Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Vijana, Munakaza Akili juu ya Miradi ya Kiroho?

Vijana, Munakaza Akili juu ya Miradi ya Kiroho?

‘Mukabizi [mupatie] Yehova mwenyewe kazi zako nayo mipango yako itafanywa imara.’​—MET. 16:3.

NYIMBO: 135, 144

1-3. (a) Vijana wote wako katika hali gani, na hilo linaweza kulinganishwa na nini? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Namna gani vijana Wakristo wanaweza kupambana muzuri zaidi na hali hiyo?

WAZIA unapanga safari ya kuenda katika muji wenye kuwa mbali kwa ajili ya tukio fulani la maana. Ili kufika huko inaomba kusafiri katika bisi kwa muda murefu. Wakati unafika mahali pa kungojea bisi, unavurugika sana kuona watu wengi na bisi nyingi. Lakini jambo la muzuri ni kwamba unajua muzuri kusudi lako, ni kusema, kuingia katika bisi yenye itaenda mahali kwenye umechagua kuenda! Ikiwa unaingia katika bisi yenye inaenda mahali pengine, hilo linaweza kumaanisha kama umepotea njia.

2 Leo, vijana wanaweza kulinganishwa na watu hao wenye kusafiri. Vijana wako na safari ya murefu ya kufanya, haiko katika bisi, lakini katika maisha. Wakati fulani wanaweza kujisikia kuwa wanavurugika kwa sababu ya nafasi zenye kujitokeza katika maisha yao na maamuzi yenye wanapaswa kukamata. Vijana, munaweza kufanya mambo yakuwe mwepesi zaidi kwenu ikiwa munajua muzuri wapi mutaenda katika maisha, ni kusema, mambo yenye munapenda kufanya katika maisha. Munapaswa kuenda wapi?

3 Habari hii itajibia ulizo hilo kwa kutia moyo vijana watumie maisha yao ili kumufurahisha Yehova. Hilo linamaanisha kutia Yehova katika sehemu zote za maisha yao, kama vile, masomo, kazi, madaraka ya familia na mambo mengine. Na linamaanisha pia kujikaza ili kufikia miradi ya kiroho. Vijana wenye wanaendelea kukaza akili yao juu ya kumutumikia Yehova wanaweza kuwa hakika kama atawabariki ili wakuwe na maisha ya muzuri.​—Soma Methali 16:3.

SABABU GANI MUJIWEKEE MIRADI YA KIROHO?

4. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

4 Ni muzuri kujiwekea miradi ya kiroho mbele ya wakati. Sababu gani? Tutachunguza sababu tatu. Sababu mbili za kwanza zinaonyesha kama kujikaza ili kufikia miradi ya kiroho kunatia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova. Sababu ya tatu inakazia faida ya kujiwekea miradi ya kiroho mbele ya wakati katika maisha.

5. Ni sababu gani ya kwanza yenye kutuchochea tujiwekee miradi ya kiroho?

5 Sababu ya kwanza ya kujiwekea miradi ya kiroho ni kuonyesha Yehova kama tuko wenye shukrani kwa upendo wake na kwa mambo yote yenye ametufanyia. Muandikaji mumoja wa zaburi alisema hivi: ‘Ni vema kumutolea Yehova shukrani . . . Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya utendaji wako; kwa sababu ya kazi za mikono yako, ninapiga vigelegele kwa shangwe.’ (Zab. 92:1, 4) Kijana, fikiria mambo yote yenye Yehova amekufanyia; amekupatia maisha, Biblia, na kutaniko, amekusaidia ujue kweli juu yake, na amekupatia tumaini ajabu la wakati wenye kuja. Kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza ni njia ya kuonyesha shukrani kwa Mungu juu ya baraka hizo, na hilo linakufanya umukaribie zaidi.

6. (a) Miradi ya kiroho iko na matokeo gani juu ya urafiki wako pamoja na Yehova? (b) Mutu anaweza kujiwekea miradi gani wakati angali mudogo?

