Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kupata Uhuru wa Kweli

Namna ya Kupata Uhuru wa Kweli

‘Mwana akiwaweka ninyi huru, kwa kweli mutakuwa huru.’​—YOH. 8:36.

NYIMBO: 54, 36

1, 2. (a) Ni nini inaonyesha kama watu wanajikaza sana ili kupata uhuru? (b) Hilo limeleta matokeo gani?

LEO, watu wanazungumuza sana juu ya kutendewa kwa usawa na kuwa huru. Watu katika maeneo mengi ya dunia wanataka kuwa huru kutoka katika mateso, ubaguzi, na umaskini. Wengine wanaomba wakuwe na uhuru wa kusema, wa kuchagua, na wa kuishi namna wanataka. Inaonekana kama kila mahali watu wengi wanapenda kufanya mambo yenye wanapenda na kuishi namna wanapenda.

2 Lakini, watu wanatumia njia zenye hazifae ili kutimiza tamaa hizo. Wanafanya maandamano, wanapinga mambo yenye kufanyika, wanaasi, na hata kupenda kuleta mabadiliko. Lakini, mambo hayo yanaleta matokeo yenye watu wanapenda kupata? Hapana. Mara nyingi yanaleta mateso na kifo. Mambo hayo yote yanaonyesha tena kama maneno yenye Mufalme Sulemani aliandika kwa uongozi wa roho ya Mungu ni ya kweli; aliandika hivi: ‘Mwanadamu amemutawala mwanadamu kwa kumuumiza.’​—Mhu. 8:9.

3. Tunaweza kufanya nini ili tupate furaha na kutosheka?

3 Yakobo, mwanafunzi Mukristo, alionyesha siri ya kupata furaha ya kweli na kutosheka. Aliandika hivi: ‘Yeye anayechunguza ndani ya sheria kamilifu iliyo ya uhuru na ambaye anadumu [anaendelea] katika hiyo . . . atakuwa mwenye furaha katika kuitenda.’ (Yak. 1:25) Yehova mwenye alitutolea sheria hiyo kamilifu, anajua muzuri zaidi mambo yenye wanadamu wako nayo lazima ili wakuwe na furaha na kutosheka kabisa. Alipatia bibi na bwana wa kwanza, ni kusema, Adamu na Eva, mambo yote yenye walikuwa nayo lazima ili wakuwe na furaha; kutia ndani uhuru wa kweli.

WAKATI WANADAMU WALIKUWA NA UHURU WA KWELI

4. Adamu na Eva walifurahia uhuru gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

4 Wakati tunasoma sura mbili za kwanza za kitabu cha Mwanzo, tunaona wazi kama Adamu na Eva walikuwa na uhuru wenye watu wengi leo wanapenda kupata; walikuwa na vitu vyote vyenye walikuwa navyo lazima, hawakuogopa jambo lolote, na hakuna mutu mwenye aliwatendea bila haki. Hawakuhangaika juu ya chakula, kazi, magonjwa, na kifo. (Mwa. 1:27-29; 2:8, 9, 15) Hilo linamaanisha kama uhuru wenye Adamu na Eva walikuwa nao haukukuwa na mipaka? Acha tuone.

5. Tofauti na mawazo ya watu wengi, inaomba nini ili watu wakuwe na uhuru?

5 Watu wengi leo wanafikiri kama ili wakuwe na uhuru wa kweli, wanapaswa kufanya jambo lolote na mambo yote yenye wanapenda, hata iwe watapata matokeo gani. Kitabu kimoja kinasema kama uhuru ni “uwezo wa kukamata maamuzi na kuyatimiza.” (The World Book Encyclopedia) Lakini, kinaongezea pia kama watu wako na uhuru ikiwa serikali haiwatilie mipaka yenye haiko ya haki, yenye haiko ya lazima, na yenye haina usawaziko. Hilo linamaanisha kama mipaka fulani ni ya lazima ili kila mutu afaidike na uhuru wenye amepewa. Lakini, tunaweza kujiuliza hivi: Ni nani mwenye kuwa na haki ya kuamua ikiwa mipaka fulani ni yenye haki, ya lazima, na yenye usawaziko?

6. (a) Sababu gani Yehova tu ndiye mwenye kuwa na uhuru wenye hauna mipaka? (b) Wanadamu wanaweza kuwa na uhuru wa namna gani, na sababu gani?

