Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 49

Mambo Yenye Kitabu ya Walawi Inatufundisha Kuhusu Namna ya Kutendea Wengine

Mambo Yenye Kitabu ya Walawi Inatufundisha Kuhusu Namna ya Kutendea Wengine

“Unapaswa kumupenda mwenzako kama wewe mwenyewe.”​—LAW. 19:18.

WIMBO 109 Tupendane Sana Kutoka Ndani ya Moyo

KIFUPI YA HABARI *

1-2. Ni mambo gani tulizungumuzia mu habari yenye ilitangulia, na ni mambo gani tutazungumuzia mu hii habari?

 MU HABARI yenye ilitangulia, tulizungumuzia mashauri ya muzuri yenye kuwa mu sura ya 19 ya kitabu ya Mambo ya Walawi. Kwa mufano, mu mustari wa 3, Yehova aliambia Waisraeli kama walipaswa kuheshimia wazazi wao. Tuliona namna gani leo tunapaswa kutumikisha ile shauri ili kusaidia wazazi wetu wapate mambo yenye wako nayo lazima, kuwatia moyo, na kuwafariji na kuwasaidia waendelee kumutumikia Yehova. Mu ileile andiko, Mungu alikumbusha watu wake kuhusu ulazima wa kushika Sabato. Lakini tulijifunza kama hata kama hatushikake Sabato leo, tunaweza kutumia kanuni yenye kuwa mu ile sheria, kwa kupanga wakati wetu muzuri ili kufanya mambo ya kiroho. Kama tunafanya vile, ile itaonyesha kama tuko tunajikaza kuwa watakatifu, sawa vile Mambo ya Walawi 19:2 na 1 Petro 1:15 inaonyesha.

2 Mu hii habari, tutaendelea kuzungumuzia sura ya 19 ya kitabu ya Mambo ya Walawi. Ni mambo gani tunaweza kujifunza mu hii sura kuhusu namna ya kuonyesha kama tunahangaikia wale wenye kuwa na ulemavu fulani, kuhusu kuwa wanyoofu mu mambo ya biashara, na kuhusu kuonyesha wengine upendo? Tunapenda kuwa watakatifu sawa vile Mungu yeye ni mutakatifu, kwa hiyo basi, muache tuzungumuzie mambo fulani yenye tunaweza kujifunza mu ile sura.

ONYESHA HURUMA WALE WENYE KUWA NA ULEMAVU FULANI

Mambo ya Walawi 19:14 inatutia moyo kuwa na mawazo na matendo ya namna gani kuelekea mutu mwenye ni kiziwi ao kipofu? (Ona fungu ya 3-5) *

3-4. Kulingana na Mambo ya Walawi 19:14, namna gani kiziwi na kipofu walipaswa kutendewa?

3 Soma Mambo ya Walawi 19:14. Yehova anapenda watu wake waonyeshe huruma wale wenye kuwa na ulemavu fulani. Kwa mufano, Waisraeli hawakupaswa kulaani kiziwi. Kulaani kiziwi ilitia ndani kumuogopesha ao kusema jambo fulani ya mubaya juu yake. Kufanyia vile kiziwi ni mubaya sana! Juu hangeweza kusikia mambo yenye walikuwa wanasema juu yake, ao hangeweza kujitetea.

4 Zaidi ya ile, mu mustari wa 14 tunajifunza kama watumishi wa Mungu, hawakupaswa kutia “kizuizi mbele ya kipofu.” Kitabu moja, yenye inazungumuzia magumu ya watu wenye kuwa na ulemavu fulani wa kimwili, inasema hivi: “Mu eneo ya Israeli ya zamani [watu walemavu] walikuwa wanatumikishwa mubaya na kutendewa mubaya.” Pengine watu fulani wenye hawana roho ya muzuri, wangetia kizuizi fulani mbele ya kipofu juu ajiumize ao juu walipenda tu wamucheke. Ile ni kukosa huruma! Lakini kupitia sheria yenye Yehova alipatia watu wake, alipenda kuwasaidia waone kama walipaswa kuonyesha huruma wale wenye kuwa na ulemavu fulani.

