Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 49

Kuko Wakati wa Kufanya Kazi na Wakati wa Kupumuzika

Kuko Wakati wa Kufanya Kazi na Wakati wa Kupumuzika

“Mukuje . . . mahali kwenye hakuna watu ili mupumuzike kidogo.”​—MK. 6:31.

WIMBO 143 Endeleeni Kufanya Kazi, Kesheni, na Kusubiri

KIFUPI CHA HABARI *

1. Namna gani watu wengi wanaona kazi?

MAHALI kwenye unaishi, namna gani watu wengi wanaona kazi na kupumuzika? Mu inchi za mingi, watu wako wanatumika sana na wanatumika saa mingi kuliko zamani. Watu wenye kutumika sana, mara mingi hawana wakati wa kupumuzika, hawana wakati wa kupitisha pamoja na familia zao, ao kutimiza mahitaji ya familia zao. (Muh. 2:23) Tena, watu fulani hawapendake kufanya kazi kabisa na wanatafuta sababu za kutetea juu ya nini hawafanye kazi.​—Mez. 26:13, 14.

2-3. Yehova na Yesu walionyesha mufano gani juu ya kazi?

2 Watu wengi katika dunia wanatumika sana ao hawatumike kabisa. Lakini fikiria namna Yehova na Yesu wanaona kazi. Kwa kweli, Yehova anapenda kazi. Yesu alionyesha waziwazi jambo hilo wakati alisema hivi: “Baba yangu anaendelea kufanya kazi mupaka sasa, na mimi ninaendelea kufanya kazi.” (Yoh. 5:17) Fikiria kazi yote yenye Mungu alifanya wakati aliumba malaika wengi sana na ulimwengu muzima. Pia, tunaona vitu mingi vya muzuri vyenye Mungu aliumba hapa ku dunia. Njo maana muandikaji mumoja wa zaburi alisema hivi: “Kazi zako ni nyingi sana, Ee Yehova! Umezifanya zote kwa hekima. Dunia imejaa vitu vyenye umefanya.”​—Zb. 104:24.

3 Yesu alimuiga Baba yake. Alimusaidia Yehova wakati “alitayarisha mbingu.” Alikuwa pamoja naye ‘akiwa fundi wa kazi.’ (Mez. 8:27-31) Kisha, wakati Yesu alikuwa ku dunia, alifanya kazi ya muzuri sana. Aliona kazi hiyo kuwa chakula, na mambo yote yenye alifanya ilionyesha kabisa kama Mungu njo mwenye alimutuma.​—Yoh. 4:34; 5:36; 14:10.

4. Mufano wa Yehova na Yesu unaweza kutufundisha nini juu ya kupumuzika?

4 Je, mufano wenye Yehova na Yesu walionyesha wa kutumika kwa bidii, unamaanisha kama hatupaswe kupumuzika? Hapana kabisa. Yehova hawezi kuchoka hata kidogo, kwa hiyo hana lazima ya kupumuzika kisha kufanya jambo fulani. Lakini Biblia inasema kama, kisha kuumba mbingu na dunia, Yehova “alipumuzika na kustarehe.” (Kut. 31:17) Maana yake, Yehova aliacha kuumba vitu na akatumia wakati fulani ili kufurahia vitu vyenye alikuwa amefanya. Na hata kama Yesu alitumika kwa bidii wakati alikuwa ku dunia, alijikaza kuwa na wakati wa kupumuzika na wakati wa kula chakula pamoja na marafiki wake.​—Mt. 14:13; Lu. 7:34.

5. Watumishi wengi wa Mungu wako na tatizo gani?

5 Biblia inatia moyo watumishi wa Mungu wapende kazi. Wanapaswa kutumika kwa bidii kuliko kuwa wavivu. (Mez. 15:19) Pengine unafanya kazi ya kimwili ili kutimiza mahitaji ya familia yako. Na wanafunzi wote wa Kristo wako na daraka la kuhubiri habari njema. Lakini, unapaswa pia kupata wakati wa kutosha ili kupumuzika. Wakati fulani, iko nguvu kwako kupata wakati wa kufanya kazi ya kimwili, kuhubiri, na kupumuzika? Namna gani tunaweza kuamua muda wenye tutapitisha ili kufanya kazi na muda wenye tutapitisha ili kupumuzika?

