Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 47

Utaendelea Kuwa na Imani ya Nguvu?

Utaendelea Kuwa na Imani ya Nguvu?

“Mioyo yenu isivurugike. Mukuwe na imani.”​—YOH. 14:1.

WIMBO 119 Tunapaswa Kuwa na Imani

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni ulizo gani yenye tunaweza kujiuliza?

 WAKATI unafikiriaka matukio ya wakati wenye kuja, ni kusema, kuharibiwa kwa dini ya uongo, shambulizi ya Gogu wa Magogu na vita ya Armagedoni, ile inakufanyaka uhangaike wakati fulani? Ulishakajiuliza, ‘Nitaendelea kubakia muaminifu wakati hii matukio ya kuogopesha itafika?’ Kama ni vile, maneno ya Yesu yenye kuwa mu andiko yetu ya musingi inaweza kukusaidia. Yesu aliambia hivi wanafunzi wake: “Mioyo yenu isivurugike. Mukuwe na imani.” (Yoh. 14:1) Imani ya nguvu itatusaidia kuvumilia magumu yoyote yenye inaweza kutokea wakati wenye kuja.

2. Tunaweza kufanya nini ili imani yetu ikuwe nguvu, na tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Jambo yenye inaweza kutusaidia kufanya imani yetu ikuwe nguvu ili kuvumilia magumu ya wakati wenye kuja, ni kufikiri juu ya namna tunatendaka wakati imani yetu inajaribiwa leo. Wakati tunafikiri juu ya ile, tunaweza kujua ni wapi inaomba kufanyia kazi juu imani yetu ikuwe nguvu. Kila jaribu yenye tunashinda inafanya imani ikuwe nguvu zaidi. Ile itatusaidia kuvumilia magumu ya wakati wenye kuja. Mu hii habari, tutazungumuzia majaribu ine yenye wanafunzi wa Yesu walipata yenye ilionyesha kama walikuwa na lazima ya imani zaidi. Kisha, tutaona ikiwa tunaweza kufanya nini wakati majaribu ya vile inatufikia leo, na tutaona namna inaweza kututayarisha ili kuvumilia magumu ya wakati wenye kuja.

IMANI KAMA MUNGU ATATIMIZA MAHITAJI YETU

Tunaweza kupambana na magumu ya kupata makuta, lakini imani itatusaidia tuendelee kukaza akili yetu juu ya faida za Ufalme (Ona fungu ya 3-6)

3. Kulingana na Matayo 6:30, 33 ni jambo gani Yesu alifasiria waziwazi kuhusu imani?

3 Ni jambo ya kawada kwa kichwa ya familia kutafutia bibi na watoto wake chakula ya kutosha, nguo na fasi ya kulala. Sikuzote haiko mwepesi kufanya vile mu hizi nyakati zenye kuwa nguvu. Wamoja kati ya waamini wenzetu wamepoteza kazi, na hata kama wako najikaza ili kupata kazi ingine hawaipate. Wengine wanakatala kazi fulani juu ni kazi yenye haifae kwa Wakristo. Mu zile hali zote, inaomba kuwa na imani ya nguvu kama Yehova ataendelea kutimiza mahitaji ya familia yetu. Yesu alihakikishia ile wanafunzi wake mu Mahubiri Yake ya ku Mulima. (Soma Matayo 6:30, 33.) Wakati tunaamini kabisa kuwa Yehova hawezi kutuacha, tutakaza akili yetu juu ya faida za Ufalme. Na wakati tunaona vile Yehova iko natutimizia mahitaji yetu ya kimwili, ile itafanya tumukaribie zaidi na itafanya imani yetu ikuwe nguvu.

4-5. Ni nini ilisaidia familia moja wakati ilikuwa nguvu kwao kupata mahitaji ya kimwili?

4 Tuone namna Yehova alisaidia familia moja mu Venezuela wakati ilihangaika sana juu ya kupata mahitaji yao ya kimwili. Zamani, familia ya Castro ilikuwaka na ferme, na ni mule njo walikuwa natumika ili kupata makuta. Lakini wanaume fulani wenye kuwa na bunduki waliwanyanganya ile ferme na kuwafukuza. Castro Miguel, baba wa familia, anasema hivi: “Leo, tunalimaka tu mu shamba fulani ya kidogo yenye tulijikopeshaka kwa mutu fulani. Kila siku nilikuwa namulilia Yehova juu atusaidie tupate yenye tuko nayo lazima kwa ajili ya ile siku.” Mu hii familia ya Castro maisha iko nguvu. Lakini, juu wako na imani kabisa ya kama Yehova iko na uwezo ya kuwapatia mahitaji yao ya kila siku, wote wanaendelea kukusanyika na kuhubiri kwa ukawaida. Juu wanaendelea kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza mu maisha yao, Yehova anaendelea kuwapatia mambo yenye wako nayo lazima.

