Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 50

Musikilize Sauti ya Muchungaji Mwema

Musikilize Sauti ya Muchungaji Mwema

“Watasikiliza sauti yangu.”​—YOH. 10:16.

WIMBO 3 Nguvu Yangu, Tumaini Yangu, Ninakutegemea

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni sababu gani moja ilifanya Yesu alinganishe wafuasi wake na kondoo?

 YESU alilinganisha urafiki wake na wafuasi wake, pamoja na uhusiano wenye ulikuwa kati ya muchungaji na kondoo wake. (Yoh. 10:14) Ile ulinganisho ni yenye kufaa kabisa. Kondoo wanajuaka muchungaji wao na wanasikilizaka sauti yake. Turiste moja anasema hivi: “Miye na wenzangu tulipenda kukamata picha kondoo fulani, na tulijaribu kuwaita karibu na siye. Lakini, hawakupenda kutufuata juu walikuwa hawajue sauti zetu. Kisha, kijana moja muchungaji alikuja na wakati tu aliwaita, mara moja wakamufuata.”

2-3. (a) Namna gani wafuasi wa Yesu wanaonyesha kama wako wanasikiliza sauti yake? (b) Ni mambo gani tutazungumuzia mu hii habari na habari yenye kufuata?

2 Mufano wa ule turiste, unatukumbusha maneno ya Yesu kuhusu kondoo wake, ni kusema, wanafunzi wake. Alisema hivi: “Watasikiliza sauti yangu.” (Yoh. 10:16) Lakini Yesu iko mbinguni. Namna gani tunaweza kusema kama tuko tunamusikiliza? Njia moja ya maana sana ya kuonyesha kama tuko tunasikiliza sauti ya bwana wetu, ni kutumikisha mafundisho yake mu maisha yetu.​—Mt. 7:24, 25.

3 Mu hii habari na habari yenye kufuata, tutazungumuzia mafundisho fulani ya Yesu. Kama vile tutaona, Yesu alitundisha kama tunapaswa kuacha kufanya mambo fulani na kama tunapaswa kufanya mambo ingine. Tutazungumuzia kwanza mambo mbili yenye muchungaji mwema anatuamuru tuache kufanya.

“MUACHE KUHANGAIKA SANA”

4. Kulingana na Luka 12:29, ni nini inaweza kufanya ‘tuhangaike sana’?

4 Soma Luka 12:29. Yesu aliambia wafuasi wake ‘waache kuhangaika sana’ kuhusu mahitaji yao ya kimwili. Tunajua kama kila mara, shauri ya Yesu inakuwaka ya hekima na ya muzuri. Tunapenda kuitumikisha, lakini wakati fulani inaweza kuwa nguvu kufanya vile. Juu ya nini?

5. Pengine ni juu ya nini watu fulani wanahangaika sana juu ya mahitaji yao ya kimwili?

 5 Watu fulani, wanaweza kuhangaika sana kuhusu namna watapata chakula, nguo, na nyumba. Pengine wanaishi fasi kwenye watu wengi ni maskini, na ni nguvu sana kupata kazi. Inaweza kuwa nguvu kwao kupata makuta ya kuhangaikia familia yao. Ao pengine, mutu mwenye alikuwa na daraka ya kuhangaikia familia yao anaweza kufa na anaacha familia yote bila makuta ya kuwasaidia. Pengine coronavirus ilifanya watu wengi wapoteze kazi na mushahara. (Muh. 9:11) Kama tulishakapatwa na jambo fulani kati ya hii mambo ao jambo ingine, namna gani tunaweza kufuata muongozo wa Yesu wa kuacha kuhangaika sana?

