Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tutiane Moyo, Zaidi Sana Leo

Tutiane Moyo, Zaidi Sana Leo

‘Acheni tufikiriane . . . , tutiane moyo, na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri munavyoona siku ile kuwa inakaribia.’​—EBR. 10:24, 25.

NYIMBO: 90, 87

1. Sababu gani mutume Paulo aliomba Wakristo Waebrania watiane moyo “na kufanya hivyo zaidi”?

SABABU gani tunapaswa kujikaza zaidi kutia wengine moyo? Katika barua yake kwa Waebrania, mutume Paulo anatupatia sababu ya kufanya hivyo. Aliwaambia hivi: ‘Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe, kama vile wengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo, na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri munavyoona siku ile kuwa inakaribia.’ (Ebr. 10:24, 25) Kisha miaka tano tu, Wakristo Wayahudi wenye waliishi Yerusalemu wangeona “siku ya Yehova” inakaribia na kutambua alama yenye Yesu alikuwa amewapatia ili wakimbie kutoka katika muji huo na kuokoa uzima wao. (Mdo. 2:19, 20; Lu. 21:20-22) Siku hiyo ya Yehova ilifika katika mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wakati Waroma walileta hukumu ya Yehova juu ya Yerusalemu.

2. Sababu gani tunapaswa kufikiria zaidi juu ya kutiana moyo leo?

2 Leo, tuko na sababu za kuamini kama siku ‘kubwa na yenye kuogopesha sana’ ya Yehova iko karibu. (Yoe. 2:11) Nabii Sefania alisema hivi: ‘Ile siku kubwa ya Yehova iko karibu. Iko karibu, nayo inaharakisha sana!’ (Sef. 1:14) Onyo hilo la unabii linahusu pia siku zetu. Kwa sababu siku ya Yehova inakaribia, Paulo anatuambia “tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri.” (Ebr. 10:24) Kwa hiyo, tunapaswa kupendezwa zaidi na ndugu zetu ili tuweze kuwatia moyo wakati wowote wako lazima wa kutiwa moyo.

NI NANI WENYE KUWA NA LAZIMA YA KUTIWA MOYO?

3. Mutume Paulo alisema nini juu ya kutia wengine moyo? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

3 ‘Hangaiko katika moyo wa mutu linaufanya uiname, lakini neno njema linaufanya ushangilie.’ (Met. 12:25) Maneno hayo ni ya kweli kabisa. Sisi wote tuko na lazima ya kutiwa moyo mara kwa mara. Paulo alionyesha kama hata ule mwenye kuwa na daraka la kutia wengine moyo, yeye pia iko na lazima ya kutiwa moyo. Aliandikia hivi Wakristo wenye walikuwa wanaishi Roma: ‘Ninatamani kuwaona ninyi, ili niwape sehemu ya zawadi ya kiroho kusudi mufanywe imara; ao, badala ya hivyo, kwamba kuwe na ubadilishanaji wa kitia-moyo kati yenu, kila mumoja kupitia imani ya mwingine, yenu na yangu pia.’ (Rom. 1:11, 12) Kwa kweli, Paulo mwenye alitia sana wengine moyo, yeye pia alikuwa na lazima ya kutiwa moyo wakati fulani.​—Soma Waroma 15:30-32.

4, 5. Ni nani wenye tunaweza kutia moyo leo, na sababu gani?

4 Wale wenye kuishi maisha ya kujitoa wanastahili kupongezwa. Kati yao kuko mapainia waaminifu. Wengi wao wamejinyima mambo mengi katika maisha yao ili waweze kufanya kazi ya upainia. Ni hivyo pia juu ya wamisionere, waangalizi wa muzunguko na bibi zao, na wale wenye kutumika kwenye biro za tawi ao biro za kutafsiri. Watu hao wote wanajinyima mambo fulani katika maisha yao ili waweze kutumia wakati mwingi zaidi katika utumishi mutakatifu. Kwa hiyo, wanastahili kutiwa moyo. Na wale wenye zamani walikuwa katika utumishi wa wakati wote na wangali na hamu ya kufanya utumishi huo, lakini hawawezi kuufanya kwa sababu fulani, wanafurahi pia wakati wanatiwa moyo.