5 Hata kama Miguel na Yurai bibi yake, wako napitia ile hali ya nguvu, wako nakaza akili juu ya namna Yehova iko nawahangaikia. Wakati fulani, Yehova alitumia ndugu na dada ili kuwapatia vitu vyenye walikuwa navyo lazima na ili kuwasaidia wapate kazi. Na wakati ingine, Yehova alitumia biro ya tawi ili kuwatolea misaada. Yehova hayawaachaka hata kidogo. Matokeo? Wote wako najionea vile imani yao iko naendelea kuwa nguvu. Kisha kufasiria mufano moja yenye kuonyesha vile Yehova aliwasaidia, Yoselin, mutoto wao mukubwa mwanamuke, anasema hivi: “Inatiaka moyo sana wakati unajionea waziwazi mukono wa Yehova. Yehova ni rafiki yangu, na niko hakika kama sikuzote atanisaidia.” Anaongezea hivi: “Majaribu yenye tumepata mu familia yetu, imetutayarisha kwa ajili ya majaribu ya nguvu zaidi ya wakati wenye kuja.”

6. Namna gani unaweza kufanya imani yako ikuwe nguvu wakati unapambana na magumu ya kupata makuta?

6 Uko napambana na magumu ya kupata makuta? Kama ni vile, uko mu kipindi ya nguvu. Lakini, ikuwe hali yako iko ya nguvu namna gani, unaweza kutumia ile nafasi ili kufanya imani yako ikuwe nguvu. Sali, kisha usome maneno ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 6:25-34 na uifikirie sana. Ufikirie mifano fulani ya mu siku zetu yenye inaonyesha namna Yehova iko naendelea kutimiza mahitaji ya wote wenye wanaendelea kufanya kazi yake kwa bidii. (1 Ko. 15:58) Kufanya vile, itakusaidia ukuwe hakika kama vile Baba yako wa mbinguni alisaidia wengine mu hali za vile na weye atakusaidia. Anajua muzuri mahitaji yako, na anajua namna ya kukupatia ayo. Wakati unajionea mukono wa Yehova mu maisha yako, ile itafanya imani yako ikuwe nguvu zaidi ili uweze kuvumilia magumu ya nguvu zaidi ya wakati wenye kuja.​—Hab. 3:17, 18.

IMANI YA KUVUMILIA “UPEPO MUKALI”

Imani ya nguvu inaweza kutusaidia kuvumilia upepo wowote mukali, ikuwe upepo halisi ao wa mufano (Ona fungu ya 7-11)

7. Kulingana na Matayo 8:23-26, namna gani “upepo mukali” ulijaribu imani ya wanafunzi?

7 Siku moja, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mu bahari, kisha upepo mukali ukatokea. Yesu alitumia ile tukio ili kufundisha wanafunzi wake waelewe kama walikuwa na lazima ya imani zaidi. (Soma Matayo 8:23-26.) Wakati upepo ulikuwa nguvu sana na kufanya maji ianze kuingia mu mashua, Yesu yeye alikuwa nalala. Wanafunzi wake waliogopa sana; kwa hiyo, walianza kumulamusha na kumuomba awaokoe. Lakini Bwana Yesu akawauliza hivi kwa upole: “Sababu gani munaogopa sana, ninyi wenye imani kidogo?” Wanafunzi walipaswa kuelewa kama Yehova alikuwa na uwezo wa kumulinda Yesu na wote wenye walikuwa naye. Tunajifunza nini? Imani ya nguvu inaweza kutusaidia kuvumilia upepo wowote mukali, ikuwe ni upepo halisi ao wa mufano.

8-9. Namna gani imani ya Anel ilijaribiwa, na ni nini ilimusaidia?

