Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 12

Upendo Unatusaidia Kuvumilia Hata Kama Wanatuchukia

Upendo Unatusaidia Kuvumilia Hata Kama Wanatuchukia

“Mambo haya ninawaamuru ninyi, kwamba mupendane. Kama ulimwengu unawachukia ninyi, munajua kwamba umenichukia mimi mbele ya kuwachukia ninyi.”​—YOH. 15:17, 18.

WIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia

KIFUPI CHA HABARI *

1. Kulingana na Matayo 24:9, juu ya nini hatupaswe kushangaa wakati watu wanatuchukia?

YEHOVA alituumba na uwezo wa kupenda wengine na wa kutaka wengine pia watupende. Wakati mutu fulani anatuchukia, tunajisikiaka mubaya sana na pengine tunaweza kufikia hata kuogopa. Kwa mufano dada Georgina, mwenye kuishi mu Ulaya, anasema hivi: “Wakati nilikuwa na miaka 14, mama yangu alinichukia juu nilikuwa ninamutumikia Yehova. Nilijisikia mubaya sana na nilijisikia kuwa peke yangu. Na niliwaza kama pengine sikukuwa mutu muzuri.” * Ndugu mumoja mwenye kuitwa Danylo anasema hivi: “Wakati maaskari walinipiga, walinitukana na kuniambia kama wangenifanya mubaya juu niko Shahidi wa Yehova, niliogopa na nilijiona kuwa wa bure.” Matendo ya vile inafanyaka tujisikie mubaya sana. Lakini ile haitushangaze juu Yesu alitabiri kama watu watatuchukia.​—Soma Matayo 24:9.

2-3. Juu ya nini watu wanachukia wafuasi wa Yesu?

2 Ulimwengu unachukia wafuasi wa Yesu. Juu ya nini? Juu kama Yesu, ‘hatuko sehemu ya ulimwengu.’ (Yoh. 15:17-19) Hata kama tunaheshimia serikali za wanadamu, hatuziabudu ao kuabudu vitu kama vile bendera ao wimbo wa taifa. Tunamuabudu tu Yehova. Tunategemeza haki ya Mungu ya kutawala wanadamu. Lakini Shetani na “uzao” wake wanakataa kama Mungu njo iko na ile haki. (Mwa. 3:1-5, 15) Njo maana tunahubiri kama Ufalme wa Mungu tu njo wenye utamaliza magumu yote, na kama utaharibu hivi karibuni wale wote wenye kuupinga. (Da. 2:44; Ufu. 19:19-21) Ile ni habari ya muzuri kwa wapole, lakini hapana kwa waovu.​—Zb. 37:10, 11.

3 Pia, watu wanatuchukia juu tunaishi kulingana na kanuni za haki za Mungu. Zile kanuni ziko tofauti kabisa na mwenendo mubaya sana wa watu leo. Kwa mufano, watu wengi wanakubali matendo ya uasherati yenye inafanana na ile yenye watu wa Sodoma na Gomora walikuwa wanafanya. Mungu aliwaharibu juu ya ile matendo! (Yud. 7) Juu tunatii sheria za Mungu zenye zinatukataza kufanya matendo ya vile, watu wengi wanatuzarau na kusema kama hatuna akili!​—1 Pe. 4:3, 4.

4. Ni sifa gani zinaweza kutupatia nguvu wakati watu wanatuchukia?

4 Ni nini itatusaidia kuvumilia wakati watu wanatuchukia na wakati wanatutukana? Tunapaswa kuamini kabisa kama Yehova atatusaidia. Kama ngao, imani yetu inaweza “kuzimisha mishale yote yenye kuwaka moto ya ule muovu.” (Efe. 6:16) Lakini, zaidi ya imani tuko na lazima pia ya sifa ya upendo. Juu ya nini? Ni juu upendo “haukasirike haraka.” Unafunika na unavumilia mambo yote yenye kuumiza. (1 Ko. 13:4-7, 13) Tuone sasa namna kumupenda Yehova, kupenda waabudu wenzetu na hata maadui wetu kunatusaidia tuvumilie wakati watu wanatuchukia.