Kuliko kuhangaika juu ya namna tutapata mahitaji yetu ya kimwili, tunapaswa kuendelea kutia nguvu tumaini yetu katika Yehova (Ona fungu ya 6-8) *

6. Fasiria mambo yenye ilifikia mutume Petro siku moja.

6 Siku moja, mutume Petro na mitume wengine, walikuwa mu mashua katika bahari ya Galilaya saa ya zoruba wakati waliona Yesu akitembea juu ya maji. Petro alisema hivi: “Bwana, kama ni wewe, uniamuru nikuje kwenye uko juu ya maji.” Kisha Yesu akamuambia: “Kuja.” Petro akatoka katika mashua, “akatembea juu ya maji na kuenda kwenye Yesu alikuwa.” Ona jambo yenye ilitokea kisha. “Wakati aliangalia ile zoruba yenye upepo mukali, akaogopa. Na wakati alianza kuzama, akasema kwa sauti kubwa: ‘Bwana, niokoe!’” Yesu akanyoosha mukono wake na akamuokoa. Ni jambo ya maana tusisahau kama, Petro angeweza kutembea juu ya maji kama tu angeendelea kumuangalia Yesu. Lakini wakati Petro aliangalia zoruba, akaogopa na akakuwa na mashaka na akaanza kuzama.​—Mt. 14:24-31.

7. Mufano wa Petro unaweza kutufundisha mambo gani?

7 Mufano wa Petro unaweza kutufundisha mambo fulani. Wakati Petro alitoka inje ya mashua na kusimama juu ya maji, hakutazamia kama zoruba ingemukengeusha na aanze kuzama. Alipenda abakie juu ya maji, mupaka afike kwenye bwana wake alikuwa. Lakini alishindwa kukazia uangalifu kusudi yake. Kusema kweli, hatuwezi kutembea juu ya maji, lakini tunakutanaka na majaribu ya imani. Kama tunasahau Yehova na ahadi zake, tutaanza kuzama kiroho. Kwa hiyo, hata kama tuko na magumu ya namna gani, tunapaswa kuendelea kukaza akili yetu kwa Yehova na kuhusu uwezo wake wa kutusaidia. Tunaweza kufanya vile namna gani?

8. Ni nini inaweza kutusaidia kuepuka kuhangaika sana kuhusu mahitaji yetu ya kimwili?

8 Kuliko kuhangaika sana kuhusu magumu yetu, ni jambo ya maana sana kumutumainia Yehova. Tusisahau kama, Baba yetu mwenye upendo Yehova, anatuahidi kama atahangaikia mahitaji yetu ya kimwili kama tunatia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza. (Mt. 6:32, 33) Kila mara anakuwaka anatimiza ile ahadi. (Kum. 8:4, 15, 16; Zb. 37:25) Kama Yehova anakulisha ndege na maua, kusema kweli, hatuna lazima ya kuhangaika juu ya mambo yenye tutakula ao kuvala! (Mt. 6:26-30; Flp. 4:6, 7) Sawa vile tu upendo unachochea wazazi watimizie watoto wao mahitaji yao ya kimwili, upendo unachochea pia Baba yetu wa mbinguni kuhangaikia mahitaji ya kimwili ya watu wake. Ndiyo, tunapaswa kuwa hakika kama Yehova atatuhangaikia!