8 Tuzungumuzie mufano wa dada Anel. Ni dada mwenye hajaolewa mwenye kuishi Puerto Rico. Tuone namna gani jaribu yenye alivumilia ilifanya imani yake ikuwe nguvu. “Upepo mukali” wenye alipata, ulikuwa upepo halisi. Jaribu yake ilianza mu 2017 wakati upepo mukubwa wenye kuitwa Maria uliharibu nyumba yake. Na ile upepo ilifanya apoteze kazi yake. Anel anasema hivi: “Ilikuwa kipindi ya nguvu sana, na nilihangaika. Lakini, nilimutegemea Yehova kupitia sala, na sikuruhusu mahangaiko inizuie kufanya mambo ya lazima.”

9 Anel anasema kama jambo ingine yenye ilimusaidia kuvumilia, ni utiifu. Anasema hivi: “Kutii muongozo wenye tengenezo ilitoa kulinisaidia nibakie mwenye kutulia. Nilijionea vile Yehova alinisaidia kwa kunipatia musaada wa kiroho na wa kimwili kupitia ndugu na dada. Yehova alinipatia mambo mingi zaidi kupita yenye niliomba, na ile ilifanya imani yangu ikuwe nguvu zaidi.”

10. Unaweza kufanya nini kama uko napambana na “upepo mukali”?

10 Na weye uko napambana na ‘upepo fulani mukali’ mu maisha yako? Pengine uko nateseka juu ya musiba fulani wa asili. Ao pengine ni upepo wa mufano, sawa vile ugonjwa fulani wa nguvu wenye ulishakakufanya uvunjike moyo na haujue ufanye nini. Ni kweli, wakati fulani unaweza kuvunjika moyo, lakini, usiache ile ikuzuie kumutumainia Yehova. Umukaribie zaidi katika sala. Ufikiri sana juu ya mambo yenye Yehova alishakafanya ili kukusaidia. Ile itafanya imani yako ikuwe nguvu. (Zb. 77:11, 12) Ukuwe hakika kama, ikuwe leo ao kesho, Yehova hawezi kukuacha.

11. Juu ya nini tunapaswa kutii wale wenye kutuongoza?

11 Nini ingine inaweza kukusaidia kuvumilia majaribu? Kumbuka ile Anel alisema, utiifu. Ujikaze kutumainia watu wenye Yehova na Yesu wanatumainia. Wakati fulani wale wenye wamewekwa ili kutuongoza, wanaweza kutupatia muongozo fulani wenye tunaona kama hauko wa maana. Lakini, Yehova anabariki mutu mwenye kutii. Neno yake na mambo yenye watumishi wake waaminifu wamejionea, inatuonyesha wazi kama utiifu unaokoa uzima. (Kut. 14:1-4; 2 Ny. 20:17) Ufikiri sana juu ya mifano ya wale ndugu na dada. Kufanya vile, kutakuchochea kuazimia kufuata muongozo wa tengenezo ya Yehova, leo na wakati wenye kuja. (Ebr. 13:17) Na zaidi ya ile, hautaogopa tena upepo mukali, ni kusema, taabu kubwa yenye itatokea hivi karibuni.​—Mez. 3:25.

IMANI YA KUVUMILIA UKOSEFU WA HAKI

Kama tunaendelea kusali, imani yetu itakuwa nguvu (Ona fungu ya 12)

12. Kulingana na andiko ya Luka 18:1-8 kuko upatano gani kati ya kuwa na imani na kuvumilia ukosefu wa haki?

12 Yesu alijua kama ukosefu wa haki ungejaribu imani ya wanafunzi wake. Juu ya kuwasaidia wavumilie aliwapatia mufano wenye kuwa mu kitabu ya Luka. Yesu aliwaelezea historia ya mujane mumoja mwenye aliendelea kulilia muamuzi mumoja mwenye hakukuwa mwenye haki amupatie haki. Ule mujane alikuwa hakika kama akikazana atapata kile alikuwa natafuta. Na ni vile ilikuwa. Ule muamuzi alifikia kujibia ombi yake. Tunajifunza nini? Yehova ni Mungu mwenye haki. Njo maana Yesu alisema hivi: “Kwa hakika, je, Mungu hatahakikisha kuwa haki imefanywa kwa ajili ya wachaguliwa wake wenye wanamulilia muchana na usiku?” (Soma Luka 18:1-8.) Kisha aliongezea hivi: “Wakati Mwana wa binadamu atafika, je, kweli atapata imani hii katika dunia?” Wakati tunateseka juu hatukutendewa kwa haki, tunapaswa kuonyesha kama tuko na imani ya nguvu, sawa ya ule mujane, kwa kuendelea kuvumilia. Kama tunakuwa na imani ya vile, tunaweza kuwa hakika kabisa kama Yehova atatusaidia. Tunapaswa pia kuamini kama sala iko na nguvu. Wakati fulani, sala zetu zinaweza kujibiwa mu njia yenye hatukutazamia.

