Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wema​—Unaweza Kufanya Nini ili Kukomalisha ile Sifa?

Wema​—Unaweza Kufanya Nini ili Kukomalisha ile Sifa?

KWA kawaida sisi wote tunapenda wengine watuone kuwa watu wema ao wazuri. Lakini, haiko mwepesi kuonyesha wema mu ulimwengu wa leo. Watu wengi “hawapendi wema.” (2 Ti. 3:3) Wanafuata kanuni zao wenyewe juu ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa, kwa kweli, wanasema kama “wema ni ubaya na ubaya ni wema.” (Isa. 5:20) Pia, ni nguvu kuwa watu wema kwa sababu mambo yenye ilitufikia zamani mu maisha, pengine ilikuwa na matokeo ya mubaya juu yetu, na kwa sababu hatuko wakamilifu. Kwa hiyo, tunaweza kujisikia kama Anne. * Hata kama amemutumikia Yehova kwa miaka mingi, anasema hivi: “Ni nguvu sana kwangu kuamini kama ninaweza kuwa mutu mwema.”

Jambo la kufurahisha ni hili: Sisi wote tunaweza kukomalisha sifa ya wema! Inatokana na roho takatifu ya Mungu na roho yake iko na nguvu zaidi kuliko vishawishi vya mubaya vya ulimwengu, watu wenye kutuzunguka, uzaifu wetu, na mambo yenye ilitufikia mu maisha. Tuchunguze basi maana ya wema na tujifunze namna tunaweza kuonyesha muzuri zaidi ile sifa.

WEMA NI NINI?

Kwa kifupi, wema ni sifa ao hali ya kuwa mwema ao mutu muzuri. Inatia ndani mwenendo muzuri na tabia ya muzuri, bila kuwa na ubaya wowote. Wema unaonekana kupitia matokeo ya muzuri yenye unaletea wengine. Ni sifa ya muzuri yenye tunaonyesha kwa kutendea wengine mambo ya muzuri.

Inawezekana kabisa umeona kuwa watu fulani wako tayari kufanyia watu wa familia yao na marafiki wao mambo ya muzuri, lakini, je, inatosha tu kufanya vile ili kuwa mutu mwema? Kwa kweli, hatuna uwezo wa kuonyesha wema kila wakati, kwa sababu Biblia inasema kama “hakuna mwenye haki katika dunia mwenye anafanya mema sikuzote na hafanyake zambi.” (Muh. 7:20) Mutume Paulo alisema hivi kwa moyo wote: “Ninajua kwamba ndani yangu, ni kusema, katika mwili wangu, hamukae jambo lolote la muzuri.” (Ro. 7:18) Kwa hiyo, ikiwa tunapenda kuwa na ile sifa, ni wazi kama tunapaswa kujifunza kupitia mufano wa Yehova, Chanzo cha wema.

“YEHOVA NI MWEMA”

Yehova Mungu anaweka kanuni za mambo mema ao ya muzuri. Biblia inasema hivi juu yake: “Wewe ni mwema na kazi zako ni za muzuri. Unifundishe masharti yako.” (Zb. 119:68) Tuzungumuzie basi mambo mbili yenye kutajwa mu andiko hilo juu ya wema wa Yehova.

Yehova ni mwema. Sifa ya wema iko kati ya sifa za Yehova; haiwezi kuachanishwa na sifa zake zingine. Fikiria mambo yenye ilitokea wakati Yehova alimuambia Musa hivi: “Nitapitisha wema wangu wote mbele ya uso wako.” Wakati Yehova alimuonyesha Musa utukufu wake kutia ndani wema wake, Musa alisikia maneno hii: “Yehova, Yehova, Mungu mwenye rehema na huruma, hakasirike haraka na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu na kweli, mwenye kuonyesha upendo mushikamanifu kwa maelfu, mwenye kusamehe kosa na uovu na zambi, lakini hatakosa hata kidogo kupatia azabu wenye kosa.” (Kut. 33:19; 34:6, 7) Hilo linaonyesha wazi kama Yehova ni Mwema kabisa katika njia zote. Hata kama Yesu njo alikuwa mwanadamu mwenye alionyesha mufano muzuri zaidi wa kuwa mwema, alisema hivi: “Hakuna mutu mwema isipokuwa mumoja tu, Mungu.”​—Lu. 18:19.

