Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wanaume Wenye Kuwa na Madaraka—Muige Mufano wa Timotheo

Wanaume Wenye Kuwa na Madaraka—Muige Mufano wa Timotheo

MWAKA jana katika dunia yote, maelfu ya wanaume waliwekwa kuwa wazee na watumishi wa huduma katika makutaniko ya Mashahidi wa Yehova. Ikiwa uko kati ya ndugu hao wapendwa, kwa kweli, unafurahia pendeleo lako mupya la utumishi.

Lakini, unaweza kuwa pia na wasiwasi kidogo. Jason, kijana mwenye kuwa muzee wa kutaniko, anasema hivi: “Wakati niliwekwa kuwa muzee, mwanzoni nilijisikia kama ninalemewa na madaraka yangu ya mupya.” Musa na Yeremia waliona kama hawana uwezo wa kutimiza madaraka mapya yenye Yehova alikuwa amewapatia. (Kut. 4:10; Yer. 1:6) Ikiwa unajisikia pia hivyo, namna gani unaweza kumaliza hali hiyo na kuendelea kufanya maendeleo? Fikiria mufano wa mwanafunzi Mukristo Timotheo.​—Mdo. 16:1-3.

UIGE MUFANO WA TIMOTHEO

Pengine, Timotheo alikaribia kueneza miaka 20 ao alikuwa na miaka 20 hivi wakati mutume Paulo alimuomba aanze kusafiri pamoja naye. Kwa sababu Timotheo alikuwa kijana, pengine mwanzoni hakukuwa anajiamini na pengine alisita kutumika katika mugawo wake mupya. (1 Tim. 4:11, 12; 2 Tim. 1:1, 2, 7) Lakini, kisha kupita miaka kumi, Paulo aliambia hivi kutaniko la Filipi: ‘Ninatumaini katika Bwana Yesu kumutuma Timotheo kwenu upesi [haraka] . . . Kwa maana sina mutu mwingine yeyote aliye na muelekeo kama wake.’​— Flp. 2:19, 20.

Ni nini ilimusaidia Timotheo akuwe muzee muzuri hivyo? Ona mambo sita yenye mufano wake unaweza kukufundisha.

1. Alihangaikia kabisa watu. Paulo aliambia hivi ndugu katika Filipi: ‘[Timotheo] atajali kwa unyoofu mambo yenu.’ (Flp. 2:20) Kwa kweli, Timotheo alijali ao alihangaikia watu. Alipenda wamukaribie Yehova, na alikuwa tayari kujitoa kabisa kwa ajili yao.

Epuka kuiga mufano wenye kujulikana wa mutu fulani mwenye kutembeza bisi mwenye anahangaikia zaidi kufika kwa wakati kila mahali penye iko anaenda kuliko kukamata watu. William, mwenye amekuwa muzee mwenye kuheshimiwa kwa miaka 20, anashauria hivi ndugu wenye wamepewa madaraka hivi karibuni: “Mupende ndugu na dada. Mukaze akili juu ya mahitaji yao kuliko kukaza akili juu ya namna mambo yanapaswa kusimamiwa na kupangwa katika kutaniko.”

2. Aliweka faida za kiroho pa nafasi ya kwanza. Ili kuonyesha tofauti kati ya mufano wa Timotheo na wa wengine, Paulo alisema hivi: “Wengine wote wanatafuta faida zao wenyewe, wala si zile za Kristo Yesu.” (Flp. 2:21) Paulo alikuwa Roma wakati alikuwa anaandika maneno hayo. Aliona kama ndugu huko walikuwa wanahangaikia sana mambo yao ya kipekee. Kwa kadiri fulani, hawakujitoa ili kufanya kazi ya kiroho. Lakini Timotheo hakukuwa hivyo! Wakati nafasi za kuendeleza habari njema zilijitokeza, alikuwa na roho kama ya Isaya, mwenye alisema hivi: “Mimi hapa! Nitume mimi!”​—Isa. 6:8.

Namna gani unaweza kuwa na usawaziko juu ya madaraka yako ya kipekee na ya kiroho? Kwanza, uweke mambo ya maana pa nafasi ya kwanza. Paulo alitoa shauri hili: ‘Muhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi.’ (Flp. 1:10) Tia pa nafasi ya kwanza mambo yenye Mungu anaona kuwa ya maana zaidi. Pili, ufanye maisha yako kuwa mepesi. Achana na mambo yenye kumaliza nguvu na kupoteza wakati. Paulo alimushauria Timotheo hivi: ‘Zikimbie tamaa zinazotukia ujanani, lakini fuatilia uadilifu, imani, upendo, amani.’​—2 Tim. 2:22.