5 Ndugu na dada wenye wanabakia bila kuoa ao kuolewa kwa sababu wanapenda kutii sheria ya kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu,” wanastahili pia kutiwa moyo. (1 Kor. 7:39) Vilevile, bibi wenye kutumika kwa bidii wanafurahi wakati bwana zao wanawaambia maneno yenye kutia moyo. (Met. 31:28, 31) Pia, Wakristo wenye wanabakia waaminifu hata kama wanapatwa na mateso ao wanapambana na magonjwa wanastahili kutiwa moyo. (2 Tes. 1:3-5) Yehova na Yesu wanatia moyo watumishi hao wote waaminifu.​—Soma 2 Wathesalonike 2:16, 17.

WAZEE WANAJIKAZA KUTIA WENGINE MOYO

6. Wazee wako na daraka gani kama vile Isaya 32:1, 2 inaonyesha?

6 Soma Isaya 32:1, 2. Kupitia ndugu watiwa mafuta na ‘wakubwa’ wenye kuwaunga mukono, ni kusema, wazee wa kutaniko wenye kuwa sehemu ya kondoo wengine, Yesu Kristo anatia moyo na kutolea muongozo wale wenye kuwa na huzuni na wenye kuvunjika moyo katika wakati huu wenye tuko na lazima ya musaada. Wazee hao hawako “mabwana” juu ya imani ya wengine lakini ni “wafanyakazi wenzi” kwa ajili ya furaha ya ndugu zao.​—2 Kor. 1:24.

7, 8. Zaidi ya kutia wengine moyo kwa maneno, namna gani wazee wanaweza kujenga wengine?

7 Mutume Paulo alituwekea mufano wenye tunapaswa kuiga. Aliandikia hivi Wakristo wa Thesalonike wenye walikuwa wanateswa: ‘Tukiwa na upendo mwororo kwa ajili yenu, tulipendezwa vema kuwapa ninyi, si habari njema ya Mungu tu, bali pia nafsi zetu wenyewe, kwa sababu ninyi mulikuwa wapendwa kwetu.’​—1 Tes. 2:8.

8 Ili kuonyesha kama haitoshe tu kusema neno lenye kutia moyo, Paulo aliambia hivi wazee wa Efeso: “Ni lazima muwasaidie wale walio zaifu, na lazima muyakumbuke maneno ya Bwana Yesu, aliposema, ‘Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.’” (Mdo. 20:35) Zaidi ya kutia moyo ndugu zake, Paulo alikuwa tayari ‘kutumiwa kabisa kwa ajili’ yao. Paulo alionyesha kupitia matendo yake kama alikuwa tayari kufanya jambo lolote kwa ajili yao. (2 Kor. 12:15) Vilevile, wazee hawapaswe tu kutia moyo na kufariji ndugu zao kwa maneno, lakini pia wanapaswa kufanya hivyo kupitia matendo yao na kuonyesha kama wanapendezwa kabisa nao.​—1 Kor. 14:3.

9. Namna gani wazee wanaweza kutoa mashauri kwa njia yenye kutia moyo?

9 Kutia wengine moyo kunaweza kutia ndani kuwatolea mashauri, lakini wakati wanafanya hivyo pia, wazee wanapaswa kuiga mufano wenye kuwa katika Biblia juu ya namna ya kutoa mashauri kwa njia yenye kutia moyo. Yesu alionyesha mufano muzuri zaidi wa kufanya hivyo kisha kufa na kufufuliwa kwake. Alikuwa na mashauri mazito ya kutolea makutaniko fulani katika Asia Ndogo; lakini alifanya hivyo namna gani? Mbele ya kutoa mashauri, alipongeza kwanza makutaniko ya Efeso, Pergamamu, na Thiatira. (Ufu. 2:1-5, 12, 13, 18, 19) Aliambia hivi kutaniko la Laodikia: ‘Wale wote ninaowapenda, mimi ninawakaripia na kuwatia nizamu. Kwa hiyo ukuwe mwenye bidii na utubu.’ (Ufu. 3:19) Wazee wanapaswa kuiga mufano wa Kristo wakati wanataka kutoa mashauri.

