Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Tutaonana Katika Paradiso!”

“Tutaonana Katika Paradiso!”

“Utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.”​—LU. 23:43.

NYIMBO: 145, 139

1, 2. Watu wako na mawazo gani mbalimbali juu ya paradiso?

NDUGU na dada wengi wa inchi mbalimbali walikuwa wamekuja mu muji wa Seoul, Korea, kwa ajili ya mukusanyiko. Wakati walikuwa wanatoka mu kiwanja kwenye walifanyia mukusanyiko, Mashahidi wa inchi hiyo waliwazunguka. Wengi kati yao walikuwa wanapepeana na kuambiana hivi: “Tutaonana katika Paradiso!” Hilo lilikuwa tukio lenye kugusa moyo sana. Unawaza walikuwa wanazungumuzia paradiso gani?

2 Leo, watu wako na mawazo mbalimbali juu ya paradiso. Wamoja wanasema kama paradiso ni jambo la kuwazia tu. Wengine wanasema kama paradiso ni nafasi yoyote kwenye wako na furaha. Mutu mwenye kuwa na njaa sana mwenye anakaa pembeni ya meza kubwa yenye kujaa chakula, anaweza kuona kuwa iko mu paradiso. Wakati mutu anaona nafasi ya kupendeza, kama vile bonde lenye kujaa maua, anaweza kusema hivi: “Ee, hii ni paradiso kabisa!” Unawaza Paradiso ni nini? Uko na tumaini kama Paradiso itakuja?

3. Ni wapi Biblia inazungumuzia Paradiso kwa mara ya kwanza?

3 Biblia inazungumuzia paradiso yenye ilikuwa wakati wa zamani na paradiso yenye itakuwa wakati wenye kuja. Biblia inazungumuzia Paradiso kwa mara ya kwanza mu kitabu cha kwanza cha Biblia. Mu Biblia ya Katoliki ya Douay Version, yenye ilitafsiriwa kutoka katika luga ya Kilatini, andiko la Mwanzo 2:8 linatafsiriwa hivi: “Bwana Mungu alikuwa amepanda paradiso ya raha tangu mwanzo: kwenye aliweka mutu mwenye alikuwa amefanya.” (Ni sisi tunakazia maneno yenye kuwa katika rangi nyeusi.) Maandishi ya Kiebrania inasema bustani ya Edeni. Neno “Edeni” linamaanisha “Raha,” na bustani hiyo ilikuwa nafasi ya kufurahisha kabisa. Ilikuwa nafasi ya muzuri sana, ilikuwa na chakula mingi na kulikuwa amani kati ya watu na wanyama.​—Mwa. 1:29-31.

4. Juu ya nini tunaweza kusema kama bustani ya Edeni ilikuwa paradiso?

4 Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “bustani” linatafsiriwa pa·raʹdei·sos mu Kigiriki. Kitabu kimoja chenye kiliandikwa na M’Clintock na Strong kinasema kama wakati Mugiriki alisikia neno pa·raʹdei·sos, angeweza kuwazia bustani kubwa ya muzuri sana yenye kulindwa ili kitu chochote kisiiharibu, yenye miti mikubwa-mikubwa ya matunda na mito midogo-midogo ya maji safi yenye kuwa na majani pembeni-pembeni, kwenye makundi ya paa na kondoo ingeweza kula majani.​—Linganisha na Mwanzo 2:15, 16.

5, 6. Juu ya nini Adamu na Eva walipoteza pendeleo la kuishi mu Paradiso, na watu fulani wanaweza kujiuliza nini?

5 Yehova alitia Adamu na Eva mu bustani ya namna hiyo, ni kusema, paradiso. Lakini, juu walikosa kumutii Yehova, walipoteza pendeleo la kuishi mu Paradiso; walipoteza pendeleo hilo kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya watoto wao. (Mwa. 3:23, 24) Hata kama hakuna mutu mwenye aliendelea kuishi mu Paradiso hiyo, inaonekana kama iliendelea kuwa mupaka wakati wa Garika ya siku za Noa.

