Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 6

Endelea Kuwa Muaminifu-Mushikamanifu!

Endelea Kuwa Muaminifu-Mushikamanifu!

“Mupaka wakati nitakufa, sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!”​—YOB. 27:5.

WIMBO 34 Kutembea kwa Utimilifu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Namna gani Mashahidi tatu wenye kuzungumuziwa katika fungu hili wanabakia waaminifu-washikamanifu kwa Yehova?

WAZIA Mashahidi tatu wa Yehova wenye wanajikuta mu hali hizi. (1) Siku moja, wakati kijana mumoja mwanamuke iko ku masomo, mwalimu anaomba wanafunzi wote katika somo wafanye sikukuu fulani. Kijana huyo mwanamuke anajua kama sikukuu hiyo haimupendeze Mungu, kwa hiyo anakataa kwa heshima kujiunga nao. (2) Kijana mwanaume mwenye haya anahubiri nyumba kwa nyumba. Anatambua kama mwanafunzi mumoja wa ku masomo yao anaishi katika nyumba yenye kufuata. Mwanafunzi huyo alikuwa amechekelea Mashahidi wa Yehova wakati wenye ulipita. Lakini kijana huyo mwanaume anaenda kwenye ile nyumba na anapiga hodi bila kuogopa. (3) Mwanaume mumoja anatumika sana ili kutimizia watu wa familia yake mahitaji yao, na siku moja mukubwa wake wa kazi anamuomba afanye jambo fulani la udanganyifu ao lenye kuvunja sheria. Hata kama mwanaume huyo anaweza kupoteza kazi yake, anafasiria kama anapaswa kuwa munyoofu ao muaminifu na kutii sheria kwa sababu Mungu anaomba watumishi wake wafanye vile.​—Ro. 13:1-4; Ebr. 13:18.

2. Tutazungumuzia maulizo gani, na juu ya nini?

2 Unaona kuwa watu hao tatu wanaonyesha sifa gani? Unaweza kuona sifa fulani, kama vile uhodari na unyoofu. Lakini wote wanaonyesha sifa ingine ya maana sana, ni kusema, sifa ya uaminifu-mushikamanifu. Kila mumoja wao anaonyesha ushikamanifu kwa Yehova. Kila mumoja wao anakataa kuvunja kanuni za Mungu. Sifa ya uaminifu-mushikamanifu njo yenye inawachochea watende vile. Kwa kweli, Yehova anajivunia kabisa kila mumoja wao kwa sababu anaonyesha ile sifa. Na sisi tunapenda kumufanya Baba yetu wa mbinguni ajivunie uaminifu-mushikamanifu wetu. Tuzungumuzie basi maulizo hii: Uaminifu-mushikamanifu, maana yake nini? Juu ya nini ni jambo la lazima tukuwe waaminifu-washikamanifu? Na tunaweza kufanya nini ili tuazimie zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu katika wakati huu wa magumu?

UAMINIFU-MUSHIKAMANIFU, MAANA YAKE NINI?

3. (a) Uaminifu-mushikamanifu wetu maana yake nini? (b) Ni mifano gani yenye inaweza kutusaidia kuelewa maana ya uaminifu-mushikamanifu?

