Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 52

Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova

Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova

“Watoto ni uriti kutoka kwa Yehova.”​—ZB. 127:3, maelezo ya chini.

WIMBO 134 Watoto​—Amana Kutoka kwa Mungu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Yehova anapatia wazazi daraka gani?

YEHOVA aliumba mwanaume na mwanamuke wa kwanza wakiwa na tamaa ya kuzaa watoto. Njo maana Biblia inasema hivi: “Watoto ni uriti kutoka kwa Yehova.” (Zb. 127:3, maelezo ya chini) Maana yake nini? Wazia rafiki yako wa sana anakupatia feza za mingi sana ili umuwekee. Utajisikia namna gani? Inawezekana utaona kama anakuonyesha heshima kwa sababu anakutumainia. Lakini pengine utakuwa na wasiwasi juu ya namna utachunga feza hizo muzuri. Yehova, rafiki yetu wa sana, anapatia wazazi jambo fulani la kuchunga lenye kuwa la maana sana kuliko feza. Anawapatia daraka la kusaidia watoto wao wakuwe salama na wakuwe na furaha.

2. Tutazungumuzia maulizo gani?

2 Ni nani anapaswa kuamua ikiwa bibi na bwana wanapaswa kuzaa watoto na ni wakati gani wanapaswa kufanya vile? Na wazazi wanapaswa kufanya nini ili kusaidia watoto wao wakuwe na maisha yenye furaha? Fikiria kanuni fulani zenye kupatikana katika Neno la Mungu zenye zinaweza kusaidia bibi na bwana Wakristo wakamate maamuzi ya muzuri.

HESHIMIA UAMUZI WA BIBI NA BWANA

3. (a) Ni nani anapaswa kuamua ikiwa bibi na bwana watazaa watoto? (b) Watu wa familia na marafiki wa bibi na bwana wanapaswa kukumbuka kanuni gani ya Biblia?

3 Katika desturi fulani, watu wanatazamia bibi na bwana wazae watoto kisha tu kuoana. Watu wa familia yao na marafiki wao wanaweza kukaza sana bibi na bwana wazae watoto bila kukawia. Jethro, ndugu mumoja wa Asia, anasema hivi: “Mu kutaniko, wale wenye wako na watoto wanakaza bibi na bwana wenye hawana watoto wazae watoto.” Jeffrey, ndugu mwingine wa Asia, anasema hivi: “Watu fulani wanaambia bibi na bwana wenye hawana watoto kama hawatapata mutu wa kuwachunga wakati watazeeka.” Lakini, kila bibi na bwana wanapaswa kuamua wao wenyewe ikiwa watazaa watoto. Huo ni uamuzi wao; na ni daraka lao. (Gal. 6:5, maelezo ya chini) Kwa kweli, marafiki na watu wa familia wanapenda bibi na bwana wenye wanatokea kuoana wakuwe na furaha. Lakini wote hawapaswe kusahau kama uamuzi wa kuzaa watoto ao hapana ni uamuzi wa bibi na bwana.​—1 Te. 4:11.

4-5. Ni mambo gani mbili yenye bibi na bwana wanapaswa kuzungumuzia, na ni wakati gani wanapaswa kuzungumuzia ile mambo? Fasiria.

4 Bibi na bwana wenye wanaamua kuzaa watoto wanapaswa kuzungumuzia mambo mbili ya maana sana: Jambo la kwanza, ni wakati gani wanapenda kuzaa watoto? Jambo la pili, wanapenda kuzaa watoto ngapi? Ni wakati gani wanapaswa kuzungumuzia ile mambo? Na juu ya nini ni jambo la maana sana wazungumuzie ile mambo mbili?