NAMNA YA KUWA NA MAWAZO YENYE KUFAA JUU YA KAZI NA KUPUMUZIKA

6. Namna gani andiko la Marko 6:30-34 linaonyesha kama Yesu alikuwa na mawazo yenye kufaa juu ya kazi na kupumuzika?

6 Ni jambo la maana tukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya kazi. Mufalme Sulemani aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika kama kila kazi iko na wakati wake wenye uliwekwa. Alitaja wakati wa kupanda, kujenga, kulia, kucheka, kucheza, na wakati wa kufanya mambo ingine. (Muh. 3:1-8) Kwa kweli, sehemu mbili za maana za maisha ni kufanya kazi na kupumuzika. Yesu alikuwa na mawazo yenye kufaa juu ya kazi na kupumuzika. Wakati fulani, mitume walirudia kisha kuhubiri sana. Walikuwa na mambo mingi ya kufanya na “hawakupata hata wakati wa kula chakula.” Yesu aliwaambia hivi: “Mukuje ninyi wenyewe mahali kwenye hakuna watu ili mupumuzike kidogo.” (Soma Marko 6:30-34.) Yesu alijua kama yeye na wanafunzi wake walikuwa na lazima ya kupumuzika, hata kama kila mara hawakupata wakati wa kupumuzika kama vile walipenda.

7. Kujifunza mambo yenye Sheria ilisema juu ya Sabato kutatusaidia namna gani?

7 Wakati fulani, sisi wote tuko na lazima ya kupumuzika ao kufanya mambo ingine kuliko ile yenye tunazoea kufanya kila siku. Mupango wenye Mungu alifanya kwa ajili ya watu wake wakati wa zamani unatuonyesha vile; mupango huo ni Sabato ya kila juma. Hata kama leo hatuongozwe na Sheria ya Musa, tunaweza kupata faida kwa kujifunza mambo yenye sheria hiyo ilisema juu ya Sabato. Mambo yenye tutajifunza juu ya Sabato itatusaidia tuchunguze mawazo yetu juu ya kazi na kupumuzika.

SABATO: WAKATI WA KUPUMUZIKA NA KUMUABUDU MUNGU

8. Kulingana na Kutoka 31:12-15, Sabato ilikuwa siku ya nini?

8 Neno la Mungu linasema kama kisha kufanya kazi ya kuumba kwa “siku” sita, Mungu alipumuzika, ni kusema, aliacha kuumba vitu ku dunia. (Mwa. 2:2) Lakini, Yehova anapenda kazi, na katika njia fulani “anaendelea kufanya kazi.” (Yoh. 5:17) Yehova alifanya kazi kwa “siku” sita na akapumuzika “siku” ya saba na aliambia pia Waisraeli wapumuzike kila siku ya saba. Mungu alisema kama Sabato ilikuwa alama kati yake na Israeli. Ilikuwa siku ya “pumuziko kamili . . . , kitu kitakatifu kwa Yehova.” (Soma Kutoka 31:12-15.) Sheria yenye ilikataza kufanya kazi ilihusu kila mutu, kutia ndani watoto, watumwa, na hata wanyama wenye walitumiwa katika mashamba. (Kut. 20:10) Ilisaidia watu wakaze akili zaidi juu ya mambo ya kiroho.

9. Katika siku za Yesu, watu fulani walikuwa na mawazo gani yenye haifae juu ya Sabato?

9 Siku ya Sabato ilikuwa muzuri kwa watu wa Mungu; lakini, viongozi wengi wa dini katika siku za Yesu walitunga sheria kali sana juu ya Sabato. Walisema kama hata kukata masuke fulani ya nafaka za kula ao kuponyesha mutu mwenye alikuwa mugonjwa ilikuwa kuvunja sheria ya Sabato. (Mk. 2:23-27; 3:2-5) Ile mawazo haikupatana na mawazo ya Mungu, na Yesu alionyesha waziwazi jambo hilo wale wenye walimusikiliza.

Familia ya Yesu ilitumia Sabato ili kukaza akili juu ya mambo ya kiroho (Picha hii inapatana na fungu la 10) *

