Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ubatizo​—Ni wa Maana Sana kwa Wakristo

Ubatizo​—Ni wa Maana Sana kwa Wakristo

‘Ubatizo . . . unawaokoa ninyi sasa pia.’​—1 PET. 3:21.

NYIMBO: 52, 41

1, 2. (a) Wazazi fulani wanakuwa na mawazo gani wakati mutoto wao anapenda kubatizwa? (b) Sababu gani wale wenye kupenda kubatizwa wanaulizwa ikiwa wamejitoa kwa Yehova? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

WAZAZI fulani Wakristo wanaangalia mutoto wao mwanamuke mwenye tunaweza kuita Maria; anasimama pamoja na wale wenye kupenda kubatizwa. Kwa sauti kubwa na yenye kuwa wazi, anajibia maulizo mbili yenye musemaji anauliza. Muda mufupi kisha hapo, anabatizwa.

2 Wazazi wa Maria walijivunia mutoto wao kwa sababu alikamata uamuzi wa kujitoa kabisa kwa Yehova na kubatizwa. Lakini mbele ya hapo, mama yake alikuwa na maulizo yenye yalimuhangaisha. Alikuwa anajiuliza hivi: ‘Maria amekomaa kabisa ili kubatizwa? Ameelewa kabisa uzito wa jambo lenye anataka kufanya? Haingekuwa muzuri zaidi angojee kwanza mbele abatizwe?’ Hayo ni maulizo yenye wazazi wengi wenye upendo wanajiuliza wakati mutoto wao anasema kama anapenda kubatizwa. (Mhu. 5:5) Kwa kweli, uamuzi wa kujitoa kwa Mungu na kubatizwa ni hatua za maana zaidi zenye mutu anapaswa kufanya katika maisha yake.​—Ona kisanduku “ Umekwisha Kujitoa kwa Yehova?

3, 4. (a) Namna gani mutume Petro alionyesha kama ubatizo ni jambo la maana? (b) Sababu gani ubatizo unaweza kulinganishwa na kazi ya kujenga safina katika siku za Noa?

3 Wakati alikuwa anazungumuzia ubatizo, mutume Petro alilinganisha ubatizo na kazi ya kujenga safina yenye Noa alifanya. Aliandika hivi: “Lile ambalo linalingana na hili linawaokoa ninyi sasa pia, yaani [ni kusema], ubatizo.” (Soma 1 Petro 3:20, 21.) Safina ilikuwa jengo lenye kuonekana lenye lilionyesha kabisa kama Noa alijitoa kabisa ili kufanya mapenzi ya Mungu. Noa alifanya kwa uaminifu kazi yenye Yehova alikuwa amemupatia. Kwa kweli, matendo yenye kuonyesha imani yalimuokoa Noa na familia yake wakati wa Garika. Mufano wa Petro unatoa wazo gani kubwa?

4 Kujenga safina kulionyesha kama Noa alikuwa na imani katika Mungu. Vilevile, kubatizwa mbele ya watu kunaonyesha wazi jambo fulani. Kunaonyesha nini? Kunaonyesha kama mwanafunzi amejitoa kwa Yehova kwa musingi wa imani yake katika Kristo mwenye alifufuliwa. Kama Noa, wanafunzi wenye wamejitoa kwa Mungu wanafanya kwa utii kazi yenye Yehova amewapatia. Kama vile tu Noa aliokoka Garika, watu waaminifu wenye wamebatizwa wataokoka wakati ulimwengu huu muovu utafikia mwisho wake. (Mk. 13:10; Ufu. 7:9, 10) Hilo linafanya kujitoa kwa Mungu na kubatizwa kuwa jambo la maana sana. Mutu mwenye anachelewesha bila sababu uamuzi wake wa kubatizwa anatia katika hatari tumaini lake la kupata uzima wa milele.

5. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

5 Kwa sababu ubatizo ni jambo la maana sana, tutazungumuzia maulizo tatu. Biblia inafundisha nini juu ya ubatizo? Mutu anapaswa kukamata hatua gani mbele ya kubatizwa? Sababu gani mwalimu Mukristo anapaswa kuelewa muzuri kama ubatizo ni jambo la maana wakati anafundisha mutoto wake ao mwanafunzi mwengine wa Biblia?

MAMBO YENYE BIBLIA INAFUNDISHA JUU YA UBATIZO

6, 7. (a) Ubatizo wenye Yohana alifanya ulikuwa na maana gani? Eleza. (b) Ni ubatizo gani wa pekee wenye Yohana alifanya?

