Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 50

Yehova Anafanya Mupango ili Ukuwe Huru

Yehova Anafanya Mupango ili Ukuwe Huru

“Munapaswa . . . kutangaza uhuru katika inchi kwa ajili ya wakaaji wake wote.”​—LAW. 25:10.

WIMBO 22 Ufalme Umesimamishwa​—Na Uje!

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. (a) Yubile ni nini? (Ona kisanduku “ Yubile Ilikuwa Nini?”) (b) Kulingana na Luka 4:16-18, Yesu alizungumuzia nini?

KATIKA inchi fulani, watu wanafanyaka sikukuu ya mwaka wa 50 wa utawala wa mufalme ao malkia (mufalme mwanamuke). Mara mingi mwaka huo wa 50 unaitwa mwaka wa yubile ya mutawala. Sherehe za yubile zinaweza kufanya siku moja, juma moja, ao hata zaidi, na furaha yenye zinaletea watu inaisha haraka.

2 Tutazungumuzia yubile ya muzuri zaidi, ya muzuri hata zaidi kuliko Yubile ya mwaka muzima yenye ilifanywa kisha kila miaka 50 katika Israeli ya zamani. Yubile hiyo ya zamani ilipatia Waisraeli uhuru. Juu ya nini tunapaswa kujifunza juu ya Yubile hiyo? Juu mwaka wa Yubile ya Israeli unatukumbusha mupango muzuri sana wa uhuru wa milele wenye Yehova iko anafanya hata leo, uhuru wenye Yesu alizungumuzia.​—Soma Luka 4:16-18.

Katika Israeli, Yubile ilileta furaha na wale wenye walikuwa watumwa walirudia mu familia yao na kwenye mashamba ya uriti wao (Picha hii inapatana na fungu la 3) *

3. Kulingana na Mambo ya Walawi 25:8-12, Yubile ililetea Waisraeli faida gani?

3 Kuchunguza kwanza Yubile yenye Mungu alipanga kwa ajili ya watu wake wa zamani kutatusaidia tuelewe muzuri maana ya maneno yenye Yesu alisema wakati alizungumuzia uhuru. Yehova aliambia Waisraeli hivi: “Munapaswa kutakasa mwaka wa makumi tano (50) na kutangaza uhuru katika inchi kwa ajili ya wakaaji wake wote. Itakuwa Yubile kwenu, na kila mumoja wenu atarudia kwenye uriti wake na kila mumoja wenu atarudia katika familia yake.” (Soma Mambo ya Walawi 25:8-12.) Katika habari yenye ilitangulia, tuliona namna Sabato ya kila juma ililetea Waisraeli faida. Sasa, Yubile ililetea Waisraeli faida gani? Wazia Mwisraeli anakamata deni, kisha anashindwa kulipa deni hilo. Sasa analazimika kuuzisha shamba lake ili kulipa deni hilo. Katika mwaka wa Yubile, alipaswa kurudishiwa shamba hilo. Kwa hiyo, mwanaume huyo angeweza ‘kurudia kwenye uriti wake’ na uriti wa watoto wake haungepotea. Wazia hali ingine: Mwanaume mwenye anapata magumu ya nguvu anafikia kuuzisha mutoto wake mumoja, ao hata kujiuzisha yeye mwenyewe, katika utumwa ili kulipa deni. Katika mwaka wa Yubile, mutumwa huyo alipaswa ‘kurudia katika familia yake.’ Kwa hiyo, hakuna mutu mwenye angebakia mutumwa milele! Mupango huo unaonyesha kama Yehova alihangaikia kabisa watu wake!

4-5. Juu ya nini ni jambo la maana tujifunze juu ya Yubile ya Waisraeli?

4 Yubile ilikuwa na faida gani ingine? Yehova alisema hivi: “Hakuna mutu kati yako mwenye anapaswa kuwa maskini, kwa sababu hakika Yehova atakubariki katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia ili uikamate kuwa uriti.” (Kum. 15:4) Hilo ni tofauti kabisa na mambo yenye iko inafanyika mu dunia leo: mara mingi matajiri wanaendelea kuwa matajiri zaidi na maskini wanaendelea kuwa maskini zaidi!

