Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unakumbuka?

Unakumbuka?

Unaweza kujibu maulizo hii yenye kutegemea magazeti Munara wa Mulinzi ya 2019?

“Hakuna silaha yenye itafanywa juu yako yenye itafanikiwa.” (Isa. 54:17) Ahadi hii ya Mungu maana yake nini?

Tunaweza kutumainia kama Mungu atatulinda na nguvu zenye kuharibu, kwa mufano, atatulinda na “mulipuko wa watu wenye kuonea.” (Isa. 25:4, 5) Maadui wetu hawataweza hata kutuangamiza kabisa-kabisa.​—w19.01, uku. 6-7.

Namna Mungu alitendea Wakanaani na Waisraeli waasi, inaonyesha namna gani haki yake?

Mungu aliharibu watu wenye walifanya matendo ya ngono yenye kuchukiza ao wale wenye walitendea mubaya wanamuke na watoto. Alibariki watu wenye walikuwa watiifu kwake na wenye walitendea wengine kwa haki.​—w19.02, uku. 22-23.

Tunapaswa kufanya nini kama tuko pale wakati mutu mwenye haiko Shahidi anasali?

Tunaweza kubakia kimya na kujiendesha kwa heshima lakini hatutasema “amina” na hatutakamatana mikono na watu wengine wakati wa sala. Tunaweza kutoa sala yetu wenyewe ya kimya-kimya.​—w19.03, uku. 31.

Juu ya nini kutendea mutoto mubaya kingono ni kosa nzito sana?

Kutendea mutoto mubaya kingono ni kumutendea mutoto zambi, ni kutendea kutaniko zambi, ni kutendea wakubwa wa serikali zambi, na ni kumutendea Mungu zambi. Katika inchi kwenye sheria inaomba kujulisha wakubwa wa serikali mashitaka ya kutendea watoto mubaya kingono, wazee wanatii sheria hiyo.​—w19.05, uku. 9-10.

Namna gani unaweza kubadilisha ao kufanya muzuri zaidi mutazamo wenye unatawala akili yako?

Mambo ya maana ya kufanya ni hii: Uzungumuze na Yehova katika sala. Ufikiri sana na uko na muradi wa kujichunguza. Uchague marafiki wako kwa hekima.​—w19.06, uku. 11.

Tunaweza kufanya nini leo ili kujitayarisha kwa ajili ya mateso?

Tunapaswa kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova. Tukuwe hakika kama Yehova anatupenda na hatatuacha hata kidogo. Tusome Biblia kila siku, na kusali kwa ukawaida. Tukuwe hakika kama ahadi za Ufalme wa Mungu zitatimia. Tuweke katika akili maandiko yenye tunapendaka sana na nyimbo za kumusifu Yehova.​—w19.07, uku. 2-4.

Tunaweza kufanya nini ili kusaidia watu wa jamaa yetu waokolewe?

Ni jambo la maana tujitie pa nafasi yao, tuwahubirie kupitia mwenendo wetu muzuri, na tuwaonyeshe uvumilivu na heshima.​—w19.08, uku. 15-17.

Namna gani tunapumuzishwa, kama vile Yesu aliahidi mu Matayo 11:28?

Tuko na waangalizi wazuri sana, tuko na marafiki wazuri sana, na tuko na kazi ya muzuri sana.​—w19.09, uku. 23.

Namna gani Mungu anaweza kutupatia hamu na nguvu za kutenda? (Flp. 2:13)

Wakati tunasoma Neno la Mungu na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma, Mungu anatutia nguvu, ni kusema, anatupatia hamu ya kufanya mapenzi yake na nguvu za kutenda. Roho yake inaweza kufanya uwezo wetu wa kizalikio ukuwe muzuri zaidi.​—w19.10, uku. 21.

Ni mambo gani ya maana yenye tunapaswa kufanya mbele ya kukamata uamuzi fulani muzito?

Mambo tano ya kufanya ni hii: Utafute habari kwa uangalifu. Usali ili upate hekima. Uchunguze nia yako. Ukuwe na miradi yenye kuwa wazi. Ukuwe na usawaziko.​—w19.11, uku. 27-29.

Wazo la kutokufa kwa nafsi lilitokana na mambo yenye Shetani alimuambiaka Eva?

Inaonekana ni hapana. Shetani alimuambia Eva kama hatakufa, hakumuambia kama ataonekana tu kuwa mwenye kufa. Hakuna hata wazo moja la dini ya uongo lenye liliokoka Garika. Inawezekana fundisho la kutokufa kwa nafsi lilianzishwa mbele Mungu asambaze watu wenye walikuwa wanajenga munara wa Babeli.​—w19.12, uku. 15.