Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 51

“Yehova . . . Anaokoa Wale Wenye Kuvunjika Moyo”

“Yehova . . . Anaokoa Wale Wenye Kuvunjika Moyo”

“Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo; anaokoa wale wenye kuvunjika moyo.”​—ZB. 34:18, maelezo ya chini.

WIMBO 30 Baba Yangu, Mungu Wangu, Rafiki Yangu

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

WAKATI fulani, tunaweza kufikiria namna maisha ni ya mufupi na ‘yenye kujaa taabu.’ (Yob. 14:1) Ile inaweza kufanya tuvunjike moyo wakati fulani. Watumishi fulani wa Yehova wa zamani walijisikiaka pia kuwa wenye kuvunjika moyo. Wamoja kati yao walipendaka hata wakufe. (1 Fa. 19:2-4; Yob. 3:1-3, 11; 7:15, 16) Lakini kila mara, Yehova alikuwa anawatia moyo na kuwatia nguvu kwa sababu walimutumainia. Habari yao iliandikwa katika Biblia ili itufariji na itufundishe.​—Ro. 15:4.

2 Mu hii habari, tutazungumuzia watumishi fulani wa Yehova wenye walivumilia magumu yenye kuvunja moyo. Tutazungumuzia Yosefu mwana wa Yakobo, mujane Naomi na Rutu binti-mukwe wake, Mulawi mwenye aliandika Zaburi ya 73, na mutume Petro. Namna gani Yehova aliwatia nguvu? Na mifano yao inaweza kutufundisha nini? Majibu ya ile maulizo itatuhakikishia kama “Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo,” na “anaokoa wale wenye kuvunjika moyo.”​—Zb. 34:18, maelezo ya chini.

YOSEFU ALICHUKIWA NA ALITENDEWA BILA HAKI

3-4. Ni nini ilimupata Yosefu wakati alikuwa kijana?

Yosefu alikuwa na miaka 17 hivi wakati alilota ndoto mbili zenye zilitoka kwa Mungu. Zile ndoto zilionyesha kama siku moja Yosefu angekuwa na mamlaka na watu wa familia yake wangemuheshimia. (Mwa. 37:5-10) Lakini muda mufupi kisha Yosefu kulota zile ndoto, maisha yake ilibadilika kabisa. Kuliko kumuheshimia, ndugu zake walimuuzisha katika utumwa. Kisha wakati fulani, alianza kutumika mu nyumba ya ofisa Mumisri mwenye aliitwa Potifa. (Mwa. 37:21-28) Mu wakati kidogo tu, Yosefu hakukuwa tena kwao pamoja na baba yake mwenye alimupenda sana. Lakini alikuwa sasa mutumwa mwenye kuzarauliwa mu nyumba ya ofisa mupagani katika Misri.​—Mwa. 39:1.

4 Kisha, mambo ilifikia kuwa mubaya sana. Bibi ya Potifa alimushitaki Yosefu kama alijaribu kulala naye kinguvu. Bila hata kutafuta kujua kama ile mashitaka ilikuwa ya kweli, Potifa alimutia Yosefu katika gereza, na mule Yosefu alifungwa katika minyororo. (Mwa. 39:14-20; Zb. 105:17, 18) Fikiria namna Yosefu alijisikia wakati alishitakiwa ile mambo ya mubaya. Na fikiria namna ile mashitaka ingefanya watu waseme mubaya juu ya jina la Yehova. Kwa kweli, ile ilipaswa kumufanya Yosefu avunjike moyo!

5. Yosefu alifanya nini ili aweze kupambana na hali ya kuvunjika moyo?

5 Wakati Yosefu alikuwa mutumwa na wakati alikuwa mu gereza, hakuna jambo lenye angeweza kufanya ili kubadilisha hali yake. Sasa, nini ilimusaidia aendelee kuwa na mawazo yenye kufaa? Kuliko kukaza akili juu ya mambo yenye hakukuwa na uwezo wa kufanya, alifanya kwa bidii kazi yenye alipewa. Na zaidi ya yote, aliendelea kumutia Yehova pa nafasi ya kwanza mu maisha yake. Na Yehova alibariki kila jambo lenye Yosefu alifanya.​—Mwa. 39:21-23.