5 Sisi Wakristo, hatuongozwe na Sheria ya Musa. Maana yake hatufuate sheria ya Yubile ya zamani yenye ilifanya watumwa wafanywe kuwa huru, madeni isamehewe, na watu warudie kwenye mashamba ya uriti wao. (Ro. 7:4; 10:4; Efe. 2:15) Lakini, ni jambo la maana tujifunze juu ya Yubile ya Waisraeli. Juu ya nini? Juu tunaweza kuwa na uhuru wenye unatukumbusha mupango wenye Yehova alifanya kwa ajili ya Waisraeli.

YESU ALITANGAZA UHURU

6. Juu ya nini wanadamu wako na lazima ya kufanywa kuwa huru?

6 Sisi wote tuko na lazima ya kufanywa kuwa huru kwa sababu tuko katika utumwa mubaya sana, ni kusema, utumwa wa zambi. Juu tuko watenda-zambi, tunazeeka, tunagonjwa, na tunakufa. Watu wengi wanaona kama jambo hilo ni la kweli wakati wanajiangalia mu kioo ao wakati wanaenda kwa munganga ili kupata matunzo. Pia, tunavunjika moyo wakati tunafanya zambi. Mutume Paulo alisema kama alikuwa anapelekwa ‘akiwa ametekwa kwa sheria ya zambi yenye ilikuwa ndani ya mwili wake.’ Aliongeza hivi: “Maskini mimi! Ni nani ataniokoa kutoka katika mwili wenye unapatwa na kifo hiki?”​—Ro. 7:23, 24.

7. Nabii Isaya alitabiri nini juu ya uhuru?

7 Jambo la kufurahisha ni hili: Mungu amefanya mupango ili tukombolewe, ao tuwekwe huru kutoka katika zambi. Yesu njo mwenye anatuwezesha kupata uhuru huo. Miaka zaidi ya 700 mbele Yesu akuje ku dunia, nabii Isaya alitabiri juu ya uhuru mukubwa wa wakati wenye kuja. Uhuru huo mukubwa utatimiza mambo mingi zaidi kuliko ile yenye uhuru wa mwaka wa Yubile ya Waisraeli ulitimiza. Aliandika hivi: “Roho ya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova iko juu yangu, kwa sababu Yehova alinitia mafuta ili nitangazie wapole habari njema. Alinituma ili nifunge vidonda vya wenye kuvunjika moyo, ili nitangaze uhuru kwa wale wenye walikamatwa mateka.” (Isa. 61:1) Unabii huo unahusu nani?

8. Unabii wa Isaya juu ya uhuru, unahusu nani?

8 Unabii huo wa maana juu ya uhuru ulianza kutimia kisha Yesu kuanza utumishi wake. Wakati Yesu alienda ku sinagogi katika muji wake wa Nazareti, alisomea Wayahudi wenye walikusanyika mule ile maneno ya Isaya. Yesu alionyesha kama maneno hii inamuhusu: “Roho ya Yehova iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta ili nitangazie maskini habari njema. Alinituma nitangaze uhuru kwa wale wenye walikamatwa mateka na kuona kwa vipofu, kuacha wenye kupondwa waende wakiwa wamewekwa huru, na kuhubiri mwaka wa Yehova wenye kukubalika.” (Lu. 4:16-19) Namna gani Yesu alitimiza unabii huo?

WATU WA KWANZA WENYE WALIFANYWA KUWA HURU

Yesu alitangaza uhuru mu sinagogi la Nazareti (Picha hii inapatana na fungu la 8-9)

9. Watu wengi katika siku za Yesu walikuwa wanatumaini kupata uhuru gani?

9 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, watu walianza kupata uhuru wenye Isaya alitabiri na wenye Yesu alisoma. Yesu alihakikisha jambo hilo wakati alitangaza hivi: “Leo andiko hili lenye mumesikia limetimia.” (Lu. 4:21) Pengine watu wengi wenye walisikia maneno yenye Yesu alisoma walikuwa wanangojea wakombolewe kutoka katika utawala wa Waroma. Pengine walikuwa wanawaza kama wanaume wawili wenye walisema hivi: “Sisi tulitumaini kama mutu huyo ndiye angekomboa Israeli.” (Lu. 24:13, 21) Lakini, tunajua kama Yesu hakuomba wanafunzi wake waasi utawala mukali wa Waroma. Aliwaomba walipe “Kaisari vitu vya Kaisari.” (Mt. 22:21) Sasa, namna gani Yesu aliletea watu uhuru wakati huo?

