Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 13

Namna Gani Yehova Anakulinda?

Namna Gani Yehova Anakulinda?

“Bwana ni muaminifu, na atawatia ninyi nguvu na kuwalinda kutokana na ule muovu.”​—2 TE. 3:3.

WIMBO 124 Tukuwe Washikamanifu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Juu ya nini Yesu alimuomba Yehova alinde wanafunzi wake?

USIKU wa mwisho wa maisha yake hapa ku dunia, mbele akufe, Yesu alikuwa anafikiria matatizo yenye wanafunzi wake wangepata. Juu alipenda sana wanafunzi wake, Yesu alimuomba Baba yake ‘awalinde kwa sababu ya ule muovu.’ (Yoh. 17:14, 15) Yesu alijua kama kisha yeye kurudia mbinguni, Shetani Ibilisi angeendelea kupigana vita na mutu yeyote mwenye anapenda kumutumikia Yehova. Kusema kweli, watu wa Yehova wangekuwa na lazima ya ulinzi.

2. Ni nini inatuhakikishia kama Yehova atajibia sala zetu?

2 Yehova alijibia sala ya Yesu juu alikuwa anamupenda sana. Kama tunajikaza kumupendeza Yehova atatupenda pia, na atatujibia wakati tunamuomba atusaidie na kutulinda. Sawa vile baba mwenye kuhangaikia familia yake, ni vile Yehova ataendelea kuhangaikia kwa upendo watoto wake. Na kama hafanye vile, ile inaweza kuchafua jina lake ao kuharibisha sifa yake!

3. Juu ya nini leo tuko na lazima ya ulinzi wa Yehova?

3 Leo tuko na lazima ya ulinzi wa Yehova kuliko wakati mwingine wowote. Shetani alifukuzwa mbinguni, “akiwa na kasirani kali.” (Ufu. 12:12) Amefanya watu fulani wawaze kama, wakati wanatutesa wako wanatolea “Mungu utumishi mutakatifu.” (Yoh. 16:2) Wengine wenye hawaamini Mungu wanatutesa, juu wanaona kama tuko tofauti nao. Hata ikuwe ni juu ya nini watu wanatutesa, hatuogope. Juu ya nini? Juu Neno la Mungu linasema: “Bwana ni muaminifu, na atawatia ninyi nguvu na kuwalinda kutokana na ule muovu.” (2 Te. 3:3) Sasa namna gani Yehova anatulinda? Tuzungumuzie njia mbili.

YEHOVA ANATUPATIA SILAHA

4. Kulingana na Waefeso 6:13-17, Yehova ametupatia nini yenye inaweza kutulinda?

4 Yehova ametupatia silaha zenye zinaweza kutulinda na mashambulizi ya Shetani. (Soma Waefeso 6:13-17.) Zile silaha za kiroho ziko nguvu na zinasaidia sana! Lakini kama tunapenda zile silaha zitulinde, tunapaswa kuzivaa, bila kuzitosha. Kila silaha inafananisha nini? Tuzizungumuzie basi.

5. Mukaba wa ile kweli ni nini, na juu ya nini tunapaswa kuuvaa?

5 Mukaba wa ile kweli unafananisha kweli zenye kuwa mu Neno la Mungu, Biblia. Juu ya nini tunapaswa kuvaa ule mukaba? Juu Shetani ni “baba ya uongo.” (Yoh. 8:44) Alishafanya miaka mingi sana na iko anasema uongo, na ‘amepotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu’! (Ufu. 12:9) Lakini kweli zenye kuwa mu Biblia zinatulinda juu tusidanganywe. Namna gani tunaweza kuvaa ule mukaba wa mufano? Tunaweza kufanya vile wakati tunajifunza kweli kumuhusu Yehova, wakati tunamuabudu “kwa roho na kweli,” na wakati tunajiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.​—Yoh. 4:24; Efe. 4:25; Ebr. 13:18.

