Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 49

Ufufuo Ni Tumaini la Kweli!

Ufufuo Ni Tumaini la Kweli!

“Niko na tumaini kwa Mungu . . . kwamba kutakuwa ufufuo.”​—MDO. 24:15.

WIMBO 151 Ataita

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Watumishi wa Yehova wako na tumaini gani la muzuri?

NI JAMBO la maana sana kuwa na tumaini. Watu fulani wako na tumaini la kuwa na ndoa yenye furaha, la kukomalisha watoto wenye afya ya muzuri, ao la kupona ugonjwa fulani wa mubaya. Sisi Wakristo tunaweza kuwa na tumaini la kupata ile mambo. Lakini tuko na tumaini lingine la maana zaidi. Tuko na tumaini la kuishi milele, na tunatumaini kama wapendwa wetu wenye wamekufa wataishi tena.

2 Mutume Paulo alisema hivi: “Niko na tumaini kwa Mungu . . . kwamba kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.” (Mdo. 24:15) Haiko Paulo njo alikuwa wa kwanza kuzungumuzia tumaini la ufufuo. Yobu, muzee wa ukoo, alizungumuzia pia tumaini hilo. Alikuwa hakika kama Mungu atamukumbuka na kumufufua ili aishi tena.​—Yob. 14:7-10, 12-15.

3. Namna gani 1 Wakorinto sura ya 15 inaweza kutusaidia?

3 Fundisho la “kufufuliwa kwa wafu” liko kati ya mafundisho yenye kuwa “musingi” wa mafundisho yote ya Kikristo. (Ebr. 6:1, 2) Mambo yenye Paulo alisema juu ya ufufuo inapatikana mu 1 Wakorinto sura ya 15. Bila shaka mambo yenye aliandika ilitia moyo Wakristo wa karne ya kwanza. Inaweza kututia moyo sisi pia na kutusaidia tukuwe hakika kama tumaini la ufufuo lenye pengine tumekuwa nalo kwa muda murefu ni la kweli.

4. Ni nini inatusaidia tukuwe hakika kama wapendwa wetu watafufuliwa?

4 Kufufuliwa kwa Yesu kunatusaidia tukuwe hakika kama wapendwa wetu wenye wamekufa watafufuliwa. Ufufuo wa Yesu ulikuwa kati ya “habari njema” yenye Paulo alitangazia Wakorinto. (1 Ko. 15:1, 2) Kwa kweli, alisema kama ikiwa Mukristo angekosa kuamini kama Yesu alifufuliwa, imani yake ingekuwa ya bure. (1 Ko. 15:17) Kuamini kama Yesu alifufuliwa njo kunatusaidia tukuwe hakika kama watu wengine pia watafufuliwa.

5-6. Maneno yenye kuwa mu 1 Wakorinto 15:3, 4 inatusaidia tukuwe na tumaini gani?

5 Ku mwanzo wa mazungumuzo ya Paulo kuhusu ufufuo, alisema mambo tatu juu ya Yesu: (1) “Kristo alikufa kwa ajili ya zambi zetu.” (2) “Alizikwa.” (3) “Alifufuliwa siku ya tatu (3) kulingana na Maandiko.”​—Soma 1 Wakorinto 15:3, 4.

6 Kwa sababu Yesu alikufa, alizikwa, na kufufuliwa, tunaweza kupata faida gani? Nabii Isaya alitabiri kama Masiya ‘angeondolewa katika inchi ya wazima’ na ‘kupewa kaburi pamoja na waovu.’ Lakini alitabiri jambo lingine. Alisema kama Masiya angebeba ‘zambi ya watu wengi.’ Yesu alifanya vile kwa kutoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi. (Isa. 53:8, 9, 12; Mt. 20:28; Ro. 5:8) Kwa hiyo, kwa sababu Yesu alikufa, alizikwa, na kufufuliwa, tuko kabisa na tumaini la kukombolewa kutoka katika zambi na kifo na kuonana na wapendwa wetu wenye wamekufa.