10. Yesu alifanya watu wakuwe huru kutoka katika utumwa gani?

10 Mwana wa Mungu alikuja kusaidia watu wapate uhuru katika njia mbili. Njia ya kwanza, Yesu alifanya watu wakuwe huru kwa kuwasaidia waachane na mafundisho ya uongo ya viongozi wa dini. Wayahudi wengi wa wakati huo walikuwa watumwa wa mafundisho na desturi za uongo. (Mt. 5:31-37; 15:1-11) Watu wenye walikuwa wanajiita kuwa viongozi wa kiroho walikuwa vipofu kwa njia fulani. Kwa sababu walimukataa Masiya na kweli yenye alifundisha, waliendelea kuwa vipofu na zambi zao hazikusamehewa. (Yoh. 9:1, 14-16, 35-41) Kupitia mafundisho yake na mufano wake muzuri, Yesu alionyesha watu wanyenyekevu namna wangepata uhuru wa kiroho, ni kusema, kuachana na mafundisho ya uongo.​—Mk. 1:22; 2:23–3:5.

11. Ni katika njia gani ya pili Yesu alifanya watu wakuwe huru?

11 Njia ya pili, Yesu alisaidia wanadamu wakuwe huru kwa kuwakomboa kutoka katika utumwa wa zambi yenye waliriti. Kupitia bei ya ukombozi ya Yesu, Mungu anaweza kusamehe zambi za watu wenye wanaonyesha imani na wenye wanakubali bei ya ukombozi yenye Mungu alitoa. (Ebr. 10:12-18) Yesu alisema hivi: “Kama Mwana anawaweka ninyi huru, mutakuwa huru kwelikweli.” (Yoh. 8:36) Kwa kweli, uhuru huo ulikuwa mukubwa zaidi kuliko uhuru wenye Waisraeli walipata katika mwaka wa Yubile! Kwa mufano, mwanaume mwenye aliwekwa huru katika mwaka wa Yubile angeweza kuwa mutumwa tena, na angefikia kufa.

12. Ni nani njo walikuwa wa kwanza kupata uhuru wenye Yesu alitangaza?

12 Siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33, Yehova alitia mafuta kupitia roho yake takatifu mitume na wanaume na wanamuke wengine waaminifu. Aliwafanya kuwa wana wake ili wakati wenye kuja wafufuliwe na kuenda kutawala pamoja na Yesu mbinguni. (Ro. 8:2, 15-17) Wao njo walikuwa wa kwanza kupata uhuru wenye Yesu alitangaza mu sinagogi la Nazareti. Wanaume na wanamuke hao hawakukuwa tena watumwa wa mafundisho ya uongo na desturi za viongozi wa dini ya Wayahudi zenye hazikupatana na Maandiko. Pia, Mungu aliwaona kuwa wamewekwa huru kutoka katika utumwa wa zambi yenye inaongoza kwenye kifo. Yubile ya mufano yenye ilianza mu mwaka wa 33 wakati wanafunzi wa Kristo walitiwa mafuta, itaisha ku mwisho wa Utawala wa Yesu wa Miaka Elfu Moja. Ni mambo gani itakuwa imetimizwa wakati huo?

MAMILIONI INGINE YA WATU WATAFANYWA KUWA UHURU

13-14. Zaidi ya Wakristo watiwa-mafuta, ni nani wenye wanaweza kupata uhuru wenye Yesu alitangaza?

13 Leo, mamilioni ya watu wenye moyo muzuri kutoka mu mataifa yote wanaitwa “kondoo wengine.” (Yoh. 10:16) Mungu hakuwachagua ili watawale pamoja na Yesu mbinguni. Lakini, wako na tumaini lenye kutegemea Biblia la kuishi milele hapa ku dunia. Hilo njo tumaini lako?