6 Sababu ya pili ni kwamba wakati unajikaza kufikia miradi ya kiroho, unaanza kujifanyia matendo mazuri mbele za Yehova. Hilo litakufanya umukaribie hata zaidi. Mutume Paulo alitoa ahadi hii: ‘Mungu hakose kuwa mwadilifu hivi kwamba asahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili ya jina lake.’ (Ebr. 6:10) Unaweza kujiwekea miradi ya kiroho hata kama ungali mudogo. Christine alikuwa na miaka kumi wakati alijiwekea muradi wa kusoma kwa ukawaida habari juu ya maisha ya Mashahidi waaminifu. Wakati alikuwa na miaka 12, Toby alijiwekea muradi wa kusoma Biblia yote nzima mbele abatizwe. Maxim alikuwa na miaka 11 na mudogo yake Noemi alikuwa na miaka 10 wakati walibatizwa. Wote wawili walijiwekea muradi wa kufanya utumishi wa Beteli. Ili waendelee kukaza akili juu ya muradi wao, walibandika kwenye kibambazi katika nyumba yao kikaratasi cha ombi la kutumika kwenye Beteli. Kwa kweli, unaweza kufikiria miradi fulani yenye kuwa ya maana kwako na kisha uanze kutumika ili kuifikia.​—Soma Wafilipi 1:10, 11.

7, 8. (a) Namna gani kujiwekea miradi kunaweza kufanya ikuwe vyepesi kukamata maamuzi? (b) Sababu gani kijana mumoja aliamua kama hatasoma masomo ya juu?

7 Sababu ya tatu ya kutuchochea kujiwekea miradi ya kiroho mbele ya wakati katika maisha ni kwamba hilo linaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri. Vijana wanapaswa kukamata maamuzi juu ya masomo, kazi, na mambo mengine. Kukamata maamuzi ni kama vile kuchagua barabara ya muzuri wakati unafika mahali kwenye barabara nyingi zinakutana. Ikiwa unajua ni wapi unaenda, itakuwa vyepesi kuchagua barabara ya muzuri. Vilevile, ikiwa unajua miradi yako, itakuwa vyepesi kwako kukamata maamuzi ya muzuri. Methali 21:5 inasema hivi: ‘Mipango ya mwenye bidii bila shaka inaleta faida.’ Ikiwa unajiwekea miradi ya muzuri wakati ungali mudogo, hautakawia kupata matokeo ya muzuri. Damaris alijionea jambo hilo wakati alipaswa kukamata uamuzi wa maana wakati alikuwa angali kijana.

8 Damaris alipata alama nyingi wakati alimaliza masomo ya segondere. Ikiwa angependa angekubali kusoma kwa bure mambo ya sheria kwenye masomo ya juu, lakini aliamua kutumika kwenye benki. Sababu gani? Anasema hivi: “Nilijiwekea mbele ya wakati muradi wa kuwa painia. Ni kusema nilipaswa kutumika kwa saa fulani tu. Ikiwa ningepata diplome ya masomo ya juu katika mambo ya sheria, ningepata feza nyingi, lakini ingekuwa vigumu kwangu kupata kazi ya kutumika kwa saa fulani tu.” Damaris amefanya kazi ya upainia kwa miaka 20. Anaona kama alijiwekea muradi wa muzuri na alikamata uamuzi wa muzuri wakati alikuwa kijana? Anasema hivi: “Kwenye benki mahali kwenye ninafanya kazi, ninakutana na wanasheria wengi. Wanafanya kazi yenye ningekuwa ninafanya ikiwa ningesoma masomo ya mambo ya sheria. Lakini, wengi hawafurahie kazi zao. Uamuzi wangu wa kufanya kazi ya upainia ulinisaidia kuepuka mahangaiko katika kazi ya kimwili na ulikuwa mwanzo wa miaka mingi ya furaha katika kazi ya Yehova.”

