Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 51

Unamujua Yehova Muzuri Kabisa?

Unamujua Yehova Muzuri Kabisa?

“Wale wenye kujua jina lako watakutegemea wewe; hautaacha hata kidogo wale wenye kukutafuta, Ee Yehova.”​—ZB. 9:10.

WIMBO 56 Fanya Kweli Iwe Njia Yako ya Maisha

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Kama vile mufano wa Angelito unaonyesha, kila mumoja wetu anapaswa kufanya nini?

WAZAZI wako ni Mashahidi wa Yehova? Kama ni vile, ukumbuke kama hauwezi kuwa rafiki ya Yehova kwa sababu tu wazazi wako ni marafiki wa Yehova. Ikuwe wazazi wetu wanamutumikia Mungu ao hapana, kila mumoja wetu anapaswa kufanya yeye mwenyewe urafiki wake pamoja na Yehova.

2 Fikiria mufano wa ndugu mwenye kuitwa Angelito. Watu wote wa familia yake walikuwa Mashahidi wa Yehova. Lakini, wakati alikuwa kijana, hakukuwa anajisikia kuwa karibu na Mungu. Anasema hivi: “Nilikuwa ninamutumikia Yehova juu tu nilipenda kufanya mambo yenye watu wa familia yangu walikuwa wanafanya.” Lakini, Angelito aliamua kutumia wakati zaidi ili kusoma na kufikiri sana juu ya Neno la Mungu, na akaanza kusali kwa Yehova mara mingi zaidi. Alipata matokeo gani? Angelito anasema hivi: “Nilitambua kama njia moja tu ya kunisaidia nimukaribie zaidi Yehova, Baba yangu, ni kujikaza kumujua mimi mwenyewe.” Mufano wa Angelito unaleta maulizo fulani ya maana: Kuko tofauti gani kati ya kumujua Yehova na kumujua muzuri kabisa? Na tunaweza kufanya nini ili tumujue Yehova muzuri kabisa?

3. Kuko tofauti gani kati ya kumujua Yehova na kumujua muzuri kabisa?

3 Tunaweza kusema kama mutu anamujua Yehova kama anajua jina lake ao mambo fulani yenye amesema na kufanya. Lakini, kumujua Yehova muzuri kabisa kunatia ndani mambo mingi. Tunapaswa kutumia wakati ili kujifunza juu ya Yehova na sifa zake za muzuri sana. Ni kwa kufanya vile tu njo tunaweza kuanza kuelewa juu ya nini anasema ao kufanya mambo fulani. Hilo litatusaidia kujua ikiwa anakubali mawazo, maamuzi, na matendo yetu. Kisha kujua mambo yenye Yehova anapenda tufanye, tunapaswa kuifanya.

4. Kuchunguza mifano ya watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia kutatusaidia namna gani?

4 Watu fulani wanaweza kutuchekelea kwa sababu tunapenda kumutumikia Yehova, na wanaweza kutupinga hata zaidi wakati tunaanza kujiunga na watu wake. Lakini, kama tunamutegemea Yehova, hawezi kutuacha hata kidogo. Wakati tunamutegemea Yehova, tutakuwa tuko tunaanzisha urafiki pamoja na Mungu wenye utaendelea maisha yetu yote. Tunaweza kumujua Yehova muzuri kabisa? Ndiyo, tunaweza! Mifano ya watu wenye hawakukuwa wakamilifu, kama vile Musa na Mufalme Daudi, inaonyesha kama inawezekana. Wakati tunazungumuzia mambo yenye walifanya, tutajibu maulizo mbili yenye kufuata: Ni nini iliwasaidia wafikie kumujua Yehova? Na mifano yao inaweza kutufundisha nini?

MUSA ALIONA “ULE MWENYE HAONEKANE”

5. Musa alichagua kufanya nini?

5 Musa alichagua kumutumikia Mungu. Wakati Musa alikuwa na miaka karibu 40, alichagua kujiunga na watu wa Mungu, ni kusema, Waebrania, kuliko kujulikana kuwa “mwana wa binti ya Farao.” (Ebr. 11:24) Musa alikataa kuwa na cheo cha juu. Musa alijiunga na Waebrania, wenye walikuwa watumwa mu inchi ya Misri hata kama alijua kwamba Farao, mutawala mwenye nguvu zaidi mwenye alionwa kuwa mungu, angemukasirikia. Musa alikuwa na imani kabisa! Alimutegemea Yehova. Kumutegemea Mungu njo lilikuwa jambo la maana lenye lilifanya Musa akuwe na urafiki wa sana pamoja na Yehova, urafiki wenye uliendelea maisha yake yote.​—Mez. 3:5.