6 Watu fulani wanaweza kujiuliza hivi: ‘Kutakuwa tena Paradiso ku dunia siku moja?’ Kuko mambo yenye kuhakikisha vile? Kama unatumainia kuishi mu Paradiso pamoja na watu wenye unapenda, uko na sababu za muzuri za kuwa na tumaini hilo? Unaweza kufasiria juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama kutakuwa paradiso wakati wenye kuja?

MAMBO YENYE KUHAKIKISHA KAMA KUTAKUWA PARADISO WAKATI WENYE KUJA

7, 8. (a) Mungu alimupatia Abrahamu ahadi gani? (b) Pengine ahadi yenye Mungu alimupatia Abrahamu ilimufanya afikirie nini?

7 Nafasi ya muzuri kwenye tunaweza kupata majibu ya maulizo juu ya Paradiso ni mu Biblia, kwa sababu inatoka kwa Yehova, mwenye aliumba Paradiso ya kwanza. Fikiria mambo yenye Mungu alimuambia rafiki yake Abrahamu. Mungu alisema kama angefanya uzao wa Abrahamu uongezeke “kama chembe za muchanga pembeni ya bahari.” Kisha, Yehova alimupatia Abrahamu ahadi hii ya maana sana: “Kupitia uzao wako mataifa yote ya dunia yatajipatia baraka kwa sababu umesikiliza sauti yangu.” (Mwa. 22:17, 18) Kisha, Mungu alipatia mwana wa Abrahamu na mujukuu (munkana) wake ahadi ileile.​—Soma Mwanzo 26:4; 28:14.

8 Mu Biblia, hakuna jambo lenye kuonyesha kama Abrahamu aliwaza kuwa wanadamu wangepata zawabu ao baraka yao ya mwisho mbinguni. Kwa hiyo, wakati Mungu aliahidi kama “mataifa yote ya dunia” ingebarikiwa, Abrahamu alipaswa kufikiria kama baraka hizo zitakuwa ku dunia. Lakini, je, kuko mambo ingine mu Biblia yenye kuhakikisha kama kutakuwa paradiso ku dunia?

9, 10. Ni ahadi gani zingine zenye zinatupatia sababu ya kutumainia kama kutakuwa paradiso wakati wenye kuja?

9 Kupitia roho yake, Mungu alimuongoza Daudi, muzao mumoja wa Abrahamu, azungumuzie wakati wenye kuja wakati “waovu hawatakuwa tena.” (Zb. 37:1, 2, 10) Lakini, “wapole watariti dunia, na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.” Tena, Daudi alitabiri hivi: “Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.” (Zb. 37:11, 29; 2 Sa. 23:2) Unawaza ahadi hizo zilisaidia namna gani watu wenye walipenda kufanya mapenzi ya Mungu? Walikuwa na sababu ya kutumainia kama siku moja watu wenye haki tu njo watakuwa mu dunia na kama itakuwa tena paradiso kama vile bustani ya Edeni.

10 Kisha wakati fulani, Waisraeli wengi wenye walikuwa wanasema kama wanamuabudu Mungu, walimukataa na kuacha ibada safi. Kwa hiyo, Mungu aliruhusu Wababiloni washinde watu wake, waharibu inchi yao, na kupeleka wengi kati yao katika uhamisho. (2 Ny. 36:15-21; Yer. 4:22-27) Lakini, manabii wa Mungu walitabiri kama watu wake wangerudia mu inchi yao kisha miaka 70. Na unabii huo mbalimbali ulitimia. Lakini, unabii huo uko pia na maana kwetu leo. Wakati tunazungumuzia unabii fulani kati ya unabii huo, tutaona namna unatupatia sababu za kutumainia kama kutakuwa paradiso ku dunia wakati wenye kuja.

