Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Umutumikie Yehova, Mungu wa Uhuru

Umutumikie Yehova, Mungu wa Uhuru

“Mahali palipo na roho ya Yehova, pana uhuru.” ​—2 KOR. 3:17.

NYIMBO: 49, 73

1, 2. (a) Sababu gani watu wa wakati wa Paulo walikuwa wanazungumuza sana juu ya utumwa na uhuru? (b) Paulo alisema kama ni nani mwenye kuwa Chanzo cha uhuru wa kweli?

WAKRISTO waliishi kati ya watu wa Roma wenye walijisifu kwamba wanajua sheria, ni wenye haki, na wako na uhuru. Lakini, Utawala wa Roma ulipata nguvu na utukufu mwingi kwa sababu watumwa ndio walifanya kazi ngumu. Wakati fulani, katika Utawala wa Roma, mutu mumoja kati ya watu tatu alikuwa mutumwa. Kwa kweli, watu wa kawaida, na hata Wakristo, walikuwa wanazungumuza sana juu ya utumwa na uhuru.

2 Barua za mutume Paulo zinaeleza mambo mengi juu ya uhuru. Lakini kusudi la utumishi wake halikukuwa kubadilisha hali ya maisha ya watu ao kufanya mabadiliko ya politike, jambo lenye watu wa wakati huo walikuwa wanatafuta. Kuliko kutegemea kiongozi yeyote mwanadamu ao kikundi fulani cha watu ili kupata uhuru, Paulo na Wakristo wenzake walijikaza sana ili kusaidia wengine wajifunze juu ya habari njema ya Ufalme wa Mungu na faida ya bei sana ya zabihu ya ukombozi ya Kristo Yesu. Paulo aliambia Wakristo wenzake ni nani mwenye kuwa Chanzo cha uhuru wa kweli. Kwa mufano, katika barua yake ya pili kwa Wakristo Wakorintho, alisema hivi waziwazi: “Yehova ndiye Roho; na mahali palipo na roho ya Yehova, pana uhuru.”​—2 Kor. 3:17.

3, 4. (a) Sababu gani Paulo alisema maneno yenye kupatikana kwenye 2 Wakorintho 3:17? (b) Tunapaswa kufanya nini ili tukuwe na uhuru wenye kutoka kwa Yehova?

3 Katika barua hiyo yenye aliandikia Wakorintho, Paulo alikuwa amezungumuzia juu ya utukufu wa Musa wakati alishuka kutoka kwenye Mulima Sinai, kisha kuwa mbele za malaika wa Yehova. Kisha tu kuona Musa, watu waliogopa na Musa aliweka utaji ao kitambaa kwenye sura yake. (Kut. 34:29, 30, 33; 2 Kor. 3:7, 13) Paulo alifasiria hivi: ‘Lakini kunapokuwa na tendo la kugeuka kumuelekea Yehova, utaji unaondolewa mbali.’ (2 Kor. 3:16) Maneno ya Paulo yanamaanisha nini?

4 Kama vile tulijifunza katika habari yenye ilitangulia, Yehova Muumbaji wa vitu vyote, ndiye tu mwenye kuwa na uhuru kamili na wenye hauna mipaka. Kwa hiyo, inafaa kusema kama kwenye Yehova iko na “mahali palipo na roho ya Yehova,” kuko uhuru. Lakini, ili kufurahia uhuru huo na kupata faida, tunapaswa ‘kugeuka kumuelekea Yehova,’ ni kusema, kuwa na urafiki wa pekee pamoja naye. Waisraeli katika jangwa hawakuona kwa njia ya kiroho mambo yenye Yehova alikuwa anawatendea. Ni kama vile mioyo na akili zao zilikuwa zimefunikwa, walipenda kutumia uhuru wao mupya ili kutimiza tamaa zao wenyewe.​—Ebr. 3:8-10.

5. (a) Roho ya Yehova inatoa uhuru wa namna gani? (b) Namna gani tunajua kama mutu anaweza kuwa mutumwa ao katika gereza lakini anaendelea kuwa na uhuru wenye Yehova anatoa? (c) Tutajibia maulizo gani?

