Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 12

Tuhangaikie Namna Wengine Wanajisikia

Tuhangaikie Namna Wengine Wanajisikia

“Ninyi wote . . . mujitie pa nafasi ya wengine.”​—1 PE. 3:8.

WIMBO 90 Tianeni Moyo

KIFUPI CHA HABARI *

1. Kulingana na 1 Petro 3:8, juu ya nini tunafurahia kuwa pamoja na watu wenye wanahangaikia namna tunajisikia na hali yetu ya muzuri?

TUNAFURAHIA kuwa pamoja na watu wenye wanahangaikia namna tunajisikia na kuhangaikia hali yetu ya muzuri. Wanajaribu kujitia pa nafasi yetu, ni kusema, kutambua mawazo yetu na namna tunajisikia. Wanatambua mambo yenye tuko nayo lazima na wanatutolea musaada, wakati fulani wanafanya vile hata mbele tuwaombe musaada. Tunapendezwa na watu wenye wanaonyesha kama ‘wanajitia pa nafasi’ * yetu.​—Soma 1 Petro 3:8.

2. Juu ya nini tunapaswa kujikaza ili kujitia pa nafasi ya wengine?

2 Kwa sababu tuko Wakristo, sisi wote tunataka kuwa na sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine. Lakini, kwa kweli, haiko mwepesi sikuzote kuonyesha ile sifa. Juu ya nini? Sababu moja ni kwamba hatukamilike. (Ro. 3:23) Kwa kawaida tunajifikiria sisi wenyewe kwanza; kwa hiyo, tunapaswa kujikaza sana ili kufikiria wengine. Pia, wamoja kati yetu wanaweza kuona kuwa haiko mwepesi kujitia pa nafasi ya wengine kwa sababu ya namna walikomaa ao kwa sababu ya mambo fulani yenye iliwafikia mu maisha. Tena, tunaweza kuchochewa na tabia ya watu wenye kutuzunguka. Katika siku hizi za mwisho, watu wengi hawahangaikie namna wengine wanajisikia. Lakini, ni “wenye kujipenda wenyewe.” (2 Ti. 3:1, 2) Ni nini inaweza kutusaidia tushinde ile magumu yenye inafanya ikuwe nguvu kwetu kuhangaikia namna wengine wanajisikia?

3. (a) Tunaweza kufanya nini ili tukomalishe sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine? (b) Tutazungumuzia nini mu habari hii?

3 Tunaweza kukomalisha sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine kwa kuiga mufano wa Yehova Mungu na Mwana wake, Yesu Kristo. Yehova ni Mungu mwenye upendo, na anaonyesha mufano muzuri zaidi wa kuhangaikia wengine. (1 Yo. 4:8) Yesu alionyesha kwa ukamilifu sifa za Baba yake. (Yoh. 14:9) Wakati alikuwa ku dunia, alionyesha kupitia mufano wake namna mwanadamu anaweza kuonyesha huruma. Mu habari hii, tutazungumuzia kwanza namna Yehova na Yesu wameonyesha kama wanahangaikia namna wengine wanajisikia. Kisha, tutazungumuzia namna tunaweza kuiga mufano wao.

MUFANO WA YEHOVA WA KUHANGAIKIA WENGINE

4. Namna gani andiko la Isaya 63:7-9 linaonyesha kama Yehova anahangaikia namna watumishi wake wanajisikia?

4 Biblia inafundisha kama Yehova anahangaikia namna watumishi wake wanajisikia. Kwa mufano, fikiria namna Yehova alijisikia wakati Waisraeli wa zamani walikuwa wanateseka. Neno la Mungu linasema hivi: “Katika taabu zao zote, yeye alitaabika.” (Soma Isaya 63:7-9.) Kisha, kupitia nabii Zekaria, Yehova alisema kama wakati watu wake wanatendewa mubaya, ni kama vile yeye njo anatendewa mubaya. Yehova aliambia watumishi wake hivi: “Mutu yeyote mwenye anawagusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.” (Zek. 2:8) Huo ni mufano muzuri sana wenye kuonyesha namna Yehova anahangaikia watu wake!