5. Namna gani tunaweza kuonyesha huruma wale wenye kuwa na ulemavu fulani?

5 Yesu alionyesha huruma wale wenye walikuwa na ulemavu fulani. Ona ujumbe wenye alimutumia Yohana mubatizaji: “Sasa vipofu wanaona, vilema wanatembea, wenye ukoma wanafanywa kuwa safi, viziwi wanasikia, [na] wafu wanafufuliwa.” Kisha kuona ile miujiza yote yenye Yesu alifanya, “watu wote . . . wakamusifu Mungu.” (Lu. 7:20-22; 18:43) Wakristo wanapenda kabisa kuiga mufano wa Yesu kwa kuonyesha huruma wale wenye kuwa na ulemavu fulani. Tuko na huruma, na tunavumilia wale wenye kuwa na ulemavu. Lakini, Yehova hakutupatia uwezo wa kufanya miujiza, kama vile Yesu. Hata vile, tuko na pendeleo kubwa sana ya kutangazia habari njema kuhusu paradiso watu wenye kuwa vipofu kiroho na kimwili. Mu ile paradiso, watu watakuwa na afya ya muzuri sana ya kimwili na ya kiroho (Lu. 4:18) Ile habari njema tayari inafanya watu wengi wamusifu Mungu.

UKUWE MUNYOOFU MU MAMBO YA BIASHARA

6. Namna gani mambo yenye kuzungumuziwa mu sura ya 19 ya Mambo ya Walawi inatusaidia kuelewa muzuri zaidi zile Amri Kumi?

6 Mistari fulani yenye kuwa mu Mambo ya Walawi sura ya 19 inatusaidia kuelewa mambo yenye ilizungumuziwa mu Amri Kumi. Kwa mufano, amri ya munane ilisema tu hivi: “Haupaswe kuiba.” (Kut. 20:15) Mutu fulani anaweza kuwaza kama, ikiwa hayakamataka kitu yenye haiko yake, ile inaonyesha kama iko anatii ile amri. Kumbe inawezekana anaibaka mu njia zingine.

7. Namna gani mufanyabiashara anaweza kuvunja amri ya munane kuhusu wizi?

7 Mufanyabiashara fulani anaweza kuwaza kama haiko mwizi juu tu hayakamataka kitu ya mutu mwingine. Lakini tuseme nini kuhusu kukosa unyoofu mu mambo ya biashara? Sawa vile inaonyeshwa mu Mambo ya Walawi 19:35, 36, Yehova alisema hivi: “Hamupaswe kutumia vipimo vya uongo, ili kupima urefu, uzito, ao ujazo. Munapaswa kutumia mizani yenye kuwa sawa, vipimo vyenye kuwa sawa, kipimo chenye kuwa sawa cha vitu vyenye kukauka, na kipimo chenye kuwa sawa cha vitu vya majimaji.” Mufanyabiashara mwenye angetumia mizani ao vipimo vya uongo, juu ya kudanganya wa clients wake, tunaweza kusema kama alikuwa anawaiba. Mistari ingine ya Mambo ya Walawi sura ya 19 inafasiria ile pia wazi.

Kulingana na Mambo ya Walawi 19:11-13, ni jambo gani Mukristo mwenye ni mufanyabiashara anaweza kuchunguza kuhusu namna anafanya kazi yake? (Ona fungu ya 8-10) *

8. Namna gani mafasirio yenye kuwa mu Mambo ya Walawi 19:11-13 ilisaidia Wayahudi watumikishe kanuni yenye ilikuwa nyuma ya ile amri ya munane, na ile inaweza kutuletea faida gani?

8 Soma Mambo ya Walawi 19:11-13. Maneno ya mwanzo-mwanzo ya Mambo ya Walawi sura ya 19:11 inasema hivi: “Hamupaswe kuiba.” Mustari wa 13 unaonyesha uhusiano wenye kuwa kati ya wizi na kukosa unyoofu mu mambo ya biashara; ile mustari inasema hivi: “Haupaswe kumupunja mwenzako.” Kwa hiyo, kuko uhusiano kati ya wizi na kukosa unyoofu mu mambo ya biashara. Amri ya munane inasema kama kuiba ni mubaya, lakini mafasirio yenye kuwa mu kitabu ya Mambo ya Walawi ilisaidia Wayahudi kuelewa namna ya kutumia kanuni yenye ilikuwa nyuma ya ile sheria, ni kusema, namna wangekuwa wanyoofu mu mambo yote yenye walifanya. Tunaweza kupata faida sana wakati tunafikiria mawazo ya Yehova juu ya wizi na kukosa unyoofu. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Wakati nafikiria Mambo ya Walawi 19:11-13, naona kabisa kama niko na lazima ya kufanya mabadiliko mu maisha yangu, zaidi sana mu njia yenye nafanya biashara?’