5 Lakini, uhuru wenye roho ya Yehova inatoa, ni zaidi ya kukombolewa kutoka katika utumwa wa kimwili. Unapita sana mambo yote yenye wanadamu wanaweza kutimiza. Roho ya Yehova inaweza kutuweka huru kutoka katika zambi na kifo, na pia kutoka katika utumwa wa ibada ya uwongo na desturi zake. (Rom. 6:23; 8:2) Uhuru huo ni wa ajabu kabisa! Mutu anaweza kupata faida za uhuru huo hata kama iko katika gereza ao katika utumwa. (Mwa. 39:20-23)Ni hivyo ilikuwa juu ya Dada Nancy Yuen na Ndugu Harold King, wenye walifungwa katika gereza kwa miaka mingi kwa sababu ya imani yao. Kwenye JW Télédiffusion, unaweza kuwaona na kusikia namna wanaeleza mambo yenye walipambana nayo. (Angalia chini ya kichwa KUULIZWA MAULIZO NA USHUHUDA> KUVUMILIA MAJARIBU.) Lakini, tunapaswa kufikiria juu ya maulizo haya: Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaona uhuru wetu kuwa jambo la maana? Na tunaweza kufanya nini ili kutumia uhuru huo kwa hekima?

TUONE UHURU WENYE MUNGU AMETUPATIA KUWA WA MAANA SANA

6. Namna gani Waisraeli walikosa shukrani juu ya uhuru wenye Yehova alikuwa amewapatia?

6 Wakati tunaelewa kama zawadi yenye tumepewa ni ya maana sana, tunachochewa kuonyesha shukrani kwa ule mwenye ametupatia zawadi hiyo. Waisraeli hawakuonyesha shukrani juu ya uhuru wenye Yehova aliwatolea wakati aliwakomboa kutoka katika utumwa wa Misri. Miezi fulani kisha kukombolewa, walianza kutamani chakula na vinywaji vyenye walikuwa navyo katika Misri na kunungunika juu ya mambo yenye Yehova alikuwa anawatolea, walipenda hata kurudia Misri. Wazia, namna waliweka pa nafasi ya kwanza ‘samaki, matango na matikiti-maji na vitunguu vya majani na vitunguu na vitunguu saumu’ kuliko uhuru wenye Mungu alikuwa amewapatia, uhuru wa kuabudu Mungu wa kweli Yehova. Ndiyo sababu Yehova aliwakasirikia sana. (Hes. 11:5, 6, 10; 14:3, 4) Mufano wao unapaswa kutufundisha jambo fulani!

7. Namna gani Paulo alitenda kulingana na shauri lake lenye kupatikana kwenye 2 Wakorintho 6:1, na namna gani tunaweza kumuiga?

7 Mutume Paulo alishauria Wakristo wote wasikose kuonyesha shukrani juu ya uhuru wenye Mungu amewapatia kwa upendo kupitia Mwana wake, Yesu Kristo. (Soma 2 Wakorintho 6:1.) Kumbuka namna Paulo alisumbuliwa sana na zamiri yake kwa sababu alikuwa anajisikia kama iko mutumwa wa zambi na kifo. Lakini, alisema maneno haya ya kushukuru: “Shukrani kwa Mungu kupitia Yesu Kristo Bwana wetu!” Sababu gani? Alifasiria Wakristo wenzake hivi: ‘Kwa maana sheria ya ile roho ambayo inatokeza uzima katika muungano na Kristo Yesu imewaweka ninyi huru kutoka katika sheria ya zambi na kifo.’ (Rom. 7:24, 25; 8:2) Kama Paulo, sisi pia tunapaswa kuwa wenye shukrani kwa sababu Yehova ametuweka huru kutoka katika utumwa wa zambi na kifo. Kupitia zabihu ya ukombozi, tunaweza kumutumikia Mungu wetu na zamiri safi na kufurahia kabisa kufanya hivyo.​—Zab. 40:8.

Unatumia uhuru wako wa kuchagua ili kuendeleza faida za Ufalme ao faida zako mwenyewe? (Picha hizi zinapatana na fungu la 8-10)

8, 9. (a) Mutume Petro alitoa onyo gani juu ya kutumia uhuru wetu? (b) Tunapambana na hatari gani leo?

8 Lakini, zaidi ya kuonyesha shukrani, tunapaswa kuwa waangalifu ili tusitumie mubaya hata kidogo uhuru wetu wa maana sana. Mutume Petro alituonya tuepuke kutumia uhuru wetu kuwa sababu ya kutenda kulingana na tamaa zetu za kimwili. (Soma 1 Petro 2:16.) Kwa kweli, onyo hilo linatukumbusha jambo lenye lilipata Waisraeli katika jangwa. Na leo pia kuko hatari hiyo, pengine hata zaidi. Kuliko wakati mwingine wowote, Shetani na ulimwengu wake wanatutolea vitu vyenye kuvutia sana katika mambo ya kuvaa na kujipamba, kula na kunywa, mambo ya kujifurahisha, na mambo mengine mengi. Watu wenye kufanya matangazo ya biashara wanatumia kwa ujanja watu wenye kupendeza ili kuonyesha kama tunapaswa kuuza vitu vyenye hatuna navyo lazima kabisa. Ni mwepesi sana kuangukia katika mitego hiyo na kutumia mubaya uhuru wetu!