Mukaba: Kweli zenye kuwa mu Neno la Mungu

6. Bamba la kifua la haki ni nini, na juu ya nini tunapaswa kulivaa?

6 Bamba la kifua la haki linafananisha kanuni za haki za Yehova. Juu ya nini tunapaswa kuvaa bamba la kifua? Sawa vile bamba la kifua linalindaka moyo wa askari, ni vile pia bamba la kifua la haki linalindaka moyo wetu wa mufano, ao utu wetu wa ndani, juu mambo ya mubaya ya ulimwengu huu isituharibishe. (Mez. 4:23) Yehova anatazamia kama tutamupenda na kumutumikia kwa moyo wetu wote. (Mt. 22:36, 37) Lakini, Shetani yeye anajaribu kugawanya moyo wetu kwa kutufanya tupende mambo ya ulimwengu huu yenye Yehova anachukia. (Yak. 4:4; 1 Yo. 2:15, 16) Na kama anashindwa, atafanya yake yote ili kutuchochea tufanye mambo fulani yenye haimupendeze Yehova.

Bamba la kifua: Kanuni za haki za Yehova

7. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunavaa bamba la kifua la haki?

7 Tunaonyesha kama tunavaa bamba la kifua la haki wakati tunatii kanuni za haki za Yehova juu ya mambo yenye kuwa sawa na mambo yenye kuwa makosa na wakati tunaishi kulingana na zile kanuni. (Zb. 97:10) Watu fulani wanawaza kama kanuni za Yehova zinatufunga-funga. Lakini kama tunaacha kutumikisha kanuni za Biblia mu maisha yetu, tutakuwa sawa askari mwenye anatosha bamba lake la kifua wakati vita ilishakolea, juu anawaza kama liko kilo sana. Ile ni kukosa akili kabisa! Lakini, wale wenye wanamupenda Yehova wanajua kama amri zake “haziko muzigo muzito,” zinawalinda.​—1 Yo. 5:3.

8. Kuvaa kwenye miguu yetu viatu ambavyo ni utayari wa kutangaza habari njema ya amani maana yake nini?

8 Paulo alitutia moyo tuvae kwenye miguu yetu viatu ambavyo ni utayari wa kutangaza habari njema ya amani. Mu maneno ingine, alipenda kusema kama sikuzote tunapaswa kuwa tayari kuhubiri habari njema ya Ufalme. Wakati tunahubiria wengine, tunatia nguvu imani yetu. Inatia moyo kabisa kuona namna mu dunia yote watu wa Yehova wako wanatumia nafasi mbalimbali ili kutangaza habari njema. Kwa mufano, wanahubiri ku kazi, ku masomo, fasi ya biashara, nyumba kwa nyumba, wakati wanaenda kuuza vitu fulani, wakati wanatembelea watu wa familia wenye hawako mashahidi, wakati wanazungumuza na watu wenye wanafahamiana nao, ao hata wakati hakuna namna watoke ku nyumba. Kama tunaogopa sana na tunaacha kuhubiri, tutakuwa sawa askari mwenye anatosha viatu vyake wakati wa vita. Itakuwa mwepesi aumizwe ku miguu na itakuwa nguvu kwake kujilinda wakati wa vita. Tena, itafanya ikuwe nguvu kwake kufuata maagizo ya kiongozi wake.

Viatu: Utayari wa kuhubiri habari njema

9. Juu ya nini tunapaswa kubeba ile ngao kubwa ya imani?

9 Ngao kubwa ya Imani inafananisha imani yetu kwa Yehova. Tunaamini kama atatimiza ahadi zake zote. Ile imani itatusaidia “kuzimisha mishale yote yenye kuwaka moto ya ule muovu.” Juu ya nini tunapaswa kubeba ile ngao kubwa? Ni juu inatulinda tusidanganywe na mafundisho ya waasi-imani na inafanya tusivunjike moyo wakati watu wanachambua-chambua imani yetu. Bila imani, itakuwa nguvu kwetu kumutii Yehova wakati watu wanatuchochea kufanya mambo yenye haipatane na kanuni zake. Lakini, kila wakati tunakataa kufanya mambo yenye Yehova hapende, ikuwe ku kazi ao ku masomo, ile itakuwa sawa vile tunabeba ngao yetu ya mufano. (1 Pe. 3:15) Tena, kila wakati tunakataa kazi yenye kulipa feza mingi na yenye haituruhusu kumutumikia Yehova kwa uwezo wetu wote, ile nayo itakuwa sawa vile tunabeba ngao yetu ya mufano. (Ebr. 13:5, 6) Na kila wakati tunamutumikia Yehova hata kama watu wanatupinga, ile inaonyesha kama ngao yetu iko inatulinda.​—1 Te. 2:2.