5 Kwa kawaida, mbele mwanaume na mwanamuke waoane, wanapaswa kuzungumuzia jambo la kuzaa watoto. Juu ya nini wanapaswa kufanya vile mbele waoane? Sababu moja ni hii: ni jambo la maana wapatane juu ya jambo hilo. Pia, wanapaswa kuchunguza ikiwa wako tayari kutimiza daraka hilo. Wamoja wameamua wangojee mwaka moja ao mbili mbele wazae watoto kwa sababu kukomalisha watoto kutawaomba watumie wakati mingi na nguvu mingi. Wanafikiri kama kungojea wakati kidogo kutawasaidia wazoee kwanza maisha ya ndoa na wakaribiane zaidi.​—Efe. 5:33.

6. Juu tunaishi katika nyakati za hatari, bibi na bwana fulani wamekamata uamuzi gani?

6 Wakristo wengine wameamua kufuata mufano wa wana watatu wa Noa na bibi zao. Bibi na bwana hao hawakuzaa watoto haraka. (Mwa. 6:18; 9:18, 19; 10:1; 2 Pe. 2:5) Yesu alifananisha wakati wetu na “siku za Noa,” na kwa kweli tunaishi katika “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.” (Mt. 24:37; 2 Ti. 3:1) Njo maana, bibi na bwana fulani wameamua wasizae kwanza watoto ili wafanye mambo mingi katika kazi ya Yehova.

Wakati wanaamua ikiwa watazaa watoto na ikiwa watazaa watoto ngapi, bibi na bwana wenye hekima wanapaswa “kuhesabia garama” (Picha hii inapatana na fungu la 7) *

7. Namna gani kanuni zenye kupatikana mu Luka 14:28, 29 na Mezali 21:5 zinaweza kusaidia bibi na bwana?

7 Wakati wanaamua ikiwa watazaa watoto na ikiwa watazaa watoto ngapi, bibi na bwana wenye hekima wanapaswa “kuhesabia garama.” (Soma Luka 14:28, 29.) Wazazi wenye uzoefu wanahakikisha kama haiombe tu feza ili kukomalisha watoto, lakini inaomba pia wakati na nguvu mingi. Kwa hiyo, ni jambo la maana bibi na bwana wafikirie maulizo hii: ‘Itaomba sisi wawili tufanye kazi ya kimwili ili kutimiza mambo ya lazima ya familia yetu? Tunakubaliana juu ya mambo yenye familia yetu iko nayo lazima kabisa? Kama itaomba sisi wawili tufanye kazi ya kimwili, ni nani atachunga watoto wetu? Ni nani mwenye atachochea mawazo na matendo yao?’ Bibi na bwana wenye wanazungumuzia ile maulizo, wanatumia maneno ya Mezali 21:5.​Soma.

Bwana mwenye upendo anapaswa kufanya nguvu yake yote ili kusaidia bibi yake (Picha hii inapatana na fungu la 8)

8. Ni magumu gani yenye bibi na bwana Wakristo wanapaswa kungojea, na bwana mwenye upendo anapaswa kufanya nini?

8 Kila muzazi anapaswa kutumia wakati mingi na nguvu mingi ili kuhangaikia mutoto. Kwa hiyo, kama bibi na bwana wako na watoto wengi wenye wanaachiana miaka kidogo, itakuwa nguvu kwa wazazi kuhangaikia kila mutoto. Bibi na bwana wenye walikuwa na watoto wengi wadogo walisema kama haiko mwepesi kabisa kukomalisha watoto. Mama anaweza kujisikia kuwa mwenye kuchoka kimwili na kiakili. Kwa sababu ya kuchoka, anaweza kushindwa kujifunza, kusali, na kuhubiri kwa ukawaida. Pia, inaweza kuwa nguvu kwake kufuata mikutano kwa uangalifu na kufaidika na mikutano hiyo. Kwa kweli, bwana mwenye upendo anapaswa kufanya nguvu yake yote ili kusaidia bibi yake kuhangaikia watoto wao, ku mikutano na ku nyumba. Kwa mufano, anaweza kusaidia bibi yake kufanya kazi za mu nyumba. Atajikaza sana kuongoza Ibada ya Familia kwa ukawaida ili wote wafaidike na programu hiyo. Na baba Wakristo wanapaswa kuhubiri kwa ukawaida pamoja na familia zao.