3 Wakati neno uaminifu-mushikamanifu linatumiwa juu yetu sisi watumishi wa Mungu, linamaanisha kumupenda Yehova kwa moyo wote na kujitoa kwake kwa moyo wote, na hilo linatuchochea kutia mapenzi yake pa nafasi ya kwanza katika maamuzi yetu yote. Tuchunguze habari fulani juu ya namna neno uaminifu-mushikamanifu linatumiwa mu Biblia. Maana ya kwanza ya neno la Biblia lenye kutafsiriwa “uaminifu-mushikamanifu,” ni kuwa kamili, bila kasoro, ao muzima. Kwa mufano, Waisraeli walikuwa wanamutolea Yehova zabihu za wanyama, na Sheria ilisema kama wanyama hao walipaswa kuwa bila kasoro. * (Law. 22:21, 22) Watu wa Mungu hawakuruhusiwa kutoa munyama mwenye alikuwa anakosa muguu, sikio, ao jicho; na hawangepaswa kutoa munyama mwenye kuwa mugonjwa. Yehova aliona kama ni jambo la maana munyama wa zabihu akuwe kamili, bila kasoro, ao muzima. (Mal. 1:6-9) Tunaweza kuelewa juu ya nini Yehova anapendezwa na kitu chenye hakina kasoro ao chenye kuwa kamili. Kwa mufano, wakati tunauza kitu fulani kama vile tunda, kitabu, ao kifaa fulani, hatupendi kile chenye kuwa na matundu ao chenye kukosa sehemu fulani. Tunapenda kitu chenye kuwa kamili, chenye hakina kasoro, ao chenye kuwa kizima. Yehova naye anataka upendo na ushikamanifu wenye tunamuonyesha ukuwe vile; unapaswa kuwa kamili, bila kasoro, ao muzima.

4. (a) Juu ya nini mutu mwenye hakamilike anaweza kuwa muaminifu-mushikamanifu? (b) Kulingana na Zaburi 103:12-14, Yehova hatuombe nini?

4 Je, tunapaswa kuwaza kama ni lazima tukuwe wakamilifu ili tukuwe waaminifu-washikamanifu? Kwa kweli, tunaweza kuona kama tunafanyaka makosa mingi. Fikiria sababu mbili zenye zinaweza kutufanya tusiwaze kama tunapaswa kuwa wakamilifu ili tukuwe waaminifu-washikamanifu. Kwanza, Yehova hakazie akili makosa yetu. Neno lake linatuambia hivi: “Kama ungekuwa unaangalia makosa, Ee Yah, basi ni nani, Ee Yehova, angeweza kusimama?” (Zb. 130:3) Anajua kama hatuko wakamilifu, tuko wanadamu watenda-zambi, na iko tayari kutusamehe. (Zb. 86:5) Pili, Yehova anajua mipaka yetu, na hatuombe tufanye mambo yenye kupita uwezo wetu. (Soma Zaburi 103:12-14.) Kwa hiyo, ni katika maana gani tunaweza kuwa kamili, bila kasoro, ao wazima mu macho yake?

5. Namna gani upendo unasaidia watumishi wa Yehova wakuwe waaminifu-washikamanifu?

5 Upendo unasaidia watumishi wa Yehova wakuwe waaminifu-washikamanifu. Upendo wetu na ushikamanifu wetu kwa Mungu, Baba yetu wa mbinguni, unapaswa kuendelea kuwa kamili, bila kasoro, ao muzima. Kama upendo wetu unabakia vile hata wakati tunajaribiwa, hilo linaonyesha kama tuko waaminifu-washikamanifu. (1 Ny. 28:9; Mt. 22:37) Tufikirie tena wale Mashahidi tatu wenye tulizungumuzia ku mwanzo wa habari hii. Juu ya nini walitenda vile? Je, ule kijana mwanamuke hapendake kujifurahisha ku masomo? Ao ule kijana mwanaume anapenda kupatishwa haya ku mulango? Ao ule mwanaume mwenye kuwa na familia anapenda kupoteza kazi yake? Hapana. Lakini, wanajua kama kanuni za Yehova ni za haki, na wanakaza akili yao juu ya mambo yenye kumufurahisha Baba yao wa mbinguni. Upendo wao kwake unawachochea kumutia pa nafasi ya kwanza katika maamuzi yenye wanakamata. Kwa kufanya vile, wanaonyesha kama wako waaminifu-washikamanifu.

JUU YA NINI NI JAMBO LA LAZIMA TUKUWE WAAMINIFU-WASHIKAMANIFU?