Uumbaji wa Yehova unaonyesha kama yeye ni mwema

Kazi za Yehova ni za muzuri. Wema wa Mungu unaonekana katika mambo yote yenye anafanya. “Yehova ni mwema kwa wote, na rehema yake inaonekana katika kazi zake zote.” (Zb. 145:9) Yehova anaonyesha wema bila ubaguzi, anapatia watu wote uzima na mambo yenye wako nayo lazima ili waendelee kuishi. (Mdo. 14:17) Anatuonyesha pia wema wake wakati anatusamehe. Muandikaji mumoja wa zaburi aliandika hivi: “Wewe, Ee Yehova, uko mwema na uko tayari kusamehe.” (Zb. 86:5) Tunaweza kuwa hakika kama “Yehova hatawaima jambo lolote la muzuri wale wenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu.”​—Zb. 84:11.

‘UJIFUNZE KUTENDA MEMA’

Tuliumbwa kwa mufano wa Mungu, kwa hiyo, tunaweza kuwa wema na tunaweza kufanyia wengine mambo mema ao ya muzuri. (Mwa. 1:27) Hata hivyo, Neno la Mungu linaomba watumishi wake ‘wajifunze kutenda mema.’ (Isa. 1:17) Lakini namna gani tunaweza kukomalisha ile sifa yenye kupendeza? Tunaweza kufanya vile mu njia tatu. Tuone njia hizo.

Kwanza, tunaweza kusali ili kuomba roho takatifu, yenye inaweza kutusaidia sisi Wakristo tukuwe wema mbele ya macho ya Mungu. (Gal. 5:22) Kwa kweli, roho ya Mungu inaweza kutusaidia tujifunze kupenda mambo yenye kuwa ya muzuri na kuchukia mambo yenye kuwa ya mubaya. (Ro. 12:9) Kwa kweli, Biblia inasema kama Yehova anaweza kutufanya kuwa “imara katika kila tendo na neno la muzuri.”​—2 Te. 2:16, 17.

Pili, tunapaswa kusoma Neno la Mungu lenye liliongozwa na roho yake. Wakati tunafanya vile, Yehova anaweza kutufundisha “njia yote ya mambo ya muzuri” na kutupatia “vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.” (Mez. 2:9; 2 Ti. 3:17) Kusoma Biblia na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma, kunajaza moyo wetu mambo ya muzuri juu ya Mungu na mapenzi yake. Kwa kufanya vile, tunaongeza katika hazina yetu, ni kusema katika moyo wetu, mambo yenye inaweza kutusaidia wakati mwingine.​—Lu. 6:45; Efe. 5:9.

Tatu, tunajikaza sana “kuiga mambo ya muzuri.” (3 Yo. 11) Biblia iko na mifano yenye tunaweza kuiga. Kwa kweli, Yehova na Yesu njo wanaonyesha mufano muzuri zaidi. Lakini, tunaweza pia kuchunguza mifano ya watu fulani wenye walijulikana kuwa watu wema. Pengine unaweza kufikiria watu wawili, ni kusema, Tabita na Barnaba. (Mdo. 9:36; 11:22-24) Unaweza kupata faida kwa kujifunza mambo yenye Biblia inasema juu yao, na mambo yenye walifanya ili kusaidia wengine. Fikiria mambo fulani yenye unaweza kufanya ili kusaidia watu fulani mu familia yako ao mu kutaniko lenu. Na usikose kufikiria faida zenye Tabita na Barnaba walipata kwa sababu ya kuonyesha wengine wema. Wewe pia unaweza kupata faida kama hizo.

Tunaweza kufikiria pia mifano ya watu wa siku zetu wenye wanafanya mema. Kwa mufano, fikiria mufano wa wazee wa kutaniko ‘wenye kupenda wema’ wenye wanatumika sana. Pia fikiria dada waaminifu wenye kupitia maneno na matendo yao ni “walimu wa mambo ya muzuri.” (Tit. 1:8; 2:3) Dada mumoja mwenye kuitwa Roslyn anasema hivi: “Dada mumoja mwenye kuwa rafiki yangu anajikaza sana kusaidia na kutia moyo wengine mu kutaniko. Anafikiria hali yao na mara mingi anawapatia zawadi za kidogo-kidogo ao kuwasaidia mu njia zingine zenye kufaa. Ninamuona kabisa kuwa mutu mwema.”