NAMNA YA KUFUNDISHA WATOTO WAMUPENDE YEHOVA

9-10. Wazazi wanapaswa kufanya nini ili kusaidia watoto wao?

9 Ni mambo gani fulani yenye wazazi wanapaswa kufanya ili kusaidia watoto wao wamupende Yehova? Wanaweza kufanya nini ili kulinda watoto wao na hatari za ulimwengu huu muovu? Fikiria mambo fulani yenye wazazi wanaweza kufanya.

10 Umuombe Yehova musaada katika sala. Fikiria mufano wa Manoa na bibi yake, wenye walimuzaa Samsoni. Wakati Manoa na bibi yake walijua kama watazaa mutoto mwanaume, Manoa alimuomba Yehova muongozo juu ya namna ya kukomalisha mutoto wao.

11. Namna gani wazazi wanaweza kuiga mufano wa Manoa, wenye kuzungumuziwa mu Waamuzi 13:8?

11 Nihad na bibi yake Alma, wenye kuishi katika inchi ya Bosnia na Herzegovina, walijifunza mambo mingi kupitia mufano wa Manoa. Wanasema hivi: “Kama Manoa, tulimuomba Yehova atufundishe namna ya kuwa wazazi wazuri. Na Yehova alijibu sala zetu mu njia mbalimbali: kupitia Maandiko, vichapo vyenye kutegemea Biblia, mikutano ya kutaniko, na mikusanyiko.”​—Soma Waamuzi 13:8.

12. Yosefu na Maria walionyesha watoto wao mufano gani?

12 Uwafundishe kupitia mufano wako. Mambo yenye unasema ni ya maana; lakini, inawezekana mambo yenye unafanya njo yenye itachochea sana watoto wako. Tunaweza kuwa hakika kama Yosefu na Maria walionyesha Yesu na watoto wao wengine mufano muzuri sana. Yosefu alifanya kazi kwa bidii ili kutimiza mahitaji ya familia yake. Tena, Yosefu alitia moyo watu wa familia yake wapende mambo ya kiroho. (Kum. 4:9, 10) Yosefu alikuwa anapeleka familia yake Yerusalemu “kila mwaka” kwenye sikukuu ya Pasaka, hata kama sheria haikumuomba afanye vile. (Lu. 2:41, 42) Inawezekana baba fulani wa siku zake waliona kama kupeleka familia yote Yerusalemu halikukuwa jambo la lazima, na ilikuwa kupoteza wakati, na feza. Lakini, ni wazi kama Yosefu aliona mambo ya kiroho kuwa ya maana sana na alifundisha watoto wake vile. Maria pia alijua Maandiko muzuri. Kupitia maneno na matendo yake, kwa kweli, alifundisha watoto wake wapende Neno la Mungu.

13. Namna gani bwana mumoja na bibi yake walifuata mufano wa Yosefu na Maria?

13 Nihad na Alma, wenye tumekwisha kuzungumuzia, walipenda kufuata mufano wa Yosefu na Maria. Namna gani kufanya vile kulisaidia wafundishe mutoto wao mwanaume amupende Mungu na kumutumikia? Wanasema hivi: “Kupitia namna yetu ya kuishi, tulijikaza kumuonyesha mutoto wetu mwanaume kama ni muzuri kuishi kulingana na kanuni za Yehova.” Nihad anaongeza hivi: “Ukuwe na tabia zenye unapenda mutoto wako akuwe nazo.”

14. Juu ya nini wazazi wanapaswa kujua marafiki wa watoto wao?

14 Saidia watoto wako wachague marafiki wazuri. Baba na mama wote wawili wanapaswa kujua marafiki wa watoto wao na mambo yenye watoto wao wako wanafanya. Maana yake, wazazi wanapaswa kujua watu wenye watoto wao wanazungumuzaka nao ku adresi za Enternete za kupashana habari na ku telefone zao. Marafiki hao wanaweza kuchochea mawazo na matendo ya watoto.​—1 Ko. 15:33.