10. Kulingana na Matayo 12:9-12, Yesu alikuwa na mawazo gani juu ya Sabato?

10 Yesu na wanafunzi wake Wayahudi walishika Sabato kwa sababu walikuwa wanaongozwa na Sheria ya Musa. * Lakini Yesu alionyesha kupitia maneno na matendo yake kama iliomba kuwa na usawaziko juu ya kushika Sabato na kama haikukuwa mubaya kufanya matendo ya muzuri ili kusaidia wengine siku ya Sabato. Alisema waziwazi hivi: “Inaruhusiwa kufanya jambo la muzuri siku ya Sabato.” (Soma Matayo 12:9-12.) Hakuona kama kufanya tendo fulani la muzuri ili kusaidia wengine ilikuwa kuvunja sheria ya Sabato. Matendo ya Yesu ilionyesha kama alielewa sababu ya maana sana yenye ilifanya Mungu aambie Waisraeli wapumuzike siku ya Sabato. Juu siku hiyo watu wa Mungu hawakufanya kazi zao za kila siku, hilo liliwasaidia wakaze akili juu ya mambo ya kiroho. Yesu alikomalia mu familia yenye ilikuwa inatumia Sabato ili kufanya mambo ya kiroho. Mambo yenye Yesu alifanya wakati alikuwa mu muji wake wa Nazareti inaonyesha jambo hilo. Biblia inasema hivi: “Kulingana na desturi [ya Yesu] siku ya Sabato, akaingia katika sinagogi na akasimama ili kusoma.”​—Lu. 4:15-19.

UKO NA MAWAZO GANI JUU YA KAZI?

11. Ni nani mwenye alimuonyesha Yesu mufano muzuri juu ya kazi?

11 Kwa kweli, Yosefu alimufundisha Yesu, mwana wake mwenye alikuwa analea, kazi ya useremala na pia mawazo ya Mungu juu ya kazi. (Mt. 13:55, 56) Na inawezekana Yesu aliona namna Yosefu alikuwa anafanya kazi kwa bidii kila siku ili kutimiza mahitaji ya familia yake, yenye ilikuwa na watu wengi. Njo maana, kisha wakati fulani, Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: “Mufanyakazi anastahili malipo yake.” (Lu. 10:7) Kwa kweli, Yesu alijua namna ya kufanya kazi kwa bidii.

12. Ni maandiko gani yenye kuonyesha mawazo ya Biblia juu ya kazi?

12 Mutume Paulo pia alijua namna ya kufanya kazi kwa bidii. Kazi yake kubwa ilikuwa kutoa ushahidi juu ya jina la Yesu na mambo yenye Yesu alifundisha. Lakini, Paulo alikuwa anafanya kazi ili kutimiza mahitaji yake. Watesalonike walijua kama alifanya “kazi ya jasho na ya taabu,” ‘alitumika usiku na muchana’ ili asiwekee mutu yeyote “muzigo muzito.” (2 Te. 3:8; Mdo. 20:34, 35) Wakati Paulo aliandika juu ya kazi yake, pengine alikuwa anazungumuzia kazi yake ya kutengeneza mahema. Wakati alikuwa Korinto, alibakia pamoja na Akila na Prisila na ‘alifanya kazi pamoja nao, kwa maana kazi yao ilikuwa kutengeneza mahema.’ Kusema kama Paulo alitumika “usiku na muchana” hakumaanishe kama alikuwa anatumika bila kupumuzika. Siku fulani, hakukuwa anafanya kazi ya kutengeneza mahema, kwa mufano siku ya Sabato. Siku hiyo, alikuwa anapata nafasi za kuhubiria Wayahudi, wenye hawakukuwa wanatumika pia siku ya Sabato.​—Mdo. 13:14-16, 42-44; 16:13; 18:1-4.

13. Mufano wa Paulo unaweza kutufundisha nini?

13 Mutume Paulo alionyesha mufano muzuri. Alipaswa kufanya kazi ya kimwili; lakini, alikuwa pia anafanya kwa ukawaida “kazi takatifu ya habari njema ya Mungu.” (Ro. 15:16; 2 Ko. 11:23) Alishauria wengine wafanye pia vile. Njo maana, Akila na Prisila walikuwa ‘wafanyakazi wenzake katika Kristo Yesu.’ (Ro. 12:11; 16:3) Paulo alishauria Wakorinto wakuwe na “mambo mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.” (1 Ko. 15:58; 2 Ko. 9:8) Hata Yehova alimuongoza mutume Paulo aandike hivi: “Kama mutu yeyote hataki kufanya kazi, basi asikule pia chakula.”​—2 Te. 3:10.

14. Yesu alipenda kusema nini wakati alisema maneno yenye kuwa mu Yohana 14:12?

14 Kazi ya maana zaidi katika siku hizi za mwisho ni kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Kwa kweli, Yesu alitabiri kama wanafunzi wake wangefanya kazi kubwa zaidi kuliko yeye! (Soma Yohana 14:12.) Hakupenda kusema kama tutafanya miujiza kama yeye. Lakini, alipenda kusema kama wanafunzi wake wangehubiri na kufundisha katika eneo kubwa zaidi, wangehubiri na kufundisha watu wengi zaidi, na wangefanya vile kwa wakati murefu zaidi kuliko yeye.