9. Sababu gani vijana wetu wanastahili kupongezwa kabisa?

9 Maelfu ya vijana katika makutaniko katika dunia yote wanastahili kupongezwa kabisa. Wanajitoa kwa Yehova na kukaza maisha yao juu ya miradi ya kiroho. Vijana hao wanafurahia kabisa maisha na wakati huohuo wanajifunza kufuata muongozo wa Yehova katika mambo yote. Hilo linatia ndani mambo kama vile masomo, kazi, na maisha ya familia. Sulemani aliandika hivi: ‘Mutegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Mutambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.’ (Met. 3:5, 6) Katika kutaniko la Kikristo, Yehova anaona vijana kuwa wa maana, anawapenda sana na anawatolea ulinzi, muongozo, na baraka.

UJITAYARISHE MUZURI ILI KUTOA USHAHIDI

10. (a) Sababu gani tunapaswa kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza? (b) Namna gani tunaweza kuwa walimu wazuri zaidi katika kazi ya kuhubiri?

10 Kijana mwenye anakaza maisha yake juu ya kumupendeza Yehova, anaona kazi ya kuhubiri kuwa ya maana sana. Yesu Kristo alisema kama “lazima habari njema ihubiriwe kwanza.” (Mk. 13:10) Kwa sababu kazi ya kuhubiri ni ya haraka sana, inapaswa kuwa jambo la maana zaidi katika maisha yetu. Unaweza kujiwekea muradi wa kuhubiri zaidi kwa ukawaida? Unaweza kuwa painia? Utafanya nini ikiwa haupate furaha zaidi katika kazi ya kuhubiri? Na namna gani unaweza kuwa mwalimu muzuri zaidi wakati unatoa ushahidi? Hatua hizi mbili za musingi zinaweza kukusaidia: Ujitayarishe muzuri, na usichoke kuzungumuza na wengine juu ya mambo yenye unaamini. Unaweza kushangaa kuona namna unaweza kupata furaha nyingi wakati unahubiria wengine.

Namna gani unajitayarisha ili kutoa ushahidi? (Picha hizi zinapatana na fungu la 11, 12)

11, 12. (a) Vijana wanaweza kufanya nini ili kujitayarisha kutoa ushahidi? (b) Namna gani kijana mumoja alitumia nafasi yenye alipata ili kutoa ushahidi kwenye masomo?

11 Unaweza kuanza kwa kutafuta jibu la ulizo lenye wanafunzi wenzako wanazoea kuuliza, kama vile, “Sababu gani unaamini Mungu?” site yetu ya Internete jw.org iko na video ya kusaidia vijana wajizoeze wao wenyewe namna ya kujibia ulizo hilo. Unaweza kuangalia kwenye kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > VIJANA. Hapo utapata video yenye kichwa “Maoni ya Vijana Wenzako​—Kumuamini Mungu?” Video hiyo itakusaidia kutayarisha jibu lako. Unaweza kupata musaada kupitia maandiko yenye kuchaguliwa muzuri. Kwa mufano, unaweza kutumia maandiko haya matatu ili kufasiria mambo yenye unaamini​—Waebrania 3:4, Waroma 1:20, na Zaburi 139:14. Unaweza kutumia video hizo ili kutayarisha majibu ya maulizo mbalimbali.​—Soma 1 Petro 3:15.

12 Ikiwa unapata nafasi, utie moyo wanafunzi wenzako wafungue wao wenyewe site yetu ya Internete jw.org. Ni hivyo Luca alifanya. Darasa lao lilikuwa linazungumuza juu ya dini mbalimbali, na Luca akaona kama kitabu chenye walikuwa wanatumia kilikuwa na habari za uwongo juu ya Mashahidi wa Yehova. Hata kama aliogopa kwanza, aliomba ruhusu ya kurekebisha mawazo hayo ya uwongo, na mwalimu wake alikubali. Luca hakufasiria tu mambo yenye anaamini, lakini pia alionyesha darasa lote site yetu ya Internete. Mwalimu alipatia kila mwanafunzi kazi ya nyumbani ya kuangalia video ya picha zenye kuchorwa kwenye ubao yenye kichwa Mushinde Mwenye Kukuchokoza Bila Kumupiga. Luca alifurahi kwa sababu aliweza kutoa ushahidi muzuri.

