Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Juu ya nini Wakristo wanapaswa kuwa waangalifu wakati wanatumikisha programu za kielektroniki za kutumiana ujumbe?

Mashahidi wa Yehova fulani wanatumikisha teknolojia ya sasa juu ya kuendelea kuzungumuza na watu wa familia yao na mashahidi wenzao. Lakini, Mukristo mwenye kukomaa kiroho atatia mu akili hii shauri: “Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha, lakini wenye hawana uzoefu wanaendelea mbele na kupata matokeo ya mubaya.”​—Mez. 27:12.

Tunajua kama Yehova anapenda kutulinda. Lakini, hatupaswe kufanya urafiki na wale wenye kuleta migawanyiko, watengwa, ao wale wenye wanaleta mafundisho ya uongo. (Ro. 16:17; 1 Ko. 5:11; 2 Yo. 10, 11) Mu kutaniko, munaweza kuwa watu fulani wenye kuwa na mwenendo wenye unapingana na maandiko. (2 Ti. 2:20, 21) Tunapaswa kukumbuka ile jambo wakati tuko tunachagua marafiki. Lakini, inaweza kuwa nguvu sana kuchagua marafiki wazuri kupitia programu za kielektroniki za kutumiana ujumbe.

Ni muzuri kuwa muangalifu sana wakati unapenda kuchagua marafiki wazuri na uko mu kikundi kikubwa cha watu wenye kutumikisha programu fulani ya kutumiana ujumbe. Wakristo fulani wenye walijiingiza mu vikundi vikubwa, walipata matokeo ya mubaya. Sasa namna gani ndugu ao dada anaweza kuwa muangalifu wakati ile kikundi iko na mamia ao maelfu ya watu? Haiwezekane kujua muzuri watu wote wa ile kikundi ao kujua hali yao ya kiroho. Zaburi 26:4 inasema: “Sishirikiane na watu wadanganyifu, na ninaepuka wale wenye kuficha namna wako.” Hamuone kama hii andiko inatutia moyo kutumikisha programu za kielektroniki za kutumiana ujumbe ili kuzungumuza tu na watu wenye tunajua muzuri?

Hata kama iko mu kikundi kidogo cha watu wenye wanatumikisha programu fulani ya kutumiana ujumbe, Mukristo anapaswa kuwa muangalifu sana kuhusu wakati wenye anapitisha na wale watu, na pia kuhusu mambo yenye wale watu wanazoea kuzungumuzia. Hatupaswe kuwaza kama, tunalazimika kujibia kila ujumbe wenye tunapata hata kama unazungumuzia nini na hata kama walikamata wakati ngapi juu ya kuuandika. Paulo alishauria Timoteo akuwe muangalifu na watu wenye ‘wanapiga porojo na wenye wanajiingiza katika mambo ya watu wengine.’ (1 Ti. 5:13) Leo pia, hali ya vile inaweza kutokea hata mu njia ya kielektroniki.

Mukristo mwenye kukomaa kiroho hatasema-sema mubaya mashahidi wengine ao kutangaza mambo yao ya kipekee kwa watu wengine. Hawezi kusikiliza wakati wengine wako wanafanya vile. (Zb. 15:3; Mez. 20:19) Tena ataepuka kusema-sema habari fulani mu njia yenye inaonyesha kama iko mubaya zaidi na ataepuka kurudilia-rudilia habari yenye haiko hakika, lakini pia hapaswe kusikiliza habari ya vile. (Efe. 4:25) Ku site yetu ya jw.org na pia kila mwezi ku JW Télédiffusion tunapata habari za muzuri sana zenye zinategemea Biblia, na pia ripoti za kweli zenye tunaweza kutumainia.

Mashahidi fulani wanatumikisha programu za kielektroniki za kutumiana ujumbe juu ya kuuza ao kuuzisha vitu fulani, juu ya kufanya matangazo ya biashara yao, ao juu ya kuonyesha wengine kama wako na lazima ya wafanyakazi. Ile yote inahusu tu mambo ya biashara, lakini haihusu mambo ya kiroho. Wakristo wenye ‘hawana upendo wa feza’ wanaepuka kutumikisha ndugu zao mubaya juu wapate feza.​—Ebr. 13:5.

Tuseme nini kuhusu kutumikisha programu za kielektroniki za kutumiana ujumbe ili kuomba feza kwa ajili ya ndugu wenye kuwa mu uhitaji, ao kwa ajili ya wale wenye wamepata musiba? Kwa kweli, tunapenda ndugu zetu na tunawahangaikia, na kila mara tunawasaidia wale wenye wako na lazima ya musaada na tunawatia moyo. (Yak. 2:15, 16) Lakini kujaribu kufanya vile kupitia vikundi vikubwa vya programu za kielektroniki, kunafanya ikuwe nguvu sana kwa biro ya tawi ao kwa wazee wa kutaniko kuwasaidia. (1 Ti. 5:3, 4, 9, 10, 16) Na hatupende watu waanze kuwaza kama, sisi njo tulichaguliwa juu ya kusaidia ndugu zetu.

Tunapenda kufanya mambo yenye itamuletea Mungu utukufu. (1 Ko. 10:31) Njo maana, wakati unaamua kutumikisha programu fulani ya kielektroniki ya kutumiana ujumbe ao hata kutumikisha teknolojia ingine, fikiria hatari na ukuwe muangalifu.