Ngao: Imani yetu katika Yehova na katika ahadi zake

10. Kofia ya chuma ya wokovu ni nini, na juu ya nini tunapaswa kuivaa?

10 Kofia ya chuma ya wokovu ni tumaini lenye Yehova anatupatia, ni kusema, zawabu yenye atapatia wale wote wenye wanafanya mapenzi yake. Na hata kama wanakufa, atawafufua. (1 Te. 5:8; 1 Ti. 4:10; Tit. 1:1, 2) Kama vile kofia ya chuma inalinda kichwa ya askari, ni vile pia tumaini letu la wokovu linalinda uwezo wetu wa kufikiri. Namna gani? Ile tumaini inatusaidia tuendelee kukaza akili juu ya ahadi za Mungu na inatusaidia tusilemewe na magumu. Namna gani tunaweza kuvaa ile kofia ya chuma? Ni kwa kuendelea kuwa na mawazo yenye inapatana na mapenzi ya Mungu. Kwa mufano, tunafanya vile wakati tunaweka tumaini letu katika Mungu, hapana katika utajiri wenye hauko hakika.​—Zb. 26:2; 104:34; 1 Ti. 6:17.

Kofia: Tumaini la uzima wa milele

11. Upanga wa roho ni nini, na juu ya nini tunapaswa kuutumia?

11 Upanga wa roho ni Neno la Mungu Biblia. Ule upanga uko na nguvu ya kufunua waziwazi uwongo wowote, na unasaidia watu wasikuwe tena watumwa wa mafundisho ya uwongo na tabia za mubaya. (2 Ko. 10:4, 5; 2 Ti. 3:16, 17; Ebr. 4:12) Funzo la kipekee na mazoezi yenye tunapata mu tengenezo la Mungu, njo njia zenye zinatusaidia kujua namna ya kutumikisha muzuri ule upanga. (2 Ti. 2:15) Zaidi ya zile silaha, Yehova anatulinda pia kupitia njia zingine. Ni njia gani?

Upanga: Neno la Mungu, Biblia

USIPIGANE PEKE YAKO

12. Tuko na lazima pia ya nini, na juu ya nini?

12 Askari mwenye kuwa na uzoefu anajua kama yeye peke hawezi kupigana na kikundi kikubwa cha maaskari na kupata ushindi; lakini iko na lazima ya musaada wa maaskari wenzake. Vilevile, sisi peke yetu hatuwezi kupigana na Shetani na watu wake na tupate ushindi. Njo maana tuko na lazima ya musaada wa ndugu na dada zetu. Yehova alishatupatia “ushirika muzima wa ndugu” wa mu dunia yote wenye wako tayari kutusaidia.​—1 Pe. 2:17.

13. Kulingana na Waebrania 10:24, 25, utapata faida gani wakati unaenda ku mikutano?

13 Njia moja ya kupata musaada, ni kuenda ku mikutano yetu. (Soma Waebrania 10:24, 25.) Wakati fulani tunaweza kuvunjika moyo, na kama ile inatokea, mikutano yetu inaweza kututia moyo. Wakati tuko kule, maelezo yenye ndugu na dada wanatoa inatutia moyo. Hotuba na vipindi vyenye vinatolewa kule vinatuchochea tuendelee kumutumikia Yehova. Na pia mazungumuzo yenye kujenga yenye tunakuwaka nayo mbele na kisha mukutano, inatutiaka moyo. (1 Te. 5:14) Tena, mikutano yetu inatupatia nafasi ya kusaidia wengine na ile inatuletea furaha. (Mdo. 20:35; Ro. 1:11, 12) Pia, mikutano yetu inatusaidiaka mu njia ingine. Inatusaidia tukuwe wahubiri na walimu wazuri zaidi. Kwa mufano, inatusaidia tujue namna ya kutumikisha muzuri Vyombo Vyetu vya Kufundishia. Kwa hiyo, utayarishe muzuri mikutano ya kutaniko. Na wakati uko ku mukutano, usikilize kwa uangalifu. Kisha mukutano, utumikishe mazoezi yenye umepata. Wakati unafanya vile utakuwa ‘askari muzuri wa Kristo Yesu.’​—2 Ti. 2:3.

