Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Sababu gani Mashahidi wa Yehova wanazoea kuchapa mutume Paulo akiwa mwenye upala ao mwenye kuwa na nywele kidogo?

Kwa kweli, hakuna mutu leo mwenye anaweza kuwa hakika kabisa juu ya sura ya mutume Paulo. Michoro na picha zenye kupatikana katika vichapo vyetu ni ufundi wa kuchora, hazitegemee ushuhuda fulani wenye kupatikana katika vitu vya zamani vyenye vimechimbuliwa.

Lakini, kuko mambo fulani yenye yanaweza kuonyesha namna Paulo alikuwa anafanana. Kwa mufano, gazeti Le Phare de la Tour de Sion la tarehe 1 Mwezi wa 3, 1902, lilitaja jambo moja, lilisema hivi: “Kuhusu namna Paulo alifanana: . . . Katika kitabu ‘Acts of Paul and Thecla,’ . . . chenye kiliandikwa katika mwaka wa 150 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, kuna mafasirio juu ya sura ya Paulo, pengine yenye kuwa ya muzuri zaidi na yenye kuwa ya kweli. Yanaonyesha kama alikuwa mutu mufupi, mwenye kuwa na upala, mwenye kuwa na miguu yenye kupengamia ndani, mwenye kuwa na makiki yenye kukutana, na mwenye kuwa na pua murefu kidogo.’”

Kitabu The Oxford Dictionary of the Christian Church (chapa ya mwaka wa 1997) kinasema hivi juu ya maandishi hayo ya zamani: “Inawezekana kama kitabu ‘Acts’ kiko na habari fulani za zamani za kweli.” Kitabu The Acts of Paul and Thecla kiliheshimiwa katika miaka ya zamani kwa sababu kuko maandishi 80 ya Kigiriki ya kitabu hicho, na tafsiri mbalimbali katika luga zingine. Kwa hiyo, picha ao michoro yetu inapatana na mafasirio fulani ya zamani yenye kuzungumuzia sura ya mutume Paulo.

Kumbuka kwamba, kuko mambo mengine ya maana zaidi kuliko sura ya mutume Paulo. Hata wakati Paulo alikuwa anafanya kazi yake ya kuhubiri, watu fulani wenye walikuwa na mawazo ya kimwili walikuwa wanamuchambua kwa kusema kwamba ‘kuwapo kwake mwenyewe kimwili [kulikuwa] zaifu na maneno yake ni yenye kuzaraulika.’ (2 Kor. 10:10) Lakini hatupaswe kusahau kama alifikia kuwa Mukristo kwa sababu Yesu alimutokea kwa muujiza. Tunaweza pia kufikiria mambo yenye Paulo alitimiza akiwa “chombo kilichochaguliwa [na Kristo] ili kupeleka jina [la Yesu] kwa mataifa.” (Mdo. 9:3-5, 15; 22:6-8) Na ufikirie namna tunaweza kufaidika kwa kusoma vitabu vyenye Yehova alimuongoza kuandika kupitia roho yake.

Paulo hakujisifu juu ya mambo yenye alitimiza mbele ya kuwa Mukristo; na hakufasiria namna alikuwa anafanana. (Mdo. 26:4, 5; Flp. 3:4-6) Lakini alionyesha kwa unyenyekevu namna alijiona. Alisema hivi: ‘Mimi ni mudogo zaidi kati ya mitume, nami sifae kuitwa mutume.’ (1 Kor. 15:9) Kisha aliandika hivi: ‘Mimi, niliye mutu mudogo kuliko aliye mudogo zaidi kati ya watakatifu wote, nilipewa fazili hizi zisizostahiliwa, ili niwatangazie mataifa habari njema juu ya utajiri usiopimika wa Kristo.’ (Efe. 3:8) Kwa kweli, ujumbe huo ni wa maana zaidi kuliko mambo yoyote yenye kuhusu sura ya Paulo.