9 Shauri la Petro linahusu pia mambo mazito zaidi katika maisha, kama vile maamuzi yetu juu ya masomo, kazi, na mambo yenye tunapenda kufikia katika maisha. Kwa mufano, kwenye masomo vijana wanachochewa kutumika sana ili waweze kuingia kwenye masomo za juu. Wanachochewa kuamini kama masomo ya juu inasaidia mutu apate kazi yenye mushahara mukubwa na ya hali ya juu. Na mara nyingi wanawapatia habari zenye zinaweza kufanya ionekane kama wale wenye walisoma masomo ya juu wanapata mushahara muzuri kuliko wale wenye walisoma tu masomo ya segondere. Kwa sababu wanapaswa kukamata maamuzi yenye yatakuwa na matokeo makubwa juu ya maisha yao yote, vijana wanaweza kuvutiwa na mambo hayo yote. Vijana hao na wazazi wao wanapaswa kukumbuka nini?

10. Tunapaswa kukumbuka nini wakati tunatumia uhuru wetu ili kukamata maamuzi ya kipekee?

10 Watu fulani wanaweza kufikiri kama, kwa sababu mutu anapaswa kuchukua maamuzi ya kipekee katika mambo hayo, wanapaswa kuwa na uhuru wa kuchagua mambo yenye wanapenda ikiwa tu zamiri yao haiwasumbue. Pengine wanafikiria maneno haya yenye Paulo aliambia Wakristo Wakorintho juu ya chakula: ‘Kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na zamiri ya mutu mwingine?’ (1 Kor. 10:29) Ni kweli kwamba tuko na uhuru wa kufanya maamuzi ya kipekee juu ya masomo na kazi, lakini tunapaswa kukumbuka kama uhuru wetu uko na mipaka na maamuzi yote yenye tunakamata yako na matokeo. Ndiyo sababu mutume Paulo alisema kwanza hivi: “Mambo yote ni halali [ao, yanaruhusiwa] lakini si mambo yote yaliyo na faida. Mambo yote ni halali, lakini si mambo yote yanayojenga.” (1 Kor. 10:23) Kwa kweli, hilo linatusaidia kuona kama kuko mambo ya maana zaidi ya kufikiria kuliko tu mambo yenye tunapenda wakati tunatumia uhuru wetu katika hali zote za maisha yetu.

TUTUMIE KWA HEKIMA UHURU WETU ILI KUMUTUMIKIA MUNGU

11. Sababu gani tumewekwa huru?

11 Wakati Petro alituonya tuepuke kutumia mubaya uhuru wetu, alionyesha pia sababu gani. Alitushauria tutumie uhuru wetu “kama watumwa wa Mungu.” Kwa hiyo, kusudi kubwa lenye limefanya Yehova atuweke huru kutoka katika sheria ya zambi na kifo kupitia Yesu ni ili tuishi maisha ya kujitoa kwake “kama watumwa wa Mungu.”

12. Noa na familia yake walituwekea mufano gani?

12 Njia ya muzuri zaidi ya kujilinda ili tusitumie mubaya uhuru wetu na tusikuwe tena watumwa wa tamaa za ulimwengu, ni kufuatia kabisa mambo ya kiroho. (Gal. 5:16) Kwa mufano, fikiria Noa na familia yake. Waliishi katika ulimwengu wenye kujaa mambo ya jeuri na uasherati. Lakini, hawakufuatia tamaa ao mambo yenye watu wenye kuwazunguka walikuwa wanafanya. Namna gani waliweza kufanya hivyo? Waliamua kuendelea kufanya kwa bidii kazi yote yenye Yehova alikuwa amewapatia; kujenga safina, kukusanya na kuweka chakula kwa ajili yao na wanyama, na kuonya watu wengine. ‘Noa alifanya kulingana na mambo yote ambayo Mungu alikuwa amemuamuru. Hivyo ndivyo alivyofanya.’ (Mwa. 6:22) Matokeo yalikuwa nini? Noa na watu wa familia yake waliokoka wakati ulimwengu uliharibiwa.​—Ebr. 11:7.