6 Kuhusu uhuru, ni jambo la maana tukumbuke kama Yehova Mungu tu ndiye mwenye kuwa na uhuru kamili na wenye hauna mipaka. Sababu gani? Kwa sababu yeye ni Muumbaji wa vitu vyote, na mweza yote mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi katika ulimwengu wote. (1 Tim. 1:17; Ufu. 4:11) Kumbuka maneno ya muzuri yenye Mufalme Daudi alisema wakati alikuwa anaeleza mamlaka makubwa zaidi yenye Yehova mwenyewe iko nayo. (Soma 1 Mambo ya Nyakati 29:11, 12.) Kwa hiyo, viumbe vyote mbinguni na duniani wako na uhuru wenye kuwa na mipaka. Wanapaswa kuelewa kama Yehova Mungu iko na mamlaka kamili ya kuamua mambo yenye kuwa haki, ya lazima, na yenye usawaziko. Kwa kweli, kuanzia mwanzo Yehova Mungu aliwekea mipaka wanadamu wenye alikuwa ameumba.

7. Ni mambo gani fulani ya kawaida yenye kutuletea furaha?

7 Hata kama mwanzoni Adamu na Eva walifurahia uhuru katika njia mbalimbali, uhuru wao ulikuwa na mipaka. Mipaka fulani ilikuwa ya kawaida. Kwa mufano, wazazi wetu wa kwanza walijua kama ili waendelee kuishi walipaswa kupumua, kula, kulala, na kufanya mambo mengine. Wangejisikia kama hawana uhuru kwa sababu walipaswa kufanya mambo hayo? Hapana. Yehova alihakikisha kama wanapata furaha na kutosheka hata wakati wanafanya mambo ya kawaida kama hayo. (Zab. 104:14, 15; Mhu. 3:12, 13) Kwa kweli, sisi wote tunafurahia kupumua hewa safi, kula chakula chenye tunapendaka, na kulala usiku ili kupumuzika. Tunafurahia kufanya mambo hayo ya lazima bila kujisikia hata kidogo kama tunalazimishwa ao kuwa ni muzigo kwetu. Kwa kweli, Adamu na Eva walifurahia pia kufanya mambo hayo.

8. Mungu alipatia wazazi wetu wa kwanza amri gani, na sababu gani?

8 Yehova alipatia Adamu na Eva amri yenye kuwa wazi ya kujaza dunia na kuitunza. (Mwa. 1:28) Je, amri hiyo iliwanyima uhuru kwa njia fulani? Hapana kabisa! Walipewa amri hiyo ili wanadamu waweze pia kuchangia katika kutimizwa kwa kusudi la Muumbaji wao, ni kusema, kufanya dunia yote ikuwe paradiso na makao ya milele ya wanadamu wakamilifu. (Isa. 45:18) Leo watu hawavunje amri ya Mungu wakati wanaamua kubakia bila kufunga ndoa ao kubakia bila kuzaa watoto katika ndoa. Hata hivyo, watu wengi zaidi wanafunga ndoa na wanakomalisha watoto hata kama wanajua kwamba haiko vyepesi kufanya hivyo. (1 Kor. 7:36-38) Sababu gani? Kwa sababu watu wanatazamia kupata furaha na kutosheka wakati wanafanya hivyo. (Zab. 127:3) Katika maisha yao, Adamu na Eva wangepata baraka ya kufurahia milele ndoa yao na familia yao.

NAMNA UHURU WA KWELI ULIPOTEA

9. Sababu gani amri ya Mungu yenye kuwa katika Mwanzo 2:17 ilikuwa yenye haki, ya lazima, na yenye usawaziko?

9 Yehova alipatia Adamu na Eva amri ingine, na aliwaambia waziwazi malipizi yenye wangepata ikiwa wangeivunja. Aliwaambia hivi: ‘Kuhusu matunda ya muti wa ujuzi wa mema na mabaya usikule, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika.’ (Mwa. 2:17) Amri hiyo ilikosa haki kwa njia fulani, haikukuwa ya lazima ao ilikuwa yenye kukosa usawaziko? Ilinyima Adamu na Eva uhuru? Hapana kabisa. Kwa kweli, watu fulani wenye kuwa na elimu ya Biblia wanatoa maelezo yenye kuonyesha kama amri hiyo ilikuwa yenye hekima na yenye kupatana na akili. Kwa mufano, mutu mumoja mwenye elimu anasema hivi: “Kwa kifupi amri za Mungu zenye kuwa katika [Mwanzo 2:16, 17] zinaonyesha kama Mungu tu ndiye anajua mambo yenye kuwa mema . . . kwa ajili ya wanadamu na Mungu tu ndiye anajua mambo yenye haiko mema . . . kwao. Ili wafurahie ‘mema,’ wanadamu wanapaswa kumutumainia Mungu na kumutii. Ikiwa wanakataa kumutii, wataachwa ili waamue wao wenyewe mambo yenye kuwa mema . . . na yenye haiko mema.” Huo ni muzigo wenye wanadamu hawangeweza kubeba kwa nguvu zao wenyewe.