14. Tuko na musaada gani ingine?

14 Tena, mamilioni ya malaika wenye nguvu wako pale juu ya kutusaidia. Fikiria mambo yenye malaika moja tu anaweza kufanya! (Isa. 37:36) Halafu jeshi la malaika wenye nguvu? Ni ajabu! Hakuna mutu yeyote, wala malaika muovu wa Shetani mwenye anaweza kujilinganisha na jeshi la Yehova lenye nguvu. Yehova njo Mungu Mweza-yote, kwa hiyo, wakati iko ngambo yetu, tutakuwa tu na nguvu zaidi kuliko wapinzani wetu hata wakuwe wangapi! (Amu. 6:16) Tukuwe hakika kama ile njo kweli! Kwa hiyo, usisahau ile mawazo wakati mufanyakazi mwenzako, mwanafunzi mwenzako ao mutu wa familia yako anasema ao anafanya jambo fulani lenye linakuvunja moyo. Kumbuka kama hauko peke yako mu hii vita, juu uko unafuata muongoza wa Yehova.

YEHOVA ATAENDELEA KUTULINDA

15. Kulingana na Isaya 54:15, 17, juu ya nini tuko hakika kama hakuna mutu mwenye anaweza kuzuia watu wa Mungu waendelee kuhubiri?

15 Kuko sababu mingi zenye zinafanya watu wenye kuwa mu ulimwengu wenye kutawaliwa na Shetani watuchukie. Kwa mufano, hatujiingizake mu mambo ya politike wala mambo ya vita. Tunajulisha watu jina la Mungu, tunahubiri kama ni Ufalme wa Mungu tu njo wenye utaleta amani, na tunatii kanuni za haki za Mungu. Tunaonyesha watu waziwazi kama mutawala wa ulimwengu huu ni muovu na muuaji. (Yoh. 8:44) Na tunatangaza kama hivi karibuni ulimwengu wa Shetani utaharibiwa. Na tuko hakika kama, hakuna siku Shetani na watu wake watatuzuia kuhubiri. Lakini, tutaendelea kumusifu Yehova mu kila njia yenye tunaweza! Hata kama Shetani iko na nguvu sana, hakuwezaka na hataweza kuzuia ujumbe wa ufalme uendelee kuhubiriwa mu dunia yote. Ile yote inawezekana juu Yehova iko anatulinda.​—Soma Isaya 54:15, 17.

16. Namna gani Yehova ataokoa watu wake wakati wa taabu kubwa?

16 Sasa ni mambo gani iko inatuchunga mbele yetu? Wakati wa taabu kubwa, Yehova atatuokoa mu njia mbili zenye kushangaza. Kwanza, ataokoa watumishi wake waaminifu wakati atachochea wafalme wa hii dunia waharibu Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo. (Ufu. 17:16-18; 18:2, 4) Na pili, ataokoa watu wake wakati ataharibu sehemu yenye inabakia ya ulimwengu wa Shetani ku vita ya Armagedoni.​—Ufu. 7:9, 10; 16:14, 16.

17. Ni faida gani tunapata wakati tunabakia karibu sana na Yehova?

17 Wakati tunabakia karibu sana na Yehova, hakuna kitu chenye Shetani anaweza kufanya ili kutuumiza milele. Lakini, kusema kweli, ni yeye njo ataharibiwa milele. (Ro. 16:20) Njo maana uvae silaha zote za kiroho, bila kuzitosha! Usijaribu kupigana hii vita ya kiroho peke yako. Tegemeza ndugu na dada zako. Na ufuate muongozo wa Yehova. Ukuwe hakika kama, ukifanya vile, Baba yako wa mbinguni mwenye upendo atakutia nguvu na kukulinda.​—Isa. 41:10.

WIMBO 149 Wimbo wa Ushindi

^ fu. 5 Biblia inatuahidi kama, Yehova atatutia nguvu na atatulinda. Mu hii habari tutapata majibu ya maulizo yenye kufuata: Juu ya nini tuko na lazima ya ulinzi wa Yehova? Namna gani Yehova anatulinda? Na tunapaswa kufanya nini juu Yehova atusaidie?