15. Wazazi wanaweza kujifunza nini kupitia mufano wa Jessie?

15 Wazazi wanaweza kufanya nini kama hawajue mambo mingi juu ya ordinatere ao vyombo vingine vya kielektroniki? Jessie, baba mumoja mu inchi ya Ufilipino, anasema hivi: “Hatukujua mambo mingi juu ya vyombo vya kielektroniki. Lakini jambo hilo halikutuzuia kuonyesha watoto wetu hatari za vyombo vya kielektroniki.” Jessie hakukataza watoto wake kutumia vyombo vya kielektroniki juu tu hakujua mambo mingi juu ya vyombo hivyo. Anasema hivi: “Nilitia moyo watoto wangu watumie vyombo vyao vya kielektroniki ili kujifunza luga mupya, kutayarisha mikutano, na kusoma Biblia kila siku.” Kama uko muzazi, je, umesoma na kuzungumuzia pamoja na watoto wako mashauri yenye usawaziko juu ya kutuma ujumbe ku telefone, kutia picha ku Enternete ao kuzitumia wengine, yenye unaweza kupata katika sehemu “Vijana” yenye kuwa ku jw.org®? Je, umeangalia pamoja nao video Uko Mutumwa wa Vyombo Vyako vya Kielektroniki? na video Tumia kwa Hekima Site za Enternete za Kupashana Habari? * Habari hizo zinaweza kusaidia sana wakati unafundisha watoto wako namna ya kutumia vyombo vya kielektroniki kwa hekima.​—Mez. 13:20.

16. Wazazi wengi wamefanya mipango gani, na wamepata matokeo gani?

16 Wazazi wengi wanajikaza sana kufanya mipango ya kusaidia watoto wao wapitishe wakati pamoja na ndugu na dada wenye kuonyesha mufano muzuri katika kazi ya Mungu. Kwa mufano, N’Déni na Bomine, bwana mumoja na bibi yake mu inchi ya Côte d’Ivoire, mara mingi walikuwa wanapangisha mwangalizi wa muzunguko kwao. N’Déni anasema hivi: “Kufanya vile kulisaidia sana mutoto wetu mwanaume. Alianza kufanya kazi ya upainia na leo iko mwangalizi wa badala.” Unaweza pia kufanya mipango ili watoto wako wapitishe wakati pamoja na ndugu na dada kama hao?

17-18. Ni wakati gani wazazi wanapaswa kuanza kufundisha watoto?

17 Anza kufundisha watoto wakati wangali wadogo sana. Wazazi watapata matokeo ya muzuri zaidi kama wanaanza kufundisha watoto wao wakati wangali wadogo sana. (Mez. 22:6) Fikiria mufano wa Timoteo, mwenye kisha wakati fulani, alianza kusafiri pamoja na mutume Paulo. Eunike, mama ya Timoteo, na Loisi, tate (ao nkambo) yake walimufundisha “tangu utoto.”​—2 Ti. 1:5; 3:15.

18 Jean-Claude na Peace, bwana mwingine na bibi yake mu inchi ya Côte d’Ivoire, waliweza kufundisha watoto wao wote sita wamupende Yehova na kumutumikia. Ni nini iliwasaidia waweze kufanya vile? Walifuata mufano wa Eunike na Loisi. Wanasema hivi: “Tulikazia Neno la Mungu katika watoto wetu tangu utoto, muda mufupi tu kisha wao kuzaliwa.”​—Kum. 6:6, 7.

19. Inaomba nini ili kukazia Neno la Mungu katika watoto wako?

19 “Kukazia” Neno la Yehova katika watoto wako, maana yake nini? “Kukazia” maana yake “kufundisha na kukumbusha kwa kurudilia-rudilia.” Ili kufanya vile, wazazi wanapaswa kupitisha wakati kwa ukawaida pamoja na watoto wao. Wakati fulani, wazazi wanaweza kuvunjika moyo juu wanapaswa kurudilia-rudilia maagizo ya Yehova kwa watoto wao. Hata hivyo, wazazi wanapaswa kujikaza kuona kama ile njo njia ya kusaidia watoto wao waelewe Neno la Mungu na kulitumia.