6. Mufano wa Musa unaweza kutufundisha nini?

6 Jambo hilo linatufundisha nini? Kama Musa, sisi wote tunapaswa kuamua ikiwa tutamutumikia Yehova na kujiunga na watu wake. Inaweza kuomba kujiima mambo fulani ili tumutumikie Mungu, na watu wenye hawamujue Yehova wanaweza kutupinga. Lakini, kama tunamutegemea Baba yetu wa mbinguni, tunaweza kuwa hakika kama atatutegemeza!

7-8. Musa aliendelea kujifunza nini?

7 Musa aliendelea kujifunza juu ya sifa za Yehova na kufanya mapenzi yake. Kwa mufano, wakati Yehova alimuomba Musa atoshe taifa la Israeli katika utumwa, Musa aliogopa na mara mingi alimuambia Yehova kuwa hastahili. Jibu la Mungu lilionyesha kama alikuwa na huruma, ni kusema, alielewa namna Musa alikuwa anajisikia na alimusaidia. (Kut. 4:10-16) Kwa hiyo, Musa aliweza kumutangazia Farao ujumbe muzito wa hukumu. Kisha Musa aliona namna Yehova alitumia uwezo wake wakati aliokoa Waisraeli lakini akaharibu Farao na majeshi yake mu Bahari Nyekundu.​—Kut. 14:26-31; Zb. 136:15.

8 Kisha Musa kutosha Waisraeli mu inchi ya Misri, walinungunika mara kwa mara juu ya mambo mbalimbali. Lakini, Musa aliona namna Yehova alionyesha uvumilivu sana mu namna alitendea watu wake wenye alikuwa ametosha katika utumwa. (Zb. 78:40-43) Pia, Musa aliona namna Yehova alionyesha unyenyekevu wa pekee wakati aliamua kama hataharibu tena Waisraeli kwa sababu Musa alimuomba afanye vile.​—Kut. 32:9-14.

9. Kulingana na Waebrania 11:27, Musa alikuwa na urafiki wa namna gani pamoja na Yehova?

9 Kisha kutoka Misri, urafiki kati ya Musa na Yehova ulifikia kuwa wenye nguvu sana, ni kama vile alikuwa anamuona Baba yake wa mbinguni. (Soma Waebrania 11:27.) Biblia inaonyesha kama urafiki huo ulikuwa wenye nguvu sana kwa kusema hivi: “Yehova alikuwa anazungumuza na Musa uso kwa uso, kama vile mwanadamu anazungumuza na mwanadamu mwingine.”​—Kut. 33:11.

10. Ili tumujue Yehova muzuri kabisa, tunapaswa kufanya nini?

10 Jambo hilo linatufundisha nini? Ili tumujue Yehova muzuri kabisa, hatupaswe tu kujifunza juu ya sifa zake lakini tunapaswa pia kufanya mapenzi yake. Mapenzi ya Yehova leo ni kwamba “watu wa namna zote waokolewe na wapate ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli.” (1 Ti. 2:3, 4) Njia moja ya kufanya mapenzi ya Mungu ni kufundisha wengine juu yake.

11. Wakati tunafundisha wengine juu ya Yehova, namna gani tunafikia kumujua muzuri zaidi?

11 Mara mingi, ni wakati tunafundisha wengine juu ya Yehova njo tunafikia sisi wenyewe kumujua muzuri zaidi. Kwa mufano, tunaona kabisa kama Yehova ni mwenye huruma wakati anatusaidia kupata watu wenye wanapenda kuwa marafiki wake. (Yoh. 6:44; Mdo. 13:48) Tunaona nguvu za Neno la Mungu wakati tunaona wanafunzi wetu wa Biblia wanaacha tabia za mubaya na kuanza kuvaa utu mupya. (Kol. 3:9, 10) Na tunaona mambo yenye kuhakikisha kabisa kama Mungu iko na uvumilivu wakati anatolea watu wa eneo letu nafasi mbalimbali za kujifunza juu yake ili wafikie kuokolewa.​—Ro. 10:13-15.

12. Kulingana na Kutoka 33:13, Musa alimuomba Yehova nini, na juu ya nini?

12 Musa hakuona urafiki wake pamoja na Yehova kuwa jambo la kawaida tu. Hata wakati Musa alifanya matendo yenye nguvu katika jina la Mungu, alimuomba Mungu kwa heshima amusaidie amujue muzuri zaidi. (Soma Kutoka 33:13.) Musa alikuwa na miaka zaidi ya 80 wakati alimuomba Yehova vile, lakini alijua kama alikuwa angali na mambo mingi ya kujifunza juu ya Baba yake wa mbinguni mwenye upendo.