6. (a) Juu ya nini ni jambo la lazima ukuwe muaminifu-mushikamanifu? (b) Namna gani Adamu na Eva walishindwa kuonyesha uaminifu-mushikamanifu?

6 Juu ya nini ni jambo la lazima kila mumoja wetu akuwe muaminifu-mushikamanifu? Ni jambo la lazima ukuwe muaminifu-mushikamanifu kwa sababu Shetani amemushitaki Yehova, na amekushitaki wewe pia. Malaika huyo mwenye alimupinga Mungu alijifanya mwenyewe kuwa Shetani, ao “Mupinzani,” kuanzia mu bustani ya Edeni. Alimuharibishia Yehova sifa kwa kusema kama Yehova ni Mutawala mubaya, mwenye kujipenda mwenyewe, na mudanganyifu. Jambo la kuhuzunisha ni hili: Adamu na Eva walimuunga Shetani mukono ili kumupinga Yehova. (Mwa. 3:1-6) Maisha katika Edeni iliwatolea nafasi mingi sana za kutia nguvu upendo wao kwa Yehova. Lakini, wakati Shetani alitokeza ile mashitaka, upendo wao haukukuwa kamili, bila kasoro, ao muzima. Kisha wakati fulani, ulizo hili lilipaswa kujibiwa: Mwanadamu yeyote angeweza kubakia mushikamanifu kwa Yehova Mungu kwa sababu ya kumupenda? Katika maneno ingine, wanadamu wako na uwezo wa kuonyesha uaminifu-mushikamanifu? Ulizo hilo lilitokezwa juu ya Yobu.

7. Kulingana na Yobu 1:8-11, namna gani Yehova aliona uaminifu-mushikamanifu wa Yobu? Namna gani Shetani aliona uaminifu-mushikamanifu wa Yobu?

7 Yobu aliishi wakati Waisraeli walikuwa wanaishi mu inchi ya Misri. Wakati huo, hakuna mutu mwingine mwenye alikuwa muaminifu-mushikamanifu kama yeye. Kama vile sisi, hakukuwa mukamilifu. Alifanya makosa. Lakini, Yehova alimupenda Yobu kwa sababu ya uaminifu-mushikamanifu wake. Inaonekana kabisa kuwa, tayari Shetani alikuwa amemuchokoza Yehova juu ya uaminifu-mushikamanifu wa wanadamu. Kwa hiyo, Yehova alimuonyesha Shetani kama Yobu alikuwa muaminifu-mushikamanifu. Maisha ya Yobu ilionyesha waziwazi kama Shetani ni musema-uongo! Shetani alimuomba Yehova amuruhusu ajaribu uaminifu-mushikamanifu wa Yobu. Yehova alikuwa anamutumainia rafiki yake Yobu, kwa hiyo, aliruhusu Shetani amujaribu.​—Soma Yobu 1:8-11.

8. Shetani alifanya nini ili kumushambulia Yobu?

8 Shetani hana huruma, na iko muuaji. Alishambulia vitu vya Yobu, kwa kufanya Yobu apoteze kila kitu chenye alikuwa nacho, kwa kuua watumishi wake, na kumuharibishia sifa katika eneo. Alishambulia familia ya Yobu, kwa kuua watoto wake kumi wapendwa. Kisha alishambulia mwili wa Yobu, kwa kumuletea ugonjwa mubaya wa majipu yenye maumivu kuanzia ku kichwa mupaka ku miguu. Bibi ya Yobu alivurugika na alikuwa na huzuni sana; kwa hiyo alimuambia Yobu avunje uaminifu-mushikamanifu wake, amulaani Mungu na akufe. Yobu mwenyewe alipenda akufe, lakini alibakia muaminifu-mushikamanifu. Kisha, Shetani alitumia njia ingine ili kumushambulia. Alitumia wanaume tatu wenye walikuwa marafiki wa Yobu. Wanaume hao walimutembelea Yobu na walifanya siku mingi kwake, lakini hawakumufariji hata kidogo. Kuliko kumufariji, walimuambia maneno mingi yenye haina huruma na kumuchambua kwa ukali. Walisema kama ni Mungu njo alikuwa anamuletea Yobu mateso hayo na kama hakukuwa anahangaikia uaminifu-mushikamanifu wake. Na hata walisema kama Yobu alikuwa mutu mubaya mwenye alistahili kupatwa na ile mambo ya mubaya yenye ilikuwa inamupata!​—Yob. 1:13-22; 2:7-11; 15:4, 5; 22:3-6; 25:4-6.

