Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Wakati Shetani alimuambia Eva kama akikula tunda la muti wa ujuzi wa mema na mabaya hatakufa, alipenda kuanzisha mu akili ya Eva wazo la kutokufa kwa nafsi lenye watu wengi wanaamini leo?

Inaonekana ni hapana. Ibilisi hakumuambia Eva kama akikula tunda lenye Mungu aliwakataza, angeonekana tu kuwa mwenye kufa lakini sehemu fulani ya mwili wake yenye haionekane (yenye watu fulani wanaita leo nafsi yenye haiwezi kufa) ingeendelea kuishi nafasi fulani. Kupitia nyoka, Shetani alimuambia Eva kama akikula tunda la muti huo, ‘hakika hangekufa’ hata kidogo. Shetani alipenda kusema kama Eva angeendelea kuishi na kufurahia maisha ya muzuri ku dunia, bila kuongozwa na Mungu.​—Mwa. 2:17; 3:3-5.

Ikiwa fundisho la kutokufa kwa nafsi kama vile linafundishwa leo halikuanza katika Edeni, basi lilianza wakati gani? Hatujue kabisa. Tunajua kama ibada zote za uongo ziliharibiwa katika Garika ya siku za Noa. Hakuna hata wazo moja la dini ya uongo lenye lilibakia kwa sababu ni Noa na familia yake tu njo waliokoka, na wote walikuwa waabudu wa kweli.

Kwa hiyo, fundisho la kutokufa kwa nafsi ya mwanadamu, kama vile linafundishwa leo, lilianza kisha Garika. Wakati Mungu alivuruga luga za watu katika Babeli na kuwasambaza “juu ya uso wote wa dunia,” kwa kweli, walienda na wazo lenye kusema kama wanadamu wako na nafsi yenye haiwezi kufa. (Mwa. 11:8, 9) Hata ikuwe wazo hilo la uongo lilianza wakati gani, tunaweza kuwa hakika kama Shetani Ibilisi, “baba ya uongo,” njo mwenye alianzisha wazo hilo na alifurahi wakati aliona linaenea sana.​—Yoh. 8:44.