13. Njia moja ya kuonyesha kama tunaona urafiki wetu pamoja na Mungu kuwa wa maana sana ni gani?

13 Jambo hilo linatufundisha nini? Hata kama tumemutumikia Yehova kwa miaka mingi ao kidogo, hatupaswe hata kidogo kuona urafiki wetu pamoja naye kuwa jambo la kawaida tu. Njia moja ya kuonyesha kama tunaona urafiki wetu pamoja na Mungu kuwa wa maana sana ni kuzungumuza naye katika sala.

14. Juu ya nini sala ni ya maana sana ili kujifunza juu ya Mungu?

14 Siri ya kufanya urafiki wenye nguvu na mutu fulani ni kuzungumuza naye kwa ukawaida. Kwa hiyo, umukaribie Mungu kwa kusali kwake kwa ukawaida na usiogope kumuelezea mawazo yako ya ndani kabisa. (Efe. 6:18) Krista, mwenye kuishi mu inchi ya Uturuki, anasema hivi: “Kila wakati ninamuelezea Yehova mawazo yangu katika sala na kuona namna ananisaidia, ninamupenda na kumutegemea zaidi. Kuona namna Yehova anajibu sala zangu kumenisaidia nimuone Yehova kuwa Baba yangu na Rafiki yangu.”

MUTU MWENYE KUFURAHISHA MOYO WA YEHOVA

15. Yehova alisema nini juu ya Mufalme Daudi?

15 Mufalme Daudi alizaliwa mu taifa lenye lilikuwa limejitoa kwa Yehova Mungu. Daudi hakumuabudu Yehova kwa sababu tu alizaliwa katika familia yenye ilikuwa inamuabudu Yehova. Alifanya urafiki wake mwenyewe pamoja na Mungu, na Mungu alimupenda sana. Yehova mwenyewe alisema kama Daudi alikuwa “mutu mwenye kufurahisha moyo [wake].” (Mdo. 13:22) Ni nini ilimusaidia Daudi akuwe rafiki wa sana wa Yehova?

16. Daudi alijifunza nini juu ya Yehova wakati alikuwa anaangalia uumbaji?

16 Daudi alijifunza juu ya Yehova kupitia uumbaji. Wakati Daudi alikuwa kijana, alipitisha saa mingi inje wakati alikuwa anachunga kondoo za baba yake. Pengine ni wakati huo njo alianza kufikiri sana juu ya vitu vyenye Yehova ameumba. Kwa mufano, wakati Daudi aliangalia anga usiku, hakuona tu maelfu ya nyota lakini alitambua pia sifa za Ule mwenye aliumba nyota hizo. Jambo hilo lilimuchochea Daudi aandike hivi: “Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu; na anga lenye kuwa juu linatangaza kazi ya mikono yake.” (Zb. 19:1, 2) Wakati Daudi alifikiri juu ya namna wanadamu waliumbwa, aliona kama Yehova ni mwenye hekima sana. (Zb. 139:14) Wakati Daudi alijikaza kuelewa kazi ya Yehova, alitambua kama hakukuwa kitu kabisa kwa kulinganishwa na Yehova.​—Zb. 139:6.

17. Tunaweza kujifunza nini kama tunafikiri sana juu ya uumbaji?

17 Jambo hilo linatufundisha nini? Upendezwe na uumbaji. Usiangalie tu vitu vya muzuri vyenye Yehova ameumba, lakini ushangazwe sana na vitu vyenye unaona! Mu maisha yako ya kila siku, fikiri sana juu ya mambo yenye vitu vyenye kukuzunguka, kama vile mimea, wanyama, na watu, vinakufundisha juu ya Yehova. Ukifanya vile, kila siku utajifunza mambo mingi juu ya Baba yako mwenye upendo. (Ro. 1:20) Na kila siku utamupenda Yehova hata zaidi.

18. Kulingana na Zaburi ya 18, Daudi alitambua nini?

18 Daudi alitambua kama Yehova alikuwa anamusaidia. Kwa mufano, wakati Daudi aliua simba na dubu ili wasikule kondoo za baba yake, alitambua kama ni Yehova njo alimusaidia kuua wanyama hao wakali sana. Wakati alimushinda Goliati, mupiganaji murefu na munene sana, aliona waziwazi kama ni Yehova njo alikuwa anamuongoza. (1 Sa. 17:37) Na wakati Daudi aliponyoka Mufalme Sauli mwenye wivu, alitambua kama Yehova njo alimuokoa. (Zb. 18, utangulizi) Daudi angekuwa mutu mwenye kiburi, angewaza kama alifanya ile mambo yote kwa nguvu yake mwenyewe. Lakini, Daudi alikuwa munyenyekevu, njo maana alikuwa anaona mukono wa Yehova mu maisha yake.​—Zb. 138:6.