6 Ubatizo wenye Yohana Mubatizaji alikuwa anafanya, ndio ubatizo wa kwanza wenye kuzungumuziwa katika Biblia. (Mt. 3:1-6) Wale wenye walibatizwa na Yohana walifanya hivyo ili kuonyesha kama wametubu zambi zao zenye walifanya kwa kuvunja Sheria ya Musa. Lakini, kwa kweli ubatizo wa maana zaidi wenye Yohana alifanya haukuhusu kutubu. Yohana alikuwa na pendeleo la pekee la kubatiza Yesu, Mwana wa Mungu, mwenye alikuwa mwanadamu mukamilifu. (Mt. 3:13-17) Yesu hakukuwa na zambi; kwa hiyo, hakukuwa na sababu ya kutubu. (1 Pet. 2:22) Ubatizo wake ulionyesha kama anajitoa ili kufanya mapenzi ya Mungu.​—Ebr. 10:7.

7 Kisha Yesu kuanza kuhubiri, wanafunzi wake pia walibatiza watu. (Yoh. 3:22; 4:1, 2) Kama ubatizo wenye Yohana alikuwa anafanya, ubatizo huo ulionyesha kama watu wametubu zambi zenye walifanya kwa kuvunja Sheria ya Musa. Lakini, kisha kufa na kufufuliwa kwa Yesu, ubatizo ungekuwa na maana ingine kwa wanafunzi wake.

8. (a) Kisha kufufuliwa, Yesu alipatia wanafunzi wake amri gani? (b) Ubatizo wa Kikristo maana yake nini? Eleza.

8 Katika mwaka wa 33, Yesu mwenye alifufuliwa alijionyesha kwa kikundi cha watu zaidi ya 500, kulikuwa wanaume, wanawake, na pengine hata watoto. Pengine ni wakati huo ndio alisema hivi: ‘Kwa hiyo muende mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, muwabatize katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.’ (Mt. 28:19, 20; 1 Kor. 15:6) Kwa kweli, inawezekana kama mamia ya wanafunzi wake walikuwa hapo wakati Yesu alitoa amri ya kufanya wanafunzi. Kwa hiyo, Yesu alionyesha kama wale wenye wangekubali kuwa Wakristo wangepaswa kubatizwa. (Mt. 11:29, 30) Mutu yeyote mwenye angependa kumutumikia Mungu kwa njia yenye anakubali, angepaswa kujua na kukubali daraka la Yesu katika utimizo wa kusudi la Yehova. Kisha kufanya hivyo, mutu huyo alipaswa kubatizwa. Hiyo ndiyo aina ya kubatizwa katika maji yenye Mungu angekubali. Biblia inatoa ushuhuda mwingi wenye kuonyesha kama wakati wa mitume, wanafunzi wapya wa Kristo walielewa maana ya ubatizo. Na hawakufikiri kama walipaswa kungojea ili kubatizwa.​—Mdo. 2:41; 9:18; 16:14, 15, 32, 33.

USIKAWIE

9, 10. Ubatizo wa Mwethiopia na wa mutume Paulo, unaweza kutufundisha nini?

9 Soma Matendo 8:35, 36. Fikiria mufano wa mwanaume Mwethiopia mwenye alikuwa ameamini dini ya Wayahudi mwenye alikuwa anarudi nyumbani kisha kutoka kuabudu huko Yerusalemu. Kisha kuchochewa na malaika wa Yehova, Filipo alimukaribia Mwethiopia huyo na ‘akamutangazia habari njema juu ya Yesu.’ Mwethiopia huyo alitenda namna gani? Jambo lenye alifanya lilionyesha wazi kama alipendezwa kabisa na kweli zenye alikuwa amejifunza. Alipenda kutenda kulingana na mupango wa Yehova; kwa hiyo, alibatizwa bila kukawia.