9. Mufano wa ndugu fulani na bibi yake unaweza kutufundisha nini?

9 Tufikirie mufano moja wenye kuonyesha namna Yehova anahangaikia mahitaji yetu ya kimwili. Ndugu fulani na bibi yake wenye walikuwa mu utumishi wa wakati wote, waliendaka siku moja kukamata dada fulani wenye walikuwa wanaishi mu kambi ya wakimbizi juu waende pamoja nao ku mikutano. Njo maana, walitumia zaidi ya saa moja mu gari yao ya zamani ili kufika kule. Ule ndugu anasema hivi: “Kisha mukutano, tulialika wale dada ku nyumba lakini tulikumbuka kama hatukukuwa hata na chakula ya kuwapatia.” Ule ndugu na bibi yake walifanya nini? Ndugu anaendelea kusema hivi: “Wakati tulifika ku nyumba, tulikuta mbele ya mulango yetu chakula mingi. Hatukujua hata mutu mwenye aliiacha pale. Yehova alituhangaikia.” Kisha wakati fulani, gari ya ule ndugu na bibi yake iliharibika. Ilikuwa nawasaidia mu mahubiri, lakini hawakukuwa na makuta ya kuitengenezesha. Walipeleka ile gari fasi kwenye wanatengenezaka magari ili kuona kama ingewaomba makuta ngapi juu ya kuitengeneza. Kisha mwanaume moja akakuja na kuuliza: “Hii gari ni ya nani?” Ule ndugu alisema kama ni yake, na kama ile gari iliomba itengenezewe. Ule mwanaume alisema hivi: “Hakuna shida. Bibi yangu anapendaka sana gari ya hivi na ya rangi ya hivi. Unapenda nikupatie makuta ngapi juu ya ile gari?” Ule ndugu akamuuzisha ule mwanaume gari yake. Makuta yenye ule ndugu alipata ilimusaidia kuuza gari ingine. Ndugu anasema hivi: “Tulikuwa na furaha sana ku mwisho ya ile siku. Tulijua kama ile haikutokea bure. Ilikuwa mukono wa Yehova.”

10. Namna gani Zaburi 37:5 inatutia moyo tusihangaikie sana mahitaji yetu ya kimwili?

10 Wakati tunasikiliza muchungaji mwema na kuacha kuhangaika sana juu ya vitu vya kimwili, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatuhangaikia. (Soma Zaburi 37:5; 1 Pe. 5:7) Fikiria magumu fulani yenye ilitajwa mu  fungo ya 5. Mupaka leo, Yehova anaweza kutumia kichwa ya familia ao mukubwa fulani wa kazi juu ya kutusaidia kuhangaikia mahitaji yetu ya kila siku. Kama kichwa ya familia hana tena uwezo wa kuhangaikia familia yake, ao kama tulipoteza kazi, Yehova atatuhangaikia mu njia ingine. Tunapaswa kuwa hakika kama atafanya vile. Sasa, tuzungumuzie basi jambo ingine yenye muchungaji mwema anatuambia tuache kufanya.

“MUACHE KUHUKUMU”

Kama hatukaze akili yetu juu ya namna watu wanaonekana kwa inje, ile inaweza kutusaidia tuache kuwahukumu (Ona fungu ya 11, 14-16) *

11. Kulingana na Matayo 7:1, 2, Yesu alituambia tuache kufanya nini, na juu ya nini haiko mwepesi kufanya vile?

11 Soma Matayo 7:1, 2. Yesu alijua kama wanadamu hawakamilike na mara mingi wanakuwaka na muelekeo wa kukazia akili makosa ya wengine. Njo maana alisema hivi: “Muache kuhukumu.” Tunaweza kujikaza juu tusihukumu waamini wenzetu. Lakini kila mara haiko mwepesi kufanya vile juu hatukamilike. Tukiona kama wakati fulani tunakuwa na muelekeo wa kuhukumu wengine, tunapaswa kufanya nini? Tunapaswa kumusikiliza Yesu na kufanya yote yenye tunaweza ili kuacha kuhukumu wengine.

12-13. Namna gani kufikiri sana juu ya namna Yehova alitendea Mufalme Daudi kunaweza kutusaidia tuache kuhukumu wengine?