19. Mufano wa Daudi unaweza kutufundisha nini?

19 Jambo hilo linatufundisha nini? Hatupaswe tu kumuomba Yehova musaada. Tunapaswa pia kujikaza ili kutambua wakati anatusaidia na namna anatusaidia. Kama tunatambua kwa unyenyekevu mipaka yetu, tutaona waziwazi kama Yehova anatusaidia kufanya mambo yenye hatuna uwezo wa kufanya. Na kila wakati tunaona namna Yehova anatusaidia, urafiki wetu pamoja naye utakuwa wenye nguvu zaidi. Isaac, ndugu mumoja wa Fiji mwenye amemutumikia Yehova kwa miaka mingi, aliona kama jambo hilo ni la kweli. Anasema hivi: “Wakati ninafikiria maisha yangu, ninaona namna Yehova amenisaidia tangu wakati nilianza kujifunza Biblia mupaka leo. Kwa hiyo, ninamuona Yehova kuwa mutu wa kweli.”

20. Urafiki wa Daudi pamoja na Mungu unaweza kutufundisha nini?

20 Daudi aliiga sifa za Yehova. Yehova alituumba na uwezo wa kuiga sifa zake. (Mwa. 1:26) Wakati tunajifunza zaidi juu ya sifa za Yehova, tutakuwa na uwezo zaidi wa kumuiga. Daudi alifikia kumujua muzuri kabisa Baba yake wa mbinguni, njo maana alikuwa anamuiga katika namna alitendea wengine. Fikiria mufano moja tu. Daudi alimutendea Yehova zambi wakati alifanya uzinifu na Bat-sheba na kisha akafanya mipango ili bwana yake auawe. (2 Sa. 11:1-4, 15) Lakini, Yehova aliamua kumuonyesha Daudi rehema, juu yeye pia alikuwa ameonyesha wengine rehema. Juu Daudi alikuwa na urafiki wenye nguvu pamoja na Yehova, Waisraeli walimupenda sana na Yehova alimutumia kuwa mufano kwa wafalme wengine wa Israeli.​—1 Fa. 15:11; 2 Fa. 14:1-3.

21. Kulingana na Waefeso 4:24 na 5:1, matokeo itakuwa nini kama tunakuwa “waigaji wa Mungu”?

21 Jambo hilo linatufundisha nini? Tunapaswa kuwa “waigaji wa Mungu.” Wakati tunamuiga Mungu, tunapata faida sisi wenyewe na tunajifunza mambo mingi juu yake. Wakati tunaiga sifa zake, tunaonyesha kama tuko watoto wake.​—Soma Waefeso 4:24; 5:1.

TAFUTA KUMUJUA YEHOVA MUZURI ZAIDI

22-23. Matokeo itakuwa nini kama tunatumia mambo yenye tunajifunza juu ya Yehova?

22 Kama vile tumeona, tunaweza kujifunza juu ya Yehova kupitia uumbaji na kupitia Neno lake, Biblia. Kitabu hicho cha pekee kiko na mifano mingi sana ya watumishi waaminifu wa Mungu wenye tunaweza kuiga, kama vile Musa na Daudi. Yehova amefanya sehemu yake. Tunapaswa kufanya sehemu yetu kwa kujifunza mambo mingi juu yake kadiri tunaweza.

23 Tutaendelea kujifunza juu ya Yehova milele na milele. (Muh. 3:11) Jambo la maana haiko kujua mambo mingi juu yake, lakini ni namna tunatumia mambo yenye tunajua. Kama tunatumia mambo yenye tunajifunza na kujikaza kumuiga Baba yetu mwenye upendo, ataendelea kutukaribia zaidi. (Yak. 4:8) Anatuhakikishia kupitia Neno lake kama hataacha hata kidogo wale wenye kumutafuta.

WIMBO 80 “Onjeni Mwone Kwamba Yehova Ni Mwema”

^ fu. 5 Watu wengi wanaamini kama Mungu iko, lakini hawamujue muzuri kabisa. Kumujua Yehova maana yake nini, na mufano wa Musa na wa Mufalme Daudi unaweza kutufundisha nini juu ya kuwa na urafiki wa sana pamoja naye? Tutajibu ile maulizo katika habari hii.