Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Mwenye Haki Atashangilia Katika Yehova”

“Mwenye Haki Atashangilia Katika Yehova”

DIANA iko na miaka zaidi ya 80 na ameteseka sana kwa miaka fulani yenye imepita. Bwana yake, mwenye alikuwa na ugonjwa wa kupoteza akili wenye kuitwa Alzheimer na mwenye alikuwa mu nyumba ya kutunzia wazee, alikufa. Watoto wake wawili wanaume walikufa pia, na alikuwa na kansere ya maziba. Lakini wakati ndugu na dada wanamuona Diana ku mikutano ao mu kazi ya mahubiri, wanaona kama iko na shangwe ao furaha sikuzote.

John alikuwa mwangalizi mwenye kusafiri kwa miaka zaidi ya 43. Alipenda sana mugao wake na hakuwazia kuwa angefanya jambo ingine yoyote. Lakini alilazimika kuacha kazi ya kusafiri ili ahangaikie mutu fulani wa jamaa yake mwenye kuwa mugonjwa. Wakati ndugu na dada wenye walikuwa wanamujua John wanakutana naye ku mukusanyiko, wanaona kuwa hajabadilika hata kidogo. Angali na furaha sana.

Ni nini inasaidia Diana na John waendelee kuwa na furaha? Namna gani mutu mwenye kuteseka anaweza kuwa na furaha? Namna gani mutu anaweza kuwa mwenye furaha hata kama anapaswa kuacha mugao wake wenye anapenda? Biblia inatupatia jibu. Inasema hivi: “Mwenye haki atashangilia katika Yehova.” (Zb. 64:10) Tunaweza kuelewa muzuri kweli hiyo kama tunajua mambo yenye itatuletea furaha ya kuendelea na mambo yenye haiwezi kutuletea furaha hiyo.

FURAHA YENYE KUWA YA MUDA

Mara mingi, mambo fulani inaletea watu furaha. Kwa mufano, fikiria mwanaume na mwanamuke wenye kupendana na wenye wanaoana. Ao fikiria mutu fulani mwenye anakuwa muzazi ao mwenye anapata mugao mupya mu kazi ya Yehova. Ile mambo inaleta furaha kwa sababu yote ni zawadi kutoka kwa Yehova. Alitupatia zawadi ya ndoa, uwezo wa kuzaa watoto, na kazi ya kufanya mu tengenezo lake.​—Mwa. 2:18, 22; Zb. 127:3; 1 Ti. 3:1.

Lakini, mambo fulani yenye kuleta furaha inaweza kuwa ya muda. Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, bibi ao bwana anaweza kukosa uaminifu kwa mwenzake ao anaweza kufa. (Eze. 24:18; Ho. 3:1) Watoto wanaweza kukosa kutii wazazi wao na Mungu, na pengine wanaweza hata kutengwa na kutaniko. Kwa mufano, wana wa Samweli hawakumutumikia Yehova kwa njia yenye alikubali, na Daudi alipata magumu mingi mu familia yake kwa sababu alifanya zambi pamoja na Bat-sheba. (1 Sa. 8:1-3; 2 Sa. 12:11) Wakati mambo kama ile inatokea, hailete furaha lakini inaleta huzuni na maumivu mingi.

Vilevile, wakati fulani hatuwezi kuendelea kufanya mugao fulani mu kazi ya Yehova kwa sababu tunakuwa wagonjwa ao tunapaswa kuhangaikia familia yetu, ao kwa sababu ya mabadiliko katika tengenezo. Wakristo wengi wenye walipaswa kuacha mugao wao wanasema kama wanakumbuka sana namna uliwafanya wakuwe wenye furaha.

Tunaweza kuona kwa vyepesi kuwa furaha yenye kuletwa na ile mambo haiendelee sikuzote. Kwa hiyo, kuko aina fulani ya furaha yenye inaendelea hata wakati maisha inakuwa nguvu? Ndiyo. Kwa sababu Samweli, Daudi, na wengine hawakupoteza furaha yao wakati walikuwa na magumu.

FURAHA YENYE KUENDELEA

Yesu alijua maana kabisa ya furaha. Mbele akuje ku dunia, Biblia inasema kama ‘alifurahi mbele [ya Yehova] wakati wote.’ (Mez. 8:30) Lakini, wakati alikuja ku dunia, alipaswa kupambana na magumu makali wakati fulani. Hata hivyo, Yesu alipata furaha katika kufanya mapenzi ya Baba yake. (Yoh. 4:34) Tuseme nini juu ya saa za mwisho-mwisho za maisha yake zenye maumivu? Biblia inasema hivi: “Kwa sababu ya furaha yenye iliwekwa mbele yake, alivumilia muti wa mateso.” (Ebr. 12:2) Kwa hiyo, mambo mbili yenye Yesu alisema juu ya furaha ya kweli, inaweza kutufundisha mambo mingi.

Wakati fulani, wanafunzi 70 walirudia kwa Yesu kisha wao kuhubiri. Walikuwa na furaha kwa sababu ya mambo yote yenye walikuwa wamefanya, hata kufukuza pepo wachafu. Lakini Yesu aliwaambia hivi: “Musifurahi kwa sababu roho waovu wanawatii, lakini mufurahi kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.” (Lu. 10:1-9, 17, 20) Kwa kweli, kukubaliwa na Yehova njo jambo ya maana zaidi na kunaleta furaha zaidi kupita mugao wowote wa pekee.