KUTIA WENGINE MOYO HAIKO DARAKA LA WAZEE TU

Wazazi, munazoeza watoto wenu watie wengine moyo? (Picha hizi zinapatana na fungu la 10)

10. Namna gani sisi wote tunaweza kujengana?

10 Haiko wazee tu ndio wako na daraka la kutia wengine moyo. Paulo alitia moyo Wakristo wote waseme ‘neno lolote ambalo ni njema kwa ajili ya kujenga kulingana na uhitaji ili liwape wasikiaji lile linalofaa.’ (Efe. 4:29) Kila mumoja wetu anapaswa kuwa muangalifu ili kuona “uhitaji” wa wengine. Paulo alishauria Wakristo Waebrania hivi: ‘Munyooshe mikono inayolegea na magoti yaliyo zaifu nanyi muendelee kuifanyia miguu yenu mapito yaliyonyooka, ili kile ambacho ni kilemavu kisiteguliwe, bali afazali kiponywe.’ (Ebr. 12:12, 13) Sisi wote, kutia ndani vijana, tunaweza kujengana kwa maneno yenye kutia moyo.

11. Namna gani Marthe alisaidiwa wakati alikuwa ameshuka moyo?

11 Marthe, dada mumoja mwenye alishuka moyo kwa kipindi fulani, anaandika hivi: “Siku moja kisha kusali ili nitiwe moyo, siku hiyohiyo nilikutana na dada mumoja mwenye kukomaa mwenye alinionyesha upendo na huruma, wenye nilikuwa nao lazima kabisa wakati huo. Alinielezea pia mambo yenye yalimufikia yenye kufanana na jaribu lenye nilikuwa ninapambana nalo, na sikujisikia tena kuwa peke yangu.” Pengine, dada huyo mwenye kukomaa hakutambua namna maneno yake yangetia moyo sana Marthe.

12, 13. Ni katika njia gani zenye kufaa tunaweza kutumikisha shauri lenye kupatikana kwenye Wafilipi 2:1-4?

12 Paulo alitolea ndugu wote wa kutaniko la Filipi shauri hili: ‘Basi, ikiwa kuna kitia-moyo chochote katika Kristo, kukiwa na faraja yoyote ya upendo, kukiwa na ushirika wowote wa roho, kukiwa na upendo mwororo na huruma zozote, mufanye shangwe yangu ijae kwa kuwa muna akili ileile na muna upendo uleule, mukiunganishwa pamoja katika nafsi, mukishika wazo moja akilini. Bila kufanya jambo lolote kwa ugomvi au kwa kujisifu, bali kwa unyenyekevu wa akili mukiwaona wengine kuwa ni bora [wazuri zaidi] kuliko ninyi, mukiendelea kuangalia, si faida za kibinafsi za mambo yenu wenyewe tu, bali pia faida za kibinafsi za wengine.’​—Flp. 2:1-4.

13 Kwa kweli, sisi wote tunapaswa kujikaza kutafuta faida za ndugu na dada zetu kwa kuwatolea “faraja yoyote ya upendo,” “ushirika wowote wa roho,” na “upendo mwororo na huruma zozote” ili kuwatia moyo.

MAMBO YENYE KUTIA MOYO

14. Ni jambo gani lenye linaweza kutia mutu moyo?

14 Kusikia kama wale wenye tulisaidia zamani wanaendelea kuwa waaminifu kunaweza kututia moyo kabisa, kama vile mutume Yohana alitiwa moyo. Aliandika hivi: “Sina sababu nyingine kubwa zaidi ya kuwa na shukrani kuliko mambo haya, kwamba niwe nikisikia watoto wangu wanaendelea kutembea katika kweli.” (3 Yoh. 4) Mapainia wengi wanaweza kushuhudia namna inatia moyo sana kusikia kama watu fulani wenye walisaidia kujua kweli zamani, wanaendelea kuwa waaminifu na pengine wanafanya pia kazi ya upainia. Kukumbusha tu painia mwenye amevunjika moyo mambo yenye alifanya zamani ili kusaidia wengine, kunaweza kumufariji.