USHUHUDA WA MASHAHIDI WENGI

7-8. Nini njo inasaidia Wakristo wakuwe hakika kama Yesu alifufuliwa?

7 Ufufuo wa Yesu njo unatusaidia tukuwe na tumaini kama kutakuwa ufufuo. Njo maana tunapaswa kuamini kama Yesu alifufuliwa. Ni nini inatusaidia tukuwe hakika kama Yehova alimufufua Yesu?

8 Kuko watu wengi wenye waliona Yesu kisha kufufuliwa kwake na walielezea watu wengine juu ya jambo hilo. (1 Ko. 15:5-7) Mutu wa kwanza mwenye Paulo alitaja alikuwa mutume Petro (Kefa). Wanafunzi fulani walihakikisha kama Petro alimuona Yesu kisha kufufuliwa kwa Yesu. (Lu. 24:33, 34) Zaidi ya ile, “wale [mitume] Kumi na Mbili (12),” walimuona Yesu kisha kufufuliwa kwake. Kisha, Kristo “alitokea ndugu zaidi ya mia tano (500) kwa wakati mumoja.” Pengine aliwatokea ku mukutano wenye walifanya Galilaya wenye kuzungumuziwa mu Matayo 28:16-20. Pia, Yesu “alimutokea Yakobo,” mwenye pengine alikuwa ndugu yake. (Yoh. 7:5) Kisha kumuona Yesu, Yakobo alimuamini hata kama ku mwanzo hakuamini kama Yesu alikuwa Masiya. Jambo la kufurahisha ni kwamba, wakati Paulo aliandika barua ya kwanza kwa Wakorinto mu mwaka wa 55 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, kulikuwa kungali watu wengi wenye waliona Yesu kisha yeye kufufuliwa. Kwa hiyo, kama kulikuwa mutu mwenye alikuwa na mashaka kama Yesu alifufuliwa, angeweza kuzungumuza na wale watu ili wamuhakikishie kama Yesu alifufuliwa.

9. Namna gani ushuhuda wa Paulo wenye kuwa mu Matendo 9:3-5, unaonyesha pia kama Yesu alifufuliwa?

9 Kisha wakati fulani, Yesu alimutokea pia Paulo. (1 Ko. 15:8) Wakati Paulo (Sauli) alikuwa anaenda Damasko alisikia sauti ya Yesu mwenye alikuwa amefufuliwa na kupitia maono aliona utukufu wa Yesu mbinguni. (Soma Matendo 9:3-5.) Mambo yenye Paulo alijionea ni ushuhuda mwingine wenye kuhakikisha kama ni kweli Yesu alifufuliwa.​—Mdo. 26:12-15.

10. Kwa sababu Paulo aliamini kama Yesu alifufuliwa, ile ilimuchochea afanye nini?

10 Watu fulani wangeona ushuhuda wa Paulo kuwa wa maana sana kwa sababu zamani alikuwa anatesa Wakristo. Wakati Paulo aliamini kama Yesu alifufuliwa, alifanya yake yote ili kuhakikishia wengine jambo hilo. Wakati Paulo alikuwa anatangazia wengine kama Yesu alikufa na kisha akafufuliwa, alipata magumu mingi sawa vile kupigwa, kufungwa, na kuvunjikiwa na mashua. Lakini alivumilia ile magumu yote. (1 Ko. 15:9-11; 2 Ko. 11:23-27) Juu Paulo alikuwa hakika kabisa kama Yesu alifufuliwa, alikuwa tayari kutetea jambo hilo hata kama ingemuomba akufe. Bila shaka, ushuhuda wa Wakristo wa karne ya kwanza unatuhakikishia kama Yesu alifufuliwa. Na unatia nguvu imani yetu katika ufufuo, hauone vile?