13. Namna gani sala ilisaidia familia moja yenye ilitendewa bila haki?

13 Tufikire mufano wa dada Vero, mwenye kuishi mu Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Wakati kijiji yao ilishambuliwa na maaskari, Vero na bwana yake mwenye haiko Shahidi, na mutoto yao mwanamuke wa miaka 15 walilazimika kukimbia. Wakati walikuwa nakimbia, walikuta maaskari wenye waliwasimamisha na kuanza kuwaogopesha kama watawaua. Wakati Vero alianza kulia, ule mutoto yao mwanamuke alianza kumutuliza kwa kusali kwa sauti kubwa na kurudulia tena na tena jina Yehova mu sala yake. Wakati alimaliza kusali, mukubwa wa wale maaskari alimuuliza hivi: “Wee mutoto, ni nani alikufundishaka kusali?” Alijibia hivi: “Ni mama yangu. Alinionyeshaka namna ya kusali kwa kutumia Matayo 6:9-13.” Kisha, ule mukubwa alisema hivi: “Mutoto, weye na wazazi wako muende kwa amani, na Yehova Mungu wenu awalinde!”

14. Ni nini inaweza kujaribu imani yetu, na ni nini itatusaidia kuvumilia?

14 Habari za vile zinatusaidia kuelewa kama hatupaswe kuzarau hata kidogo nguvu ya sala. Lakini, tuseme nini kama sala zako hazijibiwe haraka, ao hazijibiwe mu njia ya kushangaza? Sawa vile mujane mwenye Yesu alizungumuzia, uendelee kusali, na ukuwe hakika kama Mungu hawezi kukuacha hata kidogo, na ataendelea kujibia sala zako kwa wakati wenye kufaa na mu njia mbalimbali. Uendelee kumuomba Yehova akupatie roho yake takatifu. (Flp. 4:13) Ukumbuke kama hivi karibuni, Yehova atakubariki sana na utasahau magumu yote ya leo. Wakati unavumilia magumu yote kwa uaminifu kupitia nguvu yenye Yehova anakupatia, ile itakupatia nguvu ya kuvumilia magumu ya wakati wenye kuja.​—1 Pe. 1:6, 7.

IMANI YA KUPAMBANA NA VIZUIZI

15. Vile Matayo 17:19, 20 inasema, ni jaribu gani yenye wanafunzi wa Yesu walipata?

15 Yesu alifundisha wanafunzi wake kama imani itawasaidia kupambana na vizuizi. (Soma Matayo 17:19, 20.) Siku moja, walishindwaka kufukuza pepo muchafu, hata kama wakati fulani walikuwa nafanya vile. Shida ilikuwa wapi? Yesu alisema kama walikuwa na lazima ya imani zaidi. Yesu aliwaambia kama ikiwa wanakuwa na imani ya kutosha, ile ingeweza kuwasaidia kuvumilia majaribu yenye ilikuwa sawa vile mulima! Na siye pia leo, tunaweza kupata magumu yenye mu njia fulani inaonekana sawa vile inatuzuia kuendelea.

Tunaweza kufikiwa na mambo ya kutuhuzunisha, lakini imani itatusaidia tuendelee kuwa na mingi ya kufanya mu kazi ya Yehova (Ona fungu ya 16)

16. Namna gani imani ilimusaidia Geydi avumilie jaribu ya kifo ya bwana yake?

16 Tufikirie mufano wa dada Geydi, mwenye kuishi Guatemala. Edi bwana yake, walimuuaka wakati walikuwa natoka wote wawili ku mukutano. Imani ya Geydi ilimusaidia namna gani kuvumilia ile hali ya kuhuzunisha sana? Anasema hivi: “Niko namutupia Yehova muzigo wangu kupitia sala, na ile njo iko nafanya nikuwe na amani. Naona vile Yehova ananihangaikia kupitia familia yangu na marafiki wa mu kutaniko. Kukuwa na mambo mingi ya kufanya mu kazi ya Yehova, kunafanya nisiumie sana na kunanisaidia nisihangaike sana juu ya mambo ya kesho. Hii jaribu yenye nimepitia imenifundisha kama, hata jaribu ya namna gani itokee wakati wenye kuja, najua kama kupitia musaada wa Yehova, Yesu na tengenezo nitaweza kuivumilia.”