Wakati mwingine, Yesu alikuwa anazungumuza na watu wengi. Mwanamuke mumoja Muyahudi alishangazwa sana na mafundisho yake, na akamuambia kama mama yake alipaswa kuwa mwenye furaha sana kwa sababu ya kuwa na mutoto kama huyo. Lakini Yesu alijibu hivi: “Hapana, lakini, wenye furaha ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulishika!” (Lu. 11:27, 28) Kujivunia watoto wetu kunaweza kutufanya tukuwe wenye furaha. Lakini jambo yenye kutuletea furaha yenye kuendelea ni kumutii Yehova na kuwa na urafiki wa muzuri pamoja naye.

Tunakuwa wenye furaha sana wakati tunajisikia kuwa Yehova anatufurahia. Na hata kama hatufurahie magumu, haifanye tuache kujisikia vile. Kwa kweli, wakati tunabakia waaminifu wakati wa magumu, furaha yetu inakuwa kubwa zaidi. (Ro. 5:3-5) Pia, Yehova anapatia roho yake wale wenye kumutumainia, na furaha ni sehemu ya tunda la roho. (Gal. 5:22) Hilo linatusaidia kuelewa juu ya nini Zaburi 64:10 inasema hivi: “Mwenye haki atashangilia katika Yehova.”

Ni nini imemusaidia John aendelee kuwa mwenye furaha?

Hilo linaonyesha pia juu ya nini Diana na John wanaendelea kuwa wenye furaha hata kama walipambana na magumu. Diana anasema hivi: “Nimemukimbilia Yehova, kama vile mutoto anaweza kumukimbilia muzazi wake.” Anaongeza hivi: “Ninajisikia kuwa amenibariki kwa kunipatia uwezo wa kuendelea kuhubiri na niko na sura ya kicheko.” Ni nini ilisaidia John aendelee kuwa mwenye furaha na aendelee kufanya mambo mingi katika utumishi kisha kuacha mugao wake? Anasema hivi: “Kuanzia mwaka wa 1998 wakati nilipewa mugao wa kufundisha ku Masomo ya Mazoezi ya Kihuduma, nimejifunza sana kipekee kuliko wakati mwingine wowote.” Anafasiria kama mabadiliko yenye yeye na bibi yake walipaswa kufanya, ilikuwa mwepesi kwa sababu sikuzote walikuwa tayari kufanya kazi yoyote yenye Yehova aliwapatia. Anaongeza hivi: “Tumefanya vile bila kuhuzunika.”

Ndugu na dada wengine wengi wamejionea kama maneno ya Zaburi 64:10 ni ya kweli. Kwa mufano, fikiria bibi na bwana fulani wenye walitumikia ku Beteli ya inchi ya Amerika kwa zaidi ya miaka 30. Kisha walipewa mugao wa kuwa mapainia wa pekee. Walisema hivi: “Ni jambo ya kawaida kuhuzunika wakati unapoteza jambo fulani yenye ulikuwa unapenda,” lakini waliongeza hivi: “Hauwezi kuhuzunika milele.” Wakati tu walifika katika mugao wao mupya, walianza kuhubiri pamoja na kutaniko. Walisema pia hivi: “Tulisali juu ya mambo fulani ya pekee. Kisha, kuona namna Yehova alijibu sala zetu kulitutia moyo sana na kulituletea furaha. Kisha tu kufika, wengine mu kutaniko walianza kufanya kazi ya upainia, na tulibarikiwa kwa kupata mafunzo mbili ya Biblia yenye kufanya maendeleo.”

‘KUWA NA SHANGWE MILELE’

Kwa kweli, haiko mwepesi sikuzote kuwa mwenye shangwe ao furaha. Kutakuwa wakati wenye tutakuwa na huzuni. Lakini Yehova anatutia moyo kupitia maneno yenye kupatikana mu Zaburi 64:10. Hata wakati tunavunjika moyo, tunaweza kuwa hakika kama, ikiwa tunabakia waaminifu hata tupatwe na magumu gani, ‘tutashangilia katika Yehova.’ Tunaweza pia kungojea kwa hamu wakati wenye ahadi ya Yehova ya “mbingu mupya na dunia mupya” itatimia. Wakati huo, kila mutu atakuwa mukamilifu na ‘atafurahi na kuwa na shangwe milele’ kwa sababu ya mambo yote yenye Yehova atafanya.​—Isa. 65:17, 18.

Fikiria faida zenye hilo litaleta. Tutakuwa na afya kamilifu na tutaamuka kila siku tukiwa na nguvu nyingi. Hata kama mambo gani ilituletea huzuni zamani, haitatuletea huzuni tena. Yehova anatuhakikishia kama “mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayataingia katika moyo.” Tutakaribisha wapendwa wetu wenye wamekufa na tutajisikia kama wazazi wa mutoto mwanamuke wa miaka 12 mwenye Yesu alifufua. Biblia inasema hivi: “Wakakuwa na furaha kubwa sana.” (Mk. 5:42) Mwishowe, kila mutu ku dunia atakuwa mwenye haki kabisa na “atashangilia katika Yehova” milele.