Huruma ilimuchochea Yehova akomboe Waisraeli katika utumwa wa Misri (Picha hii inapatana na fungu la 5)

5. Ni mufano gani wenye kuonyesha namna Yehova ametenda ili kusaidia watumishi wake wenye walikuwa wanateseka?

5 Zaidi ya kusikilia tu huruma watumishi wake wenye kuteseka, Yehova anafanya mambo mingi zaidi. Anatenda ili kuwasaidia. Kwa mufano, wakati Waisraeli walikuwa wanateseka katika utumwa mu inchi ya Misri, Yehova alielewa maumivu yao na alichochewa kumaliza ile maumivu. Yehova alimuambia Musa hivi: “Kwa kweli nimeona mateso ya watu wangu . . . , na nimesikia kilio chao . . . ninajua muzuri maumivu yenye wako nayo. Nitashuka ili kuwakomboa katika mukono wa Wamisri.” (Kut. 3:7, 8) Juu Yehova alisikilia watu wake huruma, aliwakomboa katika utumwa. Mamia ya miaka kisha pale, wakati Waisraeli walikuwa mu Inchi ya Ahadi, walishambuliwa na maadui wao. Yehova alitenda namna gani? “Aliwasikilia huruma kwa sababu ya kilio chao cha maumivu chenye kilitokezwa na wale wenye waliwakandamiza na wale wenye walikuwa wanawatendea mubaya.” Tena, Yehova alijitia pa nafasi yao, na hilo lilimuchochea awasaidie. Alituma waamuzi ili waokoe Waisraeli kutoka mu mikono ya maadui wao.​—Amu. 2:16, 18.

6. Ni mufano gani wenye kuonyesha namna Yehova alihangaikia mutumishi wake fulani mwenye hakukuwa na mawazo yenye kufaa?

6 Yehova anahangaikia namna watu wake wanajisikia, hata kama wakati fulani hawana mawazo yenye kufaa. Fikiria mufano wa Yona. Mungu alimutuma nabii huyo ili atangazie watu wa Ninawi ujumbe wa hukumu. Wakati walitubu, Mungu aliamua kama hatawaharibu tena. Lakini, Yona hakufurahia uamuzi huo. ‘Alikasirika sana’ kwa sababu unabii wake juu ya uharibifu wa Ninawi haukutimia. Lakini Yehova alimuvumilia Yona na alimusaidia kubadilisha mawazo yake. (Yon. 3:10–4:11) Kisha wakati fulani, Yona alielewa mambo yenye Yehova alimufundisha na Yehova alimutumia ili kuandika ile habari kwa faida yetu.​—Ro. 15:4. *

7. Namna Yehova alitendea watumishi wake inatuhakikishia nini?

7 Namna Yehova alitendea watu wake inatuhakikishia kama anajitia pa nafasi ya watumishi wake. Anajua maumivu na mateso ya kila mumoja wetu. Yehova ‘anajua kwa kweli moyo wa mwanadamu.’ (2 Ny. 6:30) Anaelewa mawazo yetu ya ndani zaidi, namna tunajisikia kabisa mu moyo wetu, na mipaka yetu. Na ‘hatatuacha tujaribiwe kupita vile tunaweza kuvumilia.’ (1 Ko. 10:13) Ile ahadi inatufariji sana!

MUFANO WA YESU WA KUHANGAIKIA WENGINE

8-10. Ni mambo gani yenye ilipaswa kumusaidia Yesu ahangaikie wengine?

8 Wakati Yesu alikuwa mwanadamu ku dunia, alikuwa anahangaikia sana watu wengine. Kuko karibu mambo tatu yenye ilimusaidia Yesu ahangaikie wengine. Kwanza, kama vile tumekwisha kuona, Yesu alionyesha kwa ukamilifu sifa za Baba yake wa mbinguni. Kama Baba yake, Yesu alipenda watu. Hata kama Yesu alifurahia kila kitu chenye alisaidia Yehova kufanya, ‘wana wa binadamu ndio alipenda zaidi sana.’ (Mez. 8:31) Upendo ulimuchochea Yesu ahangaikie namna wengine walikuwa wanajisikia.

9 Pili, kama Yehova, Yesu alikuwa na uwezo wa kusoma mioyo. Alikuwa na uwezo wa kujua nia za watu na namna walikuwa wanajisikia. (Mt. 9:4; Yoh. 13:10, 11) Kwa hiyo, wakati Yesu alitambua kama watu walikuwa wenye kuvunjika moyo, aliwafariji kwa sababu alikuwa anawahangaikia.​—Isa. 61:1, 2; Lu. 4:17-21.

10 Tatu, Yesu mwenyewe alipatwa na magumu fulani yenye watu wengine walikuwa nayo. Kwa mufano, inaonekana kuwa Yesu alikomalia mu familia maskini. Wakati Yesu alikuwa anatumika na Yosefu, baba yake mulezi, alijifunza kufanya kazi yenye ilimuomba atumie nguvu mingi ya kimwili. (Mt. 13:55; Mk. 6:3) Inaonekana kuwa Yosefu alikufa wakati fulani mbele Yesu amalize utumishi wake. Kwa hiyo, inawezekana kabisa kuwa Yesu alisikia maumivu ya kufiwa na mutu mwenye anapenda. Na Yesu alielewa kabisa magumu ya kuishi mu familia yenye watu wote hawana imani moja. (Yoh. 7:5) Hali hizo na hali zingine zingepaswa kumusaidia Yesu aelewe magumu ya watu wa kawaida na namna walijisikia.