Uamuzi wa Adamu na Eva ulileta matokeo ya mubaya sana! (Picha hizi zinapatana na fungu la 9-12)

10. Sababu gani kuko tofauti kati ya uhuru wa kuchagua na haki ya kuamua mema na mabaya?

10 Kisha tu kusoma amri yenye Mungu alimupatia Adamu, watu wengi wanaweza kusema kama Adamu hakupewa uhuru wa kufanya mambo yenye alipenda. Wakati wanasema hivyo wanasahau kama kuko tofauti kati ya kuwa na uhuru wa kuchagua na kuwa na haki ya kuamua mema na mabaya. Adamu na Eva walikuwa na uhuru wa kuamua ikiwa wangemutii Mungu ao hapana. Lakini, ni Yehova tu ndiye mwenye kuwa na haki yenye kuwa kamili ya kuamua mambo yenye kuwa mema na yenye kuwa mabaya. ‘Muti wa ujuzi wa mema na mabaya’ wenye ulikuwa katika bustani ya Edeni ulimaanisha jambo hilo. (Mwa. 2:9) Tunapaswa kukubali kama hatuwezi kujua sikuzote ikiwa maamuzi yetu yatakuwa na matokeo gani; na hatuwezi kujua ikiwa matokeo yatakuwa ya muzuri kila wakati. Ndiyo sababu mara nyingi tunaona watu wanakamata maamuzi wakiwa na nia ya muzuri, lakini wanapata matokeo ya mubaya, wanapata mateso, musiba, ao magumu. (Met. 14:12) Kwa kweli, wanadamu wako na mipaka katika mambo yenye wanaweza kufanya. Kupitia amri yake, Yehova alifundisha Adamu na Eva kwa upendo kama wangekuwa na uhuru wa kweli ikiwa wangemutii. Alifanya hivyo namna gani, na Adamu na Eva walifanya nini?

11, 12. Sababu gani uamuzi wa Adamu na Eva ulileta matokeo ya mubaya sana? Toa mufano.

11 Wazazi wetu wa kwanza waliamua kukosa kumutii Mungu. Eva alimusikiliza Shetani wakati alimujaribu kwa kumupatia ahadi hii: ‘Macho yenu yatafunguliwa, nanyi mutakuwa kama Mungu, mukijua mema na mabaya.’ (Mwa. 3:5) Uamuzi wenye Adamu na Eva walikamata ulifanya wakuwe na uhuru zaidi? Hapana kabisa. Uamuzi wao haukuwaletea mambo yenye Shetani alisema. Kwa kweli, bila kukawia walielewa kama kukataa muongozo wa Yehova na kufuata njia yao wenyewe kunaleta matokeo ya mubaya sana. (Mwa. 3:16-19) Sababu gani? Kwa sababu Yehova hakupatia wanadamu uwezo wa kujiamulia mema na mabaya.​—Soma Methali 20:24; Yeremia 10:23.

12 Mufano wa pilote mwenye kuendesha ndege (avion) unaweza kutusaidia kuelewa jambo hilo. Ili afike salama mahali penye anaenda, anapaswa kufuata njia yenye kukubaliwa tayari yenye ndege inapaswa kufuata. Anapaswa kutumia vyombo vya sasa vyenye kuwa katika ndege na kuendelea kuzungumuza na watu wenye kuwa chini wenye kuongoza ndege ili afike salama. Lakini, ikiwa pilote anaamua kama hatafuata muongozo huo, na kufuata njia yoyote yenye anapenda, matokeo yanaweza kuwa ya mubaya. Kama pilote huyo, Adamu na Eva walipenda kufanya mambo namna wanapenda. Walikataa muongozo wenye Mungu aliwatolea. Matokeo yalikuwa nini? Ni kama vile walifanya aksidenti ya mubaya sana ya ndege, jambo hilo liliwaletea zambi na kifo wao wenyewe na wazao wao wenye wangezaliwa wakati wenye kuja. (Rom. 5:12) Kwa sababu walijaribu kujiongoza wao wenyewe, walipoteza uhuru wa kweli wenye walikuwa wamepewa.