12 Tunaweza kupata faida wakati tunafikiri sana juu ya mufano wa Yehova. Anakazia uangalifu mambo ya muzuri yenye tunafanya. Tunaona ile mu namna alitendea Mufalme Daudi, mwanaume mwenye alifanya zambi nzito. Kwa mufano, alifanya uzinifu pamoja na Bath-sheba na alifikia hata kuuwisha bwana yake. (2 Sa. 11:2-4, 14, 15, 24) Juu ya mambo yenye Daudi alifanya, yeye na familia yake waliteseka, kutia ndani bibi zake wengine. (2 Sa. 12:10, 11) Wakati ingine, Daudi alishindwa kabisa kuonyesha kama anamutumainia Yehova wakati aliamuru wahesabie wanaume wenye walikuwa mu jeshi ya Israeli, jambo yenye Yehova hakumuambia afanye. Pengine ni kiburi na kutumainia kama alikuwa na jeshi kubwa njo ilimuchochea afanye vile. Ile ilikuwa na matokeo gani? Waisraeli 70 000 hivi walikufa na ugonjwa wa kuambukiza!​—2 Sa. 24:1-4, 10-15.

13 Kama uliishi ile wakati mu Israeli, namna gani ungeona Daudi? Je, ungemuhukumu na kusema kama hastahili rehema ya Yehova? Yehova hakumuona vile. Yehova alikaza akili juu ya uaminifu wenye Daudi alionyesha mu maisha yake, lakini pia, namna alitubu kikweli. Ile ilifanya Yehova amusamehe Daudi juu ya zambi nzito zenye alifanya. Yehova alijua kama Daudi alimupenda sana na alipenda kufanya mambo yenye ilikuwa sawa. Tuko wenye shukrani sana kuona vile Yehova anakaza akili juu ya sifa zetu za muzuri na mwenendo wetu.​—1 Fa. 9:4; 1 Ny. 29:10, 17.

14. Ni mambo gani inaweza kusaidia Wakristo kuacha kuhukumu wengine?

14 Yehova hatazamie tutende kwa ukamilifu, na siye pia hatupaswe kutazamia wengine watende kwa ukamilifu, lakini tunapaswa njo kuona mambo ya muzuri yenye kuwa ndani yao. Mara mingi ni mwepesi sana kuona uzaifu wa wengine na kuwahukumu. Mutu wa kiroho anaweza kuona uzaifu wa wengine, lakini ile haiwezi kumuzuia kutumika nao muzuri. Alimasi ao diamant yenye ingali tu vilevile, ni kusema yenye haiyabadilishwa, inawezekana isivutie sana, lakini mutu mwenye kuwa na hekima anajua kama itakuwa ya muzuri sana na yenye samani wakati itabadilishwa na kutengenezwa. Sawa vile Yehova na Yesu, hatupaswe tu kukazia akili vile watu wanaonekana kwa inje, lakini tunapaswa kuona sifa zao za muzuri.

15. Namna gani kufikiria hali ya watu wengine kunaweza kutusaidia tusiwahukumu haraka-haraka?

15 Zaidi ya kukaza akili yetu juu ya sifa za muzuri za wengine, ni nini ingine inaweza kutusaidia tusikuwe tunawahukumu haraka-haraka? Ni kujaribu kufikiria maisha yao. Tufikirie mufano wenye kufuata. Siku moja, wakati alikuwa mu hekalu, Yesu aliona mujane mwenye alitia feza mbili za kichele zenye samani kidogo sana mu sanduku ya hazina. Yesu hakujiuliza: “Juu ya nini hakutia zaidi?” Kuliko kukaza akili yake juu ya kiasi ya feza yenye ule mujane alitoa, Yesu alikaza akili yake juu ya nia na hali za ule mujane, na alimusifu juu ya yote yenye alifanya.​—Lu. 21:1-4.

