Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 6

“Kichwa cha Mwanamuke Ni Mwanaume”

“Kichwa cha Mwanamuke Ni Mwanaume”

“Kichwa cha mwanamuke ni mwanaume.”​—1 KO. 11:3.

WIMBO 13 Kristo, Kielelezo Chetu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Wakati dada iko anafikiria mutu wa kuolewa naye, anapaswa kujiuliza maulizo gani fulani?

WAKRISTO wote wako chini ya ukichwa wa Kristo, kiongozi mukamilifu. Lakini, wakati mwanamuke Mukristo anaolewa, anakuwa chini ya ukichwa wa mwanaume mwenye hakamilike. Ile inaweza kuleta matatizo. Kwa hiyo, wakati dada iko anafikiria mutu wa kuolewa naye, ni muzuri ajiulize hivi: ‘Nini njo inaonyesha kama huyu ndugu atakuwa kichwa muzuri wa familia? Anatiaka mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza mu maisha yake? Kama hapana, nini njo inafanya niwaze kama atakuwa kichwa muzuri mwenye atajikaza ili tuendelee kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova kisha ndoa yetu?’ Lakini, dada anapaswa pia kujiuliza hivi: ‘Niko na sifa gani zenye zitasaidia ndoa yetu? Niko muvumilivu na mukarimu? Niko na urafiki wa sana pamoja na Yehova?’ (Muh. 4:9, 12) Maamuzi yenye dada anakamata mbele ya kuolewa inaweza kumusaidia akuwe na furaha mu ndoa yake.

2. Tutajibia maulizo gani mu hii habari?

2 Mamilioni ya dada zetu Wakristo wanaweka mufano muzuri kwa kujitiisha kwa bwana zao. Kwa hiyo, wanastahili kupongezwa! Tunafurahia sana kumutumikia Yehova pamoja na wale wanamuke washikamanifu! Mu hii habari, tutajibia hii maulizo tatu: (1) Bibi wanapambana na matatizo gani fulani? (2) Juu ya nini dada Wakristo wanachagua kujitiisha kwa bwana zao? (3) Bibi na bwana Wakristo wanaweza kujifunza nini kuhusu kujitiisha wakati wanafikiria mufano wa Yesu, Abigaili, na Maria, bibi ya Yosefu na mama ya Yesu?

BIBI WAKRISTO WANAPAMBANA NA MATATIZO GANI?

3. Juu ya nini hakuna ndoa yenye haina matatizo?

3 Ndoa ni zawadi kamilifu kutoka kwa Mungu, lakini watu hawakamilike. (1 Yo. 1:8) Njo maana Biblia inaonya wale wenye kuoana kama watapata matatizo. Biblia inaita ile matatizo “taabu katika mwili.” (1 Ko. 7:28) Tuzungumuzie matatizo fulani yenye bibi wanaweza kupambana nayo.

4. Ni nini inaweza kufanya mwanamuke aone kama kujitiisha kwa bwana yake ni kujizaraulisha?

4 Wakati fulani, namna bibi alikomaa inaweza kufanya aone kama kujitiisha kwa bwana yake ni kujizaraulisha. Dada Marisol, mwenye anaishi mu inchi ya Amerika, anasema hivi: “Kwenye nilikomalia, mara mingi wanamuke walikuwa wanaambiwa kama wanapaswa kuwa sawasawa na wanaume mu kila kitu. Ninajua kama Yehova ameweka mupango wa ukichwa, anapenda wanamuke wajitiishe kwa bwana zao, na pia anapenda wanamuke waheshimiwe. Lakini, haiko mwepesi kuendelea kuwa na mawazo yenye kusawazika juu ya ukichwa.”