PAULO ALIREKEBISHA MAWAZO YENYE HAIKUKUWA YA KWELI

11. Pengine ni juu ya nini Wakristo fulani wa Korinto walikuwa na mawazo yenye haikukuwa ya kweli juu ya ufufuo?

11 Wakristo fulani katika muji wa Korinto, wenye ulikuwa mu eneo la Ugiriki walikuwa na mawazo yenye haikukuwa ya kweli kuhusu ufufuo. Walifikia hata kusema kama “hakuna ufufuo wa wafu.” Juu ya nini walikuwa na ile mawazo? (1 Ko. 15:12) Wanafilozofia katika Atene, muji mwingine wenye ulikuwa mu eneo la Ugiriki, walikuwa wanachekelea wazo la kuwa Yesu alifufuliwa. Inawezekana Wakristo fulani wa Korinto walianza pia kuwa na ile mawazo. (Mdo. 17:18, 31, 32) Wengine waliwaza kama ufufuo ulikuwa fundisho la mufano. Walikuwa wanasema kama mutenda-zambi alikuwa mutu “mwenye kufa” na alianza “kuishi tena” wakati alifikia kuwa Mukristo. Hata ikuwe sababu ilikuwa nini, kukataa kuamini kama Yesu alifufuliwa kulifanya imani yao ikuwe ya bure. Kama Mungu hakumufufua Yesu ni kusema Yesu hakulipa bei ya ukombozi na zambi zao hazikusamehewa. Kwa hiyo, wale wenye walikataa fundisho la ufufuo hawakukuwa na tumaini la kweli.​—1 Ko. 15:13-19; Ebr. 9:12, 14.

12. Kama vile 1 Petro 3:18, 22 inaonyesha, namna gani ufufuo wa Yesu ulikuwa tofauti na ufufuo mbalimbali wenye ulifanyika mbele Yesu afufuliwe?

12 Paulo alijua kabisa kama “Kristo [alikuwa] amefufuliwa kutoka kwa wafu.” Ufufuo wa Yesu ulikuwa wa hali ya juu sana kuliko ufufuo mbalimbali wenye ulifanyika mbele Yesu afufuliwe, kwa sababu wale watu walifikia kufa tena. Paulo alisema kama Yesu alikuwa “matunda ya kwanza ya wale wenye wamelala usingizi katika kifo.” Ni katika maana gani Yesu alikuwa matunda ya kwanza? Alikuwa mutu wa kwanza kufufuliwa na mwili wa roho na alikuwa mwanadamu wa kwanza kuenda mbinguni.​—1 Ko. 15:20; Mdo. 26:23; soma 1 Petro 3:18, 22.

WALE WENYE “WATAFANYWA KUWA WAZIMA”

13. Paulo alionyesha tofauti gani kati ya Adamu na Yesu?

13 Namna gani kifo cha mutu mumoja kingesaidia mamilioni ya watu wapate tena uzima? Paulo alijibia ile ulizo kwa njia yenye kuwa wazi. Alionyesha tofauti kati ya Adamu na Yesu wakati alizungumuzia matokeo yenye tunapata kwa sababu ya kosa la Adamu, na faida yenye tutapata kwa sababu ya kifo cha Kristo. Kuhusu Adamu, Paulo aliandika hivi: “Kifo kilikuja kupitia mwanadamu.” Zambi ya Adamu ilimuletea yeye mwenyewe kifo na pia wazao wake. Mupaka leo tunaendelea kuteseka kwa sababu Adamu alikosa kutii. Lakini, juu Mungu alimufufua Mwana wake, tunaweza kutumaini kama maisha yetu itakuwa ya muzuri wakati wenye kuja. Kuhusu jambo hili, Paulo alisema kama “ufufuo wa wafu pia unakuja kupitia mwanadamu,” ni kusema Yesu. “Kwa maana kama vile katika Adamu wote wanakufa,” “vilevile pia katika Kristo wote watafanywa kuwa wazima.”​—1 Ko. 15:21, 22.