15. Tunapaswa kujiuliza maulizo gani, na juu ya nini?

15 Kama uko na kazi ya kimwili, ujiulize hivi: ‘Ku kazi yangu, ninajulikana kuwa mufanyakazi mwenye bidii? Ninamaliza kazi kwa wakati na ninaifanya kwa uwezo wangu wote?’ Kama unajibu ndiyo, inawezekana mukubwa wako wa kazi atakutumainia. Na wafanyakazi wenzako wanaweza kuwa tayari kusikiliza habari njema. Kuhusu kazi ya kuhubiri na kufundisha, ujiulize hivi: ‘Ninajulikana kuwa muhubiri mwenye bidii? Ninajitayarisha muzuri wakati ninatembelea watu kwa mara ya kwanza? Ninarudilia haraka watu wenye kupendezwa? Na, ninafanya kwa ukawaida sehemu zingine za kazi ya kuhubiri?’ Kama unajibu ndiyo kwa ile maulizo, utapata furaha katika kazi yako ya kuhubiri.

UKO NA MAWAZO GANI JUU YA KUPUMUZIKA?

16. Yesu na mitume wake walikuwa na mawazo gani juu ya kupumuzika, lakini watu wengi leo wako na mawazo gani?

16 Yesu alijua kama wakati fulani yeye na mitume wake walikuwa na lazima ya kupumuzika. Lakini, watu wengi wa wakati huo na watu wengi leo wako kama ule mwanaume tajiri mwenye Yesu alizungumuzia katika mufano wake. Mwanaume huyo alijiambia hivi: “Tulia, kula, kunywa, na ujifurahishe.” (Lu. 12:19; 2 Ti. 3:4) Aliwaza kama raha na kupumuzika njo ilikuwa mambo ya maana zaidi mu maisha. Lakini, Yesu na mitume wake hawakuona kama raha njo lilikuwa jambo la maana zaidi mu maisha yao.

Kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya kazi na kupumuzika kutatusaidia tukaze akili juu ya kufanya mambo ya muzuri yenye inatuletea furaha (Picha hizi zinapatana na fungu la 17) *

17. Namna gani tunatumia wakati wetu wa mapumuziko?

17 Leo, tunajikaza kumuiga Yesu kwa kutumia wakati wetu wa mapumuziko ili kupumuzika na pia kufanya mema kwa kuhubiria wengine na kuhuzuria mikutano ya Kikristo. Kwa kweli, tunaona kama kufanya wanafunzi na kuhuzuria mikutano ni mambo ya maana sana, kwa hiyo, tunajikaza sana ili tuendelee kufanya kwa ukawaida ile mambo ya kiroho. (Ebr. 10:24, 25) Hata wakati tuko mu mapumuziko, tunaendelea kuheshimia programu yetu ya kuhuzuria mikutano nafasi yoyote kwenye tunapatikana na tunatafuta nafasi za kuhubiria watu wenye tunakutana nao.​—2 Ti. 4:2.

18. Mufalme wetu, Kristo Yesu, anapenda tufanye nini?

18 Tuko wenye shukrani sana juu Mufalme wetu, Kristo Yesu, hatuombe tufanye mambo yenye hatuna uwezo wa kufanya na anatusaidia tukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya kazi na kupumuzika! (Ebr. 4:15) Anapenda tukuwe tunapumuzika. Anapenda pia tufanye kazi ya kimwili kwa bidii ili kutimiza mahitaji yetu na tufanye kazi ya kufanya wanafunzi yenye kuleta furaha. Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia mambo yenye Yesu amefanya ili kutuweka huru kutoka katika utumwa fulani mubaya sana.

WIMBO 38 Atakupa Nguvu

^ fu. 5 Maandiko inatufundisha namna ya kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi na kupumuzika. Habari hii itatumia mufano wa Sabato yenye Waisraeli walikuwa wanafanya kila juma ili kutusaidia tufikirie namna tunaona kazi na kupumuzika.

^ fu. 10 Wanafunzi walikuwa wanaheshimia sana sheria ya Sabato, njo maana waliacha kwanza kutayarisha vitu vyenye wangepakaa mwili wa Yesu mupaka Sabato iishe.​—Lu. 23:55, 56.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Yosefu anapeleka familia yake ku sinagogi siku ya Sabato.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Baba mwenye anafanya kazi ya kimwili ili kutimiza mahitaji ya familia yake anatumia wakati wake wa mapumuziko ili kufanya mambo ya kiroho, hata wakati yeye na familia yake wako mu mapumuziko.