NAMNA YA KUPATA UHURU WA KWELI

13, 14. Namna gani tunaweza kupata uhuru wa kweli?

13 Watu fulani wanafikiri kama wanaweza kuwa na maisha ya muzuri zaidi ikiwa wako na uhuru wenye hauna mipaka, lakini ukweli ni kwamba uhuru huo ni kama kisu chenye kuwa na makali ngambo mbili. Ni kweli kwamba uhuru unaleta faida nyingi; lakini tunaogopa wakati tunawazia namna dunia ingekuwa ikiwa hakungekuwa mipaka yoyote. Ndiyo sababu kitabu kimoja kinasema hivi: “Sheria za kila kikundi cha watu chenye kupangwa ni ngumu kwa sababu zinapaswa kulinda watu na wakati huohuo kuwekea uhuru wao mipaka.” (The World Book Encyclopedia) Kwa kweli, zinastahili kuitwa hivyo. Fikiria tu vitabu vingi sana vya sheria vyenye wanadamu wameandika, na hesabu kubwa ya wanasheria na waamuzi wenye wanapaswa kuzielewa muzuri na kufanya ziheshimiwe.

14 Lakini, Yesu alionyesha njia ya mwepesi ya kuwa na uhuru wa kweli. Alisema hivi: ‘Mukikaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, nanyi mutaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.’ (Yoh. 8:31, 32) Maneno ya Yesu yanaonyesha kama ili kupata uhuru wa kweli inaomba kufanya mambo mbili: Kwanza, kukubali kweli yenye alifundisha, na pili, kuwa mwanafunzi wake. Ikiwa tunafanya hivyo tutapata uhuru wa kweli. Lakini, tutapata uhuru kutoka katika mambo gani? Yesu alieleza tena hivi: ‘Kila mutendaji wa zambi ni mutumwa wa zambi. . . . Mwana akiwaweka ninyi huru, mutakuwa huru kwelikweli.’​—Yoh. 8:34, 36.

15. Sababu gani uhuru wenye Yesu aliahidi unaweza kutuweka “huru kwelikweli”?

15 Ni wazi kwamba uhuru wenye Yesu aliahidi wanafunzi wake ni wa hali ya juu kuliko uhuru wenye watu wengi sana wanatafuta leo. Wakati Yesu alisema, ‘Mwana akiwaweka ninyi huru, mutakuwa huru kwelikweli,’ alikuwa anazungumuzia uhuru kutoka katika utumwa mukubwa zaidi wenye wanadamu wamepambana nao, ni kusema, kuwa ‘watumwa wa zambi.’ Zambi inatuchochea kufanya mambo mabaya na inatuzuia pia kufanya mambo yenye tunajua kuwa ni sawa ao kuishi kulingana na mambo yenye tunajua kama tuko na uwezo wa kufanya. Katika njia hiyo tuko watumwa wa zambi, na utumwa huo unaleta huzuni, maumivu, mateso, na mwishowe kifo. (Rom. 6:23) Mutume Paulo alisikia sana maumivu hayo katika moyo wake. (Soma Waroma 7:21-25.) Tutakuwa na uhuru wa kweli wenye wazazi wetu wa kwanza walikuwa nao wakati tu tutawekwa huru kutoka katika utumwa wa zambi.

16. Namna gani tunaweza kuwa huru kabisa?

16 Yesu alisema hivi: ‘Mukikaa katika neno langu.’ Maneno hayo ya Yesu yanaonyesha kama kuko mambo fulani ao mipaka fulani yenye inaombwa ili atuweke huru. Kwa sababu tuko Wakristo wenye kujitoa kwa Mungu tumejikana wenyewe na tumeamua kuishi kulingana na mipaka ya mafundisho ya Kristo. (Mt. 16:24) Kama vile Yesu aliahidi, tutakuwa huru kabisa wakati tutapata faida za zabihu yake ya ukombozi.

17. (a) Ni nini itafanya maisha yetu yakuwe na kusudi la kweli na kutosheka? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

17 Wakati sisi wanafunzi wa Yesu tunatii mafundisho yake, hilo linafanya maisha yetu yakuwe na kusudi la kweli na kutosheka. Na hilo linatupatia tumaini la kuwekwa huru kabisa kutoka katika utumwa wa zambi na kifo. (Soma Waroma 8:1, 2, 20, 21.) Katika habari yenye kufuata tutazungumuzia namna tunaweza kutumia kwa hekima uhuru wenye tuko nao leo ili kumutukuza milele Yehova, Mungu wa uhuru wa kweli.