Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unakumbuka?

Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu magazeti ya hivi karibuni ya Munara wa Mulinzi? Kama ni vile, jaribu kujibu maulizo hii:

Ni ushuhuda gani wenye kuwa katika Maandiko wenye kuonyesha kama Mungu anatusikilia huruma?

Wakati Waisraeli wa zamani walikuwa katika utumwa katika Misri, Mungu aliona mateso yao na alisikia maumivu yao. (Kut. 3:7; Isa. 63:9) Tumeumbwa kwa mufano wa Mungu, na tunaweza kusikilia wengine huruma. Anatusikilia huruma hata wakati tunaweza kujisikia kuwa hatustahili upendo wake.​—wp18.3, uku. 8-9.

Namna gani mafundisho ya Yesu ilisaidia watu washinde ubaguzi?

Wakati wa Yesu, Wayahudi wengi walikuwa na ubaguzi. Kristo alikazia lazima ya kuwa na unyenyekevu na alihukumu tabia ya kujivunia kabila. Aliomba wafuasi wake wajione kuwa ndugu na dada.​—w18.06, uku. 9-10.

Yehova hakumuruhusu Musa aingie mu Inchi ya Ahadi, hilo linatufundisha nini?

Musa alikuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova. (Kum. 34:10) Wakati walikaribia kumaliza miaka 40 mu jangwa, watu walilalamika kwa mara ya pili juu ya kukosa maji. Mungu alimuambia Musa aseme na mwamba. Lakini, Musa alipiga mwamba. Pengine Yehova alikasirika kwa sababu Musa hakufuata maagizo yenye alimupatia ao kwa sababu hakumupatia Mungu utukufu juu ya muujiza huo. (Hes. 20:6-12) Hilo linapaswa kutufundisha kama ni jambo ya maana kumutii Yehova na kumupatia utukufu.​—w18.07, uku. 13-14.

Namna gani tunaweza kukosea kwa vyepesi ikiwa tunahukumu wengine kulingana na namna wanaonekana kwa inje?

Kuko mambo tatu yenye inaweza kufanya watu wengi wachochewe na namna mutu anaonekana kwa inje: rangi ya ngozi ya mutu ao kabila yake, kiasi cha feza zenye iko nazo, na miaka yake. Ni jambo ya maana tujikaze kuona watu bila ubaguzi kama vile Mungu anawaona! (Mdo. 10:34, 35)​—w18.08, uku. 8-12.

Wakristo wenye kuzeeka wanaweza kusaidia wengine mu njia gani fulani?

Mukristo mwenye kuzeeka mwenye mugao wake umebadilika, Mungu anaendelea kumuona kuwa wa maana na anaweza kufanya mambo mingi ili kusaidia wengine. Anaweza kusaidia bibi za ndugu zetu ao bwana za dada zetu wenye hawako Mashahidi, anaweza kusaidia wale wenye hawahubiri na kukusanyika tena, anaweza kuongoza mafunzo ya Biblia, na kupanua utumishi wake.​—w18.09, uku. 8-11.

Wakristo wako na vyombo gani vya kufundishia?

Wako na karte za jw.org na mialiko. Trakte munane zenye zilitayarishwa muzuri na magazeti Munara wa Mulinzi na Amuka!. Kati ya ile vyombo kuko pia broshua fulani, vitabu mbili vya musingi vya kujifunza Biblia, na video ine zenye kufaa, kutia ndani video Sababu Gani Ujifunze Biblia?​—w18.10, uku. 16.

Namna gani Mukristo anaweza ‘kununua kweli,’ kama vile Mezali 23:23 inatuomba?

Hatulipe feza ili kujifunza kweli. Lakini, tunapaswa kutumia wakati na kujikaza sana ili kupata kweli hiyo.​—w18.11, uku. 4.

Namna Hosea alimutendea bibi yake Gomeri inaweza kutufundisha nini?

Gomeri alifanya uzinifu mara nyingi, lakini Hosea alimusamehe na hakuvunja ndoa yao. Kama bwana ao bibi ya Mukristo fulani anafanya uasherati, bibi ao bwana mwenye hana kosa anaweza kumusamehe. Wakati anafanya tena ngono na bibi ao bwana mwenye alifanya uasherati, hakutakuwa tena sababu yenye kuruhusiwa na Maandiko ya kuvunja ndoa.​—w18.12, uku. 13.