Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unakumbuka?

Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu magazeti ya hivi karibuni ya Munara wa Mulinzi? Kama ni vile, jaribu kujibu hii maulizo:

Namna gani tunapaswa kutendea watiwa-mafuta?

Tunapenda kuiga imani yao, lakini tunapaswa kuepuka kuwatendea kwa njia ya pekee. Tunapaswa kuepuka ‘kusifu-sifu wengine.’ (Yud. 16) Tunapaswa kuepuka kuwauliza maulizo ya kipekee kuhusu tumaini lao.​—w20.01, uku. 29.

Ni nini inakuhakikishia kama Yehova anakutambua?

Biblia inasema kama alikuona hata mbele uzaliwe. Anasikilizaka sala zako. Anajua mambo yenye iko mu moyo wako, na matendo yako inaweza kumufurahisha ao kumuhuzunisha. (1 Ny. 28:9; Mez. 27:11) Alikuvuta kwake.​—w20.02, uku. 12.

Ni katika hali gani fulani tunapaswa kusema ao kunyamaza?

Tunafurahia kuzungumuza kuhusu Yehova. Tunapaswa kusema wakati tunaona kama mutu fulani anafanya jambo fulani lenye linaweza kumuongoza kwenye kosa kubwa. Wazee wanapaswa kusema wakati ni lazima watoe mashauri. Tunapaswa kuepuka kuuliza (ao kueleza) habari juu ya namna kazi yetu inafanywa mu inchi mbalimbali kwenye kazi yetu inakatazwa. Tunapaswa kuepuka kusema mambo ya siri.​—w20.03, uku. 20-21.

Kuko tofauti gani kati ya nzige wenye kuzungumuziwa mu Yoeli sura ya 2 na wale wa mu Ufunuo sura ya 9?

Yoeli 2:20-29 inasema kama Mungu anafukuza nzige mbali na anatoa ahadi ya kulipia uharibifu wenye nzige hao wamefanya. Kisha, Mungu anamwanga roho yake. Ile mambo ilitimia wakati Wababiloni walishambulia Israeli na pia miaka mingi kisha pale. Ufunuo 9:1-11 inazungumuzia watiwa-mafuta wa siku zetu, wenye wanafananishwa na nzige. Wako wanatangaza ujumbe wa hukumu ya Mungu juu ya mupangilio huu muovu wa mambo na, kwa hiyo, wanafanya watu wenye kuunga mukono mupangalio huu wajisikie mubaya sana.​—w20.04, uku. 3-6.

Ni nani mufalme wa kaskazini leo?

Ni serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono. Wameshambulia watu wa Mungu kwa kukataza kazi ya kuhubiri na wameonyesha kama wanachukia Mashahidi wa Yehova. Mufalme wa kusini anaendelea kupigana na mufalme wa kaskazini.​—w20.05, uku. 13.

Sifa kenda zenye kutajwa katika Wagalatia 5:22, 23 njo sehemu zote za “tunda la roho”?

Hapana. Roho takatifu inatusaidia tukomalishe sifa zingine za muzuri, kama vile haki. (Efe. 5:8, 9)​—w20.06, uku. 17.

Mambo yenye inakuhusu yenye unatia ku Enternete inaweza kuwa na matokeo gani?

Mambo yenye unatia ku Enternete, inaweza kufanya wengine wawaze kama uko na majivuno ao hauko munyenyekevu.​—w20.07, uku. 6-7.

Wahubiri Wakristo wanaweza kujifunza nini kupitia mufano wa wavuvi wa samaki?

Wavuvi wa samaki wanaendaka kutumika saa yenye inawezekana wapate samaki, na fasi kwenye inawezekana waipate. Wanakuwaka na vyombo vyenye kufaa na wanajua kuvitumia muzuri. Wanakuwaka hodari na wanajikazaka kutumika hata wakati hali inabadilika. Sisi pia tunaweza kufanya vile mu kazi ya kuhubiri.​—w20.09, uku. 5.

Tunaweza kufanya nini ili kusaidia mwanafunzi wa Biblia amupende Yehova sana?

Tunaweza kumutia moyo akuwe anasoma Biblia kila siku na akuwe anafikiri sana juu ya mambo yenye anasoma. Na tunaweza kumufundisha namna ya kusali.​—w20.11, uku. 4.

1 Wakorinto 15:22 inasema kama “katika Kristo wote watafanywa kuwa wazima.” Wote wenye kuzungumuziwa mu ile andiko ni nani?

Mutume Paulo hakupenda kumaanisha kama kila mwanadamu atafufuliwa. Alikuwa anazungumuzia Wakristo watiwa-mafuta, ni kusema, wale wenye ‘wametakaswa katika umoja na Kristo Yesu.’ (1 Ko. 1:2; 15:18)​—w20.12, uku. 5-6.

Wakristo watiwa-mafuta watafanya nini kisha ‘kubadilishwa, kwa kufunga na kufungua jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho’?​—1 Ko. 15:51-53.

Watasaidia Yesu kuchunga watu kwa fimbo ya chuma. (Ufu. 2:26, 27)​—w20.12, uku. 12-13.