5. Watu fulani wako na mawazo gani yenye haipatane na Maandiko kuhusu wanamuke?

5 Lakini, pengine mwanamuke ameolewa na mwanaume mwenye anawaza kama wanamuke ni watu wa hali ya chini. Dada mwenye anaitwa Ivon, mwenye anaishi Amerika ya Kusini anasema hivi: “Mu eneo letu, wanaume njo wanakulaka kwanza, kisha njo wanamuke wanakula. Watoto wanamuke wanapaswa kupika na kufanya usafi. Lakini watoto wanaume wanakaa tu na kungoja mama zao na dada zao wawatumikie, na wanaambiwa kama wao njo ‘wafalme wa nyumba.’” Dada mwenye anaitwa Yingling, mwenye anaishi Asia, anasema hivi: “Mu luga yetu, watu wanazoea kusema kama haiko lazima mwanamuke akuwe na akili ao akuwe na uwezo fulani. Anapaswa tu kufanya kazi za ku nyumba, na hapaswe kuelezea bwana yake mawazo yake.” Bwana mwenye kuwa na ile mawazo yenye haina upendo na yenye haipatane na Maandiko anafanya maisha ya bibi yake ikuwe nguvu, anashindwa kufuata mufano wa Yesu, na hamufurahishe Yehova.​—Efe. 5:28, 29; 1 Pe. 3:7.

6. Bibi wanapaswa kufanya nini ili waendelee kuwa na uhusiano wa kipekee pamoja na Yehova?

6 Kama vile tuliona mu habari yenye kutangulia, Yehova anapenda bwana Wakristo watimizie familia zao mahitaji ya kiroho, wawafanye wajisikie kuwa wanapendwa, na wawatimizie mahitaji yao ya kimwili. (1 Ti. 5:8) Lakini, hata kama dada wenye kuolewa wako na mambo mingi ya kufanya, wanapaswa kutafuta wakati wa kusoma Neno la Mungu kila siku, kufikiri sana, na kusali sana kwa Yehova. Haiko mwepesi kufanya vile. Wanamuke wako na kazi mingi za kufanya, na wanaweza kuwaza kama hawana wakati na nguvu ya kufanya ile mambo ya kiroho. Lakini, ni jambo la maana watafute wakati wa kufanya vile. Juu ya nini? Juu Yehova anapenda kila mumoja wetu aendelee kuwa na uhusiano wa kipekee pamoja naye.​—Mdo. 17:27.

7. Nini njo itafanya ikuwe mwepesi zaidi kwa bibi kujitiisha kwa bwana yake?

7 Kwa kweli, wakati fulani inaweza kuomba bibi ajikaze sana ili ajitiishe kwa bwana yake mwenye hakamilike. Lakini, ikiwa anaelewa na kukubali sababu zenye kuwa mu Biblia zenye zinaonyesha juu ya nini mwanamuke anapaswa kujitiisha kwa bwana yake, itakuwa mwepesi zaidi kwake kujitiisha.

JUU YA NINI WANAMUKE WAKRISTO WANAAMUA KUJITIISHA?

8. Kama vile Waefeso 5:22-24 inaonyesha, juu ya nini bibi Mukristo anaamua kujitiisha kwa bwana yake?

8 Bibi Mukristo anaamua kujitiisha kwa bwana yake kwa sababu ni vile Yehova anapenda. (Soma Waefeso 5:22-24.) Anamutumainia Baba yake wa mbinguni, juu anajua kama mambo yote yenye anatuombaka tufanye inachochewa na upendo. Pia anajua kama Yehova hawezi kumuomba afanye mambo yenye itamuletea magumu.​—Kum. 6:24; 1 Yo. 5:3.

9. Wakati dada Mukristo anaheshimia mamlaka ya bwana yake, ile inaleta matokeo gani?

9 Ulimwengu unachochea wanamuke wasifuate kanuni za Yehova na waone kama kujitiisha ni kujizaraulisha. Kwa kweli, watu wenye kueneza ile mawazo hawamujue Mungu wetu mwenye upendo. Yehova hawezi hata kidogo kupatia watoto wake wanamuke wenye anapenda sheria yenye itawazaraulisha. Dada mwenye anajikaza sana kujitiisha kwa bwana yake, kama vile Yehova anamuomba, anasaidia familia yake ikuwe na amani. (Zb. 119:165) Anajiletea faida, analetea bwana yake faida, na watoto wake pia.

