Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Biblia inasema kama kunapaswa kuwa mashahidi wawili hivi ili kuhakikisha jambo fulani. (Hes. 35:30; Kum. 17:6; 19:15; Mt. 18:16; 1 Ti. 5:19) Lakini, chini ya Sheria ya Musa, kama mwanaume alikuta “katika eneo la mashamba” mutoto mwanamuke mwenye alikuwa anachumbiwa na kulala naye kinguvu, na mutoto huyo mwanamuke alilalamika, yeye hakukuwa na kosa la uzinifu lakini mwanaume huyo alikuwa na kosa la uzinifu. Kwa sababu wengine hawakuona ao kusikia jambo hilo, juu ya nini mutoto mwanamuke hakukuwa na kosa lakini mwanaume huyo alikuwa na kosa?

Habari yenye kuzungumuziwa mu Kumbukumbu la Torati 22:25-27 haikukuwa na kusudi la kuonyesha kama mwanaume alikuwa na kosa, kwa sababu katika habari hiyo, mwanaume alionwa tayari kuwa mwenye kosa. Sheria hiyo ilikuwa na kusudi la kuhakikisha kama mwanamuke hakukuwa na kosa. Tuzungumuzie mistari yenye inatangulia na yenye inafuata habari hiyo.

Mistari yenye inatangulia inazungumuzia mwanaume mwenye alikuta “katika muji” mutoto mwanamuke mwenye kuchumbiwa na kulala naye. Kwa kufanya vile, alifanya kosa la uzinifu, juu mutoto mwanamuke mwenye kuchumbiwa alionwa kuwa mwenye kuolewa. Tuseme nini juu ya ule mutoto mwanamuke? “Hakulalamika katika muji.” Kama angelalamika, kwa kweli wengine wangemusikia na wangemusaidia. Lakini hakulalamika. Kwa hiyo, alishiriki katika zambi ya uzinifu; njo maana wote wawili walikuwa na kosa.​—Kum. 22:23, 24.

Sheria ilizungumuzia hali ingine tofauti. Ilisema hivi: “Lakini, kama mwanaume huyo alikuta mutoto huyo mwanamuke mwenye kuchumbiwa katika eneo la mashamba na mwanaume huyo alimukamata kwa nguvu na kulala naye, mwanaume huyo mwenye alilala naye atakufa peke yake, na haupaswe kumutendea jambo lolote mutoto huyo mwanamuke. Mutoto huyo mwanamuke hakutenda zambi yenye kustahili kifo. Hali hii ni sawa na ya mutu mwenye anashambulia mwenzake na kumuua. Kwa maana mwanaume huyo alimukuta katika eneo la mashamba, na mutoto huyo mwanamuke mwenye kuchumbiwa akalalamika, lakini hapakukuwa mutu wa kumuokoa.”​—Kum. 22:25-27.

Katika hali hiyo, waamuzi waliamini mambo yenye mutoto mwanamuke alisema. Katika njia gani? Waliwazia kama ‘alilalamika, lakini hapakukuwa mutu wa kumuokoa.’ Kwa hiyo, mutoto mwanamuke hakufanya uzinifu. Lakini, mwanaume alikuwa na kosa la kulala kinguvu na mwanamuke huyo na alikuwa na kosa la uzinifu kwa sababu “alimukamata kwa nguvu [ule mwanamuke mwenye kuchumbiwa] na kulala naye.”

Kwa hiyo, hata kama sheria hiyo ilikazia kama mutoto mwanamuke hakukuwa na kosa, habari hiyo ilionyesha tu kama mwanaume alikuwa na kosa la kulala na mwanamuke huyo kinguvu na kosa la uzinifu. Tunaweza kuwa hakika kama waamuzi walikuwa ‘wanachunguza jambo hilo kwa uangalifu’ na kutoa uamuzi kulingana na muongozo wenye ulikuwa wazi wenye Mungu aliwapatia na wenye alirudilia mara kwa mara.​—Kum. 13:14; 17:4; Kut. 20:14.