17. Tunaweza kufanya nini wakati tunapata magumu yenye iko sawa vile mulima?

17 Uko nalia mupendwa wako mwenye alikufa? Panga wakati ya kusoma habari za mu Biblia za watu wenye walifufuliwaka. Ile itafanya uamini kabisa kama kutakuwa ufufuo. Uko na huzuni juu mutu wa familia yako alitengwa? Ujifunze sana juu ukuwe hakika kama njia ya Yehova ya kutoa nizamu ni ya muzuri zaidi. Ikuwe uko napambana na magumu gani, uikamate kuwa nafasi ya kufanya imani yako ikuwe nguvu. Umuelezee Yehova waziwazi namna uko najisikia. Usijitenge, lakini ujikaze kuwa karibu na ndugu na dada zako. (Mez. 18:1) Ujikaze kufanya mambo mbalimbali yenye itakusaidia kuvumilia, hata kama wakati fulani unaweza kulia kisha kukumbuka mambo yenye ilikupata. (Zb. 126:5, 6) Usiache kukusanyika, kuhubiri, na kujifunza Biblia. Na uendelee kukaza akili juu ya baraka za muzuri zenye Yehova amekutayarishia. Wakati unaona vile Yehova anakusaidia, ile itafanya imani yako katika yeye ikuwe nguvu zaidi.

“UTUPATIE IMANI ZAIDI”

18. Unaweza kufanya nini ikiwa unaona kama imani yako imeregea kidogo?

18 Kama majaribu yako, ikuwe ya zamani ao ya sasa, imefanya imani yako iregee kidogo, usivunjike moyo. Kuliko kuvunjika moyo, uone ile kuwa nafasi ya kufanya imani yako ikuwe nguvu. Na weye, sawa vile mitume wa Yesu walifanyaka, uombe hivi: ‘Unipatie imani zaidi.’ (Lu. 17:5) Zaidi ya ile, fikiri sana juu ya mifano yenye tumezungumuzia mu hii habari. Sawa vile Miguel na Yurai, ukumbuke mambo yote yenye Yehova alifanya na yenye iko nafanya ili kukusaidia. Sawa mutoto mwanamuke wa Vero na Anel, ukuwe nasali kwa Yehova bila kuacha, zaidi sana wakati uko mu jaribu ya nguvu. Na sawa vile Geydi, uelewe kama Yehova anaweza kukusaidia kupitia familia ao marafiki. Wakati unamuacha Yehova akusaidie kuvumilia magumu ya sasa, ile itafanya ukuwe hakika kama atakusaidia kuvumilia magumu yoyote ya wakati wenye kuja.

19. Yesu alikuwa hakika na mambo gani, na weye unaweza kuwa hakika na nini?

19 Yesu alisaidia wanafunzi wake waone fasi kwenye walikuwa na lazima ya imani zaidi. Lakini alikuwa pia hakika kama kupitia musaada wa Yehova wangeweza kuvumilia majaribu yenye ingetokea kisha. (Yoh. 14:1; 16:33) Alikuwa hakika kama imani ya nguvu njo itasaidia kundi kubwa ya watu kuokoka taabu kubwa. (Ufu. 7:9, 14) Utakuwa kati yao? Kupitia fazili zenye hazistahiliwe za Yehova, utakuwa kati yao kama tu unafanya yote yenye unaweza sasa ili imani yako ikuwe nguvu!​—Ebr. 10:39.

WIMBO 118 ‘Unipatie Imani Zaidi’

^ Kila mutu iko nangoya kwa hamu sana mwisho ya hii mupangilio ya mambo. Lakini, wakati fulani tunajiulizaka kama imani yetu itakuwa ingali nguvu mupaka ile siku. Mu hii habari, tutazungumuzia mifano mbalimbali na mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia ile mifano yenye inaweza kutusaidia kufanya imani yetu ikuwe nguvu.