10. Maneno ya Carol inaweza kutufundisha nini?

10 Yehova njo alianzisha mupango wa ukichwa, kwa hiyo bibi mwenye anajitiisha kwa bwana yake mwenye hakamilike anaonyesha kama anamupenda Yehova na kumuheshimia. Carol, mwenye anaishi Amerika ya Kusini, anasema hivi: “Ninajua kama bwana yangu anaweza kufanya makosa. Na ninajua kama namna ninatenda wakati anafanya makosa inaonyesha ikiwa ninaona urafiki wangu pamoja na Yehova kuwa wa maana ao hapana. Kwa hiyo, ninajikaza kuendelea kujitiisha kwa sababu ninapenda kumufurahisha Baba yangu wa mbinguni.”

11. Nini njo inasaidiaka dada mwenye kuitwa Aneese akuwe tayari kusamehe, na maneno yake inaweza kutufundisha nini?

11 Haiko mwepesi kwa bibi kuheshimia bwana yake na kujitiisha kwake ikiwa anaona kama bwana yake hahangaikie namna iko anajisikia, na hahangaikie mambo yenye iko inamusumbua. Lakini, ona namna dada mwenye kuitwa Aneese anafanyaka wakati ile inatokea. Anasema hivi: “Ninajikaza ili nisiendelee kukasirika. Ninakumbuka kama sisi wote tunafanyaka makosa. Nia yangu ni kuwa tayari kusamehe, sawa vile Yehova anafanyaka. Wakati ninasamehe, ninakuwa na amani ya akili.” (Zb. 86:5) Kama bibi iko tayari kusamehe, itakuwa mwepesi kwake kujitiisha.

MIFANO YENYE KUWA KATIKA BIBLIA INAWEZA KUTUFUNDISHA NINI?

12. Mu Biblia muko mifano gani?

12 Watu fulani wanaweza kuona kama kujitiisha ni uzaifu. Lakini ile haiko kweli. Mu Biblia muko mifano ya watu wenye walikuwa hodari, lakini walikuwa wanajitiisha. Tuone mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia mufano wa Yesu, Abigaili, na Maria.

13. (a) Juu ya nini Yesu anakuwaka anajitiisha kwa Yehova? (b) Namna gani mufano wa Yesu unaonyesha kama kujitiisha haiko uzaifu?

13 Yesu anakuwaka anajitiisha kwa Yehova, haiko juu hana akili ao uwezo. Mafundisho yake yenye kuwa wazi na mwepesi inaonyesha kama iko na akili sana. (Yoh. 7:45, 46) Yehova alijua kama Yesu iko na akili sana, njo maana alimuruhusu atumike naye wakati alikuwa anaumba ulimwengu. (Mez. 8:30; Ebr. 1:2-4) Na kisha Yesu kufufuliwa, Yehova alimupatia “mamlaka yote mbinguni na duniani.” (Mt. 28:18) Hata kama Yesu iko na uwezo sana, anamutumainiaka Baba yake ili amuongoze. Juu ya nini? Juu anamupenda Baba yake.​—Yoh. 14:31.

14. Bwana wanaweza kujifunza nini wakati wanafikiria (a) namna Yehova anaona wanamuke? (b) maneno yenye kuwa mu Mezali 31?

14 Mambo yenye bwana wanaweza kujifunza. Kama Yehova anaomba wanamuke wajitiishe kwa bwana zao, ile haimaanishe kama anaona wanamuke kuwa watu wa hali ya chini. Yehova anaonyesha kama anaona wanamuke kuwa wa maana kwa sababu hakuchagua tu wanaume ili watawale na Yesu, lakini alichagua pia wanamuke. (Gal. 3:26-29) Yehova ameonyesha kama anatumainia Mwana wake kwa kumupatia mamlaka. Vilevile, bwana mwenye hekima anatumainia bibi yake kwa kumupatia mamlaka fulani. Biblia inaonyesha mambo mbalimbali yenye bibi mwenye uwezo anaweza kufanya. Kwa mufano, anaweza kusimamia kazi za ku nyumba, kuuza na kuuzisha shamba, na kufanya biashara. (Soma Mezali 31:15, 16, 18.) Mwanamuke haiko mutumwa mwenye hana haki ya kusema mawazo yake. Tofauti na ile, bwana yake anamutumainia na kusikiliza mawazo yake. (Soma Mezali 31:11, 26, 27.) Wakati bwana anamutendea bibi yake kwa heshima, bibi yake atafurahia kujitiisha kwake.