13. Yesu alipewa kazi gani yenye yeye pia alipatia wanafunzi wake?

13 Yehova ametuomba tufanye nini leo? Kwa sababu tuko wanafunzi wa Yesu, tunajua muzuri kazi yenye Mungu ametupatia. (Soma Luka 4:18, 19.) Leo, Shetani amepofusha watu wengi, na hawatambue kama wako watumwa wa dini, vitu vya kimwili, na mambo ya politike. (2 Kor. 4:4) Tuko na pendeleo la kufuata mufano wa Yesu ili kusaidia watu wafikie kumujua na kumutumikia Yehova, Mungu wa uhuru. (Mt. 28:19, 20) Kazi hiyo haiko mwepesi, na iko na magumu mengi. Katika inchi fulani, watu wengi zaidi hawapendezwe na ujumbe wa ufalme, na hata wamoja wanakuwa wakali. Ulizo lenye kila mumoja wetu anapaswa kujiuliza ni hili: ‘Ninaweza kutumia uhuru wangu ili kutegemeza zaidi kazi ya Ufalme?’

14, 15. Namna gani watu wa Yehova wanaona kazi ya kuhubiri? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

14 Inatia moyo sana kuona kwamba watu wengi wameona kama tunaishi wakati wenye inaomba kutenda haraka na wamefanya maisha yao ikuwe mepesi ili wafanye utumishi wa wakati wote. (1 Kor. 9:19, 23) Wamoja kati yao wanatumikia katika maeneo yao; na wengine wanahamia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Hesabu inaonyesha kama katika miaka tano yenye imepita, zaidi ya watu 250 000 wameanza kazi ya upainia, na sasa kuko zaidi ya mapainia wa kawaida 1 100 000. Inafurahisha sana kuona watu wengi wanatumia uhuru wao kwa hekima ili kumutumikia Yehova!​—Zab. 110:3.

15 Ni nini ilisaidia ndugu na dada hao watumie uhuru wao kwa hekima? Fikiria mufano wa John na Judith, wenye wametumikia katika inchi mbalimbali kwa miaka 30 yenye imepita. Wanakumbuka wakati Masomo ya Mapainia yalianza katika mwaka wa 1977, yalikazia kama ni jambo la lazima kuwa tayari kuhama ili kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Ili aendelee kukaza akili juu ya muradi huo, John anasema kama alibadilisha kazi mara nyingi ili aendelee kuwa na maisha mepesi. Mwishowe, wakati walifika katika inchi ingine, waliona kama kusali kwa Yehova na kumutegemea kuliwasaidia wapambane na magumu kama vile, kujifunza luga mupya, kuzoea desturi ya mupya, na kuvumilia hali ngumu ya hewa. Miaka hiyo yenye walifanya katika utumishi huo yalikuwa na matokeo gani juu yao? John anasema hivi: “Nilijisikia kama ninazama kabisa katika kazi ya muzuri zaidi kuliko kazi zote zenye ninajua ao zenye nilifanya. Yehova akakuwa mutu wa kweli zaidi kwangu, kama vile baba mwenye upendo. Sasa ninaelewa muzuri maana ya andiko la Yakobo 4:8 lenye kusema ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’ Nilijua kama nilikuwa nimepata jambo lenye nilikuwa ninatafuta, kusudi lenye furaha katika maisha.”

16. Namna gani maelfu ya watu wametumia uhuru wao kwa hekima?

16 Lakini, tofauti na John na Judith, wengine wako na hali zenye zinawaruhusu kufanya utumishi wa wakati wote kwa muda mufupi tu. Hata hivyo, wengi wanatumia nafasi yenye kujitokeza ili kujitolea kutumika katika kazi ya ujenzi wa kiteokrasi katika dunia yote. Kwa mufano, wakati makao yetu makubwa yalikuwa yanajengwa katika Warwick, New York, ndugu na dada 27000 walijitoa kutumika; wamoja kwa majuma mbili, wengine kwa miezi fulani, wengine kwa mwaka moja, ao kwa muda murefu zaidi. Wengi wao walijinyima mambo fulani ili kutumika huko. Huo ni mufano muzuri sana wa kutumia uhuru wenye Mungu amewapatia ili kumuletea sifa na utukufu Yehova, Mungu wa uhuru!

17. Wale wenye kutumia kwa hekima uhuru wenye Mungu amewapatia, watapata baraka gani?

17 Tuko wenye shukrani kwa sababu tumefikia kumujua Yehova na tunaweza kufurahia uhuru wenye ibada ya kweli inatuletea. Tuonyeshe basi kupitia maamuzi yenye tunakamata kama tunaona uhuru huo kuwa wa maana sana. Kuliko kuutumia ovyoovyo ao kuutumia mubaya, tutumie basi uhuru wetu na nafasi zenye uhuru huo unatokeza ili kumutumikia Yehova kwa nguvu yetu yote. Ikiwa tunafanya hivyo, tunaweza kuwa na tumaini la kufurahia baraka zenye Yehova ameahidi wakati maneno ya unabii huu yatatimia: “Uumbaji wenyewe pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.”​—Rom. 8:21.