KUMUPENDA YEHOVA KUNATUSAIDIA KUVUMILIA WAKATI WATU WANATUCHUKIA

5. Yesu aliweza kufanya nini juu alimupenda Baba yake?

5 Usiku, mbele maadui wake wamuue, Yesu aliambia hivi wafuasi wake waaminifu: “Ninamupenda Baba, [kwa hiyo] ninafanya kama vile Baba aliniamuru.” (Yoh. 14:31) Juu Yesu alimupenda Yehova, aliweza kuvumilia majaribu makali yenye alipata. Kumupenda Yehova kunaweza pia kutusaidia mu ile njia.

6. Kulingana na Waroma 5:3-5, watumishi wa Yehova wanajisikia namna gani wakati wanavumilia chuki ya ulimwengu?

6 Kila mara, kumupenda Mungu kumesaidia watumishi wa Yehova wavumilie mateso. Kwa mufano, wakati tribinali kubwa na yenye nguvu ya Wayahudi iliamuru mitume waache kuhubiri, kumupenda Mungu njo kuliwachochea ‘wamutii Mungu kuwa mutawala kuliko wanadamu.’ (Mdo. 5:29; 1 Yo. 5:3) Leo pia, kumupenda Mungu sana kunasaidia ndugu zetu wabakie waaminifu, hata kama serikali zenye kuwa na nguvu na zenye hazina huruma zinawatesa. Wakati ulimwengu unatuchukia, hatuvunjike moyo, lakini tunafurahi.​—Mdo. 5:41; soma Waroma 5:3-5.

7. Tunapaswa kutenda namna gani wakati watu wa familia yetu wanatupinga?

7 Wakati watu wa familia yetu wanatupinga, ile inaweza kuwa jaribu ya nguvu sana kuvumilia. Wakati tunaanza kupendezwa na kweli, wamoja kati ya watu wa familia yetu, pengine wanaweza kufikiri kama wametudanganya. Wengine wanaweza kuwaza kama tumepoteza akili. (Linganisha na Marko 3:21.) Na pengine wanaweza hata kutupinga kwa ukali. Lakini, hatupaswe kushangaa wakati wanatupinga. Yesu alisema hivi: “Maadui wa mutu watakuwa watu wa nyumba yake mwenyewe.” (Mt. 10:36) Kwa kweli, hata kama watu wa familia yetu wanatutendea namna gani, hatupaswe kuwachukia. Kadiri upendo wetu kwa Yehova unaongezeka, na ni vile pia tunapaswa kuendelea kupenda watu. (Mt. 22:37-39) Lakini hatupaswe kuacha kutii sheria na kanuni za Biblia, juu tu ya kufurahisha mutu.

Tunaweza kuteseka wakati fulani. Lakini, tukuwe hakika kama sikuzote Yehova atakuwa pamoja na sisi ili kutufariji na kututia nguvu (Ona fungu la 8-10)

8-9. Ni nini ilimusaidia dada mumoja aendelee kuvumilia wakati walimupinga sana?

8 Georgina, mwenye tulishataja, aliweza kuvumilia hata kama mama yake alimupinga sana. Anafasiria hivi: “Miye na mama yangu tulianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Kisha miezi sita, wakati nilipenda kuanza kukusanyika, mama yangu alianza kunipinga. Lakini nilitambua kama alikuwa anazungumuza na waasi-imani, na pia alikuwa anarudilia maneno yao wakati alikuwa anazungumuza na miye. Tena, alikuwa ananitukana, kunikokota-kokota ku nywele, kunikamata nguvu ku shingo, na kutupa vitabu vyangu. Wakati nilieneza miaka 15, nilibatizwa. Juu mama yangu alipenda niache kumutumikia Yehova, alinipeleka fasi kwenye wanasaidiaka vijana wanamuke wenye kuwa na tabia ya mubaya. Na kati ya wale vijana, kulikuwa wenye walikuwa wametumia dawa za kulewesha na walikuwa wamefanya makosa makubwa. Wakati watu wenye wangepaswa kukupenda na kukuhangaikia wanakupinga, ile inakuwaka nguvu sana kuvumilia.”