Namna Yesu anakuwaka anajitiisha kwa Yehova inaweza kufundisha bibi nini? (Ona fungu la 15)

15. Mufano wa Yesu unaweza kufundisha bibi nini?

15 Mambo yenye bibi wanaweza kujifunza. Hata kama Yesu ametimiza mambo mingi, haone kama kujitiisha kwa Yehova ni kujizaraulisha. (1 Ko. 15:28; Flp. 2:5, 6) Vilevile, mwanamuke mwenye uwezo, mwenye anafuata mufano wa Yesu, hataona kama kujitiisha kwa bwana yake ni kujizaraulisha. Ataunga bwana yake mukono kwa sababu anamupenda, lakini zaidi sana kwa sababu anamupenda Yehova na kumuheshimia.

Kisha kutumia Daudi na wanaume wake chakula, Abigaili anamukaribia Daudi. Kisha anainama mupaka chini mbele yake na anamuomba asijiletee hatia ya damu kwa kulipiza kisasi. (Ona fungu la 16)

16. Kulingana na 1 Samweli 25:3, 23-28, Abigaili alipambana na tatizo gani? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

16 Abigaili alikuwa na bwana mwenye aliitwa Nabali. Nabali alikuwa mwanaume mwenye kujifikiria mwenyewe, alikuwa na kiburi, na hakukuwa na shukrani. Hata vile, Abigaili hakutumia nafasi yenye ilijitokeza ili kuachana na bwana yake. Angeweza kunyamaza na kuacha Daudi na wanaume wake waue bwana yake. Kuliko kufanya vile, alikamata mipango ili kulinda Nabali na watu wengine wa nyumba yake. Wazia uhodari wenye Abigaili alionyesha wakati alikaribia wanaume 400 wenye silaha na kuzungumuza na Daudi kwa heshima. Alikuwa hata tayari kuomba musamaha kwa ajili ya makosa ya bwana yake. (Soma 1 Samweli 25:3, 23-28.) Mara moja Daudi alitambua kama Yehova njo alitumia ule mwanamuke mwenye uhodari ili amupatie mashauri yenye alikuwa nayo lazima kusudi aepuke kufanya zambi nzito.

17. Habari juu ya Daudi na Abigaili inaweza kufundisha bwana nini?

17 Mambo yenye bwana wanaweza kujifunza. Abigaili alikuwa mwanamuke mwenye hekima. Na Daudi alitenda kwa hekima wakati alisikiliza mashauri yake. Ile ilimusaidia aepuke kuua watu wenye hawakukuwa na kosa. Vilevile, bwana mwenye hekima anasikilizaka kwa uangalifu mawazo ya bibi yake mbele akamate maamuzi ya maana. Pengine mawazo ya bibi yake itamusaidia aepuke kukamata maamuzi ya mubaya.

18. Mufano wa Abigaili unaweza kufundisha bibi nini?

18 Mambo yenye bibi wanaweza kujifunza. Bibi mwenye kumupenda Yehova na kumuheshimia anaweza kusaidia sana familia yake, hata kama bwana yake hamutumikie Yehova ao haishi kulingana na kanuni za Yehova. Hatatafuta kuachana na bwana yake bila sababu zenye kupatana na Maandiko. Kuliko kufanya vile, anaheshimia bwana yake na kujitiisha kwake. Ile inaweza kuchochea bwana yake ajifunze kumuhusu Yehova. (1 Pe. 3:1, 2) Hata kama bwana yake habadilike, Yehova anafurahi kwa sababu ule bibi anaonyesha ushikamanifu kwake kwa kuendelea kujitiisha kwa bwana yake.

19. Ni katika hali gani bibi hapaswe kutii bwana yake?

19 Lakini, bibi mwenye kujitiisha hapaswe kukubali ikiwa bwana yake anamuomba afanye jambo fulani lenye kuvunja sheria za Yehova ao kanuni zake. Kwa mufano, wazia dada iko na bwana mwenye haiko Shahidi wa Yehova. Kisha bwana yake anamuambia aseme uongo, aibe, ao afanye jambo lingine lenye halipatane na Maandiko. Wakristo wote, hata dada wenye kuolewa, wanapaswa kwanza kumutii Yehova Mungu. Kama bwana anaomba dada avunje kanuni fulani ya Biblia, dada anapaswa kukataa, na kumufasiria kwa upole lakini waziwazi juu ya nini hawezi kufanya mambo yenye anamuomba.​—Mdo. 5:29.