9. Namna gani sheria yenye kuwa mu Mambo ya Walawi 19:13 ililinda wafanyakazi?

9 Kuko jambo ingine pia ya lazima sana kuhusu unyoofu yenye Mukristo mwenye ni mufanyabiashara anapaswa kufikiria. Mambo ya Walawi 19:13 inamalizia kwa kusema hivi: “Haupaswe kubakia na mushahara wa mufanyakazi usiku wote mupaka asubui.” Zamani, mu taifa ya Israeli, wafanyakazi wenye walikuwa wanatumika mu shamba walipaswa kulipwa kila siku ku mwisho wa kazi yao. Kukosa kulipa ule mufanyakazi mushahara wake, ingefanya akose makuta ya kutimiza mahitaji ya familia yake ya ile siku. Yehova alifasiria hivi: “Iko katika uhitaji na uzima wake unategemea mushahara wake.”​—Kum. 24:14, 15; Mt. 20:8.

10. Ni jambo gani tunaweza kujifunza mu Mambo ya walawi 19:13?

10 Leo, wakubwa wengi wa kazi wanalipaka mara moja ao mara mbili kwa mwezi, lakini hapana kila siku. Hata vile, kanuni yenye kuwa mu Mambo ya Walawi 19:13 ingali ya maana hata leo. Wakubwa fulani wa kazi, wako wanatumikisha mubaya wafanyakazi wao kwa kuwalipa mushahara yenye iko chini sana kulinganisha na kazi yenye wanafanya. Wanajua kama wafanyakazi pengine hawana ya kufanya, wanapaswa tu kuendelea kutumika hata kama mushahara iko kidogo. Mu njia fulani, wale wakubwa wa kazi wako ‘wanabakia na mushahara wa wafanyakazi wao.’ Mukristo mwenye iko anatumikisha watu wengine, anapaswa kufikiria ile wazo kwa uzito sana. Muache sasa tuone jambo ingine yenye tunajifunza mu sura ya 19 ya kitabu ya Mambo ya Walawi.

KUPENDA WENZETU KAMA SIYE WENYEWE

11-12. Yesu alifasiria mambo gani waziwazi wakati alitaja maneno yenye kuwa mu Mambo ya Walawi 19:17, 18?

11 Zaidi ya kutuambia kama tunapaswa kuepuka kuumiza wengine, Mungu anapendezwa na namna tunatendea watu. Tunaweza kujifunza ile mu Mambo ya Walawi 19:17, 18. (Soma.) Yehova alisema waziwazi hivi: “Unapaswa kumupenda mwenzako kama wewe mwenyewe.” Kutenda mu ile njia, ni jambo ya maana sana kwa Mukristo mwenye anapenda kumufurahisha Mungu.

12 Yesu alionyesha kama, amri yenye kuwa mu Mambo ya Walawi 19:18 iko ya maana sana. Wakati Mufarisayo mumoja alimuuliza Yesu hivi: “Ni amri gani ndiyo kubwa zaidi katika sheria?” Yesu alimujibia kama “amri kubwa zaidi na ya kwanza” ni ile ya kumupenda Yehova kwa moyo wetu wote, kwa nafsi yetu yote, na kwa akili yetu yote. Kisha Yesu alitaja Mambo ya Walawi 19:18, yenye inasema hivi: “Ya pili kama hiyo, ni hii: ‘Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.’” (Mt. 22:35-40) Kuko njia mingi za kuonyesha wengine upendo. Lakini, hapa tena tunaweza kujifunza mambo fulani mu sura ya 19 ya Mambo ya Walawi.

13. Namna gani tunaweza kuelewa muzuri zaidi Mambo ya Walawi 19:18 wakati tunafikiria habari ya Yosefu?

13 Njia moja yenye tunaweza kuonyesha majirani wetu kama tunawapenda ni wakati tunatumikisha shauri yenye kuwa mu Mambo ya Walawi 19:18. Yenye inasema: ‘Haupaswe kulipiza kisasi wala kuweka kinyongo.’ Wengi kati yetu tunajua watu wenye wanawekaeka kinyongo, hata kwa miaka mingi, wafanyakazi wenzao, wanafunzi wenzao ao watu wa familia yao. Ukumbuke kama ndugu kumi wa Yosefu walimuwekea kinyongo, na ile ilifanya wamutendee mubaya juu walimuchukia. (Mwa. 37:2-8, 25-28) Lakini Yosefu alitenda tofauti nao! Wakati alikuwa na mamlaka alikuwa na uwezo wa kulipiza kisasi lakini hakufanya vile, aliwaonyesha huruma. Yosefu hakuwawekea kinyongo. Alitenda mu njia yenye inapatana na shauri yenye kuwa mu Mambo ya Walawi 19:18.​—Mwa. 50:19-21.