Yehova anatia moyo watu wake ‘watafute mambo ya muzuri.’ (Amo. 5:14) Kama tunafanya vile, tutapenda kanuni zake na tutapenda kabisa kufanya mema.

Tunajikaza kuwa wema na kufanya mema

Tusiwaze kama ili kutenda mema tunapaswa kufanyia wengine mambo ya ajabu ao kuwapatia zawadi za bei sana. Kwa mufano: Kusudi mumea ukomae, hatupaswe kuumwangia maji ya mingi mara moja, lakini tunapaswa kuumwangia maji ya kidogo-kidogo kila mara. Vilevile, kama tunafanya mambo ya mingi ya kidogo-kidogo ili kusaidia wengine, hilo litaonyesha kama tuko watu wema.

Bibilia inatutia moyo ‘tujitayarishe’ na tukuwe “tayari” kufanya mema. (2 Ti. 2:21; Tit. 3:1) Kama tuko waangalifu juu ya hali za wengine, tunaweza kuona namna ya kumupendeza jirani yetu “kwa faida yake, ili kumujenga.” (Ro. 15:2) Kwa mufano, tunaweza kumupatia kitu fulani chenye tuko nacho. (Mez. 3:27) Tunaweza kualika mutu fulani ili kula chakula pamoja naye ao kupitisha wakati pamoja naye ili kutiana moyo. Kama tunajua mutu fulani mwenye kuwa mugonjwa, tunaweza kumutumia barua, kumutembelea, ao kumuita kwenye telefone. Kwa kweli, tunaweza kuwa na nafasi mingi za kusema ‘neno la muzuri ili kujenga wengine kulingana na uhitaji, kusudi lipatie faida wale wenye wanalisikia.’​—Efe. 4:29.

Kama Yehova, tunatafuta kufanyia watu wote wema. Kwa hiyo, tunatendea wengine bila ubaguzi. Njia moja ya muzuri zaidi ya kufanya vile ni kuhubiria watu wote habari njema ya Ufalme. Kama vile Yesu aliamuru, tunajikaza kutendea mema hata watu wenye wanaonekana kuwa wanatuchukia. (Lu. 6:27) Haiko mubaya hata kidogo kuonyesha fazili na kufanyia wengine mema, kwa sababu “hakuna sheria juu ya mambo hayo.” (Gal. 5:22, 23) Wakati tunafanya mema hata kama watu wanatutendea mubaya ao hata kama tuko na magumu, tunaweza kuchochea wengine wakubali kweli na wamutukuze Mungu.​—1 Pe. 3:16, 17.

KUTENDA MEMA KUNATULETEA FAIDA

“Mutu muzuri anavuna zawabu ya matendo yake.” (Mez. 14:14) Ni zawabu ao faida gani fulani zenye tunaweza kupata? Wakati tunafanyia wengine mema, inawezekana kabisa kama nao pia watatutendea muzuri. (Mez. 14:22) Hata kama wengine hawatutendee muzuri, tunapaswa kuendelea kuwafanyia mema. Kwa hiyo, wanaweza kubadilisha mawazo yao na kututendea muzuri zaidi.​—Ro. 12:20.

Wengi wanaweza kushuhudia namna walipata faida kwa sababu ya kufanya mema na kuacha kufanya mambo ya mubaya. Fikiria mufano wa Nancy. Anasema hivi: “Wakati nilikuwa ninakomaa nilikuwa ninafanya mambo bila kuhangaika, nilikuwa na mwenendo muchafu, na sikukuwa na heshima. Lakini wakati niliendelea kujifunza na kutumia mu maisha yangu kanuni za Mungu za mema, nilianza kuwa na furaha sana. Sasa niko mwenye kujiheshimia.”

Sababu kubwa zaidi yenye inatuchochea kuonyesha wema ni hii: kufanya vile kunamufurahisha Yehova. Hata kama watu wengi hawaone mambo yenye tunafanya, Yehova yeye anaona. Anajua kila wakati tunafanya jambo la muzuri na wakati tuko na mawazo ya muzuri. (Efe. 6:7, 8) Anatubariki namna gani? “Mutu mwema anakubaliwa na Yehova.” (Mez. 12:2) Tuendelee basi kukomalisha sifa ya wema. Yehova anaahidi “utukufu na heshima na amani kwa kila mutu mwenye kufanya mambo ya muzuri.”​—Ro. 2:10.

^ fu. 2 Majina fulani imebadilishwa.