9. Hata kama Yobu alipambana na majaribu, alikataa kufanya nini?

9 Yobu alitenda namna gani juu ya taabu hizo zote zenye zilimupata? Hakukuwa mukamilifu. Alikaripia kwa ukali wafariji wake wenye hawakukuwa wafariji wa kweli, na alisema maneno yenye alifikia kukubali kwamba ilikuwa mazungumuzo ya ovyoovyo. Alitetea zaidi haki yake mwenyewe kuliko vile alitetea haki ya Mungu. (Yob. 6:3; 13:4, 5; 32:2; 34:5) Lakini, hata wakati hali yake ilikuwa mubaya sana, alikataa kumuacha Yehova Mungu. Alikataa kuamini uongo wa marafiki hao wenye hawakukuwa marafiki wa kweli. Alisema hivi: “Ni jambo lenye siwezi kuwazia kuwatangaza ninyi kuwa wenye haki! Mupaka wakati nitakufa, sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!” (Yob. 27:5) Ile maneno ni ya maana sana. Yobu alikataa kuacha uaminifu-mushikamanifu wake; na sisi tunaweza kumuiga.

10. Mambo yenye Shetani alimushitaki Yobu, inakuhusu namna gani?

10 Shetani anashitaki kila mumoja wetu mambo ileile yenye alimushitaki Yobu. Ile mashitaka inakuhusu namna gani? Kwa kweli, anasema kama haumupendi kabisa Yehova Mungu, kama utaacha kumutumikia ili kuokoa uzima wako, na kama uaminifu-mushikamanifu wako ni wa uongo! (Yob. 2:4, 5; Ufu. 12:10) Ile maneno inakufanya ujisikie namna gani? Inakuumiza, haiko vile? Lakini, fikiria jambo hili: Yehova anakutumainia kabisa, njo maana amekupatia nafasi ya muzuri sana. Yehova anamuruhusu Shetani ajaribu uaminifu-mushikamanifu wako. Yehova iko hakika kama unaweza kuendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu na kusaidia kuonyesha kama Shetani ni musema-uongo. Na anaahidi kama atakusaidia kufanya vile. (Ebr. 13:6) Ni pendeleo kubwa sana kutumainiwa na Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi katika ulimwengu wote! Unaona ni juu ya nini uaminifu-mushikamanifu ni wa maana sana? Unatusaidia kupinga uongo wa Shetani na kutetea jina la muzuri la Baba yetu na kuunga mukono namna yake ya kutawala. Tunaweza kufanya nini ili tuendelee kuonyesha ile sifa ya maana sana?

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI TUENDELEE KUWA WAAMINIFU-WASHIKAMANIFU LEO?

11. Mufano wa Yobu unaweza kutufundisha nini?

11 Shetani ameongeza sana mashambulizi yake katika “siku [hizi] za mwisho” zenye magumu. (2 Ti. 3:1) Katika siku hizi za mubaya, tunaweza kufanya nini ili tuazimie zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu? Tena, mufano wa Yobu unaweza kutufundisha mambo mingi. Muda murefu mbele majaribu yake ianze, Yobu alikuwa ameonyesha uaminifu-mushikamanifu mara mingi. Fikiria mambo tatu yenye mufano wake unaweza kutufundisha juu ya kuazimia zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu.

