Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unakumbuka?

Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu magazeti ya Munara wa Mulinzi ya hii mwaka? Kama ni vile jaribu kujibu hii maulizo:

Wakati Yakobo 5:11 inasema kama Yehova ni “mwenye upendo mwingi sana” na “mwenye rehema” ile inatupatia uhakikisho gani?

Tunajua kama Yehova iko tayari kusamehe makosa yetu juu ni mwenye rehema. Yakobo 5:11 inatuhakikishia kama iko tayari kufanya vile kwa upendo. Ni jambo ya muzuri na siye pia tumuige.​—w21.01, uku. 21.

Juu ya nini Yehova alianzisha mupango wa ukichwa?

Juu iko na upendo. Ukichwa unasaidia mu familia ya Yehova mukuwe amani na utaratibu. Kila mutu mu familia mwenye anaheshimia ile mupango anajua nani njo anapaswa kukamata maamuzi ya mwisho na anajua pia nani njo anapaswa kuhakikisha kama ile maamuzi inatimizwa.​—w21.02, uku. 3.

Juu ya nini Wakristo wanapaswa kuwa waangalifu wakati wanatumikisha programu za kielektroniki za kutumiana ujumbe?

Kama mutu anaamua kutumikisha programu za kielektroniki za kutumiana ujumbe, ni muzuri akuwe muangalifu wakati anapenda kuchagua marafiki wazuri. Ni nguvu sana kufanya vile mu kikundi kikubwa cha watu wenye kutumikisha programu fulani ya kutumiana ujumbe. (1 Ti. 5:13) Kuko pia hatari ya kutangaza habari yenye haiko hakika na pia kutumikisha ndugu zetu mubaya juu ya kupata feza.​—w21.03, uku. 31.

Ni sababu gani fulani zenye zilifanya Mungu aruhusu Yesu ateseke na kufa?

Kwanza, juu Yesu alitundikwa ku muti wa mateso ile ingewezesha Wayahudi wawekwe huru kutoka katika laana. (Gal. 3:10, 13) Pili, Yehova alikuwa anamutayarisha Yesu kwa ajili ya daraka yenye angepata kisha, ni kusema, kuwa Kuhani Mukubwa. Na tatu, juu Yesu alibakia muaminifu mupaka kifo ile ilionyesha kama wanadamu wanaweza kubakia waaminifu kwa Yehova hata wakati wanajaribiwa sana. (Yob. 1:9-11)​—w21.04, uku. 16-17.

Tunaweza kufanya nini kama ni nguvu kupata watu mu mahubiri?

Tunaweza kujaribu kuwatafuta kwa kuhubiri saa yenye wanaweza kuwa kwao. Tunaweza pia kujaribu kuhubiria watu fasi ingine. Na tunaweza kujaribu njia ingine, kama vile kuandika barua.​—w21.05, uku. 15-16.

Mutume Paulo alimaanisha nini wakati alisema: “Kupitia sheria nilikufa kuelekea sheria”? (Gal. 2:19)

Sheria ya Musa ilionyesha wazi kutokamilika ya wanadamu na iliongoza Waisraeli kwa Kristo. (Gal. 3:19, 24) Ile njo ilifanya Paulo amukubali Kristo. Kwa kufanya vile, Paulo “alikufa kuelekea sheria.” Ile Sheria haikukuwa tena na uwezo juu yake.​—w21.06, uku. 31.

Ni mufano gani wa uvumilivu Yehova ametuachia?

Yehova amevumilia kuchafuliwa kwa jina yake, kupingwa kwa mamlaka yake makubwa, uasi wa watoto wake fulani, mambo ya uongo yenye Shetani anaendelea kusema juu yake, kifo ya marafiki wake, kuona watu wabaya wako wanatesa wengine, na kuharibiwa kwa dunia.​—w21.07, uku. 9-12.

Ni mufano gani muzuri wa uvumilivu Yosefu alituachia?

Alivumilia wakati alitendewa mubaya na ndugu zake. Ile ilifanya ashitakiwe kwa uongo na kufungwa mu gereza kule Misri kwa miaka mingi.​—w21.08, uku. 12.

Hagai 2:6-9, 20-22 ilitabiri kutikiswa gani ya mufano?

Mataifa haikubali ujumbe wa Ufalme wenye tunaihubiria, lakini watu wengi wamevutwa kwenye kweli. Hivi karibuni mataifa itatikiswa wakati itaharibiwa.​—w21.09, uku. 15-19.

Juu ya nini hatupaswe kuacha hata kidogo kazi yetu ya kuhubiri?

Yehova anaona bidii yetu na anapendezwa nayo. Kama hatuchoke wala kuacha tutapa uzima wa milele.​—w21.10, uku. 25-26.

Namna gani Mambo ya Walawi sura ya 19 inaweza kutusaidia kutumikisha hii shauri: “Mukuwe watakatifu katika mwenendo wenu wote”? (1 Pe. 1:15)

Inawezekana maneno ya ile andiko inatoka mu Mambo ya Walawi 19:2. Sura ya 19 inatutolea mifano mingi juu ya namna tunaweza kutumikisha 1 Petro 1:15 mu maisha yetu ya kila siku.​—w21.12, uku. 3-4.