Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Katika tafsiri ya sasa ya mwaka wa 2013 ya “Biblia Takatifu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya,” Zaburi 144:12-15 inazungumuzia watu wa Mungu. Katika tafsiri ya zamani ilizungumuzia wageni wabaya wenye kutajwa kwenye mustari wa 11. Sababu gani maneno hayo yalirekebishwa?

Maneno ya Kiebrania ya zaburi hiyo yanaweza kutafsiriwa katika njia hizo mbili. Kwa hiyo, maneno yenye kutumiwa katika tafsiri ya sasa, yanategemea sababu zenye kufuata:

  1. Maneno yenye kuwa katika tafsiri ya sasa yanategemea maana ya maneno na grama ao sarufi. Neno lenye kuunganisha Zaburi 144:12-15 na mustari wenye kutangulia, linategemea maana yenye neno la kwanza katika mustari wa 12 linapewa, ni neno la Kiebrania asher. Neno asher linaweza kutafsiriwa katika njia mbalimbali. Kwa mufano, linaweza kuelewaka kuwa neno lenye kutumiwa ili kuonyesha mutu mwenye kuzungumuziwa, neno kama vile “mwenye” ao “wenye.” Neno hilo lilipewa maana ya “wenye” katika tafsiri ya zamani. Kwa hiyo, vitu vizuri vyenye kutajwa katika mustari wa 12 mupaka wa 14 vilihusu waovu wenye walitajwa katika mustari wenye kutangulia. Lakini, neno asher linaweza pia kuonyesha matokeo na linaweza kutafsiriwa “kwa hiyo,” “ili,” ao “halafu.” Tafsiri ya sasa ya mwaka wa 2013 inatumia neno “halafu” na tafsiri zingine za Biblia zinafanya hivyo pia.

  2. Namna inatafsiriwa katika tafsiri ya sasa inapatana kabisa na mistari ingine yote ya zaburi hiyo. Kutumia neno “halafu” katika mustari wa 12 kunamaanisha kwamba inaeleweka kama baraka zenye kufuata katika mustari wa 12 mupaka 14 zinahusu watu wenye haki, ni kusema, wale wenye wanaomba ‘kuwekwa huru na kukombolewa’ kutoka kwa waovu (mustari wa 11). Badiliko hilo linaonekana pia kwenye mustari wa 15 kwenye neno “furaha” linapatikana mara mbili na linapatana sasa katika njia ya muzuri. Kwa hiyo, nafasi hizo zote furaha hiyo inahusu watu walewale, ni kusema, wale “ambao Mungu wao ni Yehova!” Ukumbuke kama, maandishi ya zamani ya Kiebrania hayakuwa na alama za maandishi kama vile alama za kunukuu ao zenye kuonyesha maneno yenye mutu fulani alisema. Kwa hiyo, watafsiri wanapaswa kutafuta maana ya kweli ya maneno hayo, kwa kufikiria namna ya kuandika kwa njia ya shairi (poeme) katika Kiebrania, habari yenye kuzungumuziwa, na maandiko mengine ya Biblia yenye kuzungumuzia habari hiyo.

  3. Namna tafsiri ya sasa imetafsiri zaburi hiyo inapatana na maandiko mengine ya Biblia yenye kuzungumuzia baraka zenye Mungu anaahidi watu wake waaminifu. Kwa sababu ya marekebisho ya kutafsiri neno asher, sasa zaburi hiyo inaonyesha muzuri tumaini la musingi lenye Daudi alikuwa nalo kwamba kisha Mungu kukomboa taifa la Israeli kutoka katika mikono ya maadui wao, angebariki watu wake kwa kuwapatia furaha na vitu vingi vya muzuri. (Law. 26:9, 10; Kum. 7:13; Zab. 128:1-6) Kwa mufano, andiko la Kumbukumbu la Torati 28:4 linasema hivi: ‘Utabarikiwa uzao wa tumbo lako na mazao ya udongo wako na uzao wa munyama wako wa kufugwa, mutoto wa ngombe wako na uzao wa kundi lako.’ Kwa kweli, wakati wa utawala wa Sulemani, mwana wa Daudi, taifa lilikuwa na amani na vitu vingi vya muzuri kuliko wakati mwingine wowote. Zaidi ya hilo, mambo mbalimbali ya utawala wa Sulemani yanaonyesha mambo yenye yatakuwa katika utawala wa Masiya wakati wenye kuja.​—1 Fal. 4:20, 21; Zab. 72:1-20.

Kwa kumalizia, namna Zaburi ya 144 imetafsiriwa sasa haibadilishe namna tunaelewa mafundisho ya Biblia. Lakini, inafanya zaburi hiyo yote ionyeshe waziwazi tumaini la muzuri lenye watumishi wa Yehova wamekuwa nalo kwa muda murefu, ni kusema, Mungu kuharibu watu wabaya na kuwatolea watu wenye haki amani na vitu vingi vya muzuri.​—Zab. 37:10, 11.