14. Ni nini inaonyesha kama kanuni zenye tunapata mu Mambo ya Walawi 19:18 zingali zinatumika mupaka leo?

14 Wakristo wenye wanapenda kumufurahisha Mungu, wanapaswa kuiga mufano wa Yosefu mwenye alisamehe ndugu zake kuliko kuwatendea mubaya ili kulipiza kisasi. Ile pia njo Yesu alisema mu sala ya mufano wakati alisema kama tunapaswa kusamehe wale wenye wanatukosea. (Mt. 6:9, 12) Vilevile, Mutume Paulo alishauria Wakristo wenzake hivi: “Wapendwa, musijilipizie kisasi.” (Ro. 12:19) Tena aliwatia moyo kwa kusema hivi: “Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa kupenda hata kama mutu yeyote iko na sababu ya kulalamika juu ya mwingine.” (Kol. 3:13) Kanuni za Yehova hazibadilikake. Kanuni zenye kuwa nyuma ya ile sheria yenye kuzungumuziwa mu Mambo ya Walawi 19:18 zingali zinatumika mupaka leo.

Sawa vile tu haiko muzuri kuendelea kugusa-gusa kidonda, ni vile pia haiko muzuri kuendelea kufikiria makosa yenye wengine walitutendea. Tunapaswa kuiacha nyuma yetu (Ona fungu ya 15) *

15. Ni mufano gani unatusaidia kuelewa juu ya nini tunapaswa kusamehe na kusahau?

15 Fikiria mufano wenye kufuata. Tuseme, makosa yenye mutu alikutendea inaweza kufananishwa na vidonda. Vidonda fulani ni vya kidogo; lakini vingine vinakuwaka vikubwa. Kwa mufano, wakati uko nakata tomate, unaweza kujiumiza kidogo ku vidole. Kusema kweli italuma, lakini pengine maumivu yake haitakawia sana. Pengine kisha siku moja ao mbili hautakumbuka hata fasi kwenye ulijikataka. Vilevile, makosa fulani yenye watu wanatutendea, inaweza kuwa ya kidogo. Kwa mufano, rafiki anaweza kusema ao kufanya jambo yenye inatuumiza, lakini inaweza kuwa mwepesi kumusamehe. Lakini tuseme nini kama tuko na kidonda ya mukubwa, pengine muganga atashona kidonda yetu na kufunga bandage. Lakini kama siye tunaanza kukamata-kamata mu ile kidonda, haitapona mbio na tutajiletea tu maumivu bure. Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, mutu anaweza kufanya vile wakati wengine wanamukosea sana. Anaweza kuendelea kufikiri sana juu ya makosa yenye mwingine alimutendea. Lakini, wale wenye wanachungaka kinyongo, wanajiumizaka tu wao wenyewe. Njo maana, ni muzuri zaidi kutii shauri yenye kuwa mu Mambo ya Walawi 19:18, hauone vile?

16. Kulingana na Mambo ya Walawi 19:33, 34, namna gani Waisraeli walipaswa kutendea wakaaji wageni wenye walikuwa wanaishi nao, na ile inaweza kutufundisha nini?

16 Wakati Yehova aliamuru Waisraeli wapende wenzao, hakupenda kusema kama wanapaswa kupenda tu wale wenye walikuwa wa rangi moja ya ngozi ao wa taifa yao. Lakini aliwaambia pia kama walipaswa kupenda wageni wenye walikuwa wanaishi kati yao. Na ile njo wazo yenye tunapata kabisa mu Mambo ya Walawi 19:33, 34. (Soma.) Mugeni alipaswa kutendewa “kama mwenyeji,” na Waisraeli walipaswa “kumupenda” kama wao wenyewe. Kwa mufano, sheria ilisema kama Waisraeli walipaswa kuachia masalio wakaaji wageni na masikini. (Law. 19:9, 10) Ile kanuni kuhusu kupenda wageni, inatumika pia kwetu leo. (Lu. 10:30-37) Namna gani? Kuko mamilioni ya watu wenye wanatoka mu inchi yao na wanaenda fasi ingine, na inawezekana hata kuko wamoja kati yao wanaishi karibu na kwetu. Ni jambo ya lazima sana kutendea wale wanaume, wanamuke, na watoto kwa heshima na upendo sana.