10 Mufano wa pili ni wa mwanaume Muyahudi mwenye alikuwa anatesa Wakristo. Alizaliwa katika taifa lenye lilikuwa limejitoa kwa Mungu. Lakini, Wayahudi walikuwa wamepoteza urafiki wao wa pekee pamoja na Yehova. Mwanaume huyo alikuwa na bidii sana katika dini ya Wayahudi, lakini alijifunza njia ya muzuri zaidi. Alihubiriwa moja kwa moja na Yesu Kristo mwenye alifufuliwa na kupewa utukufu. Mwanaume huyo alitenda namna gani? Alikuwa tayari kukubali musaada wa mwanafunzi Mukristo, Anania. Juu ya mwanaume huyo, Biblia inatuambia hivi: “Naye akasimama na kubatizwa.” (Mdo. 9:17, 18; Gal. 1:14) Kwa kweli, unatambua kama mwanaume huyo Muyahudi alifikia kuitwa mutume Paulo. Kwa sababu alipendezwa na kweli yenye alijifunza juu ya daraka la Yesu katika utimizo wa kusudi la Mungu, Paulo alikamata hatua. Alibatizwa bila kukawia.​—Soma Matendo 22:12-16.

11. (a) Ni nini inachochea leo wanafunzi wa Biblia wabatizwe? (b) Tunajisikia namna gani wakati tunaona wale wenye wamejitoa kwa Yehova wanabatizwa?

11 Ni hivyo pia juu ya wanafunzi wa Biblia leo, iwe ni vijana ao watu wenye kukomaa. Wale wenye kuwa na imani na wenye kupendezwa kabisa na kweli ya Biblia wanakuwa na hamu sana ya kujitoa kwa Mungu na kubatizwa. Hotuba ya ubatizo yenye kutolewa zaidi sana kwa ajili ya watu hao ni sehemu ya maana sana ya kila mukusanyiko. Mashahidi wa Yehova wanafurahi sana wakati mwanafunzi wa Biblia anakubali kweli na kufanya maendeleo mupaka anafikia kubatizwa katika maji. Kwa kweli, wazazi Wakristo wanafurahi kuona watoto wao kati ya wanafunzi wengine wapya wenye wanapenda kubatizwa. Katika mwaka wa utumishi wa 2017, zaidi ya watu 284 000 wenye kuwa na “mwelekeo unaofaa” walionyesha kama wamejitoa kwa Yehova kwa kubatizwa katika maji. (Mdo. 13:48) Ni wazi kwamba wanafunzi hao wapya walielewa kama Wakristo wanapaswa kubatizwa. Walipaswa kutimiza mambo gani ili wastahili kubatizwa?

12. Mwanafunzi wa Biblia anapaswa kutimiza mambo gani mbele ya kubatizwa?

12 Mbele mwanafunzi wa Biblia afikie kubatizwa, anapaswa kuonyesha imani yenye kutegemea ujuzi wa kweli juu ya Mungu, makusudi yake, na mupango wake wa ukombozi. (1 Tim. 2:3-6) Imani hiyo inachochea mwanafunzi aepuke mwenendo mubaya wenye kumuchukiza Mungu na kuishi kulingana na kanuni za haki za Yehova. (Mdo. 3:19) Kwa kweli, mutu hawezi kujitoa kwa Yehova ikiwa angali anafanya matendo ya mubaya yenye yanaweza kumuzuia kuingia katika Ufalme. (1 Kor. 6:9, 10) Lakini, zaidi ya kuishi kulingana na kanuni za juu za Yehova za mwenendo, inaomba kufanya mambo mengine. Mutu mwenye kufuatia haki anapaswa pia kuhuzuria mikutano ya kutaniko na kufanya kwa bidii kazi ya kuokoa uzima ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Yesu alisema kama kazi hiyo ingefanywa na wanafunzi wake wa kweli. (Mdo. 1:8) Wakati mwanafunzi mupya anatimiza mambo hayo anaweza sasa kujitoa kwa Yehova katika sala ya kipekee na kubatizwa mbele ya watu ili kuonyesha kama amejitoa kwa Mungu.

SAIDIA WANAFUNZI WA BIBLIA WAJIWEKEE MURADI WA KUBATIZWA

Wakati unafundisha wengine unatafuta nafasi za kuwasaidia waelewe kama kubatizwa ni jambo la maana sana? (Picha hii inapatana na fungu la 13)

13. Wakati tunafundisha wengine, sababu gani tunapaswa kukumbuka kama ni lazima wabatizwe ili wakuwe Wakristo wa kweli?

13 Wakati tunasaidia watoto wetu na wanafunzi wengine wa Biblia wakamate hatua zenye kufaa, tunapaswa kukumbuka kwamba ili mutu akuwe mwanafunzi wa kweli anapaswa kubatizwa. Ikiwa tunafanya hivyo, tutazungumuzia jambo hilo waziwazi pamoja na wanafunzi wetu. Hatutajizuia kuwaelezea kwa wakati wenye kufaa kwamba kujitoa kwa Mungu na kubatizwa ni jambo la maana sana. Kwa kweli, tunapenda watoto wetu na wanafunzi wengine wa Biblia wafanye maendeleo mupaka wafikie kubatizwa!