6. Inawezekana ni nini ingine ilimusaidia Yosefu? Fasiria.

Tena, inawezekana Yosefu alitiwa moyo wakati alikuwa anafikiria ndoto zenye alilotaka. Zile ndoto zilionyesha kama angeona tena watu wa familia yake na hali yake ingekuwa muzuri zaidi. Na ni vile mambo ilikuwa. Wakati Yosefu alikuwa na miaka 37 hivi, zile ndoto zilianza kutimia mu njia ya ajabu sana!​—Mwa. 37:7, 9, 10; 42:6, 9.

7. Kulingana na 1 Petro 5:10, nini njo inaweza kutusaidia tuvumilie majaribu?

7 Mambo yenye tunajifunza. Ile habari inatukumbusha kama, mu ulimwengu huu, watu hawana huruma na wanaweza kututendea bila haki. Na hata Mukristo mwenzetu anaweza kututendea bila haki. Lakini, kama tunamuona Yehova kuwa Mwamba na Kimbilio letu, hatutavunjika moyo ao kuacha kumutumikia. (Zb. 62:6, 7; soma 1 Petro 5:10.) Kumbuka pia kwamba, inawezekana Yosefu alikuwa na miaka 17 hivi wakati alilota zile ndoto zenye zilitoka kwa Yehova. Ile inaonyesha kama Yehova anatumainia vijana wenye kumutumikia. Leo, vijana wengi wako kama Yosefu. Wao pia wanamutumainia Yehova. Na hata wamoja kati yao wamefungwa bila haki kwa sababu walikataa kuacha kumutii Yehova.​—Zb. 110:3.

WANAMUKE WAWILI WENYE WALIKUWA NA HUZUNI MINGI

8. Ni mambo gani ilimupata Naomi na Rutu?

8 Kwa sababu ya njaa kubwa, Naomi na familia yake waliacha makao yao katika Yuda na wakaenda kuishi mu inchi ingine yenye iliitwa Moabu. Wakati walikuwa kule, Elimeleki, bwana ya Naomi, akakufa, na Naomi akabakia na watoto wake wawili wanaume. Kisha wakati fulani, watoto wa Naomi walioa wanamuke wa Moabu, ni kusema, Rutu na Orpa. Kisha miaka kumi hivi, watoto wa Naomi walikufa pia, bila kuzaa watoto. (Rut. 1:1-5) Bila shaka, ile ilihuzunisha sana wale wanamuke watatu! Kwa kweli, Rutu na Orpa wangeweza kuolewa tena. Sasa, nani njo angehangaikia Naomi mwenye alikuwa amezeeka? Naomi alivunjika moyo sana mupaka akafikia kusema hivi: “Musiniite Naomi. Muniite Mara, kwa maana Mweza-Yote amefanya maisha yangu yakuwe machungu sana.” Kisha kupata ile magumu yote, Naomi aliamua kurudia Betlehemu, na Rutu akaenda pamoja naye.​—Rut. 1:7, 18-20.

Mungu alionyesha Naomi na Rutu kama anaweza kusaidia watumishi wake wapambane na hali ya kuvunjika moyo na huzuni. Anaweza kukusaidia wewe pia? (Ona fungu la 8-13) *

9. Kulingana na Rutu 1:16, 17, 22, namna gani Rutu alimutia moyo Naomi?

9 Nini njo ilimusaidia Naomi? Ni upendo mushikamanifu. Kwa mufano, Rutu alionyesha Naomi upendo mushikamanifu kwa kubakia pamoja naye. (Soma Rutu 1:16, 17, 22.) Katika Betlehemu, Rutu alitumika kwa bidii sana ili kuokota mbegu ya shayiri kwa ajili yake na Naomi. Na ile ilifanya watu waone kama Rutu alikuwa mwanamuke muzuri na mwenye bidii.​—Rut. 3:11; 4:15.

