upendo wenye Mungu iko nao kwa watumishi wake hauwezi kubadilika. Inatia moyo kujua kama Yehova hatupake watumishi wake mbiombio! Lakini, akishapenda mutumishi wake, anashikamanaka naye sana, zaidi sana mu wakati wa taabu. Faida yenye tunapata: Kujua kama Yehova iko nashikamana na siye, kunatufurahisha na kunatupatia nguvu ya kupambana na taabu, na ya kuendelea kumutumikia.​—Soma Zaburi 31:7.

11. Kulingana na Zaburi ya 86:5, nini njo inamusukumaka Yehova asamehe?

11 Upendo mushikamanifu wa Mungu unamusukuma asamehe. Wakati Yehova anaona kama mutenda-zambi anatubu na anaachana kabisa na njia yake ya zambi, upendo wake mushikamanifu unamusukuma amusamehe. Daudi, muandikaji wa zaburi, alisema hivi kuhusu Yehova: “Hajatutendea kulingana na zambi zetu, wala hajatulipa malipo yenye makosa yetu yanastahili.” (Zb. 103:8-11) Mambo ya mubaya yenye ilimufikia Daudi, ilimusaidia aelewe vile zamiri inasumbuaka mutu kisha kufanya zambi. Lakini, alijifunza pia kama Yehova iko “tayari kusamehe.” Nini njo inasukumaka Yehova asamehe? Jibu iko mu Zaburi 86:5. (Soma.) Ndiyo, sawa vile Daudi alisema mu sala yake, Yehova anasamehe juu ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu kwa wale wenye wanamuitia.

12-13. Nini njo itatusaidia kama tuko najilaumu juu ya makosa yenye tulifanyaka zamani?

12 Kama tunafanya zambi, haiko mubaya kuihuzunikia, na ni muzuri mutu ajisikie vile. Juu ya nini? Ile inaweza kutusukuma tutubu na kukamata hatua fulani ili kurekebisha makosa yetu. Hata vile, kuko watumishi fulani wa Mungu wenye hawayaachaka kujilaumu juu ya makosa yenye walifanyaka zamani. Wanawaza kama Yehova hatawasameheaka hata kama walishatubu na kuachana na njia yao ya mubaya. Kama vile njo unajisikiaka, kujifunza kama Mungu anapenda kabisa kuonyesha watumishi wake upendo mushikamanifu kutakusaidia.

13 Faida yenye tunapata: Hata kama hatukamilike, tunaweza kumutumikia Yehova kwa furaha na zamiri safi. Ile inawezekana juu “damu ya Yesu mwana wake inatusafisha kutoka katika zambi yote.” (1 Yo. 1:7) Kama unavunjika moyo juu ya makosa fulani yenye ulifanya, ukumbuke kama Yehova anapenda, ndiyo, anapenda kabisa kusamehe mutenda-zambi mwenye kutubu. Daudi alizungumuzia uhusiano fulani wenye kuwa kati ya upendo mushikamanifu na musamaha. Aliandika hivi: “Kama vile mbingu ziko juu kuliko dunia, ni vile upendo wake mushikamanifu uko mwingi kuelekea wale wenye kumuogopa. Kama vile mahali jua linatokea kuko mbali sana na mahali jua linashukia, ni vile ametia zambi zetu mbali sana na sisi.” (Zb. 103:11, 12) Kusema kweli, Yehova iko tayari “kusamehe kwa njia kubwa.”​—Isa. 55:7.

14. Daudi alitumia maneno gani ili kuonyesha namna upendo mushikamanifu wa Mungu unatulinda?

14 Upendo mushikamanifu wa Mungu unatulinda kiroho. Daudi alimuambia Yehova hivi mu sala: “Wewe ni mahali pangu pa kujificha; utanilinda nisipatwe na taabu. Utanizunguka kwa vigelegele vya shangwe ya ukombozi. . . . Mwenye kumutegemea Yehova amezungukwa na upendo wake mushikamanifu.” (Zb. 32:7, 10) Sawa vile zamani kuta zenye zilizunguka muji zilikuwa zinalinda wakaaji wake, vilevile matendo ya Yehova ya upendo mushikamanifu inatuzunguka sawa vile ukuta, ni kusema, inatulinda na mambo yote yenye inaweza kufanya tusiendelee kuwa waaminifu. Zaidi ya ile, upendo mushikamanifu wa Yehova, unamusukuma atuvute kwake.​—Yer. 31:3.