14. Je, Adamu atafufuliwa? Fasiria.

14 Paulo alimaanisha nini wakati alisema kama “katika Adamu wote wanakufa”? Paulo alikuwa anazungumuzia wazao wa Adamu, wenye waliriti zambi na kutokamilika kutoka kwa Adamu na ile inafanya wakuwe wanakufa. (Ro. 5:12) Adamu haiko kati ya wale wenye “watafanywa kuwa wazima.” Hatapata faida ya bei ya ukombozi kwa sababu alikuwa mwanadamu mukamilifu mwenye alichagua kukosa kumutii Mungu. Adamu hana tumaini lolote, sawa tu vile wale wenye “Mwana wa Binadamu” atahukumu kuwa “mbuzi,” ni kusema, wale wenye “wataharibiwa milele.”​—Mt. 25:31-33, 46; Ebr. 5:9.

Yesu njo alikuwa wa kwanza kufufuliwa ili kuenda mbinguni (Ona fungu la 15-16) *

15. Wote wenye “watafanywa kuwa wazima” ni nani?

15 Paulo alisema kama “katika Kristo wote watafanywa kuwa wazima.” (1 Ko. 15:22) Ni Wakristo watiwa-mafuta wa Korinto njo Paulo aliandikia barua yake. Na wale Wakristo wangefufuliwa ili kuenda mbinguni. Walikuwa ‘wametakaswa katika umoja na Kristo Yesu, na waliitwa ili kuwa watakatifu.’ Paulo alitaja pia “wale wenye wamelala usingizi katika kifo wakiwa katika umoja na Kristo.” (1 Ko. 1:2; 15:18; 2 Ko. 5:17) Katika barua ingine yenye kuongozwa na roho, Paulo aliandika kama wale wenye ‘kuungana pamoja na [Yesu] katika mufano wa kifo chake’ ‘wataunganishwa pia pamoja naye katika mufano wa ufufuo wake.’ (Ro. 6:3-5) Yesu alifufuliwa na mwili wa roho na akaenda mbinguni. Ni vile itakuwa kwa wale wote wenye kuwa “katika umoja na Kristo,” ni kusema, Wakristo wote watiwa-mafuta.

16. Paulo alipenda kumaanisha nini wakati alimuita Yesu kuwa “matunda ya kwanza”?

16 Paulo aliandika kama Kristo alifufuliwa akiwa “matunda ya kwanza ya wale wenye wamelala usingizi katika kifo.” Tukumbuke kama watu wengine, sawa vile Lazaro, walifufuliwa na wakaishi tena hapa ku dunia. Lakini Yesu njo alikuwa wa kwanza kufufuliwa akiwa kiumbe wa roho na kupata uzima wa milele. Angeweza kufananishwa na matunda ya kwanza ya mavuno yenye Waisraeli walikuwa wanamutolea Mungu. Zaidi ya ile, wakati Paulo alimuita Yesu kuwa “matunda ya kwanza,” alipenda kumaanisha kama kuko watu wengine wenye wangefufuliwa ili kuishi mbinguni. Sawa vile Yesu, mitume na wengine wenye kuwa “katika umoja na Kristo” wangefufuliwa ili kuishi mbinguni.

17. Ni wakati gani wale wenye kuwa “katika umoja na Kristo” wangefufuliwa ili kuishi mbinguni?

17 Wakati Paulo aliandikia Wakorinto, ufufuo wa wale wenye kuwa “katika umoja na Kristo” ulikuwa haujaanza. Kuhusu wakati wenye ule ufufuo ungeanza, Paulo aliandika hivi: “Kila mumoja kwa wakati wake mwenyewe: Kristo mwenye kuwa matunda ya kwanza, kisha wale wenye kuwa wa Kristo wakati wa kuwapo kwake.” (1 Ko. 15:23; 1 Te. 4:15, 16) Leo, tuko tunaishi mu kile kipindi cha “kuwapo” kwa Kristo chenye kilitabiriwa. Ni wazi kama mitume na Wakristo wengine watiwa-mafuta wenye walikufa, walipaswa kuchunga wakati wa kuwapo kwa Kristo ili wafufuliwe na kuenda mbinguni na ‘kuunganishwa . . . pamoja [na Yesu] katika mufano wa ufufuo wake.’

UKO NA TUMAINI LA KWELI!