14. Sababu gani hatusukume mutu yeyote abatizwe?

14 Kwa kweli, hakuna mutu mwenye anapaswa kusukuma ao kukaza mutoto ao mwanafunzi wa Biblia abatizwe. Yehova hakaze mutu yeyote amutumikie. (1 Yoh. 4:8) Lakini, wakati tunaendelea kufundisha wanafunzi wetu, tunapaswa kukazia kama kuwa na urafiki wa pekee pamoja na Mungu ni jambo la maana sana. Ikiwa mwanafunzi ni mwenye shukrani juu ya kweli yenye amejifunza juu ya Mungu na anapenda kabisa kufanya kila jambo lenye Mukristo wa kweli anapaswa kufanya, atapenda kubatizwa.​—2 Kor. 5:14, 15.

15, 16. (a) Mutu anapaswa kuwa na miaka ngapi ili astahili kubatizwa? Eleza. (b) Sababu gani mwanafunzi anapaswa kubatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova hata kama alibatizwa zamani katika dini ingine?

15 Hakuna miaka fulani yenye imewekwa yenye mutu anapaswa kueneza ili abatizwe. Watu wako tofauti, na wanafunzi fulani wanafanya maendeleo haraka kuliko wengine. Wengi wanabatizwa wakati wangali vijana, na wanaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu. Wanafunzi wengine wa Biblia wanajifunza kweli wakati wamekwisha kukomaa sana na wanaona kuwa ni jambo la maana kubatizwa; wamoja wamebatizwa na wako na miaka zaidi ya 100!

16 Mwanamuke mumoja mwenye kuzeeka mwenye alikuwa anajifunza Biblia aliuliza mwalimu wake ikiwa ilikuwa jambo la lazima kabisa abatizwe tena; alikuwa amebatizwa katika dini mbalimbali miaka yenye ilikuwa imepita. Mwanafunzi huyo na mwalimu wake walizungumuzia maandiko ya Biblia yenye kuzungumuzia jambo hilo. Mwanafunzi huyo alielewa sasa mawazo ya Biblia na akabatizwa bila kukawia. Hata kama alikuwa anakaribia kueneza miaka 80, aliona kama alipaswa kubatizwa. Kwa kweli, ubatizo wenye kukubalika unategemea ujuzi wa kweli juu ya mapenzi ya Yehova. Kwa hiyo, wanafunzi wapya wanapaswa kubatizwa hata kama hapo zamani walibatizwa katika dini ingine.​—Soma Matendo 19:3-5.

17. Mutu anapaswa kufikiria nini siku ya ubatizo wake?

17 Siku yenye mutu anabatizwa ni siku ya furaha sana. Na ni siku ya kufikiri sana juu ya maana ya jambo hilo. Mutu anapaswa kujikaza sana ili aishi kulingana na ahadi yake ya kujitoa kwa Mungu. Ndiyo sababu Yesu alilinganisha uamuzi wa kuwa Mukristo na nira. Wanafunzi wa Yesu hawaishi tena “kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili ya yeye aliyekufa kwa ajili yao na kufufuliwa.”​—2 Kor. 5:15; Mt. 16:24.

18. Tutazungumuzia maulizo gani katika habari yenye kufuata?

18 Mama ya Maria alikuwa na mawazo kama hayo katika akili yake wakati aliuliza maulizo yenye kuwa kwenye mwanzo wa habari hii. Ikiwa uko muzazi, pengine umejiuliza hivi: ‘Mutoto wangu iko tayari kabisa kubatizwa? Iko na ujuzi wa kutosha wa kumusaidia ajitoe kabisa kwa Mungu? Mutoto wangu anapaswa kusoma masomo ya juu na kupata kazi ya muzuri ya kimwili mbele ya kubatizwa? Itakuwa namna gani ikiwa mutoto wangu anabatizwa kisha anafanya zambi nzito?’ Tutazungumuzia maulizo hayo katika habari yenye kufuata na tutazungumuzia pia namna wazazi Wakristo wanaweza kuendelea kuwa na mawazo yenye kusawazika juu ya ubatizo.