11. Namna gani andiko la Isaya 11:6-9 lilitimia kwa mara ya kwanza, lakini tunaweza kujiuliza ulizo gani?

11 Soma Isaya 11:6-9. Kupitia nabii Isaya, Mungu alitabiri kama wakati Waisraeli wangerudia mu inchi yao, inchi ingekuwa na amani. Hakuna mwenye angeogopa kama atashambuliwa na wanyama ao watu. Vijana na wazee wangeishi katika usalama. Je, hilo linakukumbusha hali za amani zenye zilikuwa mu bustani ya Edeni? (Isa. 51:3) Pia, Isaya alitabiri kama, haiko tu taifa la Israeli, lakini dunia yote ‘ingejaa ujuzi juu ya Yehova kama vile maji yanafunika bahari.’ Hilo lingefanyika wakati gani? Ni wazi kama unabii huo unazungumuzia wakati wenye kuja.

12. (a) Wale wenye walirudia kutoka mu uhamisho Babiloni walipata baraka gani? (b) Ni nini inaonyesha kama unabii wenye kuwa mu Isaya 35:5-10 utatimia pia wakati wenye kuja?

12 Soma Isaya 35:5-10. Ona kama Isaya alitabiri tena kuwa Waisraeli wenye wangerudia kutoka Babiloni, hawangeshambuliwa na wanyama ao watu. Alisema kama inchi yao ingezaa chakula cha mingi cha muzuri sana kwa sababu ingekuwa na maji mingi, kama vile hali ilikuwa mu bustani ya Edeni. (Mwa. 2:10-14; Yer. 31:12) Unabii huo ungetimia tu wakati wa Waisraeli hao? Ona kama unabii huo ulisema pia kama watu wenye walikuwa vipofu, vilema wa miguu, na viziwi wangeponyeshwa. Lakini, jambo hilo halikufanyika kwa Waisraeli wenye walirudia kutoka Babiloni. Mungu alikuwa anaonyesha kama ataponyesha magonjwa yote wakati wenye kuja.

13, 14. Andiko la Isaya 65:21-23 lilitimia namna gani wakati Waisraeli walirudia kutoka Babiloni, na ni sehemu gani ya unabii huo yenye ingali itatimia? (Ona picha ku mwanzo wa habari hii.)

13 Soma Isaya 65:21-23. Wakati Wayahudi walirudia mu inchi yao, hawakukuta nyumba za muzuri ao mashamba ya mizabibu na mashamba ingine yenye kulimwa. Lakini, kwa sababu Mungu aliwabariki, mambo ilibadilika kisha wakati fulani. Wazia namna watu walifurahi wakati walijenga nyumba na kuishi ndani na wakati walikula chakula cha muzuri chenye walipanda!

14 Ona kama unabii huo unasema kuwa siku zetu “zitakuwa kama siku za muti.” Miti fulani inaishi maelfu ya miaka. Ili wanadamu wakuwe na maisha ya murefu kama ile, wanapaswa kuwa na afya ya muzuri kabisa. Na kama wangeishi mu hali zenye Isaya alitabiri, ingekuwa muzuri sana, ingekuwa paradiso! Na unabii huo utatimia!

Ahadi yenye Yesu alitoa juu ya Paradiso itatimia namna gani? (Picha hii inapatana na fungu la 15, 16)

15. Ni baraka gani fulani zenye kuzungumuziwa mu kitabu cha Isaya?

15 Fikiria namna ahadi zenye tunatoka kuzungumuzia zinaonyesha kama kutakuwa paradiso wakati wenye kuja. Dunia yote itajaa watu wenye kubarikiwa na Mungu. Hakuna mutu mwenye ataogopa kama atashambuliwa na wanyama ao watu wenye jeuri. Watu wenye kuwa vipofu, viziwi, na vilema wa miguu wataponyeshwa. Watu watajenga nyumba zao wenyewe na watapanda chakula chao wenyewe. Watakuwa na maisha ya murefu kuliko miti. Kwa kweli, Biblia inazungumuzia mambo yenye kuhakikisha kama paradiso hiyo itakuja. Lakini, watu fulani wenye tunazungumuza nao wanaweza kusema kama unabii huo mbalimbali hauonyeshe kabisa kama kutakuwa paradiso ku dunia. Unaweza kuwaambia nini? Uko na sababu gani ya muzuri yenye kukufanya utumainie kama kutakuwa paradiso ku dunia? Yesu, mutu mukubwa zaidi mwenye amepata kuishi, alitutolea sababu hiyo.