18. (a) Juu ya nini tunaweza kusema kama kutakuwa ufufuo mwingine? (b) Kama vile 1 Wakorinto 15:24-26 inaonyesha, ni mambo gani itatokea mbinguni?

18 Sasa itakuwa namna gani juu ya Wakristo washikamanifu wenye hawana tumaini la kuishi mbinguni pamoja na Kristo? Wao pia wako na tumaini la ufufuo. Biblia inasema kama Paulo na wengine wenye wataenda mbinguni watafufuliwa katika “ufufuo wa kwanza kutoka kwa wafu.” (Flp. 3:11) Ile inaonyesha kama kutakuwa ufufuo mwingine. Na inapatana na mambo yenye Yobu alisema juu ya wakati wake wenye kuja. (Yob. 14:15) “Wale wenye kuwa wa Kristo wakati wa kuwapo kwake” watakuwa mbinguni wakati Yesu ataharibu serikali yote na mamlaka yote na nguvu zote. Hata “adui wa mwisho, . . . kifo,” ataharibiwa. Kwa kweli wale wenye watafufuliwa ili kuishi mbinguni hawatakufa tena. Lakini itakuwa namna gani juu ya wengine?​—Soma 1 Wakorinto 15:24-26.

19. Wale wenye wako na tumaini la kuishi ku dunia wanaweza kutazamia nini?

19 Wale wenye wako na tumaini la kuishi ku dunia wanaweza kutazamia nini? Mambo yenye Paulo alisema inaweza kuwapatia tumaini. Alisema hivi: “Niko na tumaini . . . kwamba kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.” (Mdo. 24:15) Bila shaka, mutu mwenye haiko mwenye haki hawezi kuenda mbinguni. Kwa hiyo, ile maneno inahusu ufufuo wenye utafanyika ku dunia wakati wenye kuja.

Kuamini kama kutakuwa ufufuo kunatusaidia tutumaini kama tutakuwa na maisha yenye furaha wakati wenye kuja (Ona fungu la 20) *

20. Namna gani hii habari imetia nguvu tumaini lako katika ufufuo?

20 Bila shaka, “kutakuwa ufufuo”! Wale wenye watafufuliwa ili kuishi ku dunia watakuwa na tumaini la kuishi milele. Unaweza kuwa hakika kama ile ahadi itatimia. Ile tumaini inaweza kukufariji wakati unafikiria wapendwa wako wenye wamekufa. Wanaweza kufufuliwa wakati Kristo na wengine “watatawala wakiwa wafalme . . . ile miaka elfu moja (1000).” (Ufu. 20:6) Wewe pia unaweza kuendelea kuwa hakika kama utafufuliwa ikiwa unakufa mbele Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo uanze. “Tumaini [hilo] halikatishe tamaa.” (Ro. 5:5) Linaweza kukupatia nguvu sasa na kukusaidia umutumikie Yehova kwa furaha. Lakini kuko mambo ingine yenye tunaweza kujifunza katika 1 Wakorinto sura ya 15. Tutazungumuzia ile mambo mu habari yenye kufuata.

WIMBO 147 Uzima wa Milele Umeahidiwa

^ fu. 5 Sura ya 15 ya kitabu cha Wakorinto wa Kwanza inazungumuzia sana fundisho la ufufuo. Juu ya nini fundisho hilo ni la maana sana kwetu? Na nini njo inatusaidia tukuwe hakika kama Yesu alifufuliwa? Mu hii habari tutazungumuzia ile maulizo na maulizo ingine ya maana kuhusu ufufuo.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu njo alikuwa wa kwanza kuenda mbinguni. (Mdo. 1:9) Kati ya wanafunzi wake wenye wangeenda pia mbinguni kulikuwa Tomasi, Yakobo, Lidia, Yohana, Maria, na Paulo.

^ fu. 58 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu alifisha bibi yake kisha kumutumikia Yehova pamoja naye kwa miaka mingi. Iko hakika kama bibi yake atafufuliwa na anaendelea kumutumikia Yehova kwa ushikamanifu.