3. Alitumika kwa bidii katika utumishi mutakatifu. Paulo alikumbusha Wafilipi hivi: ‘Munaujua usibitisho alioutoa [Timotheo] juu yake mwenyewe, kwamba kama mutoto na baba yake yeye alitumika pamoja nami katika kuendeleza habari njema.’ (Flp. 2:22) Timotheo hakukuwa muvivu. Alitumika kwa bidii pamoja na Paulo, na hilo lilifanya wapendane zaidi.

Kuko kazi nyingi katika tengenezo la Mungu leo. Kazi hiyo inaleta furaha kabisa na inaweza kukufanya ukaribie ndugu na dada zako. Kwa hiyo, ujiwekee muradi wa kuwa sikuzote na “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.”​—1 Kor. 15:58.

4. Alitumikisha mambo yenye alijifunza. Paulo aliandikia Timotheo hivi: “Wewe umefuata kwa ukaribu fundisho langu, mwendo wangu wa maisha, kusudi langu, imani yangu, ustahimilivu wangu, upendo wangu, uvumilivu wangu.” (2 Tim. 3:10) Kwa sababu Timotheo alitumikisha mambo yenye alijifunza, alistahili kupewa madaraka makubwa zaidi.​—1 Kor. 4:17.

Uko na rafiki mwenye kukomaa na mwenye kuwa na uzoefu mwenye anaweza kukusaidia kukomaa zaidi kiroho? Ikiwa hauna, wewe pia unaweza kutafuta. Tom, mwenye amekuwa muzee kwa muda murefu, anakumbuka hivi: “Muzee mumoja mwenye uzoefu alipendezwa sana na mimi na alinipatia mazoezi ya muzuri sana. Mara kwa mara nilimuomba mashauri na nilitumikisha mashauri yake. Na bila kukawia hilo lilifanya nijiamini.”

5. Aliendelea kujizoeza. Paulo alishauria hivi Timotheo: ‘Ukuwe unajizoeza ujitoaji-kimungu [kushikamana na Mungu] ukiwa ni shabaha yako.’ (1 Tim. 4:7) Mutu mwenye kufanya muchezo fulani anaweza kuwa na mutu wa kumuzoeza, lakini yeye pia anapaswa kujizoeza yeye mwenyewe. Paulo alimushauria Timotheo hivi: ‘Endelea kufanya bidii katika kusoma mbele ya watu wote, katika kuhimiza, katika kufundisha. . . . Tafakari mambo haya; zama katika hayo, ili maendeleo yako yakuwe wazi kwa watu wote.’​—1 Tim. 4:13-15.

Wewe pia unapaswa kuendelea kukomalisha ufundi wako. Ukuwe mwanafunzi mwenye bidii na uelewe miongozo ya hivi karibuni ya tengenezo. Pia, uepuke kujitumainia kupita mipaka, pengine kwa kufikiri kama uko na uzoefu mwingi sana hivi kwamba unaweza kushugulikia hali yoyote bila kutafuta habari kwa uangalifu. Kama Timotheo, “jiangalie daima [sikuzote] wewe mwenyewe na kufundisha kwako.”​—1 Tim. 4:16.

6. Alitegemea roho ya Yehova. Wakati alifikiria utumishi wa Timotheo, Paulo alimukumbusha hivi: “Amana hii nzuri ilinde kupitia roho takatifu inayokaa ndani yetu.” (2 Tim. 1:14) Ili kulinda utumishi wake, Timotheo alipaswa kutegemea roho ya Mungu.

Donald, mwenye amekuwa muzee wa kutaniko kwa miaka mingi, anasema hivi: “Wanaume wenye kuwa na madaraka wanapaswa kupenda sana urafiki wao pamoja na Mungu. Wale wenye wanafanya hivyo watapata ‘nguvu zaidi.’ Ikiwa wanamuomba Mungu roho yake na kukomalisha tunda la roho hiyo, watakuwa baraka kubwa kwa ndugu zao.”​—Zab. 84:7; 1 Pet. 4:11.

UPENDE SANA PENDELEO LAKO

Inatia moyo sana kuona ndugu wengi wenye kupewa madaraka, kama wewe, wanafanya maendeleo ya kiroho. Jason mwenye tulizungumuzia kwenye mwanzo wa habari hii, anasema hivi: “Kwa wakati wote wenye nimekuwa muzee nimejifunza mambo mengi na nimejiamini zaidi. Sasa ninafurahia kabisa mugawo wangu na ninauona kuwa pendeleo la ajabu!”

Utaendelea kufanya maendeleo ya kiroho? Ujiwekee muradi wa kuiga mufano wa Timotheo. Kisha wewe pia utakuwa baraka kwa watu wa Mungu.