10. Namna gani Yehova alionyesha kuwa alihangaikia watu wenye walikuwa maskini sawa vile Naomi na Rutu?

10 Yehova alikuwa amepatia Waisraeli sheria yenye ilionyesha kama alisikilia huruma watu wenye walikuwa maskini sawa vile Naomi na Rutu. Aliambia Waisraeli kama wakati walikuwa wanavuna, hawakupaswa kuvuna sehemu zenye kuwa ku mipaka ya shamba. Walipaswa kuziachia maskini. (Law. 19:9, 10) Kwa hiyo, Naomi na Rutu hawakukuwa na lazima ya kuomba-omba chakula. Wangeweza kupata chakula mu njia yenye kufaa.

11-12. Namna gani Boazi alifanya Naomi na Rutu wakuwe na furaha?

11 Rutu alikuwa anaenda kuokota mbegu za shayiri mu shamba ya mwanaume tajiri mwenye kuitwa Boazi. Boazi aliguswa moyo sana wakati aliona namna Rutu alishikamana na Naomi mama-mukwe wake na namna alimuonyesha upendo. Ile ilimuchochea Boazi auze uriti wa familia ya Naomi na aoe Rutu. (Rut. 4:9-13) Walizaa mutoto mwenye aliitwa Obedi, mwenye alifikia kuwa tate ya Mufalme Daudi.​—Rut. 4:17.

12 Bila shaka, Naomi alifurahi sana wakati alibeba Obedi mu mikono yake, na inawezekana alisali kwa Yehova ili kumushukuru! Lakini Naomi na Rutu wangali watapata baraka zingine. Wakati watafufuliwa, watafurahi kujua kama Masiya mwenye aliahidiwa, ni kusema, Yesu Kristo, alikuwa muzao wa Obedi!

13. Habari juu ya Naomi na Rutu inaweza kutufundisha mambo gani ya maana?

13 Mambo yenye tunajifunza. Wakati tuko tunapambana na magumu, tunaweza kuvunjika moyo, na hata kushuka moyo. Pengine tunaona kama magumu yetu haitaisha. Kama tuko mu ile hali, tunapaswa kumutumainia Baba yetu wa mbinguni na kubakia karibu na ndugu na dada zetu mu kutaniko. Pengine Yehova hatamaliza magumu yetu. Tukumbuke kama, hakufufuaka bwana ya Naomi na watoto wake. Lakini alimusaidiaka kupambana na magumu yake. Sisi pia, atatusaidia tupambane na magumu yetu pengine kwa kuchochea ndugu na dada zetu watuonyeshe upendo mushikamanifu.​—Mez. 17:17.

MULAWI MWENYE ALIKUWA KARIBU KUACHA KUMUTUMIKIA YEHOVA

Muandikaji wa Zaburi ya 73 alikaribia kuacha kumutumikia Yehova kwa sababu, kuliko kukaza akili yake juu ya Yehova, alianza kusikilia wivu watu wenye walionekana kuwa na maisha ya muzuri. Ile inaweza kutufikia pia (Ona fungu la 14-16)

14. Juu ya nini Mulawi fulani alivunjikaka moyo sana?

14 Muandikaji wa Zaburi ya 73 alikuwa Mulawi. Kwa hiyo, alikuwa na pendeleo kubwa la kutumikia mahali pa ibada pa Yehova. Lakini, wakati fulani mu maisha yake, alivunjika moyo. Juu ya nini? Alianza kusikilia wivu watu wabaya na wenye kiburi. Haiko juu ya mambo ya mubaya yenye walikuwa wanafanya, lakini juu walionekana kuwa wako na maisha ya muzuri kuliko yeye. (Zb. 73:2-9, 11-14) Walionekana kama wako na kila kitu: utajiri, maisha ya muzuri na yenye haina mahangaiko. Ile ilimufanya ule Mulawi avunjike moyo mupaka akasema hivi: “Hakika nimesafisha moyo wangu bure na kunawa mikono yangu katika kukosa kuwa na hatia.” Kwa kweli, ule Mulawi alikuwa katika hatari ya kiroho.