Mbali na watu wengi, Yesu anamusikilia huruma mwanaume kiziwi na anamuponyesha (Picha hii inapatana na fungu la 11)

11. Sifa ya Yesu ya kuhangaikia watu ilionekana zaidi sana wakati gani? Fasiria. (Ona picha ku jalada ya gazeti hili.)

11 Sifa ya Yesu ya kuhangaikia watu ilionekana zaidi sana wakati alifanya miujiza. Yesu hakufanya miujiza juu tu alilazimika kufanya vile. ‘Alisikilia huruma’ watu wenye walikuwa wanateseka. (Mt. 20:29-34; Mk. 1:40-42) Kwa mufano, wazia namna Yesu alijisikia wakati alichukua mwanaume mumoja mwenye alikuwa kiziwi na kumupeleka mbali na watu wengi ili amuponyeshe ao wakati alifufua mwana mumoja tu wa mujane fulani. (Mk. 7:32-35; Lu. 7:12-15) Yesu alisikilia watu hao huruma na alipenda kuwasaidia.

12. Namna gani andiko la Yohana 11:32-35 linaonyesha kama Yesu alijitia pa nafasi ya Marta na Maria?

12 Yesu alijitia pa nafasi ya Marta na Maria. Wakati aliona huzuni yenye walikuwa nayo juu ya kifo cha Lazaro, ndugu yao, “Yesu akatokwa na machozi.” (Soma Yohana 11:32-35.) Yesu hakulia kwa sababu tu alipoteza rafiki yake wa sana. Kwa kweli, alikuwa anajua kama atamufufua Lazaro. Lakini, Yesu alilia kwa sababu alielewa kama marafiki wake wapendwa walikuwa na huzuni sana juu ya kifo cha ndugu yao.

13. Kujua kama Yesu iko na sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine kunatutia moyo. Juu ya nini?

13 Kujifunza juu ya sifa ya Yesu ya kujitia pa nafasi ya wengine kunatutia moyo sana. Kwa kweli, Yesu alikuwa mukamilifu lakini sisi hatuko wakamilifu. Hata hivyo, tunamupenda kwa sababu ya namna alikuwa anatendea watu. (1 Pe. 1:8) Tunatiwa moyo kujua kama sasa yeye ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu na iko anatawala. Hivi karibuni, atatosha mateso yote. Yesu njo anaweza kusaidia kabisa wanadamu watoke mu maumivu yenye imeletwa na utawala wa Shetani, juu naye alikuwa mwanadamu wakati fulani. Kwa kweli, ni baraka kuwa na Mutawala mwenye anaweza “kusikilia uzaifu wetu huruma.”​—Ebr. 2:17, 18; 4:15, 16.

TUIGE MUFANO WA YEHOVA NA YESU

14. Kulingana na Waefeso 5:1, 2, tunachochewa kufanya nini?

14 Wakati tunafikiria mufano wa Yehova na Yesu, tunachochewa kuonyesha zaidi sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine. (Soma Waefeso 5:1, 2.) Yehova na Yesu wako na uwezo wa kusoma mioyo, lakini sisi hatuna uwezo wa kufanya vile. Hata hivyo, tunaweza kujikaza ili kuelewa namna wengine wanajisikia na mambo yenye wako nayo lazima. (2 Ko. 11:29) Watu wenye kutuzunguka wanajifikiria wenyewe, lakini sisi tunajikaza “kuangalia, hapana faida [zetu sisi] wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.”​—Flp. 2:4.

(Picha hizi zinapatana na fungu la 15-19) *

15. Ni nani zaidi sana wanapaswa kuonyesha sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine?

15 Zaidi sana wazee wa kutaniko wanapaswa kuonyesha sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine. Wanajua kama watatoa hesabu kwa Yehova juu ya namna wanahangaikia kondoo wake. (Ebr. 13:17) Ili kusaidia Wakristo wenzao, wazee wanapaswa kujitia pa nafasi yao. Namna gani wazee wanaweza kuonyesha sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine?

16. Muzee mwenye huruma anafanyaka nini, na juu ya nini hilo ni jambo la maana?

16 Muzee mwenye huruma anapitisha wakati pamoja na ndugu na dada zake. Anauliza maulizo na kisha anasikiliza kwa uangalifu na uvumilivu. Ni jambo la maana kufanya vile zaidi sana wakati kondoo mumoja kati ya kondoo hao wapendwa anapenda kueleza mawazo yake na namna anajisikia, lakini iko na magumu ya kupata maneno yenye kufaa. (Mez. 20:5) Wakati muzee iko tayari kutoa wakati wake, hilo linafanya yeye na ndugu na dada zake watumainiane zaidi, wakuwe na urafiki wenye nguvu, na wapendane zaidi.​—Mdo. 20:37.