9 Nini njo ilisaidia Georgina avumilie? Anasema hivi: “Siku mama yangu alianza kunipinga, nilikuwa tu njo namaliza kusoma Biblia yote. Nilikuwa kabisa hakika kama nimepata kweli, na nilijisikia kuwa karibu sana na Yehova. Kila mara nilikuwa nasali kwa Yehova na alikuwa ananisikia. Wakati nilikuwa naishi fasi kwenye mama yangu aliniachaka, dada mumoja alinialika kwake, tukasoma Biblia, tukatafuta habari na kuona namna tunaweza kutumikisha ile habari mu maisha. Mu ile wakati, ndugu walikuwa wananitia moyo ku mikutano. Walinitendea sawa mutu wa mu familia yao. Nilijionea waziwazi kama Yehova iko na nguvu sana kuliko wapinzani wetu, hata wakuwe wa namna gani.”

10. Tunaweza kuwa hakika kama sikuzote Yehova atafanya nini?

10 Mutume Paulo aliandika kama hakuna kitu chenye kinaweza “kututenganisha na upendo wa Mungu wenye kuwa katika Kristo Yesu Bwana wetu.” (Ro. 8:38, 39) Hata kama tunaweza kuteseka wakati fulani, tukuwe hakika kama sikuzote Yehova atakuwa pamoja na sisi ili kutufariji na kututia nguvu. Na kama vile habari ya Georgina imeonyesha, Yehova anatusaidiaka pia kupitia ndugu na dada zetu mu kutaniko.

KUPENDA NDUGU NA DADA ZETU KUNATUSAIDIA KUVUMILIA WAKATI WATU WANATUCHUKIA

11. Namna gani upendo wenye Yesu alizungumuzia mu Yohana 15:12, 13 unasaidia wanafunzi wake? Leta mufano.

11 Usiku wenye ulitangulia kifo chake, Yesu alikumbusha wanafunzi wake wapendane. (Soma Yohana 15:12, 13.) Yesu alijua kama upendo wa kujitoa ungewasaidia waendelee kuwa na umoja, na kuvumilia wakati watu wanawachukia. Fikiria mufano wa kutaniko la Tesalonike. Tangu lianzishwe, ndugu na dada wa ile kutaniko walikuwa wanateswa. Hata vile, wale ndugu na dada walifikia kuwa mifano ya muzuri wakati walivumilia kwa uaminifu na kuonyesha upendo. (1 Te. 1:3, 6, 7) Paulo aliwatia moyo waendelee kuonyesha upendo, hata “kwa ukamili zaidi.” (1 Te. 4:9, 10) Upendo ungewachochea wafariji wale wenye kushuka moyo na wasaidie wazaifu. (1 Te. 5:14) Walifuata mashauri ya Paulo. Njo maana, mu barua yake ya pili yenye iliandikwa kisha mwaka moja hivi, Paulo alifikia kusema: “Upendo wa kila mumoja wenu unaongezeka mumoja kuelekea mwingine.” (2 Te. 1:3-5) Upendo wao uliwasaidia kuvumilia hali ya nguvu na mateso.

Upendo wa Kikristo unatusaidia kuvumilia wakati watu wanatuchukia (Ona fungu la 12) *

12. Namna gani ndugu na dada wa mu inchi fulani walionyeshana upendo wakati wa vita?

12 Fikiria mambo yenye ilimufikia Danylo, mwenye tulishataja, na bibi yake. Wakati vita ilifika mu muji wao, waliendelea kukusanyika, kuhubiri kulingana na uwezo wao, na waliwapatia pia ndugu na dada zao ku chakula yenye walikuwa nayo. Kisha, siku moja, maaskari wenye walikuwa na silaha walikuja ku nyumba ya Danylo. Danylo anasema hivi: “Waliniambia nikane imani yangu. Wakati nilikataa, walinipiga, na wakafanya sawa vile wanataka kuniua, kwa kupiga lisasi mu hewa juu ya kichwa yangu. Mbele waende, waliniogopesha kwa kusema kama watarudia kumulala bibi yangu kinguvu. Lakini bila kukawia, ndugu zetu walitutia mu train juu tuende mu muji ingine. Siwezi kusahau hata kidogo upendo wenye wale ndugu zetu walituonyesha. Na wakati tulifika mu ile muji, ndugu wa kule walitupatia chakula na walinisaidia kupata kazi na nyumba! Kwa hiyo, sisi pia tuliweza kusaidia Mashahidi wengine wenye walikimbia maeneo ya vita wapate fasi ya kuishi.” Habari za vile zinaonyesha kama upendo wenye tuko nao unatusaidia kuvumilia wakati watu wanatuchukia.