KAZI YA MAANA YENYE KUZUNGUMUZIWA MU MAMBO YA WALAWI SURA YA 19

17-18. (a) Mambo ya Walawi 19:2 na 1 Petro 1:15 inatutia moyo kufanya nini? (b) Ni kazi gani kubwa yenye Mutume Petro alitutia moyo kufanya?

17 Mambo ya Walawi 19:2 na 1 Petro 1:15 inaomba watu wa Mungu wakuwe watakatifu. Mistari ingine mingi yenye kuwa mu sura ya 19 ya kitabu ya Mambo ya Walawi inaweza kutusaidia kujua nini tunapaswa kufanya juu tukubaliwe na Yehova. Tumezungumuzia mistari fulani yenye inatuonyesha tu mambo fulani ya muzuri yenye tunapaswa kufanya na mambo fulani ya mubaya yenye tunapaswa kuepuka. * Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaonyesha kama Yehova anapenda tuendelee kutumia kanuni zake mu maisha yetu. Lakini mutume Petro anaongezea jambo ingine.

18 Tunaweza kuwa tuko tunamuabudu Yehova lakini pia tuko tunafanyia watu wengine mambo ya muzuri. Lakini Petro anatia moyo zaidi sana Wakristo wafanye jambo moja ya maana kabisa. Mbele Petro atutie moyo ili kuwa watakatifu katika mwenendo wetu wote, alisema hivi: “Mukaze akili zenu kwa ajili ya utendaji.” (1 Pe. 1:13, 15) Ile utendaji inatia ndani nini? Petro alisema kama ndugu za Kristo, wenye ni watiwa-mafuta ‘“wangetangaza kotekote sifa za muzuri zaidi” za ule mwenye’ aliwaita. (1 Pe. 2:9) Kwa kweli, Wakristo wote leo wako na pendeleo ya kushiriki mu hii kazi ya maana sana, kazi yenye inasaidia watu wengi kuliko kazi ingine. Ni pendeleo kubwa sana kwa watu watakatifu wa Mungu kushiriki kwa bidii mu hii kazi ya kuhubiri kwa ukawaida na kufundisha! (Mk. 13:10) Wakati tunajikaza kutumikisha kanuni zenye kuwa mu sura ya 19 ya Mambo ya Walawi, tunaonyesha kama tunapenda Mungu na majirani wetu. Lakini pia, tunaonyesha kama tunapenda “kuwa watakatifu” katika mwenendo wetu wote.

WIMBO 111 Mambo Yenye Kufanya Tukuwe na Furaha

^ Wakristo hawako chini ya sheria ya Musa, lakini ile sheria inazungumuzia mambo mingi yenye tunapaswa kufanya ao yenye tunapaswa kuepuka kufanya. Kama tunajifunza kuhusu ile mambo mbalimbali, inaweza kutusaidia kuonyesha upendo wengine na kumufurahisha Mungu. Hii habari itatusaidia kuelewa faida yenye tunaweza kupata kwa kuzungumuzia sura ya 19 ya kitabu ya Mambo ya Walawi.

^ Mistari fulani yenye haikuzungumuziwa mu hii habari na habari yenye ilitangulia, inazungumuzia mambo kama vile, ubaguzi, kusemea wengine mubaya, matumizi ya damu, na pia matendo ya kuzungumuza na mashetani, kutabiri wakati wenye kuja, lakini pia uasherati.​—Law. 19:15, 16, 26-29, 31.​—Ona sehemu “Maulizo ya Wasomaji Wetu” yenye kuwa mu hii gazeti.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu moja mwenye ni Shahidi wa Yehova iko anasaidia ndugu mwingine mwenye ni kiziwi wakati iko anazungumuza na munganga.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu moja mwenye iko nasimamia kazi ya kutia rangi, anapatia mufanyakazi wake mushahara.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Dada fulani anaweza kusahau kwa wepesi kama alijiumiza kidogo. Lakini, atafanya pia vile kama ni kidonda ya mukubwa?