17. Ndugu na dada wengi wanasema kama wanafurahiaka zaidi sifa gani ya wazee? Leta mufano.

17 Ndugu na dada wengi wanasema kama sifa ya wazee wa kutaniko yenye wanafurahia zaidi, ni sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine. Juu ya nini? Adelaide anasema hivi: “Ni mwepesi zaidi kuzungumuza nao, kwa sababu unajua kama watakuelewa.” Anaongeza hivi: “Unaweza kutambua kama wanajitia pa nafasi yako kupitia namna wanatenda wakati unazungumuza nao.” Ndugu mumoja mwenye kuwa na shukrani juu ya namna muzee mumoja alimutendea anasema hivi: “Niliona kuwa macho ya muzee huyo ilijaa machozi wakati nilikuwa ninamuambia juu ya hali yangu. Sitasahau jambo hilo hata siku moja.”​—Ro. 12:15.

18. Tunaweza kufanya nini ili tukomalishe sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine?

18 Kwa kweli, haiko wazee tu njo wanapaswa kuonyesha sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine. Sisi wote tunaweza kukomalisha ile sifa. Namna gani? Ujikaze ili kuelewa magumu yenye watu wa familia yako na Wakristo wenzako wako nayo. Upendezwe na vijana wenye kuwa mu kutaniko na pia wagonjwa, ndugu na dada wenye kuzeeka, na wale wenye wamefiwa na wapendwa wao. Uwaulize hali yao. Uwasikilize kabisa wakati wanakuelezea namna wanajisikia. Uwasaidie waone kama unaelewa kabisa hali yao. Uwatolee musaada mu njia yoyote yenye unaweza. Wakati tunafanya vile, tunaonyesha upendo wa kweli kupitia matendo.​—1 Yo. 3:18.

19. Juu ya nini tunapaswa kujipatanisha na hali za watu wakati tunajaribu kuwasaidia?

19 Tunapaswa kuwa tayari kujipatanisha na hali wakati tunajaribu kusaidia wengine. Juu ya nini? Juu watu wote hawatende namna moja wakati wa magumu. Watu fulani wako tayari kujieleza, lakini wengine hawapendake kuzungumuza juu ya magumu yao. Kwa hiyo, tunapenda kuwasaidia, lakini tunapaswa kuepuka kuuliza maulizo juu ya mambo ya pekee sana. (1 Te. 4:11) Hata wakati wengine wanatuelezea namna wanajisikia, pengine wakati fulani hatutakubaliana na mawazo yao. Lakini, tunapaswa kuelewa kama ni vile wanajisikia. Tunapenda kuwa wepesi wa kusikiliza, hapana wepesi wa kusema.​—Mt. 7:1; Yak. 1:19.

20. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

20 Zaidi ya kuonyesha sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine mu kutaniko, tunapenda pia kuonyesha ile sifa ya muzuri mu kazi yetu ya kuhubiri. Namna gani tunaweza kuonyesha sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine wakati tunafanya wanafunzi? Tutazungumuzia jambo hilo mu habari yenye kufuata.

WIMBO 130 Uwe Mwenye Kusamehe

^ fu. 5 Yehova na Yesu wanahangaikia namna wengine wanajisikia. Habari hii itazungumuzia mambo yenye mufano wao unaweza kutufundisha. Pia, tutazungumuzia juu ya nini tunapaswa kujitia pa nafasi ya wengine na namna tunaweza kufanya vile.

^ fu. 1 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: “Kujitia pa nafasi ya wengine” maana yake kujaribu kuelewa namna wengine wanajisikia na kujisikia namna wanajisikia. (Ro. 12:15) Mu habari hii, maneno “kujitia pa nafasi ya wengine” na “kuhangaikia wengine” iko na maana moja.

^ fu. 6 Pia, Yehova alitendea kwa huruma watu wengine waaminifu wenye walikuwa wamevunjika moyo ao wenye walikuwa na woga. Fikiria habari yenye kuzungumuzia Hana (1 Sa. 1:10-20), Eliya (1 Fa. 19:1-18), na Ebed-meleki (Yer. 38:7-13; 39:15-18).

^ fu. 65 MAFASIRIO YA PICHA: Mikutano ku Jumba la Ufalme inatutolea nafasi za mingi za kuhangaikia wengine. Tunaona (1) muzee anazungumuza kwa upendo na muhubiri kijana na mama yake, (2) baba na mutoto wake mwanamuke wanasaidia dada mwenye kuzeeka aingie mu motokari, na (3) wazee wawili wanamusikiliza kwa uangalifu dada mwenye anatafuta muongozo.