Wazazi wanapaswa kuamua namna ya kufundisha kila mutoto (Picha hii inapatana na fungu la 20) *

20. Namna gani Zaburi 127:4 inaweza kutumiwa ili kukomalisha watoto? Fasiria.

20 Ujue muzuri watoto wako. Zaburi ya 127 inalinganisha watoto na mishale. (Soma Zaburi 127:4.) Mishale inaweza kufanyizwa na vitu tofauti-tofauti na inaweza kuwa na ukubwa tofauti-tofauti; vilevile kila mutoto iko tofauti kabisa na mwenzake. Njo maana wazazi wanapaswa kujua namna ya kufundisha kila mutoto. Bibi na bwana fulani mu inchi ya Israeli ya leo wenye waliweza kusaidia watoto wao wawili wamutumikie Yehova wanaonyesha jambo lenye liliwasaidia. Wanasema hivi: “Tulikuwa tunajifunza Biblia na kila mutoto kipekee.” Kwa kweli, kila kichwa cha familia ataamua kama ni lazima ao kama inawezekana kujifunza na watoto kwa njia hiyo.

YEHOVA ATAKUSAIDIA

21. Wazazi wanaweza kutazamia musaada gani kutoka kwa Yehova?

21 Wakati fulani, wazazi wanaweza kuona kama ni nguvu sana kufundisha watoto wao, lakini watoto ni zawadi kutoka kwa Yehova. Sikuzote, iko tayari kusaidia wazazi. Iko tayari kusikiliza sala za wazazi. Na anajibu sala hizo kupitia Biblia, vichapo vyetu, na kupitia mufano na mashauri ya wazazi wengine wakomavu katika kutaniko.

22. Ni mambo fulani gani ya muzuri sana yenye wazazi wanaweza kupatia watoto wao?

22 Watu fulani wanasema kama inaomba miaka 20 ili kukomalisha mutoto, lakini kazi ya wazazi haiishake. Kati ya mambo ya muzuri sana yenye wanaweza kupatia watoto wao kuko upendo, wakati, na mafundisho yenye kutegemea Biblia. Kila mutoto atatumia kwa njia tofauti mazoezi yenye anapewa. Lakini, wengi kati yao wenye wamekomalishwa na wazazi wenye kumupenda Yehova, wanajisikia kama Joanna Mae, dada mumoja wa Asia. Alisema hivi: “Wakati ninafikiria namna wazazi wangu walinizoeza, niko mwenye shukrani sana kuona kama walinitia nizamu na walinifundisha kumupenda Yehova. Hawakunizaa tu, lakini walinisaidia nikuwe na maisha yenye maana.” (Mez. 23:24, 25) Wakristo wengi sana wanaweza pia kusema vile.

WIMBO 59 Msifuni Yah Pamoja Nami

^ fu. 5 Bibi na bwana wanapaswa kuzaa watoto? Kama watazaa watoto, wanapaswa kuzaa watoto ngapi? Na namna gani wanaweza kufundisha watoto wao wamupende Yehova na kumutumikia? Habari hii inazungumuzia mifano fulani ya wazazi wa siku zetu na inaonyesha kanuni za Biblia zenye zinaweza kutusaidia kujibu ile maulizo.

^ fu. 15 Ona pia Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1, sura 36, na Buku la 2, sura ya 11.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Bibi na bwana Wakristo wanazungumuza ikiwa watazaa watoto, wanafikiria furaha na madaraka yenye inatokana na kuzaa watoto.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Bibi na bwana wanajifunza na kila mutoto kipekee kwa sababu watoto hawana miaka ileile na uwezo uleule.