UTAKUWA KATIKA PARADISO!

16, 17. Yesu alizungumuzia Paradiso wakati gani?

16 Hata kama Yesu hakukuwa na kosa, alihukumiwa na kutundikwa ku muti ili akufe, pamoja na Wayahudi wawili watenda-mabaya pembeni yake. Mumoja kati yao alitambua kama Yesu alikuwa mufalme na akamuambia hivi: “Yesu, unikumbuke wakati utaingia katika Ufalme wako.” (Lu. 23:39-42) Ahadi yenye Yesu alipatia ule mutenda-mabaya inahusu wakati wako wenye kuja. Maneno ya Yesu inapatikana mu Luka 23:43. Watu fulani wenye elimu wanatia alama ya mukato (,) mbele ya neno “leo” na wanatafsiri ile maneno hivi: “Kwa kweli ninakuambia, leo utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.” Kuko mawazo tofauti juu ya nafasi kwenye alama ya mukato inapaswa kuingia katika ile maneno. Lakini, Yesu alimaanisha nini wakati alisema “leo”?

17 Mu luga mingi za leo, alama ya mukato inatumiwa ili kufanya maana ya musemo fulani ikuwe wazi ao ikuwe yenye kueleweka muzuri. Lakini, mu maandishi ya zamani sana ya Kigiriki yenye kupatikana, mara nyingi alama za vituo hazikutumiwa. Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: Yesu alipenda kusema, “Ninakuambia, leo utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso”? Ao alipenda kusema, “Ninakuambia leo, utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso”? Watafsiri wanatia alama ya mukato mbele ao kisha neno “leo” kulingana na mawazo yenye wako nayo juu ya jambo lenye Yesu alipenda kusema, na unaweza kuona namna hizo mbili mu Biblia za leo.

18, 19. Ni nini inatusaidia kuelewa mambo yenye Yesu alipenda kusema?

18 Lakini, kumbuka mambo yenye Yesu aliambia wanafunzi wake juu ya kifo chake. Alisema hivi: “Mwana wa binadamu atakuwa katika kaburi siku tatu muchana na usiku.” Tena alisema hivi: “Mwana wa binadamu atasalitiwa katika mikono ya watu, na watamuua, na siku ya tatu (3) atafufuliwa.” (Mt. 12:40; 16:21; 17:22, 23; Mk. 10:34) Mutume Petro anasema kama jambo hilo lilitokea. (Mdo. 10:39, 40) Kwa hiyo, Yesu hakuenda mu Paradiso siku yenye yeye na ule mutenda-mabaya walikufa. Biblia inasema kama Yesu alikuwa “katika Kaburi” kwa siku tatu, mupaka wakati Mungu alimufufua.​—Mdo. 2:31, 32. * (Ona maelezo ya chini.)

19 Kwa hiyo, Yesu alitumia maneno “Kwa kweli ninakuambia leo” ili kutoa utangulizi wa ahadi yenye alimupatia ule mutenda-mabaya. Ni vile watu walizoea kuzungumuza, hata mu siku za Musa. Wakati fulani Musa alisema hivi: “Maneno haya yenye ninakuamuru leo yanapaswa kuwa kwenye moyo wako.”​—Kum. 6:6; 7:11; 8:1, 19; 30:15.

20. Ni nini inaunga mukono namna tunaelewa maneno yenye Yesu alisema?

20 Mutafsiri mumoja wa Biblia wa Mashariki ya Kati alisema hivi: “Mu andiko hilo, neno lenye kukaziwa ni ‘leo’ na andiko hilo linapaswa kusomwa hivi: ‘Kwa kweli ninakuambia leo, utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.’ Ahadi ilitolewa ile siku na ilipaswa kutimizwa wakati wenye kuja.” Mutafsiri huyo alisema pia kama njo vile watu wanazoea kuzungumuza katika eneo hilo na hilo linaonyesha kama “ahadi ilifanywa siku fulani na itatimizwa kabisa.” Tafsiri moja ya luga ya Kisiria yenye ilitafsiriwa kumepita miaka 1 600 hivi inatafsiri andiko hilo hivi: “Amina, ninakuambia leo kama utakuwa pamoja na mimi katika Bustani ya Edeni.” Ile ahadi inatutia moyo sisi wote.