Ni mambo gani fulani yenye inaweza kutusaidia tuazimie zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu? (Picha hii inapatana na fungu la 12) *

12. (a) Kulingana na Yobu 26:7, 8, 14, Yobu alifanya nini ili amuogope Yehova na kumuheshimia? (b) Tunaweza kufanya nini ili tumuogope Mungu sana?

12 Yobu alitia nguvu upendo wake kwa Mungu kwa kujifunza kumuogopa. Yobu alitumia wakati ili kuangalia vitu vya ajabu vyenye Yehova aliumba. (Soma Yobu 26:7, 8, 14.) Alishangaa sana wakati alifikiri sana juu ya dunia, anga, mawingu, na mungurumo wa radi. Lakini alielewa kama hakukuwa anajua mambo mingi juu ya vitu vyote vyenye Yehova aliumba. Pia, aliona maneno ya Yehova kuwa ya maana. Alisema hivi juu ya maneno ya Yehova: “Nimeweka maneno yake kama hazina.” (Yob. 23:12) Yobu alimuogopa Yehova na kumuheshimia sana. Alimupenda Yehova, Baba yake, na alitaka kumupendeza. Hilo lilifanya aazimie zaidi kuendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu. Sisi pia tunapaswa kufanya kama vile Yobu. Kuliko watu wenye waliishi wakati wa Yobu, tunajua mambo mingi juu ya vitu vya ajabu vyenye Mungu aliumba. Na tuko na Biblia nzima yenye iliongozwa na roho ya Mungu ili kutusaidia kumujua muzuri kabisa. Mambo yote yenye tunajifunza inaweza kutusaidia tumuogope Yehova sana. Wakati tunamuogopa Yehova na kumuheshimia, hilo litatuchochea tumupende na kumutii na tuazimie sana kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu kwake.​—Yob. 28:28.

Tunaazimia zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu wakati tunaepuka kuangalia pornografia (Picha hii inapatana na fungu la 13) *

13-14. (a) Kama vile andiko la Yobu 31:1 linaonyesha, Yobu alifanya nini ili kuonyesha kama alimutii Mungu? (b) Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Yobu?

13 Utii wa Yobu mu mambo yote ulimusaidia aendelee kuwa muaminifu-mushikamanifu. Yobu alijua kama ili akuwe muaminifu-mushikamanifu, alipaswa kumutii Yehova. Kwa kweli, kila wakati tunamutii Yehova, hilo litatufanya tuazimie zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu kwake. Yobu alijikaza sana kumutii Mungu mu maisha yake kila siku. Kwa mufano, alikuwa muangalifu juu ya namna alikuwa anajiendesha mbele ya wanamuke. (Soma Yobu 31:1.) Kwa sababu alikuwa mwanaume mwenye kuoa, alijua kama ilikuwa mubaya kumuonyesha mapenzi mwanamuke yeyote mwenye hakukuwa bibi yake. Leo, tunaishi katika ulimwengu wenye kujaa mambo mingi yenye kutushawishi kufanya ngono. Kama vile Yobu, je, tutaepuka kabisa kukazia uangalifu kwa njia yenye haifae mutu yeyote mwenye haiko bibi ao bwana yetu? Pia, tutakataa kuangalia picha chafu ao za pornografia, hata zipatikane wapi? (Mt. 5:28) Kama tunajikaza kujizuia vile kila siku, tutaazimia zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu.

Tunaazimia zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu wakati tuko na mawazo yenye kufaa juu ya vitu vya kimwili (Picha hii inapatana na fungu la 14) *

14 Pia, namna Yobu aliona vitu vya kimwili inaonyesha kama alimutii Yehova. Alielewa kwamba, kama angetia tumaini lake katika mali yake, kufanya vile ingekuwa zambi nzito yenye ingestahili azabu ao malipizi. (Yob. 31:24, 25, 28) Mu ulimwengu wenye tunaishi ndani leo, watu wanapenda sana vitu vya kimwili. Kama tunakuwa na mawazo yenye kufaa juu ya feza na vitu vya kimwili, kama vile Biblia inatushauria, tutaazimia zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu.​—Mez. 30:8, 9; Mt. 6:19-21.