13. Sababu gani hatupaswe kuacha miradi yetu wakati magumu yanatokea?

13 Usivunjike moyo, hata kama barabara yenye unasafiri ndani inakuwa na majiwe-majiwe wakati fulani. (2 Tim. 4:2) Wakati magumu yanatokea, shikamana na miradi yako. Katharina alikuwa na miaka 17 wakati alijiwekea muradi wa kuhubiria kila mufanyakazi mwenzake. Mufanyakazi mumoja alimutukana mara nyingi, lakini hakuacha jambo hilo limuogopeshe. Mwenendo wake muzuri wakati wa magumu ulivutia mufanyakazi mwengine mwenye kuitwa Hans. Kwa hiyo, alianza kusoma vichapo vyetu, akajifunza Biblia, na kubatizwa. Katharina alikuwa amehama na hakujua mambo hayo yote. Wazia namna alijisikia miaka 13 kisha hapo, wakati alikuwa anakaa katika Jumba la Ufalme pamoja na familia yake na kusikia Hans anatangazwa kuwa musemaji mugeni! Katharina alifurahi sana kwa sababu hakuacha muradi wake wa kuhubiria wafanyakazi wenzake!

USIKENGEUSHWE

14, 15. (a) Wakati vijana wanapambana na mikazo, wanapaswa kukumbuka nini? (b) Namna gani vijana wanaweza kupiganisha mikazo ya vijana wenzao?

14 Kufikia hapa, habari hii imekutia moyo ukaze akili yako juu ya tamaa yako ya kumutumikia Yehova. Hilo linamaanisha kufuatia miradi ya kiroho katika maisha yako. Inawezekana vijana wengine wa miaka yako wanafuatia mambo ya kujifurahisha katika maisha yao, na pengine wakati fulani watakualika ujiunge nao. Wakati fulani, itakuomba kuonyesha kama unashikamana kabisa na maamuzi yenye umekamata. Usikengeushwe na mikazo ya vijana wenzako. Kwa kweli, wakati tunafikiria tena mufano wa bisi, bila shaka, hautaingia katika bisi yenye kuenda mahali pengine kwa sababu tu unaona kuwa watu wenye kusafiri katika bisi hiyo wanaonekana kuwa wako na furaha.

15 Kuko njia mbalimbali za kupambana na mikazo ya vijana wenzako. Kwa mufano, epuka hali zenye zitafanya ikuwe vigumu kushinda vishawishi vya vijana wenzako. (Met. 22:3) Na ukumbuke matokeo ya mubaya sana yenye unaweza kupata wakati unajiunga na wengine katika mwenendo mubaya. (Gal. 6:7) Jambo lingine lenye litakusaidia ni kukubali kama uko na lazima ya mashauri. Unyenyekevu utakusaidia kukubali mashauri ya wazazi na Wakristo wenye kukomaa kiroho katika kutaniko.​—Soma 1 Petro 5:5, 6.