15. Ni katika njia gani moja tunaweza kutia moyo wale wenye kutumika kwa uaminifu?

15 Waangalizi wengi wamesema namna wao na bibi zao wanatiwa moyo sana wakati kutaniko lenye walitembelea linawatumia hata barua fupi ili kuwashukuru. Wazee, wamisionere, mapainia, na ndugu na dada wa familia ya Beteli wanafurahi pia wakati tunawashukuru juu ya kazi yao ya uaminifu.

NAMNA SISI WOTE TUNAWEZA KUTIA WENGINE MOYO

16. Inaomba nini ili kutia moyo mutu fulani?

16 Inaweza kuwa makosa kufikiri kama hatuwezi kutia wengine moyo kwa sababu hatuzoee kabisa kuzungumuza na wengine. Haiombe mambo mengi ili kutia wengine moyo, pengine tunaweza tu kuonyesha sura ya kicheko wakati tunasalimia mutu. Ikiwa mutu huyo hatuonyeshe sura ya kicheko, hilo linaweza kumaanisha kama pengine iko na tatizo fulani, na kumusikiliza kunaweza kumufariji.​—Yak. 1:19.

17. Namna gani ndugu mumoja kijana alisaidiwa wakati wa magumu?

17 Henri, ndugu kijana, alihuzunika sana wakati watu wa familia yake, waliacha kweli, kutia ndani baba yake mwenye alikuwa muzee mwenye kuheshimiwa. Mwangalizi mumoja wa muzunguko alimutia Henri moyo wakati alimupeleka nafasi ya kuuzia vyakula vidogo-vidogo na akamuuzia kahawa na kumuacha afungue moyo wake. Kisha mazungumuzo hayo, Henri alitambua kama ili kusaidia watu wa familia yake warudie katika kweli, alipaswa kubakia muaminifu. Alitiwa moyo wakati alisoma Zaburi ya 46; Sefania 3:17; na Marko 10:29, 30.

Sisi wote tunaweza kujengana na kutiana moyo (Picha hizi zinapatana na fungu la 10)

18. (a) Mufalme Sulemani aliandika nini juu ya kutiana moyo? (b) Mutume Paulo alitoa shauri gani?

18 Mufano wa Marthe na Henri unaonyesha kama tunaweza kutia moyo ndugu ao dada mwenye kuwa na lazima ya faraja. Mufalme Sulemani aliandika hivi: ‘Neno linalosemwa wakati unaofaa ni njema kama nini! Kungaa kwa macho kunafanya moyo ushangilie; habari ambayo ni njema inaifanya mifupa inone.’ (Met. 15:23, 30) Zaidi ya hilo, kusomea mutu fulani mwenye kuvunjika moyo habari fulani katika gazeti Munara wa Mulinzi ao kwenye site yetu ya Internete kunaweza kumutia nguvu. Paulo anaonyesha kama kuimba pamoja nyimbo za Ufalme kunaweza kututia moyo. Aliandika hivi: ‘Muendelee kufundishana na kuonyana [ao, “kutiana moyo”] kwa zaburi, sifa kwa Mungu, nyimbo za kiroho kwa neema, mukimuimbia Yehova mioyoni mwenu.’​—Kol. 3:16; Mdo. 16:25.

19. Sababu gani hivi karibuni itakuwa jambo la maana sana kutiana moyo, na tunapaswa kufanya nini?

19 Itakuwa jambo la maana sana kutiana moyo kadiri tunaona kuwa siku ya Yehova “inakaribia.” (Ebr. 10:25) Kama vile Paulo aliambia Wakristo wenzake wa wakati wake, ‘muendelee kufarijiana na kujengana, kama vile munavyofanya.’​—1 Tes. 5:11.

Majina yamebadilishwa.