Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Ni mu njia gani mutume Paulo “alichukuliwa mupaka kwenye mbingu ya tatu (3)” na “kuingia katika paradiso”?​—2 Ko. 12:2-4.

Mu andiko la 2 Wakorinto 12:2, 3, Paulo anazungumuzia mutu fulani mwenye “alichukuliwa mupaka kwenye mbingu ya tatu (3).” Alikuwa nani? Wakati aliandikia kutaniko la Korinto, Paulo alikazia kama Mungu alikuwa anamutumia kuwa mutume. (2 Ko. 11:5, 23) Kisha alitaja ‘maono na ufunuo wa Bwana.’ Katika habari hiyo, Paulo hakutaja ndugu wengine. Kwa hiyo, inapatana na akili kusema kama alikuwa anaonyesha kuwa yeye mwenyewe njo mutu mwenye alipata maono na ufunuo.​—2 Ko. 12:1, 5.

Kwa hiyo, Paulo njo mutu mwenye “alichukuliwa mupaka kwenye mbingu ya tatu (3)” na mwenye “alichukuliwa kuingia katika paradiso.” (2 Ko. 12:2-4) Alitumia neno “ufunuo;” hilo linaonyesha kama alifunuliwa mambo yenye itatokea wakati wenye kuja.

“Mbingu ya tatu (3)” yenye Paulo aliona ni nini?

Mu Biblia, neno “mbingu” linaweza kumaanisha mbingu yenye tunaona kwa macho. (Mwa. 11:4; 27:28; Mt. 6:26) Lakini neno “mbingu” linatumiwa pia mu maana ingine. Wakati fulani, linamaanisha utawala wa wanadamu. (Da. 4:20-22) Ao linaweza kumaanisha utawala wa Mungu, kwa kutumia Ufalme wa Mungu.​—Ufu. 21:1.

Paulo aliona “mbingu ya tatu (3).” Maana yake nini? Wakati fulani, Biblia inarudilia jambo fulani mara tatu ili kukazia, ao kuonyesha uzito wa ile jambo. (Isa. 6:3; Eze. 21:27; Ufu. 4:8) Inaonekana kama wakati Paulo alizungumuzia “mbingu ya tatu (3),” alikuwa anakazia utawala wa hali ya juu zaidi na wenye kuwa wa muzuri zaidi, ni kusema, Ufalme wa Kimasiya wenye utatawaliwa na Yesu Kristo na watawala wenzake 144 000. (Ona kitabu Étude Perspicace des Écritures, Buku la 1, uku. 473, 476.) Kama vile mutume Petro aliandika, tunangojea “mbingu mupya” kulingana na ahadi ya Mungu.​—2 Pe. 3:13.

Tuseme nini juu ya “paradiso” yenye Paulo anazungumuzia?

Vilevile neno “paradiso” linaweza kumaanisha mambo mbalimbali: (1) Kwa sababu paradiso ilikuwa makao ya kwanza ya watu, “paradiso” inaweza kumaanisha dunia Paradiso ya wakati wenye kuja. (2) Inaweza kumaanisha hali ya kiroho yenye watu wa Mungu watafurahia mu ulimwengu mupya. (3) Tena, inaweza kumaanisha hali za muzuri sana zenye kuwa mbinguni, ni kusema, “paradiso ya Mungu” yenye kutajwa mu Ufunuo 2:7.​—Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2015, uku. 5 fu. 8.

Inawezekana Paulo alikuwa anazungumuzia aina hizo tatu za paradiso mu andiko la 2 Wakorinto 12:4 wakati alieleza mambo yenye aliona.

Kwa kifupi:

Inawezekana kabisa kuwa “mbingu ya tatu (3)” yenye kutajwa mu andiko la 2 Wakorinto 12:2 ni Ufalme wa Kimasiya wenye utatawaliwa na Yesu Kristo pamoja na wale 144 000, ni kusema, “mbingu mupya.”​—2 Pe. 3:13.

Ni “mbingu ya tatu (3)” kwa sababu Ufalme huo ni aina ya utawala wa hali ya juu zaidi na wenye kuwa wa muzuri zaidi.

Inawezekana kabisa “paradiso” yenye Paulo “alichukuliwa” ndani mu maono, ni (1) Paradiso yenye itakuwa ku dunia hivi karibuni, (2) paradiso ya kiroho yenye itakuwa wakati huo, yenye itaenea sana kuliko paradiso yenye tuko nayo leo, na (3) “paradiso ya Mungu” kule mbinguni yenye itakuwa kwa wakati uleule katika ulimwengu mupya pamoja na paradiso hizo zingine mbili.

Kwa hiyo, mbingu mupya na dunia mupya, vyote pamoja njo vitafanyiza ulimwengu mupya. Utakuwa mupango mupya, wenye kutia ndani serikali ao Ufalme wa mbinguni na wanadamu wenye kumutumikia Yehova mu dunia paradiso.