21. Ule mutenda-mabaya hakupewa pendeleo gani, na juu ya nini?

21 Wakati Yesu aliambia ule mutenda-mabaya juu ya Paradiso, hakukuwa anazungumuzia paradiso ya mbinguni. Ni nini inaonyesha vile? Jambo moja lenye kuonyesha vile ni hili: Ule mutenda-mabaya hakujua kama Yesu alikuwa amefanya agano pamoja na mitume wake waaminifu ili watawale pamoja naye mbinguni. (Lu. 22:29) Tena, hakukuwa hata amebatizwa. (Yoh. 3:3-6, 12) Ni wazi kama ule mutenda-mabaya hakuchaguliwa ili kuenda mbinguni. Kwa hiyo, wakati Yesu alimupatia ahadi hiyo, alipaswa kuwa alikuwa anazungumuzia paradiso ya ku dunia. Miaka fulani kisha pale, mutume Paulo alizungumuzia maono juu ya mutu mwenye “alichukuliwa kuingia katika paradiso.” (2 Ko. 12:1-4) Hata kama Paulo na mitume wengine walichaguliwa ili kuenda mbinguni kusudi watawale pamoja na Yesu, Paulo alikuwa anazungumuzia paradiso ya wakati wenye kuja. * (Ona maelezo ya chini.) Paradiso hiyo itakuwa ku dunia? Utakuwa mu ile paradiso?

MAMBO YENYE UNAWEZA KUTUMAINIA

22, 23. Unaweza kutumainia nini?

22 Kumbuka kama Daudi alizungumuzia wakati wenye watu “wenye haki watariti dunia.” (Zb. 37:29; 2 Pe. 3:13) Daudi alikuwa anazungumuzia wakati wenye watu wote ku dunia watatii kanuni za Mungu zenye haki. Unabii wenye kuwa mu Isaya 65:22 unasema hivi: “Siku za watu wangu zitakuwa kama siku za muti.” Hilo linaonyesha kama watu wenye kumutumikia Yehova mu ulimwengu wake mupya wataishi kwa maelfu ya miaka. Unaweza kutumainia jambo hilo? Ndiyo, kwa sababu kulingana na Ufunuo 21:1-4, Mungu atabariki wanadamu, na baraka moja kati ya baraka hizo ni kwamba “kifo hakitakuwa tena.”

23 Mambo yenye Biblia inafundisha juu ya Paradiso iko wazi. Adamu na Eva walipoteza pendeleo la kuishi milele mu Paradiso, lakini dunia itakuwa tena paradiso. Kama vile Mungu aliahidi, atabariki watu ku dunia. Daudi alisema kama wapole na wenye haki watariti dunia na kuishi milele juu yake. Na unabii mbalimbali wenye kuwa mu kitabu cha Isaya unatusaidia kutumainia wakati wenye tutafurahia maisha mu paradiso ya muzuri sana ku dunia. Hilo litakuwa wakati gani? Wakati ahadi yenye Yesu alipatia ule mutenda-mabaya itatimia. Unaweza kuwa mu paradiso hiyo. Wakati huo, maneno yenye ndugu na dada walisema ku mukusanyiko wenye ulifanyika mu inchi ya Korea itatimia: “Tutaonana katika Paradiso!”

^ fu. 18 Profesa Marvin Pate aliandika kama watu wengi wenye elimu wanaamini kama wakati Yesu alisema “leo,” alikuwa anamaanisha kama angekufa na kuenda mu Paradiso siku ileile, ao mu saa 24. Profesa Pate anasema tena kama ile mawazo iko na shida juu haipatane na mafundisho ingine ya Biblia. Kwa mufano, Biblia inasema kama Yesu alikuwa mu Kaburi kisha kufa na kama alienda mbinguni wakati fulani kisha kufufuliwa.​—Mt. 12:40; Mdo. 2:31; Ro. 10:7.

^ fu. 21 Ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” katika gazeti hili.