15. Namna gani kimbilio na ngome vinapatana na upendo mushikamanifu wa Yehova?

15 Daudi alitumia maneno ingine ya mufano, ili kuonyesha namna Mungu analindaka watu wake. Alisema hivi: “Mungu ni kimbilio langu salama, Mungu mwenye kunionyesha upendo mushikamanifu.” Tena Daudi alisema hivi kuhusu Yehova: “Yeye ni upendo wangu mushikamanifu na ngome yangu, kimbilio langu salama na mwokozi wangu, ngao yangu na ule mwenye nimejificha ndani yake.” (Zb. 59:17; 144:2) Juu ya nini Daudi alisema kama upendo mushikamanifu wa Yehova uko sawa vile kimbilio na ngome? Ni juu, hata kama tunaishi wapi mu hii dunia, tukiendelea tu kuwa watumishi wake, Yehova atatulinda kabisa ili tuendelee kuwa na urafiki wa muzuri pamoja naye. Andiko ya Zaburi 91 inatuhakikishia pia vile. Muandikaji wa hii Zaburi alisema hivi: “Nitamuambia Yehova: ‘Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu.’” (Zb. 91:1-3, 9, 14) Musa alitumia neno ya mufano yenye kufanana na ile ili kuzungumuzia kimbilio. (Zb. 90:1, maelezo ya chini) Tena, wakati alikaribia kufa, Musa alitumia maneno ingine ya kufanana na ile yenye kutia moyo sana. Aliandika hivi: “Mungu ni kimbilio tangu nyakati za zamani, mikono yake ya milele iko chini yako.” (Kum. 33:27) Maneno “mikono yake ya milele iko chini yako” inatufundisha nini juu ya Yehova?

16. Yehova atatusaidia mu njia gani mbili? (Zaburi 136:23)

16 Wakati tunakumbuka kama Yehova ni kimbilio yetu, ile inafanya tujisikie salama. Lakini wakati fulani, tunaweza kuvunjika moyo na kukosa ya kufanya. Kama ile inatufikia, namna gani Yehova atatusaidia? (Soma Zaburi 136:23.) Ataweka mikono yake chini yetu, ni kusema, atatuinua, na atatusaidia ili tusiendelee kuvunjika moyo. (Zb. 28:9; 94:18) Faida yenye tunapata: Kujua kama tunaweza kumutegemea Yehova kila mara, kunatuhakikishia kama atatusaidia mu njia mbili. Njia ya kwanza, hata tuishi wapi Yehova atatulinda. Njia ya pili, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, atatuhangaikia kabisa.

TUKO HAKIKA KAMA YEHOVA ATAENDELEA KUTUONYESHA UPENDO MUSHIKAMANIFU

17. Vile Mungu ni mwenye upendo mushikamanifu, tuko hakika kama atafanya nini? (Zaburi 33:18-22)

17 Hii habari imetusaidia kuelewa kama Yehova atatusaidia ili tuendelee kuwa waaminifu kwake wakati tunapata majaribu. (2 Ko. 4:7-9) Nabii Yeremia alisema hivi: “Ni kwa sababu ya upendo mushikamanifu wa Yehova ndiyo maana hatukuisha, kwa maana hakuna siku rehema zake zitafikia mwisho.” (Omb. 3:22) Kulingana na vile muandikaji wa zaburi alisema, tuko hakika kama Yehova ataendelea kutuonyesha upendo mushikamanifu. Alisema hivi: “Jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa, wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu.”​—Soma Zaburi 33:18-22.

18-19. (a) Tutachunga nini mu akili? (b) Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

18 Tutachunga nini mu akili? Mbele tuanze kumutumikia Yehova Mungu, alikuwa anatupenda sawa vile tu anapendaka watu wote. Lakini sasa juu tuko waabudu wake, tuko nafaidika pia na upendo wake mushikamanifu. Ile upendo, njo inamusukuma atuweke mu mikono yake ili kutulinda. Ataendelea kuwa karibu na siye na atatimiza ahadi zake zote kwa ajili yetu. Anapenda tukuwe marafiki wake milele! (Zb. 46:1, 2, 7) Kwa hiyo, hata tupate jaribu gani, tukuwe hakika kama Yehova atatupatia nguvu, ili tuendelee kuwa waaminifu kwake.

19 Tumejifunza namna Yehova anaonyeshaka watumishi wake upendo mushikamanifu. Njo maana, anatuomba na siye tuonyeshane upendo mushikamanifu. Tunaweza kufanya vile namna gani? Tutazungumuzia ile mu habari yenye kufuata.

WIMBO 136 Yehova Atakupatia “Malipo Kamili”

^ Upendo mushikamanifu njo nini? Yehova anaonyesha nani upendo mushikamanifu, na wenye wanaonyeshwa ile upendo mushikamanifu, wanapata faida gani? Tutapata majibu ya hii maulizo mu hii habari. Hii habari na habari yenye kufuata, zitazungumuzia ile sifa ya maana.

^ Wazo ya upendo mwingi mushikamanifu wa Mungu inapatikana pia mu maandiko ingine ya Biblia.​—Ona Nehemia 13:22; Zaburi 69:13; 106:7; na Maombolezo 3:32.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Yehova anapenda watu wote, kutia ndani watumishi wake. Picha zenye kuwa juu ya kikundi ya watu, zinaonyesha njia mbalimbali zenye Mungu anatumia ili kuonyesha kama anatupenda. Njia kubwa zaidi, ni ile ya kumutuma Yesu juu akufe kwa ajili yetu.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Yehova anatendea mu njia ya pekee watumishi wake wenye kuwa na imani katika bei ya ukombozi yenye alitoa. Zaidi ya kupenda watumishi wake sawa vile anapenda watu wengine, Yehova anaonyesha pia watumishi wake upendo mushikamanifu. Mifano ya ile upendo mushikamanifu, inaonyeshwa mu picha.