16. Toa mufano wenye kuonyesha faida ya unyenyekevu.

16 Unyenyekevu ulimusukuma Christoph akubali mashauri ya muzuri. Muda mufupi kisha kubatizwa, alianza kujizoeza kwa ukawaida nafasi ya kufanyia mazoezi. Vijana wengine walimuomba ajiunge na kikundi chao cha muchezo. Alizungumuza na muzee mumoja juu ya jambo hilo, na muzee huyo aliambia Christoph afikiri juu ya hatari fulani mbele ya kukamata uamuzi, kama vile hatari ya kuambukizwa na roho ya mashindano. Hata hivyo, Christoph alijiunga na kikundi hicho. Lakini, kisha wakati fulani alitambua kama muchezo huo ulikuwa wenye jeuri, na hata wenye hatari. Alizungumuza tena na wazee mbalimbali, na wote walimupatia mashauri yenye kutoka katika Biblia. Christoph anasema hivi: “Yehova alinitumia washauri wazuri, na nilimusikiliza hata kama ilikamata wakati fulani.” Uko munyenyekevu kabisa ili kukubali mashauri ya muzuri?

17, 18. (a) Yehova anapenda vijana leo wakuwe na maisha ya namna gani? (b) Ni hali gani yenye kuhuzunisha yenye inaweza kutokea wakati kijana amekuwa mutu muzima, na namna gani anaweza kuepuka jambo hilo? Toa mufano.

17 Biblia inasema hivi: “Ewe kijana, shangilia katika ujana wako, na moyo wako ukufanyie mema siku za ujana wako.” (Mhu. 11:9) Ndiyo, Yehova anapenda wewe kijana ukuwe na moyo wenye furaha. Habari hii imezungumuzia njia moja ya kuwa na moyo wenye furaha. Uendelee kukazia miradi ya kiroho, na kufuata mashauri ya Yehova katika mipango yako yote na maamuzi yako yote. Ikiwa unaanza kufanya hivyo mbele ya wakati, hautakawia kuona muongozo, ulinzi, na baraka za Yehova. Fikiria mashauri mengi ya muzuri yenye kupatikana katika Neno la Mungu, na uchukue kwa uzito shauri hili: ‘Mukumbuke, sasa, Muumba wako Mukubwa katika siku za ujana wako.’​—Mhu. 12:1.

18 Hakuna mutu mwenye anabakia kijana kwa muda murefu. Vijana wanakomaa haraka na kuwa watu wazima. Inahuzunisha kusema kama, wakati vijana wengi wanakuwa watu wazima, wanajuta kwa sababu walifuatia miradi yenye haifae, ao jambo la kuhuzunisha zaidi, hawakukuwa na miradi hata kidogo. Lakini, vijana wenye wanakaza akili yao leo juu ya miradi ya kiroho, watatosheka kabisa wakati watakuwa watu wazima juu ya maamuzi yenye walikamata. Mirjana alijionea jambo hilo; wakati alikuwa kijana, alikuwa na uwezo mwingi wa kufanya michezo. Aliombwa kucheza Michezo ya Olimpiki ya Wakati wa Kipindi cha Baridi, lakini aliamua kuanza utumishi wa wakati wote. Kumepita zaidi ya miaka 30 na Mirjana angali katika utumishi wa wakati wote pamoja na bwana yake. Anafasiria hivi: “Kujulikana, kusifiwa, kuwa na uwezo, na utajiri ni miradi ya muda na yenye haina maana katika maisha. Kumutumikia Mungu na kujikaza kusaidia watu kiroho kwa kiasi fulani ni miradi yenye kufaa kabisa na ya muda murefu.”

19. Taja kwa kifupi faida za kukaza akili juu ya miradi ya kiroho mbele ya wakati katika maisha.

19 Vijana katika kutaniko wanastahili kupongezwa kabisa kwa sababu wanajikaza kupambana na hali hiyo na kuazimia kukazia utumishi wa Yehova katika maisha yao. Vijana wanafanya hivyo kwa kujiwekea miradi ya kiroho na kwa kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza kabisa. Zaidi ya hilo, wanaazimia kukataa kukengeushwa na ulimwengu huu. Vijana wanaweza kuwa hakika kama kazi yao ngumu haiko ya bure. Ndugu na dada zao wanawategemeza kwa upendo, na wakati wanajitoa kabisa kwa Yehova, mipango yao katika maisha itakuwa na matokeo ya muzuri.