Tunaazimia zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu wakati tunaendelea kukaza akili yetu juu ya tumaini letu (Picha hii inapatana na fungu la 15) *

15. (a) Ni tumaini gani lenye lilimusaidia Yobu aendelee kuwa muaminifu-mushikamanifu? (b) Juu ya nini kuendelea kukumbuka tumaini lenye Yehova anatutolea kunaweza kutusaidia?

15 Yobu aliendelea kutumainia kuwa Mungu angemubariki, hilo lilimusaidia aendelee kuwa muaminifu-mushikamanifu. Alijua kama Mungu alikuwa anahangaikia uaminifu-mushikamanifu wake. (Yob. 31:6) Hata kama Yobu alipata majaribu, alikuwa hakika kama mwishowe, Yehova angemubariki. Kwa kweli, kuwa hakika na jambo hilo kulimusaidia aendelee kuwa muaminifu-mushikamanifu. Yehova alifurahia sana uaminifu-mushikamanifu wa Yobu; kwa hiyo, alimubariki sana wakati alikuwa angali mutu mwenye hakamilike! (Yob. 42:12-17; Yak. 5:11) Na wakati wenye kuja atapata baraka kubwa. Uko na tumaini kabisa kama Yehova atabariki uaminifu-mushikamanifu wako? Mungu wetu hajabadilika. (Mal. 3:6) Ikiwa tunakumbuka kama anapendezwa na uaminifu-mushikamanifu wetu, tunaweza kuendelea kutumainia katika moyo wetu wakati muzuri sana wenye kuja.​—1 Te. 5:8, 9.

16. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

16 Kwa hiyo, uazimie kuendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu! Wakati fulani, unaweza kujisikia kama hakuna mutu mwingine mwenye kuwa pembeni yako mwenye kuwa muaminifu-mushikamanifu, lakini hautakuwa peke yako hata siku moja. Utakuwa kati ya mamilioni ya watu wenye wanaendelea kuwa waaminifu-washikamanifu mu dunia yote. Utakuwa pia kati ya wanaume na wanamuke wenye imani wenye waliendelea kuwa waaminifu-washikamanifu wakati wa zamani, hata wakati walipambana na hatari ya kifo. (Ebr. 11:36-38; 12:1) Basi, sisi wote tuazimie kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu kama vile Yobu alifanya. Alisema hivi: “Sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!” Basi, uaminifu-mushikamanifu wetu umuletee Yehova utukufu milele!

WIMBO 124 Washikamanifu Sikuzote

^ fu. 5 Uaminifu-mushikamanifu, maana yake nini? Juu ya nini Yehova anapenda watumishi wake wakuwe na ile sifa? Juu ya nini ni jambo la maana kila mumoja wetu akuwe na sifa ya uaminifu-mushikamanifu? Habari hii itatusaidia kupata majibu ya Biblia juu ya ile maulizo. Pia, itatusaidia kujua muzuri namna tunaweza kuazimia zaidi kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu kila siku. Kufanya vile kutatuletea baraka kubwa.

^ fu. 3 Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “bila kasoro” kuhusu wanyama, liko na upatano na neno lenye kutafsiriwa “uaminifu-mushikamanifu” lenye kutumiwa kuhusu wanadamu.

^ fu. 50 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati Yobu alikuwa angali baba kijana, anafundisha watoto wake fulani juu ya vitu vya ajabu vyenye Yehova aliumba.

^ fu. 52 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu anakataa kujiunga na wafanyakazi wenzake ili kuangalia pornografia.

^ fu. 54 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu anashinda mukazo wa kuuza televizyo kubwa na ya bei sana yenye hana nayo lazima na yenye kupita uwezo wake

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu anatumia wakati ili kufikiri sana juu ya tumaini la Paradiso.