16. Mufano wa dada Veronica unaweza kukufundisha nini?

16 Kuhusu ulazima wa kufikiria kwa uzito hali za wengine, muache tuzungumuzie mufano wa dada Veronica. Mu kutaniko yenye alikuwa, kulikuwa mama moja mwenye alikuwa anakomalisha mutoto yake yeye peke. Veronica anasema hivi: “Niliona sawa vile hawakukuwa wanakusanyika kikawaida wala kuhubiri kikawaida. Ile ilifanya nikuwe na mawazo ya mubaya juu yao. Lakini siku moja, nilihubiri na ule mama. Alinifasiria magumu yenye alikuwa nayo, mutoto yake mwanaume alikuwa na ugonjwa fulani wa akili. Kwa hiyo, ule mama alikuwa nafanya yake yote juu ya kumutimizia mutoto yake mahitaji ya kimwili na ya kiroho. Wakati fulani, alikuwa anakusanyika mu kutaniko ingine kwa sababu ya hali ya afya ya mutoto yake.” Veronica anasema tena hivi: “Sikuwazia kama ule mama alikuwa na jaribu ya vile. Sasa namupenda sana na kumuheshimia sana juu ya yote yenye iko najikaza kufanya ili kumutumikia Yehova.”

17. Yakobo 2:8 inatuomba tufanye nini, na namna gani tunaweza kufanya vile?

17 Tunapaswa kufanya nini ikiwa tunaona kama tulimuhukumu Shahidi mwenzetu? Tunapaswa kukumbuka kama tunapaswa kupenda ndugu zetu. (Soma Yakobo 2:8.) Tunapaswa pia kusali sana kwa Yehova ili kumuomba atusaidie tuache kuhukumu wengine. Ni muzuri tuishi kulingana na sala zetu kwa kukamata wakati wa kuzungumuza na ule ndugu ao dada, mwenye tulihukumu. Ile inaweza kutusaidia tumujue muzuri zaidi. Tunaweza kumuomba ahubiri na siye ao atumie chakula pamoja na siye. Kadiri tunajikaza kumujua muzuri ndugu ao dada yetu, ni vile itaonyesha kama tuko naiga mufano wa Yehova na wa Yesu kwa kutafuta sifa za muzuri zenye kuwa mwa ule ndugu ao dada yetu. Mu ile njia, tutaonyesha kama tuko tunasikiliza amri ya muchungaji wetu mwema, yenye kutuomba kuacha kuhukumu wengine.

18. Ni nini itaonyesha kama tuko tunatii sauti ya muchungaji wetu mwema?

18 Sawa vile tu kondoo wa kawaida anasikilizaka sauti ya muchungaji wake, wafuasi wa Yesu pia wanasikilizaka sauti yake. Kama tunafanya yetu yote ili kuacha kuhangaika juu ya mahitaji yetu ya kimwili na pia kuacha kuhukumu wengine, Yehova na Yesu watabariki bidii yetu. Ikuwe tuko wa “kundi ndogo” ao wa “kondoo wengine,” tuendelee kusikiliza na kutii sauti ya muchungaji wetu mwema. (Lu. 12:32; Yoh. 10:11, 14, 16) Mu habari ya kufuata, tutazungumuzia mambo mbili yenye Yesu aliambia wafuasi wake wafanye.

WIMBO 101 Tutumike kwa Umoja

^ Wakati Yesu alisema kama kondoo wake wangesikiliza sauti yake, alipenda kusema kama wanafunzi wake wangesikiliza mafundisho yake na kuitumikisha mu maisha yao. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo mbili yenye Yesu alifundisha, ni kusema, kuacha kuhangaika sana juu ya vitu vya kimwili na kuacha kuhukumu wengine. Tutazungumuzia namna tunaweza kutumikisha ile shauri.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu moja alipoteza kazi yake, hana makuta tena ili kutimiza mahitaji ya familia yake na iko na lazima ya kupata nyumba ingine. Kama haiko muangalifu, anaweza kukengeushwa na magumu yake, na ile inaweza kufanya asahau kutia ibada ya Yehova pa nafasi ya kwanza mu maisha yake.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu moja anafika nyuma ku mukutano. Lakini anaonyesha sifa za muzuri saa yenye iko mu mahubiri ya wakati wowote, iko anasaidia mutu moja mwenye ni muzee-muzee na iko anasaidia mu kazi ya kusafisha Jumba ya Ufalme.