KUPENDA MAADUI WETU KUNATUSAIDIA KUVUMILIA WAKATI WATU WANATUCHUKIA

13. Namna gani roho takatifu ya Yehova inatusaidia tuendelee kumutumikia hata kama watu wanatuchukia?

13 Yesu aliambia wanafunzi wake wapende maadui wao. (Mt. 5:44, 45) Ni mwepesi kufanya vile? Hapana! Lakini ile inawezekana kwa musaada wa roho takatifu ya Mungu. Tunda la roho ya Mungu linatia ndani upendo, uvumilivu, fazili, upole, na kujizuia. (Gal. 5:22, 23) Zile sifa zinatusaidia kuvumilia wakati watu wanatuchukia. Watu wengi waliacha kutupinga juu bwana, bibi, mutoto, ao jirani yao aliwaonyesha zile sifa. Na wengi kati yao, wamefikia hata kuwa ndugu na dada zetu. Kwa hiyo, ukiona kama ni nguvu kupenda wale wenye wanakuchukia juu tu uko unamutumikia Yehova, umuombe akupatie roho yake takatifu. (Lu. 11:13) Na ukuwe hakika kama sikuzote kumutii Mungu njo jambo la muzuri zaidi lenye unaweza kufanya.​—Mez. 3:5-7.

14-15. Namna gani Waroma 12:17-21 ilimusaidia Yasmeen aonyeshe upendo bwana yake hata kama alikuwa anamupinga sana?

14 Fikiria mufano wa dada mwenye anaitwa Yasmeen. Wakati alifikia kuwa Shahidi wa Yehova, bwana yake aliwaza kama walimudanganya, na alijaribu kumuzuia juu asimutumikie Yehova. Alimutukana na akaambia watu wa familia yake, kiongozi fulani wa dini, na mulozi mumoja waambie bibi yake kama watamufanya mubaya juu anapenda kuachanisha familia yake. Bwana yake alikuwa hata analalamikia ndugu na kuwatukana wakati wako ku mukutano! Mara mingi Yasmeen alikuwa analia juu ya mambo yenye walikuwa wanamutendea.

15 Ku Jumba la Ufalme, familia ya kiroho ya Yasmeen ilimufariji na kumutia nguvu. Wazee walimutia moyo atumikishe mashauri yenye kuwa mu Waroma 12:17-21. (Soma.) Yasmeen anasema hivi: “Haikukuwa mwepesi kufanya vile. Lakini nilimuomba Yehova anisaidie na nilijikaza kutumikisha mambo yenye Biblia inasema. Kwa hiyo, wakati bwana yangu alitupa kimakusudi buchafu mu mafiga, nilikuwa naifagia. Wakati alinitukana, nilijibia kwa upole. Na wakati aligonjwa, nilimuhangaikia.”

Wakati tunaonyesha kama tunapenda wenye wanatupinga, ile inaweza kuwasaidia wabadilishe tabia zao (Ona fungu la 16-17) *

16-17. Mufano wa Yasmeen umekufundisha nini?

16 Yasmeen alibarikiwa juu ya kumuonyesha bwana yake upendo. Anasema hivi: “Bwana yangu alianza kunitumainia zaidi juu alikuwa anajua kama sikuzote nilikuwa nasema kweli. Alianza kunisikiliza kwa heshima wakati tulikuwa tunazungumuza juu ya mambo ya dini na alikubali kufanya amani. Sasa iko ananitia moyo kuenda ku mikutano. Tena, miye na bwana yangu tuko na uhusiano wa muzuri, na ku nyumba tuko na amani. Natumaini kama siku moja bwana yangu atakubali kweli, na tutamutumikia Yehova pamoja.”

