Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Je, maneno ya Paulo yenye kuwa mu 1 Wakorinto 15:29 inamaanisha kama Wakristo fulani wa wakati wake walikuwa wanabatizwa kwa ajili ya wafu?

Hapana, Biblia haiseme vile na vitabu vya historia haviseme vile.

Namna ile andiko inatafsiriwa mu Biblia mbalimbali inafanya watu fulani wawaze kama Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa wanabatizwa kwa ajili ya wafu. Kwa mufano, mu Biblia fulani ile andiko inatafsiriwa hivi: “Kama sivyo, wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu, watafanya nini basi?”​—La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo.

Lakini ona maneno yenye watu wawili wenye elimu ya Biblia walisema. Mwanateolojia Gregory Lockwood alisema kama mu Biblia ao mu vitabu vingine vya historia hakuna jambo lenye kuonyesha kama watu walikuwa wanabatizwa kwa ajili ya wafu. Vilevile, Profesa Gordon Fee alisema kama mu Biblia ao mu vitabu vya historia hamuna hata mufano moja wa mutu mwenye alibatizwa kwa ajili ya wafu. Ile aina ya ubatizo haizungumuziwe hata fasi moja mu agano jipya. Na hakuna jambo lenye kuonyesha kama Wakristo wa kwanza-kwanza ao makanisa yenye ilitokea kisha mitume kufa ilikuwa inafanya ile aina ya ubatizo.

Biblia inasema kama wafuasi wa Yesu walipaswa ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na kuwabatiza . . . , na kuwafundisha kushika mambo yote’ yenye Yesu aliwaamuru. (Mt. 28:19, 20) Mbele mutu abatizwe na kuwa mwanafunzi wa Yesu, alipaswa kujifunza kuhusu Yehova na Mwana wake, kuwaamini, na kuwatii. Mutu mwenye alikuwa amekufa hangeweza kufanya ile mambo yote wala Mukristo mwenye alikuwa muzima hangeweza kufanya vile pa nafasi yake.​—Muh. 9:5, 10; Yoh. 4:1; 1 Ko. 1:14-16.

Sasa Paulo alipenda kusema nini?

Watu fulani katika muji wa Korinto walikuwa wanasema kama wafu hawatafufuliwa. (1 Ko. 15:12) Paulo alipinga ile mawazo. Alisema kama alikuwa anapambana na kifo kila siku. Kusema kweli, alikuwa angali muzima. Lakini hata kama alikuwa anapambana na hatari, alikuwa hakika kama wakati angekufa, angefufuliwa kama vile Yesu, na kuwa kiumbe wa roho mwenye nguvu.​—1 Ko. 15:30-32, 42-44.

Iliomba Wakorinto waelewe kama Mukristo mutiwa-mafuta angepambana na magumu kila siku na angefikia kufa mbele afufuliwe. ‘Kubatizwa katika Kristo Yesu’ kulimaanisha pia ‘kubatizwa katika kifo chake.’ (Ro. 6:3) Kubatizwa vile kwa njia ya mufano kulionyesha kama, sawa vile Yesu, wangepata magumu na kufa. Ni kisha pale njo wangefufuliwa na kuenda mbinguni.

Zaidi ya miaka mbili kisha Yesu kubatizwa katika maji, aliambia hivi mitume wake wawili: “Kwa ubatizo wenye ninabatizwa, mutabatizwa.” (Mk. 10:38, 39) Wakati Yesu alisema ile maneno hakukuwa anabatizwa katika maji. Alimaanisha kama maisha ya uaminifu-mushikamanifu kwa Mungu ingemupeleka ku kifo. Paulo aliandika kama watiwa-mafuta ‘wangeteseka pamoja naye [Yesu] ili pia watukuzwe pamoja naye.’ (Ro. 8:16, 17; 2 Ko. 4:17) Ile inaonyesha kama wao pia wangepaswa kufa ili wafufuliwe na kuenda mbinguni.

Kwa hiyo, njia muzuri ya kutafsiri maneno ya Paulo inaweza kuwa hii: “Kama haiko vile, wale wenye wanabatizwa kwa kusudi la kuwa wafu watafanya nini? Kama wafu hawatafufuliwa hata kidogo, sababu gani wao wanabatizwa pia kwa kusudi la kuwa vile?”