15. Kulingana na Zaburi 73:16-19, 22-25, ni nini ilisaidia Mulawi mwenye aliandika ile zaburi asiendelee kuvunjika moyo?

15 Soma Zaburi 73:16-19, 22-25. Ule Mulawi ‘aliingia katika patakatifu pakubwa pa Mungu.’ Wakati alikuwa mule, inawezekana alikuwa pamoja na waabudu wengine wa Yehova, na angeweza kutulia, kufikiri muzuri, na kusali juu ya hali yake. Kisha kufanya vile, alianza kuona kama mawazo yake haikukuwa ya muzuri, na kama angefikia kupoteza urafiki wake pamoja na Yehova. Alielewa pia kama watu wabaya wako wanatembea “kwenye udongo wenye kutereza” na watakuwa na “mwisho mubaya sana.” Ili kuacha kuwa na tamaa na ili asiendelee kuvunjika moyo, ule Mulawi alipaswa kuwa na mawazo kama ya Yehova. Kisha kujikaza kuwa na mawazo kama ya Yehova, alifikia kuwa tena na amani na furaha. Alisema hivi: “Sitamani kitu chochote katika dunia isipokuwa [Yehova] tu.”

16. Mufano wa ule Mulawi unatufundisha nini?

16 Mambo yenye tunajifunza. Hatupaswe hata kidogo kusikilia wivu watu wabaya wenye wanaonekana kuwa wako na maisha ya muzuri. Furaha yao ni ya juu-juu tu na ni ya wakati kidogo. Hawana tumaini la kuishi milele. (Muh. 8:12, 13) Kama tunawasikilia wivu, tutavunjika moyo na tunaweza kupoteza hata urafiki watu na Yehova. Ikiwa unaanza kusikilia wivu watu wabaya, ufanye mambo yenye ule Mulawi alifanya. Usikilize mashauri ya Mungu yenye upendo, na upitishe wakati na watumishi wengine wa Yehova. Kama unamupenda Yehova kuliko mambo ingine yote, utakuwa na furaha ya kweli. Na utabakia katika barabara yenye inaongoza kwenye “uzima wa kwelikweli.”​—1 Ti. 6:19.

PETRO ALIVUNJIKA MOYO KWA SABABU YA UZAIFU WAKE

Wakati tunafikiria namna Petro aliacha kuvunjika moyo na akaendelea kumutumikia Yehova, sisi pia tunaweza kuacha kuvunjika moyo na kusaidia wengine waendelee kumutumikia Yehova (Ona fungu la 17-19)

17. Juu ya nini Petro alivunjika moyo?

17 Mutume Petro alikuwa mwanaume mwenye bidii, lakini wakati fulani alitenda na kusema bila kufikiri. Na ile ilifanya ahuzunike. Kwa mufano, wakati Yesu aliambia mitume wake kama angeteseka na kufa, Petro alimukemea kwa kusema hivi: “Mambo hayo hayatakupata hata kidogo.” (Mt. 16:21-23) Lakini Yesu alimurekebisha. Tena, wakati kikundi cha watu kilikuja kumukamata Yesu, Petro alitenda bila kufikiri na akakata sikio la mutumwa wa kuhani mukubwa. (Yoh. 18:10, 11) Mara ingine, Yesu alimurekebisha. Zaidi ya ile, Petro alijisifu kama, hata ikiwa mitume wengine wote wanamuacha Kristo, yeye hawezi kufanya vile hata kidogo! (Mt. 26:33) Lakini, hata kama alijitumainia sana, alifikia kuogopa wanadamu na akamukana Bwana wake mara tatu. Petro alivunjika moyo sana, na “akaenda inje na kulia kwa uchungu.” (Mt. 26:69-75) Pengine alijiuliza ikiwa Yesu angeweza kumusamehe.