17 Mufano wa Yasmeen unaonyesha kama upendo “unafunika mambo yote, . . . unatumaini mambo yote, unavumilia mambo yote.” (1 Ko. 13:4, 7) Upendo uko na nguvu sana kuliko chuki. Kama tunaonyesha wengine upendo, pengine wanaweza kubadilisha mawazo yao juu yetu, na pengine wanaweza kuacha kutupinga. Na wakati tunaendelea kuonyesha upendo, ile itamufurahisha Yehova. Lakini, hata kama wapinzani wetu wanaendelea kutuchukia, tunaweza kuendelea kuwa na furaha. Namna gani?

TUNAWEZA KUWA NA FURAHA HATA KAMA WATU WANATUCHUKIA

18. Juu ya nini tunaweza kuwa na furaha hata kama watu wanatuchukia?

18 Yesu alisema: “Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanawachukia.” (Lu. 6:22) Hatupendake watu watuchukie na hatujitafutiake mateso juu tuonekane kama tuko na imani sana. Sasa juu ya nini tunaweza kuwa na furaha hata kama watu wanatuchukia? Tuone sababu tatu. Kwanza, wakati tunavumilia, Mungu anatukubali. (1 Pe. 4:13, 14) Pili, imani yetu inakuwa yenye samani kubwa zaidi na yenye nguvu. (1 Pe. 1:7) Na tatu, tutapata zawabu kubwa zaidi, ni kusema, uzima wa milele.​—Ro. 2:6, 7.

19. Juu ya nini mitume walikuwa na furaha kisha kupigwa viboko?

19 Wakati kidogo tu kisha Yesu kufufuliwa, mitume wake walipata furaha yenye alikuwa anazungumuzia. Kisha kupigwa viboko na kuagizwa waache kuhubiri, mitume walifurahi. Juu ya nini? ‘Kwa sababu walikuwa wamehesabiwa kuwa wanastahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya jina la Yesu.’ (Mdo. 5:40-42) Kumupenda Bwana wao sana kulifanya wasiogope sana maadui wao. Na walionyesha upendo wao kwa kutangaza habari njema “bila kuacha.” Leo, ndugu na dada wengi wanaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu hata kama wako na magumu. Wanajua kama Yehova hatasahau kazi yao na upendo wao wenye walionyesha kwa ajili ya jina lake.​—Ebr. 6:10.

20. Tutaona nini mu habari yenye kufuata?

20 Tunajua kama juu mwisho hauyafika, ulimwengu utaendelea kutuchukia. (Yoh. 15:19) Lakini hatupaswe kuogopa. Vile tutaona mu habari yenye kufuata, Yehova ‘atatia nguvu . . . na kulinda’ washikamanifu wake. (2 Te. 3:3) Tuendelee basi kumupenda Yehova, kupenda ndugu na dada zetu, na hata kupenda maadui wetu. Wakati tunafuata ile shauri tutakuwa na umoja, tutakuwa nguvu kiroho, tutamuletea Yehova utukufu, na tutaonyesha kabisa kama upendo uko na nguvu sana kuliko chuki.

WIMBO 106 Tukuwe na Upendo

^ fu. 5 Mu hii habari tutaona namna kumupenda Yehova, kupenda waamini wenzetu na hata kupenda maadui wetu, kunatusaidia tumutumikie Yehova hata kama ulimwengu unatuchukia. Tutaona pia juu ya nini Yesu alisema kama tunaweza kuwa na furaha hata kama ulimwengu unatuchukia.

^ fu. 1 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 58 MAELEZO YA PICHA: Kisha maaskari kuogopesha Danylo, ndugu walimusaidia yeye na bibi yake wahame mu muji ingine, na kule, ndugu walimukaribisha kwa furaha.

^ fu. 60 MAELEZO YA PICHA: Bwana ya Yasmeen alikuwa anamupinga lakini wazee walimupatia Yasmeen mashauri ya muzuri. Yasmeen alionyesha kama alikuwa bibi muzuri na alimuhangaikia bwana yake wakati aligonjwa.