Ona fungu la 20 *

20. Nini njo inaonyesha kama Maria alikuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova?

20 Maria alikuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova. Na bila shaka, alijua muzuri Maandiko. Katika mazungumuzo yenye alifanya na Elizabeti, mama ya Yohana Mubatizaji, Maria alitaja Maandiko ya Kiebrania mara 20. (Lu. 1:46-55) Fikiria jambo hili: Hata kama Maria alikuwa muchumba wa Yosefu, malaika wa Yehova hakumutokea kwanza Yosefu. Malaika alizungumuza kwanza moja kwa moja na Maria na kumuambia kama atazaa Mwana wa Mungu. (Lu. 1:26-33) Yehova alijua Maria muzuri na alikuwa hakika kama atapenda Mwana wake na kumuhangaikia. Na bila shaka, Maria aliendelea kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova hata kisha Yesu kufa na kufufuliwa ili kuenda mbinguni.​—Mdo. 1:14.

21. Mufano wa Maria unaweza kufundisha bwana nini?

21 Mambo yenye bwana wanaweza kujifunza. Bwana mwenye hekima anafurahi wakati bibi yake anajua muzuri Maandiko. Hamukasirikie na kuwaza kama atamunyanganya ukichwa. Anatambua kama dada mwenye anajua muzuri Biblia na kanuni za Biblia anaweza kusaidia sana familia. Lakini, ni muzuri kukumbuka kuwa, hata kama bibi iko na elimu sana kuliko bwana yake, bwana njo iko na daraka la kusimamia ibada ya familia na mambo ingine ya kiroho.​—Efe. 6:4.

Mufano wa Maria, mama ya Yesu, unaweza kufundisha bibi nini kuhusu kujifunza na kufikiri sana? (Ona fungu la 22) *

22. Mufano wa Maria unaweza kufundisha bibi nini?

22 Mambo yenye bibi wanaweza kujifunza. Mwanamuke anapaswa kujitiisha kwa bwana yake. Lakini, iko pia na daraka la kuhangaikia hali yake mwenyewe ya kiroho. (Gal. 6:5) Ili kufanya vile, anapaswa kutafuta wakati wa kufanya funzo la kipekee na kufikiri sana. Ile itamusaidia aendelee kumupenda Yehova na kumuheshimia na pia aendelee kufurahia kujitiisha kwa bwana yake.

23. Wakati wanamuke wanajitiisha, ile inaletea familia na kutaniko faida gani?

23 Bibi wenye wanaendelea kujitiisha kwa bwana zao kwa sababu wanamupenda Yehova watakuwa na furaha zaidi, na watakuwa wenye kutosheka zaidi kuliko wale wenye wanakataa kutii mupango wa ukichwa wenye Yehova ameweka. Wanawekea vijana wanaume na vijana wanamuke mufano muzuri. Na wanasaidia mu familia na mu kutaniko mukuwe upendo na amani. (Tit. 2:3-5) Leo, watumishi wengi wa Yehova waaminifu ni wanamuke. (Zb. 68:11) Sisi wote, ikuwe tuko wanaume ao wanamuke, tunaweza kusaidia kutaniko likuwe na furaha. Habari yenye kufuata itazungumuzia namna tunaweza kufanya vile.

WIMBO 131 “Kile Ambacho Mungu Ameunganisha”

^ fu. 5 Yehova alipanga mwanamuke mwenye kuolewa akuwe anajitiisha kwa bwana yake. Ile inamaanisha nini? Bwana na bibi Wakristo wanaweza kujifunza mambo mingi kwa kufikiria mufano wa Yesu na wa wanamuke fulani wenye kuzungumuziwa katika Biblia.

^ fu. 68 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati alikuwa anazungumuza na Elizabeti, mama ya Yohana Mubatizaji, Maria alitaja Maandiko ya Kiebrania yenye alikuwa ameweka mu akili.

^ fu. 70 MAFASIRIO YA PICHA: Dada Mukristo anatafutaka wakati wa kujifunza Biblia ili aendelee kuwa na hali ya muzuri ya kiroho.