Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Sababu gani hairuhusiwe kutia vichapo vya Mashahidi wa Yehova kwenye site ya Internete ya kipekee ao kwenye site za Internete za kupashana habari?

Kwa sababu tunatoa vichapo vyenye kutegemea Biblia bila kuomba feza, watu fulani wanaweza kufikiri kama inaruhusiwa kuweka kopi za vichapo hivyo kwenye site zingine za kipekee za Internete ao kwenye site za Internete za kupashana habari. Lakini, kufanya hivyo kunavunja Kanuni za Matumizi * za site yetu ya Internete, na kumeleta matatizo makubwa. Kama vile inaonyeshwa wazi katika kanuni hizo za matumizi, hakuna mutu mwenye anaruhusiwa “kuweka picha, vichapo vya kielektronike, alama za kutambulisha, muziki, video, au habari fulani kwenye Internete kutoka site hii ya Internete (iwe ni katika site yoyote ya kuchangia habari ao video, ao site za Internete za kupashana habari).” Sababu gani vizuizi hivyo ni vya lazima?

Hakuna mutu mwenye anaruhusiwa kuweka vichapo vyetu vyenye kuwa na haki ya wachapishaji kwenye site zingine za Internete

Mambo yote yenye kuwa kwenye site yetu ya Internete hayapaswe kufanyiwa kopi bila ruhusa ya wachapishaji. Waasi imani na wapinzani wengine wanajaribu kutumia vichapo vyetu vyenye kuwa kwenye site yetu ya Internete ili kuchochea Mashahidi wa Yehova na watu wengine. Kusudi la site hizo ni kufanya wasomaji wakuwe na mashaka. (Zab. 26:4; Met. 22:5) Wengine wametumia alama yetu ya utambulisho ya jw.org ili kufanya matangazo juu ya vitu vyenye kuuzishwa, na katika programu za vyombo vya kielektronike kama vile telefone na tablete. Wakati tunalinda haki ya wachapishaji na alama yetu ya ulinzi, tunaruhusiwa na sheria kuzuia visitumiwe mubaya hivyo. (Met. 27:12) Lakini, ikiwa tunaachilia tu watu, hata ndugu na dada zetu, watie kwenye site zingine vitu vyetu vya kielektronike ao watumie alama yetu ya utambulisho ya jw.org ili kuuzisha biashara, tribinali haziwezi kutusaidia katika bidii yetu ya kuzuia wapinzani na kompanyi za biashara kufanya hivyo.

Site na programu za Internete za kutoa chakula cha kiroho zenye tunaweza kutumainia:

Ni hatari sana kuchukua vichapo vyetu kwenye site zingine za Internete isipokuwa tu kwenye jw.org. Ni ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ tu ndiye Yehova amepatia daraka la kutoa chakula cha kiroho. (Mt. 24:45) ‘Mutumwa’ huyo anatumia tu site zetu ili kugawanya chakula cha kiroho, ni kusema, www.pr418.com, tv.pr418.com, na wol.pr418.com. Na tuko na programu tatu tu za kutia katika vyombo vidogo-vidogo vya kielektronike kama vile tablete na telefone za hali ya juu​—JW Language®, JW Library®, na JW Library Sign Language®. Tunaweza kutumainia site na programu hizo kwa sababu hazifanye matangazo yoyote ya biashara na haziambukizwe na roho ya ulimwengu wa Shetani. Ikiwa tunapata chakula cha kiroho kupitia njia zingine, kinaweza kuwa kimebadilishwa.​—Zab. 18:26; 19:8.

Zaidi ya hilo, kuweka vichapo vyetu kwenye site zenye zinaruhusu watu waeleze mawazo yao kunatolea waasi-imani na watu wengine wenye kuchambua nafasi ya kuleta mashaka juu ya tengenezo. Ndugu fulani wamejiingiza katika mabishano kwenye Internete, na kwa kufanya hivyo wamechafua zaidi jina la Yehova. Kufanya mabishano na watu kwenye Internete haiko njia yenye kufaa ya ‘kufundisha kwa upole wale wasio na muelekeo unaofaa.’ (2 Tim. 2:23-25; 1 Tim. 6:3-5) Imeonekana pia kama watu fulani wameunda konte za uwongo kwenye site za Internete za kupashana habari ao site za Internete kwa jina la tengenezo, Baraza Lenye Kuongoza, ao kwa majina ya ndugu wenye kufanyiza baraza hilo. Lakini, hakuna ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza mwenye kuwa na site yake ya Internete ao mwenye kuwa kwenye site yoyote ya Internete ya kupashana habari.

Kuongoza watu kwenye jw.org kunasaidia kueneza “habari njema.” (Mt. 24:14) Site na programu za kielektroniki zenye tunapewa ili kutumia katika kazi yetu ya kuhubiri zinaendelea kufanywa muzuri zaidi. Tunapenda kila mutu afaidike nazo. Kama vile Kanuni za Matumizi zinaonyesha, unaweza kutumia mutu kupitia adresi ya e-mail kopi ya kielektroniki ya kichapo fulani ao kumutumia njia ya kupata jambo fulani lenye kuwa kwenye jw.org. Wakati tunaongoza watu wenye kupendezwa kwenye site zetu za Internete, tunawaonyesha njia moja tu ya kweli yenye kutoa chakula cha kiroho, ni kusema, ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara.’

^ fu. 1 Njia ya kuenda kwenye Kanuni za Matumizi inapatikana kwenye mwisho wa ukurasa wa mwanzo wa jw.org, na vizuizi hivyo vinahusu kila kitu chenye kupatikana kwenye site yetu ya Internete.