14 Hata leo, uko unapata faida fulani zenye watiwa-mafuta nao wako wanapata. Kwa sababu uko na imani katika damu ya Yesu yenye ilimwangwa, unaweza kumuomba Yehova akusamehe zambi zako. Kwa hiyo, unaweza kukubaliwa na Mungu na kuwa na zamiri ya muzuri mbele yake. (Efe. 1:7; Ufu. 7:14, 15) Fikiria pia baraka zenye uko nazo kwa sababu hauko tena mutumwa wa mafundisho ya uongo. Yesu alisema hivi: “Mutajua kweli, na kweli itawaweka ninyi huru.” (Yoh. 8:32) Ni furaha sana kuwa na uhuru huo!

15. Tunaweza kupata uhuru na baraka gani wakati wenye kuja?

15 Unaweza kupata uhuru mukubwa wakati wenye kuja. Hivi karibuni, Yesu ataharibu dini za uongo na serikali za wanadamu zenye udanganyifu. Mungu atalinda “kundi kubwa la watu” wenye kumutumikia, na kisha atawasaidia wapate baraka mu paradiso hapa ku dunia. (Ufu. 7:9, 14) Watu wengi sana watafufuliwa na watapata nafasi ya kufanywa kuwa huru kutokana na matokeo ya mubaya ya zambi yenye tuliriti kutoka kwa Adamu.​—Mdo. 24:15.

16. Ni uhuru gani mukubwa wenye wanadamu watapata wakati wenye kuja?

16 Wakati wa Utawala wa Miaka Elfu Moja, Yesu na watawala wenzake watasaidia wanadamu wakuwe wakamilifu kimwili na kiroho. Wakati huo wenye wanadamu watawekwa huru kutoka katika zambi na kutokamilika utakuwa kama Yubile katika Israeli ya zamani. Watu wote wenye kumutumikia Yehova kwa ushikamanifu ku dunia watakuwa wakamilifu, ni kusema, hawatafanya tena zambi.

Mu dunia mupya, tutafurahia kufanya kazi ya muzuri na yenye kufurahisha (Picha hii inapatana na fungu la 17)

17. Kulingana na Isaya 65:21-23, watu wa Mungu watakuwa na maisha ya namna gani? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

17 Maelezo yenye kuonyesha namna maisha itakuwa ku dunia inapatikana mu Isaya 65:21-23. (Soma.) Wakati huo, hatutakunja mikono na kubakia bila kufanya kitu. Lakini, Biblia inaonyesha kama watu wa Mungu watakuwa na kazi ya muzuri na yenye kufurahisha. Ku mwisho wa Utawala wa Yesu wa Miaka Elfu Moja, tunaweza kuwa hakika kama “uumbaji wenyewe pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.”​—Ro. 8:21.

18. Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama tutakuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuja?

18 Kama vile Yehova alifanya mupango ili Waisraeli wakuwe na wakati wa kufanya kazi na wakati wa kupumuzika, atafanya pia vile kwa ajili ya watu wake wakati wa Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu Moja. Kwa kweli, tutakuwa na wakati wa kufanya mambo ya kiroho. Ili tukuwe na furaha leo, tunapaswa kumuabudu Mungu, na tutakuwa na wakati wa kufanya vile katika dunia mupya. Wanadamu wote waaminifu watakuwa na furaha wakati wa Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu Moja, kwa sababu sisi wote tutakuwa na kazi yenye kufurahisha na sisi wote tutamutumikia Mungu.

WIMBO 142 Kushikilia Tumaini Letu

^ fu. 5 Yehova alifanya mupango wa pekee ili uhuru utangazwe katika Israeli ya zamani. Mupango huo ni Yubile. Sisi Wakristo hatuongozwe na Sheria ya Musa; lakini ni jambo la maana tujifunze mambo fulani juu ya Yubile. Katika habari hii, tutajifunza namna Yubile ya zamani inatukumbusha mupango wenye Yehova amefanya kwa ajili yetu na namna mupango huo unaweza kutuletea faida.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Katika mwaka wa Yubile, wanaume wenye walikuwa watumwa waliwekwa huru na wangeweza kurudia mu familia yao na kwenye mashamba ya uriti wao.