18. Namna gani Yesu alimusaidia Petro asiendelee kuvunjika moyo?

18 Hata vile, Petro hakuacha ile hali imufanye aendelee kuvunjika moyo. Kisha kufanya ile kosa, aliendelea kumutumikia Yehova pamoja na mitume wengine. (Yoh. 21:1-3; Mdo. 1:15, 16) Nini njo ilimusaidia? Yesu alikuwa amesali kwa ajili ya Petro ili imani yake isififie. Na Yehova alijibia ile sala ya Yesu yenye kutoka ku moyo. Pia Yesu alikuwa ameambia Petro kama wakati atarudia, atie nguvu ndugu zake. Inawezekana Petro alikumbuka ile mambo yenye kutia moyo. Kisha, Yesu alimutokea Petro wakati Petro alikuwa peke yake, na pengine alimutia moyo. (Lu. 22:32; 24:33, 34; 1 Ko. 15:5) Kisha pale, Yesu alitokea mitume wake kisha mitume wake kupitisha usiku muzima mu bahari ili kuvua samaki, lakini bila kupata kitu. Ni ile wakati njo Yesu alipatia Petro nafasi ya kuonyesha kama anamupenda. Yesu alimusamehe rafiki yake Petro na akamupatia kazi zaidi.​—Yoh. 21:15-17.

19. Namna gani Zaburi 103:13, 14 inaonyesha namna Yehova anatuona wakati tunafanya zambi?

19 Mambo yenye tunajifunza. Namna Yesu alimutendea Petro inaonyesha kama iko na huruma sawa vile Baba yake. Kwa hiyo, wakati tunafanya makosa, hatupaswe kujihukumu kupita kiasi na kufikiri kama Yehova hawezi kutusamehe hata kidogo. Tunapaswa kukumbuka kama ile njo mawazo yenye Shetani anapenda tukuwe nayo. Kuliko kuwa na ile mawazo, tukumbuke kama Yehova anatupenda, anaelewa mipaka yetu, na anapenda kutusamehe. Sisi pia tunapaswa kumuiga wakati wengine wanatukosea.​—Soma Zaburi 103:13, 14.

20. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

20 Mufano wa Yosefu, Naomi na Rutu, Mulawi, na Petro unatuhakikishia kama “Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo.” (Zb. 34:18) Anaruhusu tupate magumu na tuvunjike moyo wakati fulani. Lakini, wakati tunavumilia ile magumu kwa musaada wake, tunakuwa na imani yenye nguvu. (1 Pe. 1:6, 7) Mu habari yenye kufuata, tutaona mambo ingine yenye kuonyesha namna Yehova anasaidia watumishi wake waaminifu wenye wanavunjika moyo, pengine kwa sababu ya makosa yao ao kwa sababu ya magumu yenye wanapambana nayo.

WIMBO 7 Yehova, Nguvu Yetu

^ fu. 5 Yosefu, Naomi na Rutu, Mulawi fulani, na mutume Petro walipambana na hali zenye ziliwafanya wavunjike moyo. Mu hii habari, tutaona namna Yehova aliwafariji na kuwatia nguvu. Tutaona pia mambo yenye tunaweza kujifunza wakati tunafikiria mifano yao na namna Yehova aliwatendea kwa huruma.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Naomi, Rutu, na Orpa walihuzunika sana na kuvunjika moyo wakati bwana zao walikufa. Kisha, Rutu na Naomi walifurahi pamoja na Boazi wakati Obedi alizaliwa.